Mikutano Ya Utumishi Ya Februari
Juma Toka Februari 5
Wimbo 133
Dak. 8: Matangazo ya kwenu. Matangazo yaliyochanguliwa katika Huduma Yetu ya Ufalme.
Dak. 17: “Kufundisha Neno la Mungu kwa Kutumia Broshua.” Ndugu aliyegawiwa sehemu hii ya mkutano atazungumza na wahubiri wawili au watatu mambo mbalimbali yenye kutofautisha broshua. Kisha wanajizoeza namna ya kuzitolea watu.
Dak. 20: “‘Wajumbe wa Amani ya Kimungu’—Kusanyiko la Wilaya 1996.” Kwa maulizo na majibu. Itatolewa na mwandishi. Tia moyo ndugu wote kutengeneza mambo yao tangu sasa ili kuhudhuria sehemu zote za programu ya kusanyiko la wilaya kule kutaniko limealikwa.
Wimbo 28 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Februari 12
Wimbo 138
Dak. 10: Matangazo ya kwenu. Hali ya fedha. Sifu wahubiri katika njia yenye kufaa kwa ajili ya tegemezo lao la kifedha ambalo wanaleta kwa kutaniko na kwa kazi ya ulimwenguni ya kuhubiri habari njema ya Ufalme. Julisha kwa kutaniko kiasi cha zawadi ambacho kutaniko lilituma kwenye Tawi ya Sosaiti, ikiwa hilo linafaa.
Dak. 15: “Je! Ni Lazima Kuhubiri Tukiwa Wawili Wawili?” Mazungumzo ya makala pamoja na wasikilizaji, itatolewa na mwangalizi wa utumishi. Maandiko yanaweza kusomwa moja kwa moja kutoka katika Biblia. Uwe mwenye shauku na uwasaidie wahubiri kufuata kielelezo cha Biblia.
Dak. 20: “Tuwe Watendaji, Si Wasikiaji Tu.” Kwa maulizo na majibu. Kadiri wakati uliotolewa unaruhusu, zungumza juu ya ulazima wa kutii kwa msaada wa kitabu Auxiliaire, ukurasa 1099, mafungu 1 na 2.
Wimbo 70 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Februari 19
Wimbo 77
Dak. 10: Matangazo.
Dak. 15: Mahitaji ya kutaniko au hotuba inayotolewa na mzee ambayo inajengwa juu ya makala “Linda Hisi Yako Ya Uharaka” katika toleo la Mnara wa Mlinzi wa Oktoba 1, 1995, kurasa 25-8.
Dak. 20: “Ziara Za Kurudia Zenye Matokeo kwa Msaada wa Fundisho Bora.” Chunguzeni mawazo makuu. Onyesho moja fupi au mawili.
Wimbo 156 na sala ya kumalizia.
Juma Toka Februari 26
Wimbo 200
Dak. 10: Matangazo.
Dak. 20: “Kufaidika na Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1996—Sehemu ya 1. ” Hotuba itolewe na mwangalizi wa shule. Kumbusha maagizo kuhusu hotuba za wanafunzi kama yanavyotolewa katika Programu ya Shule ya Huduma ya Kitheokrasi ya 1996 katika toleo la Huduma Yetu Ya Ufalme la Novemba 1995.
Dak. 15: “Tunalihitaji Kutaniko.” Kwa maulizo na majibu.
Wimbo 92 na sala ya kumalizia.