Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 6-12/11
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | AMOSI 1-9
“Umutafute Yehova ili Uendelee Kuishi”
w04 15/11 uku. 24 fu. 20
Mutafuteni Yehova, Muchunguzaji wa Mioyo
Haikuwa mwepesi kwa mutu mwenye aliishi katika Israeli wakati huo kuendelea kuwa muaminifu kwa Yehova. Wakristo wote leo, vijana na wazee wanajua kama haiko mwepesi kuwa tofauti na watu wengi. Lakini kumupenda Mungu na kutaka kabisa kumufurahisha kulichochea Waisraeli fulani wafuate ibada ya kweli. Kwa furaha, Yehova aliwatolea mwaliko huu wenye kupatikana katika Amosi 5:4: “Nitafuteni mimi, mwendelee kuishi.” Ni hivyo pia leo, Mungu anawaonyesha rehema wale wenye wanatubu na kumutafuta kwa kuwa na ujuzi sahihi wa Neno lake na kufanya mapenzi yake. Haiko mwepesi kuchukua hatua hiyo, lakini kufanya hivyo kunaongoza kwenye uzima wa milele.—Yohana 17:3.
jd uku. 90-91 fu. 16-17
Mumutumikie Yehova Kulingana na Viwango Vyake vya Juu
Mwanadamu wa kwanza, Adamu, alifanya uamuzi mubaya wakati alipaswa kuchagua ni nani anastahili kutuonyesha mazuri na mabaya. Sisi tutafanya maamuzi mazuri? Amosi alionyesha kama tunapaswa kuchukua jambo hilo kwa uzito. Alisema hivi: “Chukieni yaliyo mabaya, pendeni yaliyo mema.” (Amosi 5:15) William Rainey Harper, mwenye alikuwa mwalimu mukubwa wa luga na historia ya Wayahudi katika Université ya Chicago, alisema hivi juu ya andiko hilo: “Kwa maoni [ya Amosi], ili kujua ni nini mazuri na mabaya, ni lazima kuishi kulingana na mapenzi ya Yahweh.” Hilo ni jambo kubwa la kujifunza kwa wale manabii 12. Tujiulize sasa kama tuko tayari kukubali muongozo wa Yehova ili kujua ni nini mazuri na mabaya. Kanuni zake za mazuri na mabaya zinapatikana katika Biblia na Wakristo wakomavu wenye kujua mambo, ni kusema, ‘mutumwa mwaminifu na mwenye busara,’ wanatusaidia kuelewa kanuni hizo—Mathayo 24:45-47.
Kuchukia mambo mabaya kunatusaidia kuepuka mambo yenye kumuchukiza Mungu. Kwa mufano, pengine mutu anajua hatari ya pornografia kwenye Internete na anajaribu kuiepuka. Lakini, ‘mutu aliye kwa ndani’ anaona namna gani adrese za pornografia? (Waefeso 3:16) Kama anatii agizo la Mungu lenye kupatikana katika Amosi 5:15, itakuwa mwepesi kwake kukomalisha uwezo wa kuchukia mambo mabaya. Kwa kufanya hivyo, anaweza kuwa mushindi katika vita hiyo ya kiroho.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w07 1/10 uku. 14 uku. 8
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoeli na cha Amosi
2:12. Hatupaswe kuwavunja moyo mapainia, waangalizi wenye kusafiri, wamisionere, ao wanabeteli wenye wanafanya kazi kwa bidii kwa kuwashauria waache utumishi wa wakati wote ili waishi maisha yenye watu wanaita maisha ya kawaida. Kuliko kufanya hivyo, tunapaswa kuwatia moyo waendelee kufanya kazi yao hiyo ya muzuri.
w07 1/10 uku. 14 fu. 6
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Yoeli na cha Amosi
8:1, 2—“Kikapu cha matunda ya wakati wa kiangazi” kilimaanisha nini? Kilimaanisha kama siku ya Yehova ilikuwa karibu. Matunda ya wakati wa kiangazi ilikusanywa wakati wa mwisho wa kipindi cha mavuno, ni kusema, mwisho wa mwaka wa kilimo. Wakati Yehova alimufanya Amosi aone “kikapu cha matunda ya wakati wa kiangazi,” hilo lilimaanisha kama mwisho wa Israeli ulikuwa karibu. Kwa hiyo, Mungu alimuambia Amosi: “Mwisho umewafikia watu wangu Israeli. Nami sitawasamehe zaidi tena.”
TAREHE 13-19/11
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | OBADIA 1–YONA 4
“Makosa Yako Ikufundishe”
Makosa Yake Mwenyewe Yalimufundisha
Yona alifanya nini? Alijifunza kumuonyesha Yehova shukrani kwa kumutii? Ndiyo. Kisha siku tatu, muchana na usiku katika tumbo la samaki, samaki huyo alimupeleka Yona na ‘akamutapika inchi kavu.’ (Yona 2:10) Fikiria jambo hili: kisha mambo hayo yote, haikuwa lazima Yona aogelee mupaka inchi kavu! Bila shaka, ilimuomba sasa ajue mahali ataenda, ili atoke mahali penye samaki alimutapika. Sifa yake ya kuonyesha shukrani ilijaribiwa. Andiko la Yona 3:1, 2 linasema hivi: ‘Ndipo neno la Yehova likamujia Yona mara ya pili, na kusema: Ondoka, uende Ninawi ule muji mukubwa, ukautangazie neno ninalokuambia.’ Yona atafanya nini sasa?
Yona hakusita. Tunasoma hivi: ‘Basi Yona akasimama na kuenda Ninawi kulingana na neno la Yehova.’ (Yona 3:3) Ndiyo, anatii. Ni wazi kama makosa yake mwenyewe ilimufundisha. Katika jambo hilo pia tunapaswa kuiga imani ya Yona. Sisi wote tunafanya zambi, sisi wote tunafanya makosa. (Rom. 3:23) Je, tutavunjika moyo ao tutaacha pia makosa yetu itufundishe na kuwa sasa watumishi watiifu wa Mungu?
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w07 1/11 uku. 13 fu. 5
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Obadia, cha Yona, na cha Mika
10—Namna gani Edomu ‘lilikatiliwa mbali mupaka wakati usio na kipimo’? Namna unabii ulisema, taifa la Edomu, lenye lilikuwa taifa la kweli lenye serikali na watu wenye kuishi katika eneo fulani lenye kujulikana katika dunia, liliisha. Mufalme Nabonide wa Babiloni alishambulia Edomu katikati ya miaka ya 500 hivi M.K.Y. Kuanzia miaka ya 300 M.K.Y., eneo la Edomu lilikaliwa na Wanabataea, na Waedomu walilazimika kubakia katika sehemu ya kusini ya Yuda, eneo la Negebu lenye lilifikia kuitwa Idumea. Kisha Waroma kuharibu muji wa Yerusalemu mwaka wa 70 K.K.Y., Waedomu hawakukuwa tena.
jd uku. 112 fu. 4-5
Kuwatendea Wengine Namna Mungu Anataka
Tunaweza kujifunza jambo fulani kutokana na hukumu hili ya Mungu juu ya Edomu, Inchi jirani ya Israeli: “Hupaswi kutazama tukio katika siku ya ndugu yako, katika siku ya maafa yake; wala kushangilia juu ya wana wa Yuda katika siku ya kuangamia kwao.” (Obadia 12) Kama watu wa Tiro walikuwa “ndugu” zao kwa biashara, lakini Waedomu walikuwa “ndugu” wa kweli wa Waisraeli, kwa sababu walikuwa wazao wa Esau, ndugu pacha wa Yakobo. Hata Yehova aliwaita Waedomu “ndugu” za Waisraeli. (Kumbukumbu la Torati 2:1-4) Kwa hiyo, Waedomu walionyesha chuki kwelikweli kwa kufurahi wakati Wababiloni walishambulia Wayahudi.—Ezekieli 25:12-14.
Ni wazi kama Mungu hakufurahia namna Waedomu walitendea ndugu zao Wayahudi. Lakini, tunaweza kujiuliza hivi: ‘Mungu anaweza kusema nini juu ya namna ninatendea ndugu na dada zangu?’ Tufikirie kwanza namna tunaona na kutendea ndugu mwenye tunakosana naye. Kwa mufano, Mukristo fulani amekosana na wewe ao na mutu wa familia yako. Hata kama uko na “sababu ya kulalamika,” utaendelea kuwa na kinyongo, na kukataa kumusamehe ao kukataa kujaribu kumaliza tatizo hilo? (Wakolosai 3:13; Yoshua 22:9-30; Mathayo 5:23, 24) Kama unafanya hivyo, hilo linaweza kuonekana katika namna utamutendea ndugu yako; pengine hautamuchangamukia tena, ao utaanza kumuepuka, ao tena kumusema mubaya. Tuseme kwa mufano kisha wakati fulani ndugu huyo anakosea, pengine wazee wa kutaniko wanamushauria ao wanamurekebisha. (Wagalatia 6:1) Wewe utakuwa na roho kama ya Waedomu kwa kufurahi kwa sababu ya matatizo ya ndugu huyo? Mungu anataka ufanye nini?
TAREHE 20-26/11
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MIKA 1-7
“Mungu Anataka Tufanye Nini?”
w08 15/5 uku. 6 fu. 20
Tunapaswa Kuwatendea Wengine Namna Gani?
Mungu anaona namna tunatendea ndugu na dada zetu kuwa sehemu ya maana sana ya ibada ya kweli. Zabihu za wanyama hazikuwa na maana kwa Yehova kama wale wenye walizitoa waliwatendea mubaya wanadamu wenzao. (Mika 6:6-8) Kwa hiyo, Yesu aliwaomba wanafunzi wake wakuwe ‘tayari kusuluhisha (kutengeneza) mambo upesi (mbio)’. (Mt. 5:25) Vile vile, Paulo aliandika hivi: ‘Iweni na gazabu (kasirani), lakini musitende zambi; jua lisitue mukiwa katika hali ya kuchokozeka, wala musimupe Ibilisi nafasi.’ (Efe. 4:26, 27) Kama tuko na sababu ya kukasirika, tunapaswa kufanya haraka kutengeneza mambo ili tusiendelee kuwa katika hali ya kuchokozeka ili tusimupe Ibilisi nafasi ya kutushambulia.—Luka 17:3, 4.
“Yehova Anataka Nini Kutoka Kwako?”
“Kutenda haki.” Kitabu kimoja kinasema kama neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “haki,” “linatoa pia wazo la kuwatendea watu wengine mambo yenye kuwa sawa na mema.” Mungu anataka tuwatendee wengine mambo yenye kanuni zake zinakubali kuwa sawa na mema. Tunatenda haki wakati tunawatendea wengine bila ubaguzi, kwa njia yenye kufaa, na bila udanganyifu. (Mambo ya Walawi 19:15; Isaya 1:17; Waebrania 13:18) Wakati tunawatendea wengine kwa haki, wao pia wanachochewa kututendea kwa haki.—Mathayo 7:12.
‘Kupenda fazili.’ Mungu anataka tuonyeshe sifa ya fazili na tuipende. Neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa ‘fazili’ (cheʹsedh) linaweza pia kutafsiriwa “fazili zenye upendo” ao “upendo mushikamanifu.” Mutu moja mwenye anafasiria Biblia alisema hivi: “Neno [cheʹsedh] halimaanishe tu upendo, rehema, ao fazili; linamaanisha sifa hizo zote pamoja.” Kama tunapenda sifa ya fazili, hatutalazimishwa kuionyesha; tutafurahia kusaidia wenye kuhitaji musaada. Kwa kufanya hivyo, tutapata furaha ya kutoa.—Matendo 20:35.
“Kuwa na kiasi katika kutembea na Mungu wako.” Katika Biblia, neno “kutembea” linamaanisha “kufuata mwendo fulani.” Tunatembea pamoja na Mungu wakati tunafuata njia ya maisha yenye ametuonyesha katika Biblia. Tunapaswa “kuwa na kiasi” wakati tunafuata njia hiyo. Namna gani? Kama tuko na kiasi, tutachunguza hali yetu mbele za Mungu na kutambua uzaifu wetu. Kwa hiyo, maneno “kuwa na kiasi katika kutembea na,” inamaanisha kuwa na usawaziko juu ya mambo yenye anataka tufanye na mambo yenye tunaweza kufanya.
Inapendeza kuona kama Yehova hatuombe tufanye mambo yenye kupita uwezo wetu. Anafurahi kuona tunafanya yetu yote ili kumutumikia kulingana na uwezo wetu. (Wakolosai 3:23) Anaelewa mipaka yetu. (Zaburi 103:14) Sisi pia, wakati tunatambua mipaka yetu kwa unyenyekevu, tutafurahia kutembea pamoja naye. Ni nini inakuzuia ujifunze namna unaweza kuanza kutembea pamoja na Mungu? Ukifanya hivyo, atakubariki sana.—Methali 10:22.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w07 1/11 uku. 15 fu. 6
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Obadia, cha Yona, na cha Mika
2:12—Unabii juu ya ‘kuwakusanya pamoja waliobaki wa Israeli’ ulitimia wakati gani? Ulitimia kwa mara ya kwanza katika mwaka wa 537 M.K.Y. wakati Wayahudi wenye walibakia walitoka Babiloni na kurudia katika inchi yao. Leo, unabii huo unatimia kwa “Israeli wa Mungu.” (Wagalatia 6:16) Tangu mwaka wa 1919, Wakristo watiwa-mafuta wamekusanywa pamoja “kama kundi zizini.” Kwa sababu wanaungwa mukono na ‘umati mukubwa’ wa “kondoo wengine,” tangu mwaka wa 1935, wamefanya “kelele za wanadamu.” (Ufunuo 7:9; Yohana 10:16) Wote pamoja, wanaendelesha ibada ya kweli kwa bidii.
Yehova Anataka Nini Kwetu?
Wataki tunapata baraka za Yehova, zinatuchochea kumuiga Mika. Yeye anasema hivi: ‘Nitaonyesha mutazamo wa kumungojea Mungu wa wokovu wangu.’ (Mika 7:7) Kuko upatano gani kati ya maneno hayo na sisi kutembea kwa unyenyekevu pamoja na Mungu? Mutu mwenye kuwa na mutazamo wa kungojea, ao mwenye kuendelea kungojea, havunjike moyo kwa sababu siku ya Yehova inakawia kufika. (Methali 13:12) Ni kweli kama tunapenda kuona mwisho wa ulimwengu huu muovu. Lakini, kila juma maelfu ya watu wanaanza kutembea na Mungu. Kujua hilo kunatuchochea tuendelee kungojea. Shahidi moja mwenye amemutumikia Yehova kwa miaka mingi alisema hivi: “Wakati nakumbuka miaka 55 yenye nimepitisha katika kazi ya kuhubiri, niko hakika kama, sijapoteza kitu kwa kumungojea Yehova. Lakini, nimejiepusha na mambo mengi yenye kuumiza.” Na weye unaweza kusema kama Shahidi huyo?
TAREHE 27/11–3/12
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | NAHUMU 1–HABAKUKI 3
“Tuendelee Kuwa Macho Kiroho na Wenye Bidii”
w07 15/11 uku. 10 fu. 3-5
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Nahumu, cha Habakuki, na cha Sefania
2:1. Kama Habakuki, tunapaswa kuendelea kuwa macho kiroho na wenye bidii. Tunapaswa pia kuwa tayari kubadilisha mawazo yetu kulingana na ‘karipio’ ao nizamu yoyote yenye wanaweza kututolea.
2:3; 3:16. Kwa sababu tunaamini kabisa kuja kwa siku ya Yehova, tusisahau kama siku hiyo inakuja haraka.
2:4. Ili kuokoka siku ya hukumu ya Yehova yenye kuja, tunapaswa kuvumilia kwa uaminifu.—Waebrania 10:36-38.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w07 15/11 uku. 9 fu. 2
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Nahumu, cha Habakuki, na cha Sefania
2:6—Ni ‘milango gani ya mito’ ilifunguliwa? Milango hiyo ilifananisha njia yenye maji ya Muto Tigri ilifanya katika ukuta wa Ninawi. Katika mwaka wa 632 M.K.Y. wakati majeshi ya muungano ya Wababiloni na Wamede ilikuja kupigana na Ninawi, wakaaji wa muji huo hawakuogopa hata kidogo kwa sababu muji wao ulikuwa umezungukwa na ukuta murefu; waliona kama muji huo hauwezi kuingiliwa. Lakini, mvua mukubwa ulinyesha na Muto Tigri ukajaa. Kulingana na mwanahistoria mwenye kuitwa Diodorus, muto huo “ulibomoa sehemu ya muji na kubomoa sehemu fulani ya kuta zake.” Kwa hiyo, milango ya mito ilifunguliwa, na namna ilitabiriwa, muji wa Ninawi ulikamatwa haraka kama vile moto unalunguza haraka majani yenye kukauka.—Nahumu 1:8-10.
w07 15/11 uku. 10 fu. 10
Mambo Makuu Katika Kitabu cha Nahumu, cha Habakuki, na cha Sefania
3:17-19. Hata kama pengine tutapata magumu mbele na wakati wa Har–Magedoni, tunaweza kuwa hakika kama Yehova atatupatia “nguvu” wakati tunaendelea kumutumikia kwa furaha.