Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr17 Mwezi wa 9 uku. 1
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2017)
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 4-​10/09
  • TAREHE 11-​17/09
  • TAREHE 18-​24/09
  • TAREHE 25/09–1/10
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2017)
mwbr17 Mwezi wa 9 uku. 1

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 4-​10/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 42-​45

“Ibada Safi Inarudishwa!”

w99 1/3 uku. 8 fu. 3

‘Weka Moyoni Mwako’ Hekalu ya Mungu!

Maono hayo yenye mambo mengi yenye kuchukua sura kenda za kitabu cha Ezekieli, iliwapatia Wayahudi wenye walihamishwa ahadi yenye kutia imani nguvu. Ibada safi ingerudishwa! Tangu wakati huo, hata mupaka siku zetu, maono hayo imetia moyo watu wenye kumupenda Yehova. Namna gani? Tuchunguze ili tuone kama maono hayo ya unabii wa Ezekieli ilikuwa na maana gani kwa Waisraeli wenye walihamishwa. Maono hayo iko na sehemu ine kubwa: hekalu, ukuhani, mukubwa, na inchi.

it-2 uku. 1052 fu. 8

Hekalu

Hekalu ya maono ya Ezekieli. Mwaka wa 593 M.K.Y., katika mwaka wa 14 kisha kuharibiwa kwa Yerusalemu na hekalu ya Sulemani yenye ilikuwa huko, nabii-kuhani Ezekieli alibebwa katika maono juu ya mulima murefu na akaona hekalu kubwa ya Yehova (Eze 40:1, 2). Ili kuwanyenyekeza Wayahudi wenye walihamishwa, na kuwachochea watubu, na kuwatia moyo waaminifu, Ezekieli alipewa agizo la kuelezea “nyumba ya Israeli” mambo yote yenye aliona (Eze 40:4 ; 43:10, 11). Maono inafasiria kwa uangalifu sana vipimo. Vipimo vyenye vinatumiwa ni “utete” (utete murefu ulikuwa wa metre 3 na centimetre 11) na “mikono” (mukono murefu ulikuwa wa centimetre 51,8) (Eze 40:5). Kumutolea Ezekieli vipimo hivyo kwa uangalifu, kulifanya watu fulani wafikiri kama hekalu yenye Zorobabeli angejenga kisha kurudishwa kwa Wayahudi katika inchi yao, ingekuwa na vipimo hivyo hivyo. Lakini, hakuna jambo lenye kuhakikisha wazo hilo.

w99 1/3 uku. 10 fu. 10

‘Weka Moyoni Mwako’ Hekalu ya Mungu!

Ni wazi kama mambo hayo yote iliwatia moyo Wayahudi hao wenye walihamishwa. Walihakikishia kila familia kama ingepata uriti katika inchi. (Linganisha na Mika 4:4.) Ibada safi ingechukuwa nafasi ya kwanza. Na ona kwamba katika maono ya Ezekieli, mukubwa huyo, sawa na makuhani, angeishi katika sehemu ya inchi yenye watu walitoa. (Ezekieli 45:16) Kwa hiyo, katika inchi yenye ilijengwa tena, watu walipaswa kuleta muchango wao kwa kazi ya wale wenye Yehova alichagua ili waongoze, kwa kuwaunga mukono na kukubali muongozo wao. Katika mambo yote, inchi hiyo ilikuwa mufano muzuri wa utaratibu, ushirikiano, na usalama.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-2 uku. 412 fu. 8

Jina

Israeli ilikuwa taifa lenye kubeba jina la Mungu. Kwa hiyo, kwa kukataa kufuata kanuni Zake za haki, taifa hilo lilichafua jina hilo takatifu la Mungu (Eze 43:8 ; Amo 2:7). Kwa sababu kukosa uaminifu kwa Waisraeli kulimuchochea Mungu awapatie malipizi, hilo lilitolea mataifa ingine nafasi ya kusema mubaya jina la Mungu (linganisha na Zab 74:10, 18 ; Isa 52:5). Kwa sababu hawakukubali kama malipizi hayo ilitoka kwa Yehova, mataifa hayo ilisema kama Waisraeli wanateseka kwa sababu Mungu wao Yehova anashindwa kuwalinda. Ili jina lake lisichafuliwe na mawazo kama hayo, Yehova alitenda kwa kurudisha katika inchi yao Waisraeli wenye walibakia.​—Eze 36:22-​24.

it-2 uku. 87 fu. 2

Haki

Kwa hiyo, Yehova ana haki ya kuomba watu wenye wanataka awakubali wajue kanuni zake za haki na wazifuate. (Isa 1:​17, 18; 10:​1, 2; Yer 7:​5-7; 21:12; 22:​3, 4; Eze 45:​9, 10; Amo 5:​15; Mika 3:​9-​12; 6:8; Zek 7:​9-​12)

TAREHE 11-​17/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | EZEKIELI 46-​48

“Baraka Zenye Waisraeli Wangepata Kisha Kurudishwa Katika Inchi yao”

w99 1/3 uku. 10 fu. 11-​12

‘Weka Moyoni Mwako’ Hekalu ya Mungu!

Yehova angebariki inchi yao? Unabii huo unajibu ulizo hili kwa kueleza mambo kwa njia yenye kuchangamusha moyo. Muto mudogo unateremuka kutoka kwenye hekalu na kadiri unaendelea kuteremuka, unaendelea pia kupanuka, mupaka unakuwa muto mukubwa wakati unaingia katika Bahari ya Chumvi. Huko, muto huo unapatia uzima maji yenye haina uzima, na biashara ya kuloba samaki inaendelea sana kwenye eneo moja la pembeni ya bahari. Pembeni-pembeni ya muto kuko miti mingi yenye kuzaa matunda mwaka muzima, na inatoa chakula na kuponyesha watu.​—Ezekieli 47:​1-​12.

12Kwa Wayahudi hao wenye walikuwa wamehamishwa, ahadi hii ilihakikisha mambo kwa kurudilia unabii wenye walikuwa wametolewa mbele juu ya kurudia kwao, jambo lenye walingojea sana. Zaidi ya mara moja, manabii wa Yehova waliongozwa na roho ili kuzungumuzia wakati Israeli ingejengwa tena na kusema kama ingekuwa kama paradiso. Kichwa chenye kilirudiliwa sana kilionyesha maeneo yenye haikuwa na watu inakuwa tena na uzima. (Isaya 35:1, 6, 7; 51:3; Ezekieli 36:35; 37:1-14) Kwa hiyo, watu wangengojea kwamba baraka za Yehova zenye kuleta uzima zingeteremuka kama muto kutoka kwenye hekalu yenye ilirudishwa. Kwa hiyo, taifa lenye lilikuwa limekufa kiroho lingeishi tena. Watu hao wenye walirudishwa wangebarikiwa kwa kupewa wanaume wa kiroho, wanaume wenye haki na wenye kuwa nguvu kama miti yenye kuwa pembeni-pembeni ya mito katika maono, wanaume wenye wangeongoza kazi ya kujenga tena inchi yenye iliharibiwa. Isaya pia alikuwa amezungumuzia “miti mikubwa ya uadilifu [haki]” yenye ‘wangejenga upya mahali palipokuwa pameharibiwa kwa muda murefu.’​—Isaya 61:​3, 4.

w99 1/3 uku. 10 fu. 10

‘Weka Moyoni Mwako’ Hekalu ya Mungu!

Ni wazi kama mambo hayo yote iliwatia moyo Wayahudi hao wenye walihamishwa. Walihakikishia kila familia kama ingepata uriti katika inchi. (Linganisha na Mika 4:4.) Ibada safi ingechukuwa nafasi ya kwanza. Na ona kwamba katika maono ya Ezekieli mukubwa huyo, sawa na makuhani, angeishi katika sehemu ya inchi yenye watu walitoa. (Ezekieli 45:16) Kwa hiyo, katika inchi yenye ilijengwa tena, watu walipaswa kuleta muchango wao kwa kazi ya wale wenye Yehova alichagua ili waongoze, kwa kuwaunga mukono na kukubali muongozo wao. Katika mambo yote, inchi hiyo ilikuwa mufano muzuri wa utaratibu, ushirikiano, na usalama.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w99 1/3 uku. 11 fu. 14

‘Weka Moyoni Mwako’ Hekalu ya Mungu!

Matukio hayo ndiyo ilikuwa utimizo moja tu wa maono ya Ezekieli? Hapana; jambo fulani kubwa zaidi linaonyeshwa. Kwanza, hekalu yenye Ezekieli aliona kwa kweli haingewezekana ijengwe namna ilikuwa imeelezwa. Ni kweli kwamba, Wayahudi walichukua maono hayo kwa uzito na wakafanya hata mambo fulani namna ilikuwa inesemwa katika maono ya Ezekieli. Hata hivyo, hekalu hiyo yenye aliona katika maono ilikuwa kubwa sana na hivyo haingewezekana ijengwe na kuenea juu ya Mulima Moria, mahali kwenye hekalu la kwanza lilikuwa. Tena, hekalu yenye Ezekieli aliona haikuwa ndani ya muji, ilikuwa mahali fulani mbali katika eneo la mashamba; lakini hekalu ya pili ilijengwa mahali palikuwa hekalu ya kwanza, ndani ya muji wa Yerusalemu. (Ezra 1:1, 2) Na tena, hakuna muto wa kweli wenye ulitokea ndani ya hekalu ya Yerusalemu. Kwa hiyo, Israeli la zamani liliona tu sehemu kidogo ya unabii wa Ezekieli unatimia. Hilo linamaanisha kama maono hayo yanapaswa kutimia katika maana kubwa zaidi kwa njia ya kiroho.

it-1 uku. 903 fu. 6

Mwana wa Binadamu

Katika Maandiko ya Kiebrania, maneno hayo yanapatikana sana katika kitabu cha Ezekieli, mahali Mungu anamuita nabii huyo “mwana wa binadamu” zaidi ya mara 90 (Eze 2:1, 3, 6, 8). Pengine, Yehova anatumia usemi huu ili kukazia kama nabii ni mutu wa udongo tu; kwa kufanya hivyo anaonyesha tofauti kati ya musemaji mwanadamu na Chanzo cha ujumbe huo, ni kusema, Mungu Aliye Juu Zaidi. Katika Danieli 8:17, maneno hayo-hayo yanatumiwa ili kutaja nabii Danieli.

TAREHE 18-​24/09

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | DANIELI 1-3

“Ushikamanifu kwa Yehova Unaleta Baraka”

w15 15/7 uku. 20 fu. 15-​16

Uendelee Kuwa Mwaminifu kwa Ufalme wa Mungu

Tunataka kumutumikia Yehova na zamiri safi; kwa hiyo, wakati fulani tunapaswa kuonyesha kwamba tuko tofauti kabisa na wafanyakazi wenzetu, wanafunzi wenzetu, majirani, ao watu wa jamaa yetu. (1 Pet. 2:​19) Yesu alisema kwamba watu watatuchukia kwa sababu tuko tofauti nao. Tukumbuke kwamba wengi kati ya wale wenye kutupinga hawajue jambo lolote juu ya Ufalme wa Mungu. Ndiyo maana hawaelewe sababu gani ni jambo la lazima tukuwe waaminifu kwa Ufalme kuliko kuwa waaminifu kwa serikali za wanadamu.

Ili kubaki waaminifu kwa Yehova, tunapaswa kumutii hata kama watu wanasema ao kututendea nini. (Dan. 3:​16-​18) Ni vigumu sana kuwa tofauti na watu wengine, zaidi sana kwa vijana. Wazazi, muwasaidie watoto wenu wakuwe na ujasiri kwenye masomo. Watoto wenu wanaweza kuogopa kukataa kusalimu bendera ao kukataa kufanya sikukuu zingine za inchi. Wakati wa Ibada ya Familia, munaweza kujifunza namna Yehova anaona mambo hayo. Muwafundishe namna wanaweza kueleza waziwazi na kwa heshima mambo yenye wanaamini. (Rom. 1:​16) Pia, ikiwa ni lazima, muwasaidie kwa kuzungumuza na walimu wao na kuwaelezea mambo yenye munaamini.

w13 15/1 uku. 10 fu. 13

Ukuwe Hodari Yehova Iko Pamoja na Weye!

Miaka 600 hivi mbele ya kuzaliwa kwa Yesu, watumishi wa Yehova watatu Waebrania walijionea waziwazi kwamba Mungu anabariki watu hodari na wenye imani. Mufalme Nebukadneza aliwakusanya wakubwa wa Babiloni na kuwaomba waabudu sanamu kubwa ya zahabu. Kama mutu angekataa kuabudu sanamu hiyo, wangemutupa katika tanuru ya moto. Waebrania hao watatu walimuambia Nebukadneza kwa heshima: ‘Mungu ambaye tunamutumikia anaweza kutuokoa. Yeye atatuokoa kutoka katika tanuru inayowaka moto na kutoka mukononi mwako, Ee mufalme. Lakini kama sivyo, ujue hivi, Ee mufalme, kwamba sisi hatuitumikie miungu yako, na sanamu ambayo umeisimamisha hatutaiabudu.’ (Dan. 3:16-18) Andiko la Danieli 3:19-30 linaonyesha waziwazi namna Waebrania hao watatu waliokolewa kwa njia ya muujiza. Hata kama hawatatutupa katika tanuru ya moto, tunapata majaribu mbalimbali na tunaweza kuwa hakika kama Mungu atatubariki kwa sababu tuko na imani na hatuna woga.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-2 uku. 267 fu. 10

Meshaki

Kuko sababu tatu zenye pengine ziliwachochea kuona kama chakula cha mufalme kingewatia “unajisi” ao kuwafanya wasikuwe safi: 1) Wababiloni walizoea kula wanyama wenye hawakuwa safi kulingana na Sheria ya Musa; 2) Hawakuangaikia kujua kama nyama zilichinjwa muzuri; pengine hata zengine hazikuchinjwa; 3) mara nyingi wapagani walitolea kwanza miungu yao wanyama na waliamini kama kula nyama hao ilikuwa sehemu ya ibada ya miungu hiyo.​—Dan 1:8; linganisha na 1Kor 10:18-​20, 28.

w12 15/6 uku. 17, kisanduku

“FALME HIZI ZOTE” NI FALME GANI?

Andiko la Danieli 2:44 linasema kama Ufalme wa Mungu “utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote.” Unabii huo unazungumuzia tu falme zote zenye kufananishwa na sehemu mbalimbali za sanamu yenye mufalme Nebukadneza alilota.

Tuseme nini juu ya serikali zingine zote za wanadamu? Kitabu cha Ufunuo kinazungumuzia pia wafalme na kinatoa maelezo zaidi. Kitabu hicho kinaonyesha kama “wafalme wa dunia nzima inayokaliwa” watakusanywa ili kupigana na Yehova katika ‘siku kubwa ya Mungu Mweza-Yote.’ (Ufu. 16:14; 19:19-21) Kwa hiyo, kwenye Har-Magedoni haiko tu zile serikali zenye kufananishwa na sehemu mbalimbali za sanamu ndiyo zitaharibiwa, lakini serikali zingine zote za wanadamu zitaharibiwa pia.

w01 15/10 uku. 6 fu. 4

Namna Ulimwengu Wenye Furaha Utatokea

Jibu iko katika andiko la Danieli 2:44: ‘Katika siku za wafalme hao [wenye kutawala wakati wa mwisho wa ulimwengu wa sasa,] Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaharibiwa kamwe. Na ufalme huo hautapewa watu wengine wowote; Utazivunja na kuzikomesha falme hizi zote [falme za wanadamu,] nao utasimama mupaka wakati usio na kipimo.’ Sababu gani itakuwa lazima Ufalme wa Mungu ‘uvunje’ utawala mbalimbali wa dunia? Kwa sababu utawala huo unaendelesha mawazo yenye Shetani ilianzisha katika Shamba la Edeni, ni kusema, mawazo ya kumuasi Mungu na kujiamulia mambo. Mawazo hayo haiwatolee wanadamu faida yoyote; wale wenye wanajaribu kuendelesha mawazo hayo watapambana na Muumbaji. (Zaburi 2:6-12; Ufunuo 16:14, 16) Kwa hiyo, tunapaswa kujiuliza hivi: ‘ Tunaunga mukono ao tunapinga utawala wa Mungu?’

TAREHE 25/09–1/10

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | DANIELI 4-6

“Unaendelea Kumutumikia Yehova?”

w10 15/11 uku. 6 fu. 16

Vijana, Muaache Neno la Mungu Liwaongoze

Sababu gani unapaswa kumutii Yehova hata wakati uko peke yako? Usisahau kama unaweza kuumiza ao kufurahisha moyo wa Yehova. (Mwa. 6:5, 6; Met. 27:11) Yehova anahangaikia sana matendo yako kwa sababu ‘anakujali.’ (1 Pet. 5:7) Anataka umusikilize ili upate faida. (Isa. 48:17, 18) Wakati watumishi fulani wa Yehova katika Israeli ya zamani walizarau mashauri yake, walimuhuzunisha. (Zab. 78:40, 41) Lakini, Yehova alimupenda sana nabii Danieli. Malaika alimuita mutu “mwenye kutamanika sana.” (Dan. 10:11) Sababu gani? Kwa sababu Danieli aliendelea kuwa mushikamanifu kwa Mungu, hapana mbele ya watu tu, lakini pia wakati alikuwa peke yake.​—Soma Danieli 6:​10.

w06 1/11 uku. 24 fu. 12

Unaona Mambo Matakatifu Vile Yehova Anayaona?

Haishangaze kwamba, mambo mengi juu ya maisha ya Wakristo watiwa-mafuta wa kutaniko na wakristo wengine inaonwa kuwa matakatifu. Urafiki wetu na Yehova ni jambo takatifu. (1 Mambo ya Nyakati 28:9; Zaburi 36:7) Urafiki wetu na Mungu wetu Yehova ni wa maana sana kwetu; kwa hiyo, hataacha mutu ao jambo fulani liuharibu. (2 Mambo ya Nyakati 15:2; Yakobo 4:7, 8) Sala inatusaidia tuendelee kuwa na urafiki wa sana na Yehova. Sala ilikuwa takatifu sana kwa nabii Danieli; ndiyo sababu aliendelea na desturi yake ya kusali kwa Yehova hata wakati uzima wake ulikuwa katika hatari. (Danieli 6:7-11) “Sala za watakatifu,” ao Wakristo watiwa-mafuta, zinalinganishwa na uvumba wenye ulitumiwa katika ibada kwenye hekalu. (Ufunuo 5:8; 8:3, 4; Mambo ya Walawi 16:12, 13) Ufananisho huo unakazia kama sala ni takatifu. Ni pendeleo kubwa sana kuzungumuza na Mwenye Mamulaka Makubwa Zaidi! Haishangaze kwamba tunaona sala kuwa takatifu katika maisha yetu!

w03 15/9 uku. 15 fu. 2

Sababu Gani Tusali Bila Kuacha?

Yehova alimuona namna gani Danieli? Wakati Malaika Gabrieli alikuja kujibu sala ya Danieli, alimuita nabii huyo ‘mutu mwenye kutamanika (mwenye kupendwa) sana.’ (Danieli 9:20-23) Katika unabii wa Ezekieli, Yehova alimuita Danieli kuwa mwanaume mwenye haki. (Ezekieli 14:14, 20) Ni wazi kama, sala za Danieli zilimusaidia akomalishe urafiki wake na Mungu wake maisha yake yote, jambo lenye hata Dario alitambua.​—Danieli 6:​16.

w10 15/2 uku. 18 fu. 15

“Roho na Bibi-arusi Wanaendelea Kusema: ‘Njoo!’”

Kisha Danieli kubakia usiku muzima katika shimo la simba, mufalme mwenyewe alienda huko na kusema hivi kwa sauti: ‘Ee Danieli, mutumishi wa Mungu aliye hai, je, Mungu wako unayemutumikia daima amekuokoa kutoka kwa hao simba?’ Mara moja Danieli akajibu: ‘Ee mufalme, uishi mupaka wakati usio na kipimo. Mungu wangu mwenyewe alimutuma malaika wake na kufunga vinywa vya simba, nao hawakuniangamiza, kwa kuwa nimeonekana kuwa mutu asiye na hatia mbele zake; na pia mbele yako, Ee mufalme, mimi sijafanya tendo lolote lenye kuzuru.’ Yehova alimubariki Danieli kwa sababu hakuacha kumutumikia.​—Dan. 6:​19-​22.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w07 1/9 uku. 18 fu. 5

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Danieli

4:​10, 11, 20-​22​—Muti murefu sana katika ndoto ya Nebukadneza ulifananisha nini? Kwanza, muti huo ulifananisha Nebukadneza wakati alikuwa mutawala wa serikali ya ulimwengu. Hata hivyo, kwa sababu utawala huo ulienea na ‘kufika mupaka sehemu za mwisho za dunia,’ muti huo ulipaswa kufananisha kitu fulani kikubwa zaidi. Andiko la Danieli 4:17 linapatanisha ndoto hiyo na utawala wa “Aliye Juu Zaidi” juu ya wanadamu. Kwa hiyo, muti huo, ulifananisha pia utawala mukubwa wa Yehova wa ulimwengu wote, zaidi sana kuhusu dunia. Kwa hiyo, ndoto hiyo ya muti iko na utimizo wenye sehemu mbili, ni kusema, utawala wa Nebukadneza na utawala mukubwa wa Yehova.

w88 1/10 uku. 30 fu. 3-5

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Wakati walimuleta muebrania mwenye kuitwa Danieli mbele yake, mufalme alirudilia ahadi yake kwa kusema atamuvalisha nguo za rangi ya zambarau, na mukufu (collier) ya zahabu kwenye shingo, na atamufanya kuwa wa tatu katika ufalme. Nabii alimujibu hivi kwa heshima: ‘Zawadi zako na ziwe zako mwenyewe, na tuzo zako uwape wengine. Hata hivyo, mimi nitamusomea mufalme maandishi haya, nami nitamujulisha tafsiri yake.”​—Danieli 5:​17.

Kwa hiyo, haikuwa lazima kumununua Danieli ao kumutolea zawadi ili aseme maana ya maandishi. Mufalme angebakia na zawadi zake ao kuzitolea mutu mwengine. Kama Danieli alisema maana ya maandishi, haikuwa ili apate zawadi, lakini kwa sababu Yehova, Mungu wa kweli mwenye alikuwa karibu kuleta hukumu yake juu ya Babiloni, alimupatia nguvu.

Kulingana na Danieli 5:29, kisha Danieli kusoma na kusema maana ya maandishi namna alikuwa ameahidi, mufalme akasema wamupatie zawadi zenye aliahidi. Danieli hakujivalisha mwenyewe nguo na mukufu (collier). Mufalme Belshaza alitoa amri na kusema wamuvalishe vitu hivyo. Hilo halipingane na Danieli 5:17, kwenye nabii alionyesha wazi kama hakutafuta faida yake mwenyewe.

uku. 109 fu. 22

Maneno Ine Yenye Ilibadilisha Ulimwengu

Kitendawili kikafasiriwa. Majeshi ya Wamedi na Waperse ilikuwa karibu kuangusha muji wenye nguvu wa Babiloni. Hata kama hakufurahia habari hiyo ya huzuni, Belshaza alitimiza ahadi yake. Aliwaomba watumishi wake wamuvilishe Danieli nguo ya rangi ya zambarau, wamuvalishe mukufu (collier) ya zahabu kwenye shingo yake, na kumutangaza kuwa mutawala wa tatu katika ufalme. (Danieli 5:29) Danieli hakukataa wamutendee hivyo, alitambua kama walionyesha heshima yenye kustahili Yehova. Pengine Belshaza alitumainia kama kumuheshimu nabii Danieli kungemuchochea Yehova apunguze hukumu yake. Kama aliwaza hivyo, alikuwa amejidanganya kabisa.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine