Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lv sura 3 uku. 25-35
  • Penda Watu Ambao Mungu Anapenda

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Penda Watu Ambao Mungu Anapenda
  • Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • WATU AMBAO MUNGU ANAPENDA
  • MIFANO YA BIBLIA INAYOTUFUNDISHA
  • NAMNA YA KUCHAGUA MARAFIKI
  • WAKATI MATATIZO YANATOKEA
  • WAKATI INAOMBA KUKATA URAFIKI
  • Chagua Marafiki Wenye Kumupenda Mungu
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Tunawezaje Kuchagua Marafiki Wazuri?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Yonatani Alikuwa Hodari na Mushikamanifu
    Mambo yenye unaweza kujifunza katika Biblia
  • Ubakie Muaminifu kwa Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
lv sura 3 uku. 25-35
Marafiki wenye kukomaa kiroho wanajifurahisha pamoja

SURA YA 3

Penda Watu Ambao Mungu Anapenda

“Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima.”—METHALI 13:20.

1-3. (a) Biblia inaonyesha ukweli gani usioweza kupingwa? (b) Tunaweza kufanya nini ili kupata marafiki ambao watatusaidia kufanya mambo mazuri?

KATIKA njia fulani, wanadamu wanaweza kufananishwa na mukate. Ukiingiza mukate katika maji, mukate huo utafyonza sehemu ya maji hayo. Ni hivyo pia sisi wanadamu; tunaiga ao kufyonza mawazo, kanuni, na tabia za watu tunaofanya nao urafiki, hata bila kujua.

2 Biblia inaonyesha ukweli huo usioweza kupingwa wakati inasema hivi: “Anayetembea na watu wenye hekima atakuwa na hekima, lakini anayeshirikiana na wajinga atapatwa na mabaya.” (Methali 13:20) Methali hii haizungumuzie kukutana na mutu mara chache tu. Maneno ‘kutembea na’ yanaonyesha kuwa rafiki wa sana wa mutu fulani.a Kitabu kimoja kinachofasiria maneno ya Biblia kinasema hivi juu ya andiko hilo: “Kutembea na mutu kunaonyesha kama unamupenda mutu huyo na unashikamana naye.” Kwa kawaida, tunawaiga watu tunaowapenda, sivyo? Kwa kweli, kwa kuwa tunashikamana sana na watu kwa sababu tunawapenda, watu hao wanaweza kutuchochea tutende mambo mazuri ao mabaya.

3 Ili kubaki katika upendo wa Mungu, inafaa tutafute marafiki ambao watatusaidia kufanya mambo mazuri. Tunaweza kufanya nini ili kupata marafiki kama hao? Kwa kifupi, tunaweza kuwapata kwa kupenda watu ambao Mungu anapenda, ni kusema, kwa kufanya urafiki na marafiki wa Mungu. Wazia kidogo: kunaweza kuwa marafiki wazuri zaidi kuliko marafiki wa Yehova ambao wana tabia zinazomupendeza? Tuone basi ni watu wa namna gani ndio Mungu anapenda. Tukiwajua vizuri watu ambao Yehova anapenda, haitakuwa vigumu kwetu kuchagua marafiki wazuri.

WATU AMBAO MUNGU ANAPENDA

4. Sababu gani Yehova ana haki ya kuchagua watu wanaostahili kuwa marafiki wake, na sababu gani alimuita Abrahamu “rafiki yangu”?

4 Yehova hachague marafiki wake ovyoovyo. Kwa kuwa Yeye ni Bwana, Mutawala wa ulimwengu wote, ana haki ya kufanya hivyo, na kwa hiyo, kuwa marafiki wake ni pendeleo kubwa zaidi. Basi, Yeye anachagua watu wa namna gani kuwa marafiki wake? Yehova anakaribia watu wanaomutegemea na kumuamini kabisa. Tuone mufano wa Abrahamu, mutu wa zamani ambaye anajulikana sana kwa sababu ya imani yake ya pekee. Kumuomba baba fulani atoe mutoto wake kuwa zabihu, hilo ni jaribu la imani linaloshinda majaribu yote.b Lakini, kwa kuwa Abrahamu alikuwa na imani kabisa alikuwa tayari kumutoa Isaka, mwana wake; aliamini kabisakabisa ‘kwamba Mungu alikuwa na uwezo wa kumufufua hata kutoka kwa wafu.’ (Waebrania 11:17-19) Kwa sababu Abrahamu alionyesha imani yenye nguvu na utii, Yehova alimupenda na akamuita “rafiki yangu.”—Isaya 41:8; Yakobo 2:21-23.

