Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 12/15 uku. 2
  • ‘Tembea kwa Imani, Si kwa Kuona’

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • ‘Tembea kwa Imani, Si kwa Kuona’
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2015
  • Habari za Kufanana na Zile
  • ‘Utupatie Imani Zaidi’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Tutembee Kwa Imani
    Huduma Yetu ya Ufalme—1996
  • Onyesha Imani Yako Katika Ahadi za Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
  • Imani​—Sifa Yenye Inatutia Nguvu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Ona Habari Zaidi
Huduma Yetu ya Ufalme—2015
km 12/15 uku. 2

‘Tembea kwa Imani, Si kwa Kuona’

Siku fulani mbele ya Waroma kuzunguka muji wa Yerusalemu na kuuharibu, mutume Paulo aliandika kwamba, kwa sababu Wakristo ni maaskari wema wa Kristo, walipaswa kutazamia kupata magumu kuliko kutafuta maisha ya starehe. (2 Tim. 2:3, 4) Kwa kuwa ulimwengu huu muovu unakaribia kuharibiwa, tunahitaji imani yenye nguvu ili tuendelee kutia mambo ya kiroho pa nafasi ya kwanza. (2 Kor. 4:18; 5:7) Muangalie video ‘Tembea kwa Imani, Si kwa Kuona.’ (Mufungue jw.org, kwenye VICHAPO > VIDEO.) Mutambue namna gani kupenda sana vitu vya kimwili ilikuwa mutego wenye uliongoza Nahamu na Abitali kwenye kifo. Kisha, mupate majibu ya maulizo haya.

(1) Wakati wa mitume, ‘chukizo. . . lenye kusimama katika mahali patakatifu’ lilikuwa nini, na Wakristo wenye kuishi katika muji wa Yerusalemu walipaswa kufanya jambo gani la maana? (Mat. 24:15, 16) (2) Sababu gani iliomba kuwa na imani ili kuondoka katika muji? (3) Iliomba kufanya nini ili kuondoka haraka katika muji? (4) Sababu gani Nahamu na Abitali walikawia kuondoka? (Mat. 24:17, 18) (5) Imani ya Raheli (Rachel) ilijaribiwa tena namna gani wakati wa kuondoka katika muji wa Yerusalemu? (Mat. 10:34-37; Mk. 10:29, 30) (6) Namna gani Ethani ni mufano muzuri wa imani na wa kumutumainia Yehova? (7) Wakristo walipata magumu gani katika muji wa Pela? (8) Namna gani imani ya Nahamu na Abitali ilianza kupunguka polepole? (9) Namna gani Yehova alihangaikia Wakristo katika muji wa Pela? (Mat. 6:33; 1 Tim. 6:6-8) (10) Namna gani tunaweza kuiga imani ya Abrahamu na Sara katika siku hizi za mwisho? (Ebr. 11:8-10) (11) Namna gani Nahamu na Abitali walifikia kujidanganya ili kurudia Yerusalemu, na sababu gani maamuzi yao hayakukuwa mazuri? (Lu. 21:21) (12) Kwa kweli, maisha ilikuwa namna gani katika Yerusalemu wakati Nahamu na Abitali walirudi huko? (13) Sababu gani tunapaswa kutia nguvu imani yetu leo, mbele mwisho wa ulimwengu huu ufike?—Lu. 17:31, 32; 21:34-36.

Kutembea kwa imani kunamaanisha (1) kutegemea mwongozo wa Mungu, (2) kuacha Mungu aongoze hatua zetu, na (3) kuona mambo ya kiroho kuwa ya maana sana. Kwa hiyo, tuendelee kutembea kwa imani, na kuwa hakika kwamba “ulimwengu unapitilia mbali na pia tamaa yake, lakini yeye anayefanya mapenzi ya Mungu anadumu milele.”—1 Yoh. 2:17..

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine