Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 2-8/10
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | DANIELI 7-9
“Unabii wa Danieli Ulitabiri Kutokea kwa Masiya”
it-2-F uku. 998 fu. 1
Majuma Makumi Saba
Kumaliza makosa na zambi. Kuondolewa kwa Yesu, kufufuliwa, na kufika kwake mbingini kulisaidia ili ‘kukomesha makosa na kumaliza kabisa zambi, na kufanya upatanisho kwa ajili ya kosa.’ (Dan 9:24) Agano la Sheria lilifanya ionekane wazi kama Wayahudi walikuwa wafanya-zambi, liliwahukumu na liliwaletea laana ya wavunja-sheria. Lakini, mahali zambi “zilizidi”, namna ilionyeshwa wazi kupitia Sheria ya Musa, rehema na fazili za Mungu zilizidi hata zaidi kupitia Masiya wake. (Rom 5:20) Kupitia zabihu ya Masiya, makosa na zambi za wafanya-zambi wenye kutubu yanaweza kusamehewa na malipizi kuondelewa.
it-2-F uku. 996 fu. 6
Majuma Makumi Saba
Masiya Anatokea Kisha Majuma ‘Makumi Sita na Kenda.’ Majuma “makumi sita na mbili” yenye yalifuata (Dan 9:25), ni sehemu ya majuma 70; na kwa sababu yanatajwa ya pili, yalianzia mwisho wa “majuma saba”. Ndiyo sababu “tangu kutolewa kwa lile neno” ili kujenga tena Yerusalemu mupaka ‘Masiya Aliye Kiongozi,’ kulikuwa “majuma 7” kuongeza “majuma 62,” ni kusema, majuma 69 (miaka 483), kuanzia mwaka wa 455 M.K.Y. mupaka mwaka wa 29 K.K.Y. Namna tulisema hapo juu, majira ya baridi ya mwaka huo, ni kusema, mwaka wa 29 K.K.Y., Yesu alibatizwa ndani ya maji, alitiwa mafuta na roho takatifu, na alianza kazi yake ya ‘Masiya Aliye Kiongozi’.—Luka 3:1, 2, 21, 22.
it-2-F uku. 997 fu. 2
Majuma Makumi Saba
‘Anakatiliwa mbali’ katikati ya juma. Malaika Gabrieli alimuambia Danieli hivi: ‘Baada ya yale majuma 62 Masiya atakatiliwa mbali, bila kuwa na chochote kwa ajili yake.’ (Dan 9:26) Ilikuwa wakati fulani kisha mwisho wa ‘majuma 7 kuongeza majuma 62,’ ni kusema, miaka tatu na nusu hivi kisha, ndiyo Kristo alikatiliwa mbali wakati alikufa kwenye muti wa mateso, akatoa yote alikuwa nayo, ili kukomboa wanadamu. (Isa 53:8) Tunajua kama Yesu alipitisha nusu ya “juma” katika kazi ya kuhubiri. Siku moja, pengine mwaka wa 32 K.K.Y., alitoa mufano moja, na inaonekana katika mufano huo alifananisha taifa la Wayahudi na muti wa tini (linganisha na Mt 17:15-20; 21:18, 19, 43) wenye haukutoa matunda kwa miaka “tatu”. Mutunza mizabibu alimuambia mwenye shamba la mizabibu hivi: ‘Bwana, uuache mwaka huu pia, mupaka niupalilie na kuweka mbolea; na ndipo ukizaa matunda wakati ujao, basi ni vema; lakini ikiwa sivyo, utaukata.’ (Luka 13:6-9) Pengine alikuwa akizungumuzia wakati alikuwa anawahubiria watu hao wenye mioyo migumu, kazi yenye wakati huo ilikuwa imefanya miaka tatu hivi na ilikuwa inaingia katika mwaka wa ine.
it-2-F uku. 901 fu. 5
Majuma Makumi Saba
Pengine “nusu ya juma” ni kipindi chenye kuwa katikati ya miaka saba, ni kusema, kisha miaka tatu na nusu ya “juma” hilo la miaka. Kwa sababu “Juma” la 70 lilianza karibu wakati wa majira ya baridi katika mwaka wa 29 K.K.Y., wakati Yesu alibatizwa na kuwekwa mafuta kuwa Kristo, nusu ya juma (miaka tatu na nusu) iliisha wakati wa majira ya joto ya mwaka wa 33 K.K.Y. ni kusema, wakati wa Pasaka (tarehe 14 Nisani) wa mwaka huo. Inaonekana kama siku hiyo ilikuwa tarehe 1, Mwezi wa 4, Mwaka wa 33 K.K.Y. kulingana na kalendari yetu ya leo. Mutume Paulo anaeleza kama Yesu ‘alikuja ili kufanya mapenzi ya Mungu,’ yenye ilikuwa ‘kuondolea mbali lile la kwanza [zabihu na matoleo yenye Sheria iliomba watu kutoa] ili asimamishe lile la pili’. Alifanya hivyo wakati alitoa mwili wake kuwa zabihu.—Ebr 10:1-10.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w01 15/5 uku. 27
Maulizo ya Wasomaji Wetu
Kulingana na Danieli 9:24, “Patakatifu pa Patakatifu” palitiwa mafuta wakati gani?
Danieli 9:24-27 ni unabii juu ya kutokea kwa ‘Masiya Aliye Mukubwa,’ ni kusema, Kristo. Kwa hiyo, kutia mafuta “mahali patakatifu zaidi,” hakumaanishe kutia mafuta sehemu ya ndani ya Mahali Patakatifu zaidi pa hekalu la Yerusalemu. Lakini, maneno “Mahali Patakatifu Zaidi” yanamaanisha patakatifu pa mbingu pa Mungu, ni kusema, Patakatifu Zaidi Sana pa Mbinguni, katika hekalu kubwa la kiroho la Yehova.—Waebrania 8:1-5; 9:2-10, 23.
Hekalu la kiroho la Mungu lilianza kufanya kazi wakati gani? Fikiria jambo lenye lilitokea wakati Yesu alibatizwa katika mwaka wa 29. Tangu ubatizo wake Yesu alitimiza maneno ya Zaburi 40:6-8. Kisha, mutume Paulo alionyesha kama Yesu alikuwa amesali hivi kwa Mungu: ‘Zabihu na toleo wewe haukutaka, bali ulinitayarishia mwili.’ (Waebrania 10:5) Yesu alijua kama Mungu ‘hakutaka’ watu waendelee kutoa zabihu za wanyama kwenye hekalu la Yerusalemu. Lakini, Yehova alikuwa amemutayarishia Yesu mwili mukamilifu wa mwanadamu ili autoe kuwa zabihu. Yesu alionyesha namna alijisikia katika moyo wake kwa kusema: “Tazama! Nimekuja (katika kitabu cha kukunjwa imeandikwa juu yangu) ili kufanya mapenzi yako, Ee Mungu.” (Waebrania 10:7) Yehova aliona namna gani jambo hilo? Injili ya Mathayo inasema hivi: ‘Baada ya kubatizwa, Yesu akapanda kutoka katika maji; na, tazama! mbingu zikafunguliwa, naye akaona roho ya Mungu ikishuka kama njiwa, ikija juu yake. Tazama! Pia, kulikuwa na sauti kutoka katika mbingu iliyosema: ‘Huyu ni Mwana wangu, mupendwa, ambaye nimemukubali.”—Mathayo 3:16, 17.
Mazabahu kubwa kuliko ile mazabahu ya hekalu la Yerusalemu ilianza kutumika wakati Yehova Mungu alikubali mwili wa Yesu kuwa zabihu. Mazabahu hiyo ilikuwa “mapenzi” ya Mungu, ao mupango wake wa kukubali uzima wa Yesu kama zabihu. (Waebrania 10:10) Wakati Yesu alitiwa mafuta kwa roho takatifu, hilo lilimaanisha kama Mungu alikuwa ameanzisha mupango wake wa hekalu la kiroho. Kwa hiyo, wakati Yesu alibatizwa, makao ya mbingu ya Mungu yalitiwa mafuta, ao kutengwa, ili ikuwe “Mahali Patakatifu Zaidi” katika mupango wa hekalu kubwa la kiroho.
w07 1/9 uku. 20 fu. 4
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Danieli
9:27—Ni agano gani liliendelea ‘kutendeshwa kwa ajili ya wengi’ mupaka mwisho wa juma la 70 la miaka, ao mwaka wa 36 K.K.Y.? Agano la Sheria liliondolewa mwaka wa 33, wakati Yesu alitundikwa. Lakini, kwa kuendelea kutumikisha agano lenye alifanya na Abrahamu kwa ajili ya Waisraeli wa kimwili mupaka mwaka wa 36, Yehova aliongeza kipindi cha pendeleo la pekee kwa Wayahudi kwa sababu walikuwa wazao wa Abrahamu. Agano lenye alifanya na Abrahamu linaendelea kutumika kwa ajili ya “Israeli wa Mungu.”—Wagalatia 3:7-9, 14-18, 29; 6:16.
TAREHE 9-15/10
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | DANIELI 10-12
“Yehova Aliona Wakati Wenye Kuja wa Wafalme”
dp uku. 212-213 fu. 5-6
Wafalme Wawili Wanapigana
Wafalme watatu wa kwanza ni Cyrus le Grand, Cambyse II, na Darius I. Kwa sababu Bardiya (ao pengine Gaumata, mwenye alijifanya kuwa mufalme) alitawala miezi saba tu, unabii huo hautaje utawala wake huo mufupi. Mwaka wa 490 M.K.Y., mufalme wa tatu, Darius I, alijaribu kushambulia Ugiriki kwa mara ya pili. Lakini, Waperse walipigwa sana huko Marathon na wakakimbilia Asia Ndogo. Hata kama Darius alijitayarisha muzuri sana ili kupigana vita ingine na Ugiriki, alikufa kisha miaka ine; kwa hiyo, haikuwezakana tena. Aliachia mupango huo mutoto yake Xerxès I, mwenye alimukomboa na akatawala kama mufalme ‘wa ine.’ Ni yeye Mufalme Ahasuero mwenye alimuoa Esta.—Esta 1:1; 2:15-17.
Kwa kweli, Xerxès I ‘aliwachochea wote juu ya ufalme wa Ugiriki,’ ni kusema, yale majimbo huru yote ya Ugiriki. Kitabu The Medes and Persians—Conquerors and Diplomats kinasema hivi: “Maofisa wa serikali yake wenye kutaka mambo makubwa, walimuchochea Xerxès aanzishe mashambulio kupitia inchi kavu na bahari.” Mwanahistoria Mugiriki Hérodote, wa miaka ya 400 Mbele ya Kuzaliwa kwa Yesu aliandika hivi: “Hakuna mashambulizi mengine yoyote yenye kulingana na hili.” Maandishi yake yanasema kama maaskari wa kupigania juu ya bahari walikuwa “watu 517 610. Maaskari wenye walitembea kwa miguu walikuwa 1 700 000; wenye walitembeza farasi walikuwa 80 000; na kuongezea Waarabu wenye walitembeza ngamia, na Walibya wenye walipigana kwa kutumia magari ya vita, wenye ninafikiri walikuwa 20 000 hivi. Kwa hiyo, maaskari wote pamoja walikuwa watu 2317610.”
dp uku. 213 fu. 8
Wafalme Wawili Wanapigana
Malaika alisema hivi: ‘Mufalme mwenye nguvu atasimama na kutawala kwa mamlaka makubwa sana na kufanya kulingana na mapenzi yake.’ (Danieli 11:3) Alexandre mwenye miaka 20 ‘alisimama’ na akakuwa mufalme wa Makedonia mwaka wa 336 M.K.Y. Alifikia kuwa Alexandre le Grand, ‘mufalme mwenye nguvu.’ Kwa kufuata mipango ya baba yake, Philippe II, alikamata maeneo ya Waperse huko Mashariki ya Kati. Wakati watu wake 47 000 walivuka Muto Efrati na Muto Tigri, walisambaza maaskari wa Darius III, watu 250 000 huko Gaugamela. Mwishowe, Darius akakimbia, wakamuua, na hivyo utawala wa Waperse ukafikia mwisho. Ugiriki ikakuwa serikali ya ulimwengu, na Alexandre ‘akatawala kwa mamlaka makubwa sana na kufanya kulingana na mapenzi yake.’
dp uku. 214 fu. 11
Wafalme Wawili Wanapigana
Kisha Alexandre kufa, ufalme wake ‘uligawanywa kuelekea pepo ine.’ Majenerali wake wengi hawakuelewana kisha kukamata maeneo. Jenerali Antigonus I mwenye alikuwa na jicho moja alijaribu kukamata maeneo yote ya utawala wa Alexandre. Lakini akauawa katika vita huko Ipsus, Frigia. Kufikia mwaka wa 301 M.K.Y., majenerali ine kati ya majenerali wa Alexandre walikuwa wanatawala eneo kubwa lenye kamanda wao alikuwa amekamata. Cassandre alitawala Makedonia na Ugiriki. Lysimaque alitawala Asia Ndogo na Thrasi. Séleucus I Nicator alitawala Mesopotamia na Siria. Na Ptolémée Lagus alitawala Misri na Palestina. Kama vile unabii ulikuwa umesema, eneo kubwa sana la utawala wa Alexandre liligawanywa na kuwa falme ine za Wagiriki.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w13 15/7 uku. 13 fu. 16, maelezo ya kumalizia
“Tazama! Mimi Nipo Pamoja Nanyi Siku Zote”
Andiko la Danieli 12:3 linasema kama ‘wale walio na ufahamu [Wakristo watiwa-mafuta] watangaa kama mwangaza wa anga.’ Wanafanya hivyo wakati wangali duniani kwa kushiriki kazi ya kuhubiri. Lakini, andiko la Mathayo 13:43 linazungumuzia wakati watangaa sana katika Ufalme wa mbinguni. Zamani, tulielewa kama maandiko hayo mawili yalizungumuzia jambo lilelile, ni kusema, kazi ya kuhubiri.
dp uku. 315 fu. 18
Yehova Anamuahidi Danieli Malipo ya Ajabu
Kitabu cha Danieli kinamalizika na moja kati ya ahadi za muzuri sana zenye Mungu ametolea mwanadamu. Malaika wa Yehova alimuambia Danieli hivi: “Nawe utasimama kwa ajili ya fungu lako mwishoni mwa zile siku.” Malaika huyo alimaanisha nini? Kwa sababu ‘pumuziko’ lenye alikuwa ametoka tu kutaja ilikuwa kifo, ahadi ya kwamba Danieli ‘angesimama’ wakati fulani wenye kuja, ilipaswa kumaanisha kitu kimoja tu, ni kusema, ufufuo! Hata watu fulani wenye kujifunza mambo ya Biblia walisema kama katika Maandiko ya Kiebrania, Danieli sura ya 12 ndiyo inazungumuzia mara ya kwanza kabisa ufufuo kwa njia yenye kuwa wazi. (Danieli 12:2) Lakini wanadanganyika kabisa. Danieli alijua muzuri sana tumaini la ufufuo.
TAREHE 16-22/10
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | HOSEA 1-7
“Unafurahia Upendo Mushikamanifu Kama Yehova?”
Acha ‘Sheria ya Fazili Zenye Upendo’ Ilinde Ulimi Wako
Tunapaswa kuonyesha upendo mushikamanifu katika mambo yote yenye tunatendea waabudu wenzetu wa Yehova. Hata wakati tunapambana na hali ngumu, sheria ya fazili zenye upendo haipaswe kuondoka kwenye ulimi wetu. Yehova alikasirika wakati fazili zenye upendo za wana wa Israeli zilikuwa “kama umande ambao hutoweka mapema.” (Hos. 6:4, 6) Lakini, Yehova anafurahi wakati tunakuwa na zoezi la kuonyesha fazili zenye upendo. Ona namna anabariki wale wenye kufuatilia fazili zenye upendo.
w07 15/9 uku. 16 fu. 8
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Hosea
6:6. Kuzoea zambi kunaonyesha kama mutu hana upendo mushikamanifu kwa Mungu. Hakuna zabihu za kiroho zenye zinaweza kulipia kosa hiyo.
w07 15/6 uku. 27 fu. 7
Yehova Anaona Utii Wako Kuwa wa Maana
Kuhusu jambo hilo, kumbuka kama Yehova aliwaambia watu wake wa zamani kwamba utii ulikuwa wa maana sana hata kuliko zabihu za wanyama. (Methali 21:3, 27; Hosea 6:6; Mathayo 12:7) Sababu gani Yehova aliwaambia hivyo watu wake, hata kama yeye ndiye aliwaomba watoe zabihu hizo? Kwa kweli, mutu mwenye anatoa zabihu alipaswa kuchunguza nia yake. Alipaswa kujiuliza kama anatoa zabihu hiyo ili kumupendeza Mungu, ao anafanya hivyo kwa desturi tu. Kama mutu anataka kumupendeza Mungu kwelikweli, anapaswa kujikaza kutii amri zake zote. Mungu hana lazima ya zabihu za wanyama, lakini utii ni kitu cha maana sana chenye tunaweza kumutolea.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w07 15/9 uku. 14 fu. 7
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Hosea
1:7—Nyumba ya Yuda ilionyeshwa rehema na kuokolewa wakati gani? Jambo hilo lilitokea katika mwaka wa 732 M.K.Y., katika siku za Mufalme Hezekia. Wakati huo, Yehova alimaliza shambulio la Waashuru juu ya Yerusalemu wakati alituma malaika moja aue maaskari 185 000 wa maadui usiku moja tu. (2 Wafalme 19:34, 35) Kwa hiyo, Yehova hakuokoa nyumba ya Yuda, “kwa upinde wala kwa upanga wala kwa vita, wala kwa farasi wala kwa wapanda-farasi,” lakini kwa malaika.
w05 15/11 uku. 20 fu. 16
Unabii wa Hosea Unatusaidia Kutembea Pamoja na Mungu
Pia, Mungu alitimiza ahadi hii: ‘Hakika nitafanya agano siku hiyo na munyama wa mwituni na kiumbe kinachoruka cha mbinguni na kitu kinachotambaa cha inchi, nami nitavunja kutoka katika inchi upinde na upanga na vita, nami nitawafanya walale salama salimini.’ (Hosea 2:18) Wayahudi wenye walirudi katika inchi yao waliishi kwa usalama kabisa, bila kuwaogopa wanyama. Unabii huo pia ulitimia mwaka wa 1919 K.K.Y., wakati mabaki ya Israeli wa kiroho waliwekwa huru kutoka ‘Babiloni Mukubwa,’ milki ya ulimwengu ya dini ya uwongo. Sasa, wanaishi kwa usalama na wanafurahia kuwa katika paradiso ya kiroho pamoja na waabudu wenzao wenye kuwa na tumaini la kuishi milele katika dunia. Wakristo hao wa kweli hawana tabia za wanyama.—Ufunuo 14:8; Isaya 11:6-9; Wagalatia 6:16.
g05 8/9 uku. 12 fu. 2
Wakati Upatano Utaenea Katika Ulimwengu Wote
Kwa kweli, katika Dunia viumbe watatendeana kwa njia mupya, kwa sababu Mungu atawafundisha wanadamu washikamanifu namna ya kutunza muzuri dunia, makao yao. Hata ‘atafanya agano’ kwa njia ya mufano na wanyama wote wakali, na kuwafanya wajitiishe kwa wanadamu kwa amani.—Hosea 2:18; Mwanzo 1:26-28; Isaya 11:6-8.
TAREHE 23-29/10
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | HOSEA 8-14
“Ujitoe Kabisa kwa Yehova”
w07 1/4 uku. 20 fu. 2
Kutoa Zabihu Zenye Zinamupendeza Mungu
Tena, Biblia inaonyesha kama maneno yetu ya sifa yanaweza kuonwa kuwa zabihu zenye zinatolewa kwa Yehova. Nabii Hosea alitumia maneno ‘ngombe-dume wachanga wa midomo yetu,’ yenye kuonyesha kama Mungu anaona sifa za midomo yetu kuwa moja kati ya zabihu za maana zaidi. (Hosea 14:2) Mutume Paulo aliwaambia Wakristo Waebrania mambo haya: ‘Tumutolee Mungu zabihu ya sifa, yaani, tunda la midomo ambayo hulifanyia jina lake tangazo la hazarani.’ (Waebrania 13:15) Leo, Mashahidi wa Yehova wanaendelea kuhubiri habari njema kwa bidii na kufanya wanafunzi kutoka kwa watu wa mataifa yote. (Mathayo 24:14; 28:19, 20) Wanamutolea Mungu zabihu za sifa muchana na usiku katika dunia yote.—Ufunuo 7:15.
Kukubaliwa na Mungu Kunaongoza Kwenye Uzima wa Milele
Ngombe-dume ndiye alikuwa nyama wa bei sana mwenye Waisraeli wangemutolea Yehova. Kwa hiyo, ‘ngombe-dume wachanga wa midomo yetu’ ni maneno yenye kutoka katika moyo, yenye kufikiriwa muzuri yenye inasemwa ili kumusifu Mungu wa kweli. Yehova aliwajibu namna gani wale wenye walitoa zabihu kama hizo? Alisema: “Nitawapenda kwa kupenda kwangu mwenyewe.” (Hos. 14:4) Yehova aliwasamehe wale walitoa zabihu kama hizo za sifa, aliwakubali, na alikuwa rafiki yao.
jd uku. 87 fu. 11
Umutumikie Yehova Kulingana na Viwango Vyake vya Juu
Andiko la Hosea 14:9 linatusaidia kuona faida za kuwa na mwenendo muzuri. Kufuata kanuni za Mungu kunaleta baraka na faida. Kwa sababu yeye ndiye Muumbaji wetu, anajua namna alituumba. Mambo yenye anataka tufanye ni kwa faida yetu. Tunaweza kulinganisha uhusiano wetu pamoja na Mungu, na motokari na fundi. Fundi anajua namna motokari imefanywa na namna ya kuitengeneza. Anajua kama, kisha motokari kutembea kilometre fulani, anapaswa kubadilisha mafuta. Inaweza kuwa namna gani kama mutu anazarau kanuni hiyo, pengine akiwaza kama motokari haina shida? Wakati fulani motokari yake itaharibika. Ni vile pia juu ya wanadamu. Muumbaji wetu ametupatia amri mbalimbali. Kama tunazitii tutapata faida. (Isaya 48:17, 18) Kujua jambo hilo kunatuchochea tena zaidi tuishi kulingana na kanuni zake na kutii amri zake.—Zaburi 112:1.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w05 15/11 uku. 28 fu. 7
“Njia za Yehova Zimenyooka”
Kama tunamuabudu Yehova bila unafiki na kwa kweli kabisa, atatuonyesha fazili zake zenye upendo, ao upendo mushikamanifu. Aliwaambia hivi Waisraeli waasi: ‘Mujipandie mbegu kwa uadilifu; muvune kulingana na fazili zenye upendo. Mujilimie udongo unaofaa kwa kilimo, kukiwa kungali na wakati wa kumutafuta Yehova mupaka atakapokuja na kuwatolea ninyi mafundisho kwa uadilifu.’—Hosea 10:12.
Walimungoja Masiya
Kama vile Waisraeli, Masiya angeitwa kutoka Misri. (Hos. 11:1) Mbele Herode atoe amri ya kuua watoto wanaume, malaika aliwaambia Yosefu, Maria, na Yesu waende Misri. Walibakia huko “mupaka kufa kwa Herode, ili maneno haya ya Yehova kupitia nabii [Hosea] yatimie: ‘Kutoka Misri nilimuita mwanangu.’” (Mt. 2:13-15) Ni wazi kama, Yesu hangeweza kuongoza mambo yenye ilitabiriwa juu ya kuzaliwa kwake na maisha yake ya utoto.
TAREHE 30/10–TAREHE 5/11
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOELI 1-3
“Wana Wako na Binti Zako Watatoa Unabii”
w02 1/8 uku. 15 fu. 4-5
Tunachochewa na ‘Mambo Makubwa ya Mungu’
Kisha tu kupokea roho takatifu, wanafunzi wenye walikuwa Yerusalemu walianza kuwatangazia wengine habari njema ya wokovu, walianza na watu wengi wenye walikuwa wamekusanyika asubui ya siku hiyo. Mahubiri yao yalitimiza unabii wa maana wenye Yoeli mwana wa Pethueli alikuwa ameandika miaka mia munane hivi zamani: “Nitaimimina roho yangu juu ya kila namna ya mwili, na wana wenu na binti zenu watatoa unabii. Nao wazee wenu wataota ndoto. Nao wanaume wenu vijana wataona maono; na hata juu ya watumishi wa kiume na juu ya wajakazi katika siku hizo nitaimimina roho yangu . . . kabla ya kuja kwa ile siku ya Yehova iliyo kuu na yenye kuogopesha.”—Yoeli 1:1; 2:28, 29, 31; Matendo 2:17, 18, 20.
Ni kusema Mungu angetokeza manabii wanaume na wanawake kama vile Daudi, Yoeli, na Debora, na kuwatumia ili kutabiri mambo ya wakati wenye kuja? Hapana. ‘Wana na binti, watumishi wa kiume na wajakazi’ Wakristo wangetabiri katika maana ya kwamba wangechochewa na roho ya Yehova ili kutangaza ‘mambo makubwa’ yenye Yehova alikuwa amefanya na yenye angefanya. Kwa hiyo, wangekuwa wasemaji wa Aliye Juu Zaidi. Hata hivyo, watu walifanya nini?—Waebrania 1:1, 2.
jd uku. 167 fu. 4
“Tangazeni Mambo Haya Kati ya Mataifa”
Fikiria jambo hilo kwa njia ingine. Yehova Mungu alimuambia nabii Yoeli juu ya wakati wenye watu wa kila namna watatoa unabii kwa njia ya mufano: “Kisha itakuwa kwamba nitaimimina roho yangu juu ya kila namna ya mwili, na wana wenu na binti zenu watatoa unabii. Nao wazee wenu wataota ndoto. Nao wanaume wenu vijana wataona maono.” (Yoeli 2:28-32) Siku ya Pentekoste, mwaka wa 33, mutume Petro alitumia maneno hayo juu ya kushuka kwa roho takatifu juu ya wale wenye walikusanyika katika chumba cha juu huko Yerusalemu na juu ya kazi yao ya kuhubiri ‘mambo makubwa ya Mungu.’ (Matendo 1:12-14; 2:1-4, 11, 14-21) Sasa, fikiria wakati wetu. Unabii wa Yoeli umekuwa ukitimizwa kwa njia kubwa tangu mwanzo wa miaka ya 1900. Wakristo watiwa-mafuta, wanaume na wanawake, wazee na vijana, walianza ‘kutoa unabii,’ ni kusema, kutangaza ‘mambo makubwa ya Mungu,’ na habari njema ya Ufalme, wenye umeanza kutawala mbinguni.
w07 1/10 uku. 13 fu. 2
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoeli na cha Amosi
2:32—‘Kuliitia jina la Yehova’ maana yake nini? Kuliitia jina la Mungu kunamaanisha kulijua jina hilo, kuliheshimia sana, na kumutegemea na kumutumainia mwenye jina hilo.—Waroma 10:13, 14.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w07 1/10 uku. 13 fu. 5
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoeli na cha Amosi
2:12, 13. Kutubu kwa kweli kunatoka moyoni. Kunafanyika ndani kama vile ‘kurarua mioyo yetu,’ hapana inje tu, kama vile ‘kurarua mavazi yetu.’
w07 1/10 uku. 13 fu. 3
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoeli na cha Amosi
3:14—“Bonde la uamuzi” ni nini? Ni mahali pa mufano penye Mungu anafanyia hukumu yake. Wakati wa utawala wa Mufalme Yehoshafati wa Yuda, mwenye jina lake linamaanisha “Yehova Ni Mwamuzi,” Mungu alivuruga majeshi ya mataifa jirani na hivyo akakomboa Yuda. Ndiyo sababu, mahali hapo panaitwa pia “bonde la Yehoshafati.” (Yoeli 3:2, 12) Wakati wetu, bonde hilo linafananisha mahali pa mufano penye mataifa yatapondwa-pondwa kama zabibu ndani ya shinikizo la divai.—Ufunuo 19:15.