SEHEMU YA 6 • MATENDO 15:36–18:22
“Turudie Sasa Na Tutembelee Ndugu”
Waangalizi wa muzunguko wanafanyaka kazi gani ya maana mu kutaniko ya Kikristo? Wakati tunakubali kwa kupenda migao yenye tengenezo ya Yehova inatupatia, ile inakuwaka na baraka gani? Namna gani tunaweza kufikiri na watu kupitia Maandiko, na juu ya nini tunapaswa kujipatanisha na hali ya wasikilizaji wetu? Tutapata majibu ya ile maulizo na ya maulizo ingine wakati tunasindikiza mutume Paulo mu safari yake ya pili ya umisionere.