5. Yehova anawaona namna gani watu ambao wanamutii kwa uaminifu?

5 Tunapomutii Yehova kwa uaminifu, anaona hilo kuwa jambo la lazima kabisa. Anawapenda watu ambao katika maisha yao wanaonyesha kama uaminifu wao kwake ndilo jambo la lazima sana. (2 Samweli 22:26) Kama tulivyoona katika Sura ya 1, Yehova anawafurahia sana watu wanaomutii kwa sababu wanamupenda. Andiko la Methali 3:32 linasema hivi: “Urafiki Wake uko pamoja na watu wanyoofu [ao wenye kuaminika].” Wale wanaofanya kwa uaminifu mambo ambayo Yehova anataka, anawatolea mwaliko wenye upendo: wanaweza kuwa wageni katika “hema” yake, maana yake, wanaweza kumuabudu na kumukaribia katika sala wakati wowote.—Zaburi 15:1-5.

6. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunamupenda Yesu, na Yehova anajisikia namna gani kuhusu watu wanaoonyesha kama wanamupenda Mwana wake?

6 Yehova anawapenda watu wanaomupenda Yesu, Mwana wake muzaliwa-pekee. Yesu alisema hivi: ‘Ikiwa yeyote ananipenda, atalishika neno langu, na Baba yangu atamupenda, nasi hakika tutakuja kwake na kukaa pamoja naye.’ (Yohana 14:23) Namna gani tunaweza kuonyesha kama tunamupenda Yesu? Ni kwa kushika amri zake; kama vile amri ya kuhubiri habari njema na kufanya wanafunzi. (Mathayo 28:19, 20; Yohana 14:15, 21) Tunaonyesha tena kama tunamupenda Yesu wakati ‘tunafuata hatua zake kwa ukaribu,’ kwa kufanya yetu yote ili kuiga maneno na matendo yake hata ikiwa sisi ni wanadamu wasio wakamilifu. (1 Petro 2:21) Watu ambao wanajikaza kumuiga Kristo kwa sababu wanamupenda wanafurahisha moyo wa Yehova.

7. Sababu gani ni jambo la hekima kufanya urafiki na marafiki wa Yehova?

7 Yehova anataka marafiki wake waonyeshe sifa kama vile imani, uaminifu, utii, na upendo kwa Yesu na kanuni zake. Kwa hiyo, kila mumoja wetu anapaswa kujiuliza: ‘Marafiki wangu wana sifa na tabia kama hizo? Marafiki wangu ni marafiki wa Yehova pia?’ Ni jambo la hekima kufanya urafiki na marafiki wa Yehova. Ni hivyo, kwa sababu, watu walio na sifa kama za Mungu na wanaohubiri habari njema ya Ufalme kwa bidii, wanaweza kutusaidia tufanye mambo mazuri, kama vile kuishi kupatana na ahadi tuliofanya ya kumupendeza Mungu maisha yetu yote.—Soma kisanduku chenye kichwa “Rafiki wa Kweli Ni Nani?”.

RAFIKI WA KWELI NI NANI?

Marafiki wawili wazuri wanazungumuza

Kanuni: “Rafiki wa kweli anapenda nyakati zote, naye ni ndugu aliyezaliwa kwa ajili ya wakati wa taabu.”—Methali 17:17.

Ujiulize

  • Marafiki wangu ni marafiki wa Yehova na wa Yesu pia?—Yohana 15:14, 16; Yakobo 2:23.

  • Marafiki wangu wananisaidia kuwa na tabia nzuri?—1 Wakorintho 15:33.

  • Marafiki wangu wananipenda vya kutosha hivi kwamba wanaweza kunikaripia ikiwa ninafanya kosa?—Zaburi 141:5; Methali 27:6.

  • Maneno na matendo yangu yanaonyesha kama mimi ni rafiki wa namna gani?—Methali 12:18; 18:24; 1 Yohana 3:16-18.

MIFANO YA BIBLIA INAYOTUFUNDISHA

8. Ni nini kinachokuvutia katika urafiki wa (a) Naomi na Ruthu? (b) Wale vijana watatu Waebrania? (c) Mutume Paulo na Timotheo?

8 Biblia ina mifano mingi ya watu waliofaidika kwa sababu walichagua marafiki wazuri. Unaweza kusoma juu ya urafiki wa Naomi na Ruthu, urafiki wa wale vijana watatu Waebrania walioshikamana pamoja huko Babuloni, na ule wa mutume Paulo na Timotheo. (Ruthu 1:16; Danieli 3:17, 18; 1 Wakorintho 4:17; Wafilipi 2:20-22) Lakini, acha tuzungumuzie mufano mwengine muzuri sana: urafiki wa Daudi na Yonathani.

9, 10. Sababu gani Daudi na Yonathani walikuwa marafiki sana?

9 Biblia inasema kama kisha Daudi kumuua Goliathi, ‘nafsi ya Yonathani ikashikamana na nafsi ya Daudi, na Yonathani akaanza kumupenda kama nafsi yake mwenyewe.’ (1 Samweli 18:1) Hivyo, urafiki wa nguvu ukaanza kati yao, hata ikiwa hawakuwa na umri moja. Urafiki wao uliendelea mupaka wakati Yonathani alikufa katika vita.c (2 Samweli 1:26) Sababu gani walikuwa marafiki wenye kupendana sana?

10 Ikiwa Daudi na Yonathani walikuwa marafiki sana ni kwa sababu wote wawili walimupenda Mungu na walikuwa na tamaa yenye nguvu ya kuwa waaminifu kwake. Kila mumoja wao alikuwa na sifa ambazo zilimuvutia mwenzake. Bila shaka, Yonathani alipendezwa na uhodari na bidii ya kijana Daudi ambaye alitetea jina la Yehova bila woga. Naye Daudi alimuheshimu mwanaume huyo ambaye alimushinda miaka na ambaye aliunga mukono mipango ya Yehova kwa uaminifu na kutanguliza faida za Daudi. Ona kwa mufano yale yaliyotokea wakati Daudi aliishi kama mukimbizi katika jangwa ili kukimbia hasira ya Mufalme mubaya Sauli, baba ya Yonathani. Daudi alikuwa mwenye kuvunjika moyo sana, basi, ili Yonathani aonyeshe kama alikuwa kabisa mwaminifu kwa Daudi, aliamua ‘kuenda kwa Daudi ili autie nguvu mukono wake [wa Daudi] kuhusiana na Mungu.’ (1 Samweli 23:16) Wazia namna Daudi alivyojisikia wakati rafiki yake mupendwa alikuja kumutegemeza na kumutia moyo!d

11. Mufano wa Yonathani na Daudi unatufundisha nini juu ya urafiki?

11 Mufano wa Yonathani na Daudi unatufundisha nini? Tunajifunza kama jambo la maana zaidi ambalo linapaswa kuunganisha marafiki ni kufurahia sana mambo ya kiroho. Wakati marafiki wetu ni watu walio na imani kama yetu, mwenendo kama wetu, na tamaa kama yetu ya kubaki waaminifu kwa Mungu, tunaweza kutiana moyo na kujengana, Tunapobadilishana mawazo, tunapoonyeshana jinsi tunavyojisikia na tunapozungumuzia mambo tuliyokutana nayo. (Waroma 1:11, 12) Tunapata marafiki kama hao, wanaofurahia mambo ya kiroho, kati ya waabudu wenzetu. Je, hilo linamaanisha kama kila mutu anayekuja kwenye Jumba la Ufalme ni rafiki muzuri? Hapana.

NAMNA YA KUCHAGUA MARAFIKI

12, 13. (a) Sababu gani hata katika kutaniko tunapaswa kuchagua vizuri marafiki? (b) Ni hali gani iliyotokea katika makutaniko ya wakati wa mitume, na hilo lilimusukuma mutume Paulo atoe maonyo gani mazito?

12 Hata katika kutaniko, ikiwa tunapenda kuwa na marafiki watakaotusaidia kuendelea kiroho, inafaa tuchague vizuri. Hilo halipaswe kutushangaza, sivyo? Jua kama Wakristo fulani katika kutaniko wanaweza kuchukua wakati mwingi ili kukomaa kiroho. Ni kama vile matunda fulani kwenye muti, yanaweza kuchukua wakati mwingi ili kuivya. Ndio sababu, katika kila kutaniko Wakristo wote hawakomae kiroho kwa wakati mumoja. (Waebrania 5:12–6:3) Ni vizuri tuonyeshe uvumilivu na upendo kwa wapya ao wazaifu, kwa sababu tunataka kuwasaidia wakomae kiroho.—Waroma 14:1; 15:1.

13 Mara kwa mara katika kutaniko, kunaweza kutokea hali fulani zinazotuomba tujiulize ikiwa marafiki wetu ni marafiki wazuri. Wakristo fulani wanaweza kuwa na mwenendo usiofaa. Wengine wanaweza kuwa na tabia ya kukasirika-kasirika ao kunungunika-nungunika. Hali kama hiyo ilitokea pia katika makutaniko ya wakati wa mitume. Ndugu wengi walikuwa waaminifu, lakini kulikuwa na wengine, mumoja mumoja, ambao hawakujiendesha vizuri. Kwa kuwa Wakristo fulani katika kutaniko la Korintho hawakufuata mafundisho fulani ya Kikristo, mutume Paulo alionya kutaniko hilo hivi: ‘Musipotoshwe. Mashirika mabaya yanaharibu tabia nzuri.’ (1 Wakorintho 15:12, 33) Mutume Paulo alimuonya Timotheo kama, hata kati ya Wakristo wenzake kunaweza kuwa wale ambao hawajiendeshe vizuri. Alimuambia Timotheo ajiepushe kabisa na watu hao, asifanye urafiki nao.​—2 Timotheo 2:20-22.

14. Juu ya marafiki, namna gani tunaweza kutumia kanuni iliyo katika maonyo ya mutume Paulo?

14 Namna gani tunaweza kutumia kanuni iliyo katika maonyo ya mutume Paulo? Tunapaswa kuepuka kufanya urafiki na mutu yeyote ambaye anaweza kutushawishi vibaya ao kutuharibisha, iwe katika kutaniko ao inje ya kutaniko. (2 Wathesalonike 3:6, 7, 14) Tunapaswa kulinda hali yetu ya kiroho. Usisahau, sisi ni kama mukate unaoingizwa katika maji, tunafyonza mawazo na tabia za marafiki wetu. Hatuwezi kuingiza mukate katika maji machafu na kutumaini ufyonze maji safi, vilevile hatuwezi kufanya urafiki na watu wabaya na kutumaini kuiga tabia nzuri.—1 Wakorintho 5:6.

Unaweza kupata marafiki wazuri kati ya waabudu wenzako

15. Unaweza kufanya nini ili upate katika kutaniko marafiki ambao wanahangaikia mambo ya kiroho kama wewe?

15 Ni jambo lenye kutuliza moyo kujua kama inawezekana kabisa kupata marafiki wengi wazuri kati ya waabudu wenzetu. (Zaburi 133:1) Unaweza kufanya nini ili upate katika kutaniko marafiki ambao wanahangaikia mambo ya kiroho? Ukiendelea kuwa na sifa na tabia zinazomupendeza Mungu, wengine walio na sifa kama hizo watavutiwa nawe. Tena, inaweza kuomba ukamate hatua ya kutafuta marafiki wapya. (Soma kisanduku chenye kichwa “Yale Waliyofanya ili Kupata Marafiki Wazuri,”) Tafuta marafiki walio na sifa ambazo ungetaka kuwa nazo. Fuata shauri la Biblia la ‘kupanuka,’ kwa kujikaza kuanzisha urafiki na waamini wenzako, bila ubaguzi wa rangi, wa inchi, ao wa kabila. (2 Wakorintho 6:13; 1 Petro 2:17) Usifanye urafiki na wale tu walio na umri wako. Kumbuka kama Yonathani alikuwa na miaka mingi kuliko Daudi. Ukifanya urafiki na watu wanaokushinda miaka, unaweza kufaidika na hekima yao na pia mambo waliyokwisha kuona katika maisha.

YALE WALIYOFANYA ILI KUPATA MARAFIKI WAZURI

Shivani anasema hivi: “Hapo zamani ilikuwa vigumu kwangu kupata marafiki katika kutaniko. Lakini nilitambua kama kuhubiri kwa ukawaida kulinisaidia kuonyesha sifa kama vile kutokuvunjika moyo haraka, uvumilivu, na upendo wa kujitoa kwa ajili ya wengine. Kadiri ninavyoendelea kuonyesha sifa hizo, ninaona kama wengine wenye sifa kama hizo wanapendezwa nami, na sasa nina marafiki wazuri kabisa.”

Ryan naye anasema hivi: “Nilisali ili nipate marafiki katika kutaniko. Lakini kwa wakati murefu niliwaza kama sala zangu hazikujibiwa. Kisha nikatambua kama sikuwa nafanya jambo lolote ili kupata marafiki. Lakini tangu nilipoanza kutenda kupatana na sala zangu, nimetambua kama Yehova amenijibu.”

WAKATI MATATIZO YANATOKEA

16, 17. Ndugu ao dada fulani akitukwaza, sababu gani hatupaswe kukimbia kutaniko?

16 Matatizo yanaweza kutokea mara kwa mara katika kutaniko kwa sababu watu wanatofautiana na wamekomalia katika hali tofauti. Ndugu ao dada fulani anaweza kutukwaza kwa kusema ao kufanya jambo fulani. (Methali 12:18) Wakati mwengine, matatizo yanatokea kwa sababu watu hawaelewane, ao wana mawazo tofauti na wengine. Je, matatizo hayo yatatukwaza na kutufanya tuache kukusanyika na kutaniko? Hatutafanya hivyo ikiwa tunamupenda kabisa Yehova na watu ambao anapenda.

17 Kwa kuwa Yehova ni Muumbaji wetu na anatupatia mambo ya lazima, inafaa tumupende na tujitoe kabisa kwake. (Ufunuo 4:11) Inafaa pia tuunge kutaniko mukono kwa uaminifu, kwa sababu Yehova anapendezwa kulitumia. (Waebrania 13:17) Kwa hiyo, ndugu ao dada fulani akituchukiza ao kutukwaza, hatutakimbia kutaniko ili kuonyesha kama tumekasirika. Hatuwezi kufanya hivyo kwa sababu si Yehova aliyetukwaza. Kwa kuwa tunamupenda kabisa Yehova, hatuwezi kumukataa yeye na kuwaacha watu wake!​—Zaburi 119:165.

18. (a) Tunaweza kufanya nini ili kutaniko liendelee kuwa na amani? (b) Kusamehe wakati tuna sababu nzuri ya kufanya hivyo, kutatuletea faida gani?

18 Ikiwa tunapenda kabisa ndugu na dada zetu, tutafanya nguvu ili kuwe amani katika kutaniko. Yehova haombe wale anaowapenda wawe wakamilifu, basi kwa nini sisi tufanye hivyo? Kwa hiyo, upendo utatusukuma tusiangalie makosa madogo-madogo ya wengine, na tunapaswa kukumbuka kama sisi wote ni watu wasio wakamilifu na tunafanya makosa. (Methali 17:9; 1 Petro 4:8) Upendo unatusaidia tuendelee “kusameheana kwa hiari [ao kwa kupenda].” (Wakolosai 3:13) Si vyepesi kufuata shauri hilo kila wakati. Lakini tukiwa na mawazo yasiyofaa kuhusu ndugu na dada zetu, hilo linaweza kutufanya tuwe na kinyongo, na labda tunaweza kuwaza kama kumukasirikia mutu aliyetukosea ndio njia ya kumuazibu. Lakini tujue kama tukiendelea kuwa na kinyongo, tunajitesa sisi wenyewe. Kusamehe wakati tuna sababu nzuri ya kufanya hivyo kutatuletea faida nyingi. (Luka 17:3, 4) Tutapata amani ya moyo na ya akili, tutaendeleza amani katika kutaniko, na zaidi ya hayo yote, tutapata faida kubwa zaidi ya kulinda urafiki wetu pamoja na Yehova.—Mathayo 6:14, 15; Waroma 14:19.

WAKATI INAOMBA KUKATA URAFIKI

19. Wakati gani tunapaswa kukata urafiki wetu na mutu aliyekuwa ndugu ao dada katika kutaniko?

19 Wakati fulani, itatuomba tukate urafiki wetu na mutu aliyekuwa ndugu ao dada katika kutaniko. Ikiwa anavunja sheria ya Mungu na anakosa kutubu, atatengwa na kutaniko, ao ikiwa anakana imani kwa kufundisha mambo ya uongo ao kwa kujitenga mwenyewe na kutaniko. Neno la Mungu linatuambia waziwazi ‘tuache kuchangamana katika ushirika’ na watu kama hao.e (1 Wakorintho 5:11-13; 2 Yohana 9-11) Inaweza kuwa vigumu kabisa kuepuka mutu ambaye alikuwa rafiki ao ambaye ni mutu wa jamaa. Je, tutatii kabisa agizo hilo na kuonyesha kama tunaona uaminifu wetu kwa Yehova na kwa sheria zake za haki kuwa jambo la lazima zaidi? Kumbuka, tunapomutii Yehova kwa uaminifu anaona hilo kuwa jambo la maana sana.

20, 21. (a) Sababu gani mupango wa kumutenga mutu na kutaniko ni mupango wa upendo? (b) Sababu gani tunapaswa kuchagua marafiki wetu kwa hekima?

20 Mupango wa kumutenga mutu na kutaniko ni mupango wa upendo kutoka kwa Yehova. Sababu gani? Kumuondoa mufanya-zambi asiyetubu katika kutaniko kunaonyesha kama tunamupenda Yehova, tunapenda jina lake takatifu na kanuni zake. (1 Petro 1:15, 16) Mupango huo unalinda kutaniko. Wakristo waaminifu wanalindwa na uvutano mubaya wa watu wanaofanya zambi kimakusudi na wanaweza kuendelea na ibada yao wakijua kama kutaniko ni mahali pa usalama katika dunia hii mbaya. (1 Wakorintho 5:7; Waebrania 12:15, 16) Kumuadibisha hivyo yule aliyefanya makosa ni alama ya upendo. Labda jambo hilo linaweza kumuamusha atambue makosa yake na achukue hatua zinazoombwa ili kumurudilia Yehova.—Waebrania 12:11.

21 Ni wazi kabisa, marafiki wetu wanaweza kutusaidia sana. Kwa hiyo basi, tunapaswa kuchagua marafiki wetu kwa hekima. Kwa kufanya urafiki na marafiki wa Yehova, ni kusema, kwa kuwapenda watu ambao Mungu anapenda, tutakuwa na marafiki wazuri sana. Mambo ambayo tutaiga kutoka kwao yatatusaidia ili tuwe na maisha yanayopatana na ahadi yetu kwa Yehova ya kumufurahisha katika maisha yetu.

a Neno la Kiebrania lililotafsiriwa ‘kushirikiana na’ linaweza pia kutafsiriwa ‘rafiki ya,’ ao ‘na urafiki pamoja na.’—Waamuzi 14:20; Methali 22:24, La Sainte Bible en Swahili de la R.D. Congo.

b Kwa kumuomba Abrahamu atoe mutoto wake kuwa zabihu, Yehova alionyesha mbele ya wakati namna angetoa mwana wake muzaliwa-pekee kuwa zabihu ya ukombozi. (Yohana 3:16) Lakini, Yehova alimuzuia Abrahamu kumuua Isaka, alitayarisha kondoo-dume ili itolewe zabihu pa nafasi ya Isaka.—Mwanzo 22:1, 2, 9-13.

c Daudi alikuwa kijana tu wakati alimuua Goliathi na alikuwa na miaka karibu 30 wakati Yonathani alikufa. (1 Samweli 17:33; 31:2; 2 Samweli 5:4) Yonathani alikufa akiwa na miaka 60 hivi, inaonekana alimushinda Daudi miaka 30 hivi.

d Kulingana na andiko la 1 Samweli 23:17, Yonathani alisema mambo matano ili kumutia Daudi moyo: (1) Alimuambia Daudi asiogope. (2) Alimuhakikishia Daudi kuwa Sauli hatamushinda. (3) Alimukumbusha Daudi kama atapokea ufalme, kama Mungu alivyoahidi. (4) Aliapa kama atakuwa mwaminifu kwa Daudi. (5) Alimuambia Daudi kama hata Sauli anajua kama yeye ni mwaminifu kwa Daudi.

e Ili kujua vizuri zaidi namna ya kuishi na watu waliotengwa ao waliojitenga na kutaniko, soma Nyongeza, “Namna ya Kuishi na Mutu Aliyetengwa na Kutaniko.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine