Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/96 uku. 1
  • “Fululizeni Kulinda”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Fululizeni Kulinda”
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Mulinde Akili Zenu, Mukuwe Macho!”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2023
  • Tuige Mufano wa Yesu wa Kuendelea Kukesha
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Sababu Gani Tunapaswa ‘Kuendelea Kukesha’?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Unapaswa Kufanya Nini ili Uendelee Kutambua Lazima ya Kuhubiri kwa Haraka?
    Huduma Yetu ya Ufalme—2014
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 1/96 uku. 1

“Fululizeni Kulinda”

1 Yesu aliposema maneno yanayoripotiwa katika Mathayo 26:​38-41, alikuwa akikaribia nyakati zilizo ngumu zaidi za maisha yake ya kibinadamu. Nyakati hizo zingethibitika kuwa za maana zaidi katika historia yote. Wokovu wa wanadamu wote ulikuwa hatarini. Wanafunzi wa Yesu walipaswa ‘kufululiza kulinda.’

2 Leo twasimama ukingoni mwa kufika kwa Yesu katika daraka lake lenye sehemu mbili la mkombozi na mtekeleza-hukumu. Kwa kuwa sisi ni Wakristo wenye kulinda wanaotambua uharaka wa nyakati, hatukunji mikono yetu tu na kungoja ukombozi. Tunajua kwamba tunapaswa kila wakati kuwa tayari. Ni jambo la lazima kwamba tuendelee ‘kufanya kazi kwa bidii na kujikakamua wenyewe’ katika utumishi wa Yehova. (1 Tim. 4:10) Namna gani kuhusu kila mmoja wetu tukiwa watu mmoja-mmoja? Je! sisi twafululiza kulinda?

3 Tujichunguze Wenyewe: Yesu alitoa onyo hili pia: “Jiangalieni.” (Lk. 21:​34, 35) Tunapaswa kujiangalia wenyewe, tukihakikisha kwamba tupo “wasio na lawama, wala udanganyifu, . . . kati ya kizazi chenye ukaidi, kilichopotoka.” (Flp. 2:15) Je! kila siku tunajiendesha kama Wakristo, tukiiga Yesu na kufuata kanuni zilizomo katika Neno la Mungu? Tunapaswa kutupilia mbali mwenendo wowote usio wa Kikristo ambao ni wa pekee kwa ulimwengu, ‘unaokaa katika nguvu za yule mwovu.’ (1 Yn. 5:​19, NW; Rum. 13:​11-14) Tunapojichunguza wenyewe kwa mwangaza wa Maandiko, je!, kweli sisi twafululiza kulinda kama alivyoagiza Yesu?

4 Wazee wanapaswa kubaki chonjo kwa kutimiza kwa bidii madaraka yao katika kutaniko, huku wakijua kwamba watatoa hesabu juu ya namna wanavyotunza kundi. (Ebr. 13:17) Vichwa vya familia vina daraka hasa la kuongoza nyumba zao katika njia za Yehova. (Mwan. 18:19; Yos. 24:15; ona 1 Timotheo 3:​4, 5) Pia, ni jambo la muhimu kwamba tufuate sisi sote amri ya Biblia ya kupendana wamoja kwa wengine. Hiyo ni alama ya kutambulisha Ukristo wa kweli.​—Yn. 13:35.

5 Tuwe Macho Kuwaonya Wengine: Kufululiza kulinda kunatia ndani mambo mengi kuliko kujiangalia sisi wenyewe. Tuna wajibu wa kufanya wanafunzi. (Mt. 28:​19, 20) Upendo kwa jirani yetu ungepaswa kutusukuma kumuonya ili aweze kuokoka uharibifu wa ulimwengu. Hilo ni daraka la kila Mkristo. Ni sehemu ya muhimu ya ibada yetu. (Rum. 10:​9, 10; 1 Kor. 9:16) Tunakutana mara nyingi na ubaridi au upinzani wa waziwazi tunaposhiriki katika kazi ya kuokoa uhai. Imetupasa kuendelea, hata ikiwa watu walio wengi hawajali onyo letu. (Ezek. 33:​8, 9) Upendo wa kweli kweli kwa Mungu na kwa jirani yetu utatuchochea kuvumilia.

6 Huu sio wakati wa kujisikia wenye starehe. Hatungepaswa kuruhusu mahangaiko ya maisha ya kila siku kutupumbaza, wala sisi kujiingiza katika anasa za ulimwengu huu hivi kwamba zifikie kuwa mtego. (Lk. 21:​34, 35) Ni sasa kuliko wakati mwingine wowote ule tunapaswa kutambua kwamba tunaishi kipindi kigumu. Wakati wa Yesu Kristo kutekeleza hukumu iliyotamkwa dhidi ya mfumo huu mwovu unakaribia zaidi na zaidi. Ni wale tu walio macho, chonjo, na wanaofululiza kulinda ndio watakaookolewa. Ikiwa tunatii maagizo ya Yesu na ‘tunafikia kuokoka katika hayo yote yatakayotokea,’ tutakuwa bila shaka wenye shukrani kwa Yehova.​—Lk. 21:36.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine