Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/96 uku. 2-5
  • Je! Ni Lazima Kuhubiri Tukiwa Wawili Wawili?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Je! Ni Lazima Kuhubiri Tukiwa Wawili Wawili?
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 2/96 uku. 2-5

Je! Ni Lazima Kuhubiri Tukiwa Wawili Wawili?

1 Hesabu ya wakaaji wa maeneo mengine inaongezeka haraka na inaonekana kwamba watu zaidi na zaidi wanatamani kujua sababu ya hali za ulimwenguni. Tunaona kwamba mavuno ni makubwa na kwamba hesabu ya wafanyakazi ni ndogo kwa kulinganisha ili kushugulikia kazi ya kuhubiri na kufundisha. Tunajiuliza ulizo hili: Namna gani kuwafikia watu zaidi katika wakati tunaotumia katika huduma ya Ufalme?

2 Je! umewahi kuona katika kutaniko lenu kwamba wahubiri wakati fulani wana mwelekeo wa kwenda nyumba kwa nyumba wakiwa wengi au mara nyingine wakiwa watatu watatu? Je! mara nyingi unawaona wahuribiri wengi wenye maarifa kutumika pamoja? Je! jambo hilo hufanyika kwa sababu wao hufanya kazi katika eneo lenye hatari au sababu tu ni zoea ambalo limekomalishwa kadiri miaka inavyoendelea?

3 Maandiko yanaonyesha kwamba tangu zamani sana watu huthamini kutumikia wakiwa pamoja katika utumishi wa Mungu. Wakati Yesu alipowachagua wanafunzi makumi saba ili wamtangulie kuingia katika miji fulani, yeye aliwatuma wawili wawili. (Luka 10:1) Wakati Paulo alipoanza safari yake ya umisionari, yeye alimchukua Timotheo kuwa kama msaidizi. (Mdo. 16:​1-3) Pia Solomono aliona faida ya kuwa na mwandamani; hivyo, alisema: “Wawili ni vizuri kuliko mumoja; kwa sababu wana zawabu nzuri kwa kazi yao.” Hilo halimanishi kwamba mtu hawezi kutumika peke yake katika kazi ya kuhubiri habari njema, badala yake ni kwamba tunapotokea na wengine na kusaidiana tunafaidika na mambo mengi mazuri. Katika mifano hiyo yote jambo ni kwamba wahudumu Wakristo wawili hufanya kazi pamoja. Je! tunaweza pia kuchukua zoea la kutokea watatu watatu katika huduma ya shambani?

4 Huduma Yetu Ya Ufalme ya Novemba 1991, ukurasa 1, inatoa jibu katika makala “Tuwasaidie Wengine Katika Mahubiri.” Tungeweza kusoma hivi kwenye vifungu 1 na 4: “Tangu mianzo yalo, kundi la Kikristo ni tengenezo la waeneza-evanjeli. Yesu mwenyewe aliwatayarisha wanafunzi wake kwa ajili ya mahubiri na ‘aliwatuma wawili wawili.’ (Mko. 6:7; Luka 8:1) . . .  Ijapokuwa si lazima wakati wote kuwa na mwenzi wa utumishi katika huduma, wengi kati yetu wanapenda kushindikizwa. (Mhu. 4:9) . . .  Wakati tunapomshindikiza mtu fulani katika mahubiri tunataka kufanya kazi ya kikundi. (Ona 1 Wakorinto 3:​6, 9.) Tunaweza sote wawili kutoa ushuhuda, kwa kuanzisha kwa mfano mazungumzo kwenye mlango tukihubiri mmoja baada ya mwingine.”

5 Tufanyeje wakati tunapohubiri sehemu iliyo ya hatari? Huduma Yetu Ya Ufalme ya Novemba iliyotajwa hapo juu inatoa jibu lifuatalo, kwenye fungu la 3: “Kwa sababu za kiusalama, labda ni jambo la akili kuhubiri katika vijiji fulani tukiwa wengi.” Pia, tunaweza kusoma katika kitabu Huduma Yetu (ukurasa 97, fungu 1 na ukurasa 104): “Pia, huenda ikafaa katika sehemu fulani kugawa wahubiri wawili au zaidi kwenda kufanya kazi pamoja kwa sababu nyingine.” “Kama mhubiri anafanya kazi katika sehemu au katika hali zinazoonyesha si jambo la hekima kuwa peke yake na, kwa hiyo, ni lazima mhubiri mwingine afuatane naye, wote wawili wanaweza kuhesabu wakati ikiwa wote wawili wanashiriki kutoa ushuhuda.”

6 Kulingana na maneno hayo, inaonekana wazi kwamba kwa kawaida mhubiri angepaswa kwenda kwenye milango akiwa peke yake au wawili wawili. Katika maeneo mengine yenye hatari, angefanya vizuri zaidi kuhubiri wakiwa wawili; huenda mara nyingine ikaomba kuwa wengi. Inatukia pia kwamba ndugu fulani akafuatana na dada asiye mke wake au hata mmoja wa familia ya kimnofu. Katika kisa kama hiki, ni jambo la akili kwamba kikundi kiwe chenye watu watatu hivi. Isipokuwa sababu hizo chache za kipekee, kwa kufuata kielelezo cha Bwana wetu Yesu Kristo na wanafunzi wake wa kwanza, tutajitahidi kuhubiri, ikiwezekana wawili wawili, au hata mtu pekee, kuliko watatu watatu.—1 Pet. 2:21.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine