Somo 6
Ufalme wa Mungu Ni Nini?
Ufalme wa Mungu upo wapi? (1) Mufalme wa Ufalme huo ni nani? (2)
Je! kuna watu wengine wanaoshirikiana na Mufalme katika kutawala? Ikiwa ndiyo, wao ni wangapi? (3)
Nini inayoonyesha kwamba sisi tunaishi katika siku za mwisho? (4)
Ufalme wa Mungu utafanyia nini wanadamu katika wakati ujao? (5-7)
1. Alipokuwa duniani, Yesu aliwafundisha wafuasi wake kusali kwa ajili ya Ufalme wa Mungu. Ufalme ni serikali inayoongozwa na mufalme. Ufalme wa Mungu ni serikali ya aina ya pekee. Inasimamishwa mbinguni na itatawala dunia hii. Italitakasa, au kulifanya takatifu, jina la Mungu. Itasababisha mapenzi ya Mungu kufanyika duniani kama yanavyofanyika mbinguni.—Matayo 6:9, 10.
2. Mungu aliahidi kwamba Yesu angekuwa ndiye Mufalme wa Ufalme Wake. (Luka 1:30-33) Yesu alipokuwa duniani, alihakikisha kwamba angekuwa ndiye Mutawala mwema, mwenye haki na mukamilifu. Aliporudi mbinguni, yeye hakuwekwa moja kwa moja kwenye kiti cha ufalme ili awe Mufalme wa Ufalme wa Mungu. (Waebrania 10:12, 13) Katika 1914, Yehova alimupa Yesu mamulaka ambayo Yeye alikuwa amemuahidi. Tangu hapo, Yesu alianza kutawala mbinguni akiwa Mufalme aliyewekwa na Yehova.—Danieli 7:13, 14.
3. Yehova alichagua pia wanaume na wanawake fulani waaminifu kutoka duniani ili waende mbinguni. Wao watatawala pamoja na Yesu wakiwa wafalme, mahakimu (waamuzi), na makuhani juu ya binadamu. (Luka 22:28-30; Ufunuo 5:9, 10) Yesu aliwaita hawa watawala wenzake katika ufalme wake “kundi dogo.” Hesabu yao ni watu 144 000.—Luka 12:32; Ufunuo 14:1-3.
4. Mara tu kisha Yesu kuwa Mufalme, alitupa Shetani na malaika zake waovu chini inje ya mbingu mupaka kwenye ujirani wa dunia. Hiyo ndiyo sababu mambo yamezidi kuwa mabaya hapa duniani tokea 1914. (Ufunuo 12:9, 12) Vita mbalimbali, njaa, magonjwa ya kuambukiza haraka, kuongezeka kwa uvunjaji wa sheria—mambo haya yote ni sehemu ya ile “alama” inayoonyesha kwamba Yesu ni mwenye kutawala na kwamba mufumo huu umo katika siku zao za mwisho.—Matayo 24:3, 7, 8, 12; Luka 21:10, 11; 2 Timoteo 3:1-5.
5. Karibuni Yesu atahukumu watu, akiwagawanya kama vile muchungaji anavyogawanya kondoo na mbuzi. “Kondoo” ni wale wote watakaokuwa wamehakikisha kuwa raia zake washikamanifu. Wao watapata uhai udumuo milele duniani. “Mbuzi” ni wale wote watakaokuwa wameukataa Ufalme wa Mungu. (Matayo 25:31-34, 46) Katika wakati ujao ulio karibu, Yesu ataangamiza watu wote walio mufano wa mbuzi. (2 Watesalonika 1:6-9) Ikiwa unapenda kuwa mumoja wa “kondoo” wa Yesu, unapaswa hakika kusikiliza ujumbe wa Ufalme na kutenda kulingana na yale unayojifunza.—Matayo 24:14.
6. Leo hii dunia ni yenye kugawanyika katika inchi nyingi. Kila moja ina serikali yake. Mataifa hayo yanapigana mara nyingi. Lakini Ufalme wa Mungu utachukua nafasi ya serikali zote za kibinadamu. Utatawala ukiwa serikali pekee juu ya dunia yote. (Danieli 2:44) Ndipo hakutakuwa tena vita, uuaji, na jeuri. Watu wote wataishi pamoja katika amani na umoja.—Mika 4:3, 4.
7. Katika Utawala wa Yesu wa Miaka Elfu, binadamu walio waaminifu watakuwa wakamilifu, dunia yote itakuwa paradiso. Kufikia mwisho wa ile miaka elfu, Yesu atakuwa amefanya kila jambo Mungu alimuomba kufanya. Ndipo atarudisha Ufalme kwa Baba yake. (1 Wakorinto 15:24) Kwa nini usielezee marafiki wako au watu wale unaowapenda juu ya yale Ufalme wa Mungu utafanya?
[Picha katika ukurasa wa 13]
Chini ya utawala wa Yesu, hakutakuwa tena chuki au kuwazia mwingine vibaya