Broshua: Vyombo Vya Thamani Kwa Ajili Ya Huduma
1 Fundi stadi wa kazi kwa kawaida anachukua vyombo vingi kwa ujumla, ambavyo kila kimoja kinakusudiwa kwa kazi fulani kamili. Sisi ni wahubiri wa Ufalme, tuna pamoja nasi broshua nyingi zinazotusaidia kutosheleza kwa ustadi mahitaji ya kiroho ya watu ambao tunahubiria. (Mit. 22:29) Inawezekana kwamba tunakutana na mtu mwenye kushuka moyo. Au tena, mtu anayefikiria serikali ya haki, au mtu anayejiuliza ikiwa uzima una kusudi. Jinsi gani kutumia broshua zetu ili kuwasaidia?
2 Kwa kutolea broshua “Je! Kweli Mungu Anatujali?”, tungeweza kusema:
◼“Watu fulani wanaoona mateso na udhalimu (ukosefu wa haki) unaenea ulimwenguni wana maelekeo ya kumtwika Mungu daraka hilo. Wanasema kwamba, kwa kuwa Mungu ni Mweza-Yote, ikiwa alikuwa kweli mwenye kutujali angekomesha mateso yetu. Wewe unafikiri nini? [Acha mtu ajibu.] Zaburi 72:12-14 inaonyesha kwamba Mungu hakika anatuhangaikia. Si yeye chanzo cha mateso na udhalimu. Anaahidi kwamba watenda maovu watakatiliwa mbali hivi karibuni. Boshua hii, Je! Kweli Mungu Anatujali?, inafasiria yale atakayofanya na jinsi tunavyoweza kufaidika nayo.” Tunaweza labda kufuatia mazungumzo kwa kutoa maelezo ya fungu 22, kwenye ukurasa 27.
3 Ikiwa tunatumia broshua “Lililo Kusudi la Uhai”, tunaweza kuanzisha mazungumzo kama ifuatavyo:
◼“Hakuna budi, karibu watu wote wanajiuliza juu ya uhai. Je! kusudi ni kuishi tu miaka 70 au 80 kisha kwenda katika kaburi? Au je! uhai una kusudi? Wewe unawaza nini? [Acha mtu ajibu.] Katika Zaburi 37:29, tunaona ni nini kusudi la Mungu la ajabu kuelekea mwanadamu na dunia.” Baada ya kusoma andiko, tuonyeshe picha ya ukurasa wa 31, na tufasirie ni aina gani ya uhai tutakuwa nayo katika Paradiso.
4 Tungeweza kufanya utanguluzi wa broshua “Tazama!” kwa kuonyesha picha yote ya jalada na kwa kuuliza:
◼“Kulingana nawe, ingeomba nini ili kugeuza dunia hivi? [Acha mtu atoe maelezo.] Juu ya picha hii, kila mtu ana nyumba na kazi nzuri. Amani inatawala, chakula kingi na dunia haichafuliwi. Ingawa bidii yazo nyingi, serikali za kibinadamu zinatambua kwamba haiwezikani kwazo kusimamisha ulimwengu unaofanana na huu. Hata hivyo, Biblia inatutolea uhakika wa kwamba Mungu ‘atafanya mambo yote kuwa mapya.’ [Kufungua broshua kwenye ukurasa 30, na kusoma Ufunuo 21:3, 4.] Broshua hii itakufundisha yale unapaswa kufanya ili kuishi katika ulimwengu mpya huu.” Ikiwa mtu anaonyesha kupendezwa, tufungue broshua kwenye ukurasa 3, na tuonyeshe namna tunavyoongoza funzo la Biblia.
5 Pamoja na broshua “Kuishi Milele Katika Furaha Duniani!”, tunaweza kutumia ufundi huu:
◼“Watu wengi wanafikiri kwamba watapaswa kwenda mbinguni ili kufurahia uhai wa milele, lakini tungesema nini juu ya kuishi milele duniani? [Acha mtu ajibu.] Biblia inatuhakikishia kwamba uhai wa milele unawezekana, na inatuambia jinsi ya kufikia kusudi hilo.” Kusoma Yohana 17:3. Kisha tuonyeshe msikilizaji picha namba 49, na tuulize: “Je! ungependa kuishi katika ulimwengu kama huu?” Tutolee broshua na tusikilizane kwa ajili ya ziara ya kurudia.
6 Broshua zinazungumzia habari zinazovuma, zinajibu maulizo ambayo watu wanajiuliza na zinaleta faraja. Kwa kutumia kwa ufundi vyombo hivyo, tutasaidia watu wanyofu ‘kuja kwenye ujuzi sahihi wa kweli.’ — 1 Tim. 2:4, NW.