Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 1/98 uku. 1
  • Tuseme Juu Ya Yehova Kila Siku

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Tuseme Juu Ya Yehova Kila Siku
  • Huduma Yetu ya Ufalme—1998
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Utumie Muzuri Uwezo wa Ulimi Wako
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Tumsifu Yehova Kila Siku
    Huduma Yetu ya Ufalme—2009
  • Tunamupenda Sana Yehova, Baba Yetu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Furahia Fasi Yako mu Familia ya Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2021
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—1998
km 1/98 uku. 1

Tuseme Juu Ya Yehova Kila Siku

1 Watu wanapenda kusema yale waliyo nayo ya lazima moyoni, kwa maana katika wingi wa moyo kinywa husema. (Lk. 6:45b) Na sisi, ni nini tuliyo nayo ya lazima moyoni? Mtunga-zaburi aliandika: “Na ulimi wangu utasema juu ya haki yako, na juu ya sifa yako muchana kutwa.” (Zab. 35:28) Alihisi shukrani nyingi kuelekea Yehova na aliliona kuwa pendeleo hakika kuweza kusema juu ya Mungu na kusema sifa yake katika kila hali. Kwa kuwa alimjua Yehova kikamili, mtunga-zaburi alikuwa na sababu nyingi za kushangilia. (Zab. 35:9) Tunawezaje kuiga kielelezo chake kizuri?

2 Tuseme Juu ya Yehova Nyumbani: Yehova angepaswa kuwa kichwa cha mazungumzo ya kila siku katika familia. Wazazi walio na upendo wenye nguvu kwa Yehova watasema kama iwapasavyo juu yake katika utendaji wao wote. (Kumb. 6:5-7) Hivyo, watoto watatambua kwamba baba yao na mama yao wanaishi kwa imani na wanapenda sana sheria ya Mungu. Watoto wataona hivyo funzo la Biblia katika familia kuwa wonyesho wa kweli wa ushikamanifu ambao wazazi wao wanatoa kwa Mungu.​—2 Petro 3:11.

3 Tuseme Juu ya Yehova na Ndugu Zetu: Utendaji wa kitheokrasi wa juma unatutolea nafasi nyingi za kulisha kiroho akili na moyo wetu. Sikuzote kuna mambo mazuri ambayo tunaweza kuzungumzia. (Lk. 6:45a) Je! umeona katika funzo lako la kibinafsi au katika usomaji wako wa Biblia wa kila juma wazo fulani ambalo uliweza kufurahia kipekee? Lizungumzie na ndugu na dada zako, na utawasaidia kuhisi wao pia upendo wenye kina kirefu tena zaidi kwa Yehova.​—Zab. 35:18; Ebr. 10:24.

4 Tuseme Juu ya Yehova Kando Kando Yetu: Katika mazungumzo yetu ya kila siku na majirani zetu, iwe kazini, shuleni au na washiriki wa familia yetu wasioshiriki imani yetu, ingepaswa kuwa wazi kwamba jambo la kwanza katika maisha yetu ni kutoa ushahidi juu ya Yehova. Badala ya kuiga usemi wa ovyo ovyo na wenye matusi wa ulimwengu, tungepaswa kumtukuza Yehova kupitia namna yetu ya kusema. Kila siku, katika hali zote, tuseme juu ya habari njema tuliokabiziwa kuhubiri.​—Mdo 5:42; Kol. 4:6.

5 Tukiwa waabudu wa kweli wa Yehova, tutachukua nafasi zote zinazojitokeza kila siku ili kusema juu ya Mungu wetu asiye na kifani, Yehova.​—Zab. 106:47.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine