Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/96 uku. 1
  • Tuwe Watendaji, Si Wasikiaji Tu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuwe Watendaji, Si Wasikiaji Tu
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Mukuwe Watendaji wa Neno”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
  • Tumsifu Yehova Kila Siku
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • “Musifu Jina la Yehova”
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2024
Huduma Yetu ya Ufalme—1996
km 2/96 uku. 1

Tuwe Watendaji, Si Wasikiaji Tu

1 Siku zetu, Wakristo wa kweli wanachunga moyoni kitia moyo kinachowaalika kuwa watendaji wa neno, na si wasikiaji tu. (Yak. 1:22) Hali yao inajitofautisha sana na ile ya wanaojidai kuwa wakristo ambao humtumikia Mungu kwa midomo tu. (Isa. 29:13) Yesu alionyesha wazi kwamba ni wale tu ambao wangefanya mapenzi ya Mungu ndiyo wangeokolewa.—Mat. 7:21.

2 Ibada inayotolewa pasipo matendo ya kimungu ni isiyo na maana yoyote. (Yak. 2:26) Kwa hiyo sisi tujiulize: ‘Je! matendo yangu yanaonyesha kuwa imani yangu ni ya kweli? Je! ninaishi kabisa kabisa kulingana na mambo mimi ninaamini? Namna gani naweza kumwiga Yesu vizuri zaidi?’ Kwa kujibu maulizo hayo kwa unyofu, tutaona maendeleo gani tumefanya kuhusu kutimiza mapenzi ya Mungu na yale yanayobaki kwetu kutimiza.

3 Sisi kama wanafunzi wa Yesu, mradi wetu wa maana unapaswa kuwa ule ule unaoonyeshwa na mtunga zaburi: “Tumejisifia Mungu muchana kutwa, na tutashukuru jina lako milele.” (Zab. 44:8) Ukristo ni njia ya maisha inayopaswa kuonekana na watu kila siku na katika kila jambo tunalofanya. Tunakuwa na kurizika kwingi tunapoonyesha katika kila utendaji wetu tamaa yetu ya moyoni ya kumsifu Yehova.—Flp. 1:11.

4 Kumtolea Yehova Sifa Hutia Ndani Mengi Zaidi ya Kuishi Maisha Yenye Kunyooka: Ikiwa mwenendo mwema ndilo jambo tu Mungu anaomba, tungeweza kurizika tu na jambo la kutafuta kujitengeneza zaidi. Walakini, ibada yetu yataka pia kwamba tutangaze sifa bora zaidi za Yehova na kwamba tufanye tangazo la peupe kuhusu jina lake.—Ebr. 13:15; 1 Pet. 2:9.

5 Mahubiri ya peupe ya habari njema ni mojapo ya kazi za maana sana ambazo tunapaswa kutimiza. Yesu alijitoa kwa kazi hiyo, kwa maana alijua kwamba hiyo yamaanisha uhai wa milele kwa wale wangesikiliza. (Yn. 17:3) Leo, “kuhubiri neno” ni jambo la maana sana; ni njia pekee itakayowezesha wokovu wa binadamu. (Mdo. 6:4; Rum. 10:13) Tukitambua mambo mazuri tunayoweza kupata au kupoteza kunatufanya tusikie kwa nini Paulo alituhimiza sisi ‘kuhubiri lile neno’ na ‘kufanya hivyo kwa haraka.’—2 Tim. 4:2.

6 Kumsifu Yehova kwapaswa kuchukua mahali gani katika maisha yetu? Mtunga zaburi alitangaza kwamba ilikuwa ndilo hangaiko lake muchana kutwa. Zab. 44:8 Je! hatujisikie hivyo pia? Bila shaka. Kukutana kwetu na watu wengine kunatutolea nafasi ya kusema juu ya jina la Yehova. Tutatafuta kufanya mazungumzo yaelekee mambo ya kiroho. Sisi tutajitahidi pia kushiriki kwa ukawaida katika huduma pamoja na kutaniko. Wale ambao hali zinaruhusu wanaweza kufikiria sana utumishi wa painia, njia itoayo nafasi ya kufanya mahubiri yachukue nafasi ya mbele kila siku katika maisha yetu. Neno la Mungu linatuhakikishia sisi kwamba wale wafanyao mapenzi ya Mungu kwa bidii ni wenye furaha.—Yak. 1:25.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine