Mazungumzo Ya Kirafiki Yanayoweza Kugusa Moyo
1 Mazungumzo yanaweza kusemwa kuwa ni “kubadilishana mawazo”. Kuanzisha mazungumzo ya kirafiki juu ya habari fulani inayopendeza mwingine kunaweza kuvuta uangalifu wake na kutusaidia kugusa moyo wake na ujumbe wa Ufalme. Ujuzi wa siku nyingi umeonyesha kwamba ni jambo lenye matokeo zaidi kuanzisha pamoja na watu mazungumzo ya kirafiki na yenye starehe badala ya kuwatolea hotuba.
2 Jinsi ya Kuanzisha Mazungumzo ya Kirafiki: Kuwa mwenye uwezo wa kuzungumza na mtu haimaanishi kutoa kwa vyovyote mfululizo wenye kushangaza wa mawazo na maandiko. Hilo linamaanisha kwa kifupi tu kufanya kuwe na mazungumzo ya watu wawili. Kwa mfano, mazungumzo tunayofanya na jirani yetu katika uwanja hayako magumu lakini yenye starehe. Badala ya kufikiri kimbele sentensi tutakayosema, tunajibu papo hapo mawazo anayotoa. Ikiwa tunaonyesha kupendezwa kwa kwelikweli na yale anayosema, pengine atakuwa na mwelekeo wa kurudilia mazungumzo ya namna hiyo. Ingepaswa kuwa vivyo hivyo wakati tunapotoa ushuhuda.
3 Habari kama vile jeuri, matatizo ya vijana, maswala yanayopendeza watu wa mahali, hali ulimwenguni au hata wakati unaweza kutumiwa kuanzisha mazungumzo ya kirafiki. Vichwa vya habari vinavyogusa moja kwa moja maisha ya kila siku ya watu ni vyenye matokeo sana ili kuamsha kupendezwa kwao. Wakati mazungumzo yanapoendelea, tunaweza pole kwa pole kumwelekeza kwenye ujumbe wa Ufalme.
4 Kuwa na mazungumzo yenye starehe hakumaanishi kwamba kujitayarisha kokote si kwa lazima. Kujitayarisha ni kwa lazima. Hata hivyo, hakuna lazima ya kutayarisha muhtasari ulio mgumu au kujifunza habari kwa ufahamu, badala yake hatungeweza kuwa wepesi na wenye kusema kwa wakati wenye kufaa. (Ona 1 Wakorinto 9:20-23.) Namna bora ya kujitayarisha ni kuchagua kichwa kimoja cha habari au viwili vya Biblia, katika kusudi la kugeuza mazungumzo yaelekee habari hizo. Kuchunguza upya habari za kitabu Kutoa Sababu kutakuwa msaada mkubwa kwetu.
5 Sifa za Lazima kwa Ajili ya Mazungumzo ya Kirafiki: Wakati tunapozungumza na mtu, tungepaswa kuwa wenye shauku na wanyofu. Kicheko na hali yenye furaha vitatusaidia kuonyesha sifa hizo. Tunapeleka ujumbe bora zaidi kuliko ulimwenguni; hakuna kitu kingine kinachovutia tena watu wanyofu. Ikiwa wanahisi kwamba kupendezwa tunakowaonyesha kunachochewa na nia ya kweli ya kuwatangazia habari njema, labda watachochewa kusikiliza.—2 Kor. 2:17.
6 Mazungumzo yangepaswa kuwa ni wakati wa furaha. Kwa hiyo, tuwe wema na wenye kujaa busara tunapotolea ujumbe wa Ufalme. (Gal. 5:22; Kol. 4:6). Tujikaze kumwachia msikilizaji wetu maoni mazuri. Katika njia hiyo, hata ikiwa hatufikii mara ya kwanza kugusa moyo wake, mtu huyo labda atakuwa msikivu wakati ujao Shahidi mwingine atakapoanzisha mazungumzo pamoja naye.
7 Si kwa kujua habari fulani ngumu toka mwanzo mpaka mwisho ndiko kutatuwezesha kuanzisha mazungumzo ya kirafiki. Ni kwa kuchochea tu kupendezwa kwa mtu kwa kuzungumzia habari inayomhusu. Baada ya kujitayarisha, tutakuwa wenye uwezo wa kuanzisha mazungumzo ya kirafiki na watu wote. Tujikaze kugusa mioyo ya watu tunaokutana nao kwa kuwatangazia habari bora zaidi ambayo wanastahili kusikia: baraka zisizo na mwisho za Ufalme. — 2 Pt. 3:13.