Kutokuwako Kwako Hakukosi Kutambuliwa!
1 Mara kwa mara, inafikia labda kwamba tunakosa mkutano mmoja au mikutano mingi ya kutaniko kwa kusema: “Hilo halibadili jambo; hawatatambua hata kwamba sikukuwako.” Hilo si kweli! Kama viungo vya mwili wa nyama, tunatimiza sote daraka la maana katika maisha ya kutaniko. (1 Kor. 12:12) Kutokuwako kwetu kwenye mkutano wa kila juma kunaweza kudhuru hali njema ya kiroho ya wale wenye kuwako. Ikiwa wewe hauko, uwe hakika na jambo hili: kutokuwako kwako hakukosi kutambuliwa!
2 Daraka la Maana la Kila Mmoja: Paulo alingoja kwa hamu sana kukusanyika pamoja na ndugu zake. Anatoa sababu katika Warumi 1:11, 12: “Ili niweze kuwapa baadhi ya zawadi za kiroho, . . . kwamba kupate kuwa na badilishano la kitia-moyo miongoni mwenu, kwa kila mmoja kupitia imani ya mwingine, yenu na yangu.” Kwa njia iyo hiyo, kupitia maelezo yetu, vipindi vyetu, kupitia kuwako kwetu kwenyewe, tunajengana wamoja na wengine na kutiana moyo kudumu waaminifu.—1 Thes. 5:11.
3 Je! wewe haungoji kwa hamu sana kukutana tena na Wakristo wenzako kwenye mikutano ya kutaniko? Unasikiliza kwa uangalifu maelezo yao na unathamini namna wanavyoeleza imani yao. Zawadi zao za kiroho zinachangia kukujenga. Ikiwa baadhi yao wangekuwa wasiokuwako, ungehisi kwamba kunakosekana jambo fulani la maana. Ndugu zako na dada zako wanahisi vivyo hivyo wakati unapokuwa hauko.
4 Daraka la Maana Sana la Mikutano: Kuhusiana na umuhimu wa mikutano kwa ajili ya hali yetu ya kiroho, Mnara wa Mlinzi mmoja ulisema: “Katika ulimwengu wa sasa usio na adili na wenye kukumbwa wa mizozo mingi, kutaniko la kikristo ni kimbilio la kweli la kiroho . . . , mahali pa kupumzikia penye amani na upendo. Kwa sababu hiyo, shiriki kikawaida kwenye mikutano yote.” (w93-F 15/8 11) Kila siku, tunapambana na hali zinazotia hali yetu ya kiroho katika jaribu kali. Ikiwa hatujionyeshi wenye busara, kuna hatari ya sisi kumezwa na masumbuko yetu ya kibinafsi kwa kiasi cha kupoteza mambo ya kiroho, yaliyo ya maana zaidi. Sote tuna uhitaji wa wamoja na wengine ili kupata vitia-moyo vya lazima na kubaki wenye umoja na wenye bidii katika utumishi wa Mungu.—Ebr. 10:24, 25.
5 Ni jambo la maana sana tuhudhurie kwenye mikutano. Ugonjwa au tukio jingine lisilotazamiwa linaweza kutuzuia tusiwe kwenye mikutano, lakini wakati wenye kubaki, tuazimie sikuzote kuwa miongoni mwa umati wenye kukusanyika unaomtukuza Yehova!—Zab. 26:12.