Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • rq somo 1 uku. 3
  • Jinsi Unaweza Kuvumbua Kile Mungu Anataka

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Jinsi Unaweza Kuvumbua Kile Mungu Anataka
  • Mungu Anataka Nini Kwetu?
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Biblia Ni Neno ya Mungu
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Habari Njema Yenye Iko mu Biblia Inatoka Kabisa kwa Mungu?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
  • Kwa Nini Ujifunze Kutoka kwa Mungu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Biblia: Kitabu Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
Ona Habari Zaidi
Mungu Anataka Nini Kwetu?
rq somo 1 uku. 3

Somo 1

Jinsi Unaweza Kuvumbua Kile Mungu Anataka

Ni habari gani ya lazima inayopatikana katika Biblia? (1)

Mutungaji wa Biblia ni nani? (2)

Kwa nini inakupasa ujifunze Biblia? (3)

1. Biblia ni zawadi yenye bei kutoka kwa Mungu. Ni kama barua kutoka kwa baba mwenye upendo anayotumia watoto wake. Inatuelezea kweli juu ya Mungu​—⁠Yeye ni nani na viwango vyake ni gani. Inatufasiria namna gani kushindana na matatizo, na namna gani kupata furaha ya kweli. Biblia pekee inatuelezea sisi yale tunapaswa kufanya ili tumupendeze Mungu.​—⁠Zaburi 1:​1-3; Isaya 48:​17, 18.

2. Biblia iliandikwa na watu tofauti karibu 40 katika kipindi cha miaka 1 600, kuanzia 1513 K.W.K. Inafanyizwa na vitabu vidogo 66. Wale walioandika Biblia walikuwa wenye kupuliziwa na Mungu. Waliandika mawazo yake, si mawazo yao. Kwa hiyo Mungu aliye mbinguni ndiye Mutungaji wa Biblia wala si binadamu yeyote hapa duniani.​—⁠2 Timoteo 3:​16, 17; 2 Petro 1:​20, 21.

3. Mungu alijihakikishia kwamba Biblia iweze kunakiliwa bila makosa na kulindwa. Biblia nyingi zimechapishwa kwenye mashini kuliko vitabu vingine. Si kila mutu atafurahia kukuona wewe unajifunza Biblia, lakini usiache jambo hilo likuzuie. Wakati wako ujao wa milele unategemea juu ya wewe kupata kumujua Mungu na kufanya mapenzi yake ijapokuwa upinzani wowote.​—⁠Matayo 5:​10-12; Yoane 17:⁠3.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine