Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
Toka
Ingia
Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Leo

Siku ya Pili, 2 Mwezi wa 9

Roho inachunguza ndani ya mambo yote, hata mambo mazito ya Mungu.​—1 Ko. 2:10.

Kama uko mu kutaniko ya munene na ile inafanyaka kiongozi asikutaye, unaweza kuvunjika moyo. Lakini, usiache kutoa maelezo. Tayarisha maelezo mingi ku kila mukutano. Na kama haupate nafasi ya kutoa maelezo ku mwanzo wa funzo, utakuwa na nafasi ingine ya kutoa maelezo wakati mukutano uko naendelea. Wakati uko natayarisha Funzo ya Munara wa Mulinzi fikiria namna kila fungu inapatana na kichwa ya ile habari. Kama unafanya vile, pengine utapata maelezo ya muzuri yenye unaweza kutoa. Zaidi ya ile, unaweza kutayarisha maelezo yenye kuwa mu mafungu yenye kuzungumuzia mafundisho mazito yenye iko nguvu kufasiria. Juu ya nini? Juu kutakuwa watu kidogo wenye watapenda kutoa maelezo mu ile sehemu. Sasa utafanya nini kama kisha mikutano mingi haupewe tu nafasi ya kutoa maelezo? Mbele mukutano uanze, umuambie kiongozi kama unapenda kuleta jibu ya ulizo fulani. w23.04 21-22 fu. 9-10

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Tatu, 3 Mwezi wa 9

Yosefu . . . alifanya kama vile malaika wa Yehova alimuambia, akamuchukua bibi yake na kuenda naye kwake.​—Mt. 1:24.

Yosefu alikuwa tayari kutumikisha muongozo wa Yehova, na ile njo ilifanya akuwe bwana muzuri zaidi. Zaidi ya mara tatu, Mungu alimupatia maagizo kuhusu familia yake. Kila mara alitii palepale hata kama ilikuwa nguvu. (Mt. 1:20; 2:13-15, 19-21) Juu Yosefu alitii muongozo wa Mungu, alimulinda Maria, alimutegemeza na kumuhangaikia. Fikiria namna mambo yenye Yosefu alifanya ilimusaidia Maria amupende na amuheshimie hata zaidi! Bwana, unaweza kuiga Yosefu kwa kutafuta mashauri yenye inategemea Biblia yenye inaonyesha namna unaweza kuhangaikia familia yenu. Kama unatumikisha ile mashauri hata kama ni nguvu, utaonyesha kuwa unamupenda bibi yako na utafanya ndoa yenu ikuwe muzuri zaidi. Dada wa Vanuatu, mwenye alishafanya zaidi ya miaka 20 mu ndoa, anasema hivi: “Wakati bwana yangu anatafuta muongozo wa Yehova na kuutumikisha, ile inafanyaka nimuheshimie zaidi. Najisikiaka kuwa salama na natumainiaka maamuzi yake.” w23.05 21 fu. 5

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025

Siku ya Ine, 4 Mwezi wa 9

Kutakuwa njia kubwa kule, ndiyo, njia yenye kuitwa Njia ya Utakatifu.​—Isa. 35:8.

Wayahudi wenye wangetoka mu Babiloni wangefanywa kuwa “watu watakatifu” kwa Mungu wao. (Kum. 7:6) Lakini, ile haikumanisha kama hawakukuwa na lazima ya kufanya mabadiliko ili kumufurahisha Yehova. Wayahudi wengi walizaliwa mu Babiloni, na wengi walikuwa walishazoea namna fulani ya kufikiri ya Wababiloni na kanuni zao. Miaka mingi kisha kikundi ya kwanza ya Wayahudi kurudia Yerusalemu, Gavana Nehemia alishangaa wakati aliona kama watoto wenye walizaliwaka mu Israeli hawakujifunzaka hata luga ya Wayahudi. (Kum. 6:6, 7; Ne. 13:23, 24) Zamani, Biblia iliandikwa zaidi sana mu Kiebrania. Sasa, juu wale watoto hawakujua ile luga, namna gani wangejifunza kumupenda Yehova na kumuabudu? (Ezr. 10:3, 44) Kwa hiyo, wale Wayahudi walipaswa kufanya mabadiliko makubwa. Lakini, ingekuwa mwepesi zaidi kwao kufanya ile mabadiliko mu Israeli, mwenye ibada safi ilikuwa inarudishwa pole kwa pole.​—Ne. 8:8, 9. w23.05 15 fu. 6-7

Tuchunguze Maandiko Kila Siku—2025
Karibu
Hii ni chombo ya kukusaidia kutafuta habari mu vichapo vya Mashahidi wa Yehova mu luga mbalimbali.
Kama unapenda kuchukua kichapo fulani, tafazali fungua jw.org.
  • Kiswahili (Congo)
  • Tumia Wengine
  • Préférences
  • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
  • Kanuni za Matumizi
  • Kanuni za Kutunza Siri
  • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
  • JW.ORG
  • Ingia
Tumia Wengine