Somo 1
Jinsi Unaweza Kuvumbua Kile Mungu Anataka
Ni habari gani ya lazima inayopatikana katika Biblia? (1)
Mutungaji wa Biblia ni nani? (2)
Kwa nini inakupasa ujifunze Biblia? (3)
1. Biblia ni zawadi yenye bei kutoka kwa Mungu. Ni kama barua kutoka kwa baba mwenye upendo anayotumia watoto wake. Inatuelezea kweli juu ya Mungu—Yeye ni nani na viwango vyake ni gani. Inatufasiria namna gani kushindana na matatizo, na namna gani kupata furaha ya kweli. Biblia pekee inatuelezea sisi yale tunapaswa kufanya ili tumupendeze Mungu.—Zaburi 1:1-3; Isaya 48:17, 18.
2. Biblia iliandikwa na watu tofauti karibu 40 katika kipindi cha miaka 1 600, kuanzia 1513 K.W.K. Inafanyizwa na vitabu vidogo 66. Wale walioandika Biblia walikuwa wenye kupuliziwa na Mungu. Waliandika mawazo yake, si mawazo yao. Kwa hiyo Mungu aliye mbinguni ndiye Mutungaji wa Biblia wala si binadamu yeyote hapa duniani.—2 Timoteo 3:16, 17; 2 Petro 1:20, 21.
3. Mungu alijihakikishia kwamba Biblia iweze kunakiliwa bila makosa na kulindwa. Biblia nyingi zimechapishwa kwenye mashini kuliko vitabu vingine. Si kila mutu atafurahia kukuona wewe unajifunza Biblia, lakini usiache jambo hilo likuzuie. Wakati wako ujao wa milele unategemea juu ya wewe kupata kumujua Mungu na kufanya mapenzi yake ijapokuwa upinzani wowote.—Matayo 5:10-12; Yoane 17:3.