Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr18 Mwezi wa 2 uku. 1-7
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2018)
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 5-11/02
  • TAREHE 12-18/02
  • nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 15:26
  • TAREHE 19-25/02
  • TAREHE 26/02–4/03
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2018)
mwbr18 Mwezi wa 2 uku. 1-7

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 5-11/02

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 12-13

“Mufano wa Ngano na Magugu”

w13 15/7 uku. 9-10 fu. 2-3

“Tazama! Mimi Niko Pamoja Nanyi Siku Zote”

Mambo yenye ilitokea katika shamba la mulimaji huyo inaonyesha namna gani na wakati gani Yesu angekusanya kutoka katika mataifa kikundi cha watu wenye kufananishwa na ngano, ni kusema, Wakristo watiwa-mafuta wenye watatawala pamoja naye katika Ufalme wake. Mbegu zilianza kupandwa kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33. Kukusanywa kutamalizika wakati watiwa-mafuta wenye watakuwa wangali katika dunia mwishoni mwa ulimwengu huu watatiwa muhuri kwa mara ya mwisho na kisha watainuliwa ili kuenda mbinguni. (Mt. 24:31; Ufu. 7:1-4) Kama vile kupanda juu ya mulima kunaweza kumufanya mutu aone muzuri maeneo fulani ya pembeni-pembeni, vilevile mufano huo unatusaidia kuona muzuri mambo yenye ingetokea katika kipindi cha miaka 2000 hivi. Wakati tunachunguza hali leo, tunajionea mambo gani yenye kuhusiana na Ufalme? Mufano huo unazungumuzia wakati wa kupandwa kwa mbegu, wakati wa kukomaa kwazo, na wakati wa mavuno. Habari hii itazungumuzia zaidi sana wakati wa mavuno.

YESU ANAENDELEA KULINDA WAKRISTO WATIWA-MAFUTA

Kisha mwaka wa 100, “magugu yalionekana” wakati Wakristo wa uongo walianza kuonekana katika shamba, ni kusema, ulimwengu. (Mt. 13:26) Kisha tu mwaka wa 300, Wakristo wa uongo, ni kusema, magugu, waliongezeka zaidi kuliko Wakristo watiwa-mafuta. Kumbuka kama katika mufano wa Yesu, watumwa walimuomba bwana wao ruhusa ya kuondoa magugu. (Mt. 13:28) Bwana wao aliwajibu namna gani?

w13 15/7 uku. 10 fu. 4

“Tazama! Mimi Niko Pamoja Nanyi Siku Zote”

Wakati alizungumuzia ngano na magugu, Yesu alisema hivi: ‘Acheni zikue [zikomalie] pamoja mupaka wakati wa mavuno.’ Amri hiyo inaonyesha kama tangu wakati wa mitume mupaka leo, katika dunia kumekuwa siku zote Wakristo watiwa-mafuta, ni kusema, Wakristo wenye kufananishwa na ngano. Jambo hilo linahakikishwa na mambo haya yenye Yesu aliambia wanafunzi wake: ‘Mimi niko pamoja nanyi siku zote mupaka umalizio wa mufumo wa mambo.’ (Mt. 28:20) Kwa hiyo, Yesu angewalinda Wakristo watiwa-mafuta siku zote mupaka wakati wa mwisho. Lakini, kwa sababu walifunikwa na Wakristo wenye kufananishwa na magugu, hatujue kwa kweli ni nani walikuwa sehemu ya kikundi cha Wakristo wenye kufananishwa na ngano katika kipindi hicho kirefu cha wakati. Lakini, miaka fulani mbele ya wakati wa mavuno kuanza, kikundi cha watu wenye kufananishwa na ngano kilianza kutambuliwa. Namna gani?

w13 15/7 uku. 12 fu. 10-12

“Tazama! Mimi Niko Pamoja Nanyi Siku Zote”

Jambo la kwanza ni kukusanywa kwa magugu. Yesu alisema hivi: “Katika majira ya mavuno nitawaambia wavunaji, Kwanza kusanyeni magugu na kuyafunga matita-matita [mafungu-mafungu].” Kisha 1914, malaika walianza ‘kukusanya’ Wakristo wenye kufananishwa na magugu kwa kuwatenganisha na “wana wa Ufalme,” ni kusema, watiwa-mafuta​—Mt. 13:30, 38, 41.

Wakati kazi ya kukusanya ilikuwa inasonga mbele, tofauti kati ya vikundi hivyo viwili ilianza kuonekana waziwazi zaidi. (Ufu. 18:1, 4) Katika 1919, ilionekana wazi kama Babiloni Mukubwa alikuwa ameanguka. Ni jambo gani lilionyesha kabisa tofauti kati ya Wakristo wa kweli na Wakristo wa uongo? Ni kazi ya kuhubiri. Ndugu wenye walisimamia kazi ya Wanafunzi wa Biblia walianza kukazia kama kila mwanafunzi wa Biblia anapaswa kuhubiri habari njema ya Ufalme. Kwa mufano, broshua Ni Nani Waliopewa Kazi Hii? yenye ilitolewa katika 1919 [katika Kiingereza] ilitia moyo Wakristo wote watiwa-mafuta wahubiri nyumba kwa nyumba. Broshua hiyo ilisema hivi: “Kazi hii inaonekana kuwa kubwa sana, lakini ni kazi ya Bwana, na kwa nguvu zake, tutaitimiza. Muko na pendeleo la kufanya kazi hiyo.” Je, Wanafunzi wa Biblia walikubali pendeleo hilo? Katika 1922, gazeti Munara wa Mulinzi lilionyesha kama kuanzia wakati huo na kuendelea, Wanafunzi wa Biblia waliongeza bidii yao katika kazi ya kuhubiri. Tangu wakati huo mupaka leo, kazi ya kuhubiri nyumba kwa nyumba imekuwa alama yenye kutambulisha Wakristo hao waaminifu.

Jambo la pili ni kukusanywa kwa ngano. Yesu aliwaambia malaika wake hivi: ‘Nendeni mukusanye ngano galani mwangu.’ (Mt. 13:30) Kuanzia 1919, Wakristo watiwa-mafuta wameendelea kukusanywa na kuingizwa katika kutaniko la Kikristo lenye lilianzishwa tena. Watiwa-mafuta watakuwa wangali wanaishi wakati mwisho utafika, watakusanywa kwa mara ya mwisho wakati watapokea zawadi yao ya kuenda mbinguni.​—Dan. 7:18, 22, 27.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 12:20

utambi wenye kutoa moshi: Taa yenye ilitumiwa sana ilikuwa chombo kidogo cha udongo chenye kilijazwa mafuta ya muzeituni. Utambi ulinyonya mafuta ili kuwasha moto. Maneno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “utambi wa kitani unaofifia” yanaweza kumaanisha utambi wenye unatoa moshi kwa sababu majivu inafanya mwangaza wa moto ufifie ao uzimike. Unabii wa Isaya 42:3 ulizungumuzia namna Yesu angewasikilia watu huruma; hangezima mwangaza wa moto wa mwisho wa tumaini la watu wapole na wenye kuteswa.

w16.10 uku. 32

Ulijua?

Ni kweli kwamba zamani mutu fulani angepanda kabisa magugu katika shamba la mutu mwengine?

KULINGANA na Mathayo 13:24-26, Yesu alisema hivi: ‘Ufalme wa mbinguni umekuwa kama mutu aliyepanda mbegu nzuri katika shamba lake. Watu wakiwa wamelala usingizi, adui yake alikuja na kupanda magugu katikati ya ngano, naye akaondoka. Wakati jani lilipoota na kuzaa matunda, magugu yalionekana pia.’ Waandikaji fulani wako na mashaka kama mambo yenye kuzungumuziwa katika mufano huo yalikuwa yanafanyika kabisa, lakini kulingana na maandishi ya zamani ya sheria ya Roma, jambo hilo lingefanyika.

Kamusi moja ya Biblia inasema kama kulingana na sheria ya Roma, kupanda magugu katika shamba la mutu mwengine ili kulipiza kisasi ilikuwa kuvunja sheria. Jambo hilo lilifanyika kabisa kwa sababu kulikuwa sheria yenye kulizungumuzia. Alastair Kerr, mwenye elimu ya mambo ya sheria, alisema kama katika mwaka wa 533 kisha kuzaliwa kwa Yesu, Mutawala wa Roma Justinien alitoa maandishi yake yenye kuitwa Digest. Maandishi hayo yalikuwa kifupi cha sheria ya Roma na yalikuwa na maelezo mbalimbali yenye watu wenye elimu walitoa juu ya sheria hiyo kuanzia mwaka wa 100-250 hivi kisha kuzaliwa kwa Yesu. Kulingana na Digest (Digest, 9.2.27.14), Ulpian, mumoja wa watu hao wenye elimu, alizungumuzia jambo moja lenye lilifanyika kati ya mwaka wa 101 na 200. Magugu yalikuwa yamepandwa katika shamba la mutu fulani na hilo liliharibu mimea. Digest inazungumuzia haki za mwenye shamba zenye zingemuruhusu apate malipo kutoka kwa mutu mwenye alipanda magugu, ni kusema, feza kwa ajili ya mimea yenye iliharibika.

Mambo hayo yalifanyika katika Utawala wa zamani wa Roma; hilo linaonyesha kama mambo yenye kuzungumuziwa katika mufano wa Yesu yalifanyika kabisa.

TAREHE 12-18/02

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 14-15

“Kulisha Watu Wengi Kupitia Wachache”

w13 15/7 uku. 15 fu. 2

Kulisha Watu Wengi Kupitia Wachache

Wakati anaona kikundi cha watu, Yesu anawasikilia huruma, kwa hiyo anaponyesha wagonjwa wenye kuwa kati yao na anawafundisha mambo mengi kuhusu Ufalme wa Mungu. Wakati usiku unakuwa karibu kuingia, wanafunzi wake wanamuomba awaache watu waende kwenye vijiji vya pembeni-pembeni ili wajinunulie chakula. Lakini Yesu anawaambia wanafunzi wake hivi: ‘Ninyi muwape chakula.’ Pengine maneno hayo yanawashangaza sana wanafunzi wake, kwa sababu wako na chakula kidogo sana, mikate tano na samaki mbili kidogo-kidogo.

w13 15/7 uku. 15 fu. 3

Kulisha Watu Wengi Kupitia Wachache

Yesu anawasikilia huruma; kwa hiyo, anafanya muujiza: huo ndio muujiza moja tu wenye waandikaji wote ine wa Injili wanazungumuzia. (Mk 6:35-44; Lu 9:10-17; Yoh 6:1-13) Yesu anawaambia wanafunzi wake waambie watu wakae kwenye majani mabichi na wajipange vikundi-vikundi vya watu 50 na vya watu 100. Kisha kutoa sala ya shukrani, Yesu anaanza kugawanya mikate na samaki. Kuliko kuwapa watu chakula yeye mwenyewe, Yesu anawapatia ‘wanafunzi, nao wanafunzi wanaugawia ule umati [kikundi cha watu].’ Kwa njia ya muujiza, chakula kinakuwa kingi kuliko watu! Fikiria kidogo: Yesu analisha maelfu ya watu kupitia wachache, ni kusema, wanafunzi wake.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 14:21

bila kuhesabia wanamuke na watoto wadogo: Kati ya waandikaji ine wa Injili, ni Mathayo tu ndiye anataja wanamuke na watoto wadogo wakati anafasiria muujiza huu. Inawezekana watu wote wenye walilishwa kwa njia ya muujiza walikuwa zaidi ya 15 000.

w13 15/7 uku. 15 fu. 1

Kulisha Watu Wengi Kupitia Wachache

WAZIA jambo hili. (Soma Mathayo 14:14-21.) Ni siku chache tu mbele ya Pasaka ya mwaka wa 32. Wanaume karibu 5 000 bila kuhesabia wanamuke na watoto wadogo, wanamufuata Yesu na wanafunzi wake karibu na Bethsaida, kijiji chenye kuwa upande wa kaskazini pembeni ya Bahari ya Galilaya.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 15:7

wanafiki: Neno la Kigiriki hy·po·kri·tesʹ lilitumiwa kwanza kuhusu wachezaji Wagiriki (na kisha Waroma) wenye, kwenye jukwaa, walivaa vitu fulani vikubwa-vikubwa kwenye uso ili kuongeza sauti zao. Kisha wakati fulani, neno hilo lilianza kutumiwa kwa njia ya mufano kuhusu kila mutu mwenye alificha kusudi zake za kweli ao tabia yake kwa kutenda kwa udanganyifu ao kwa unafiki. Hapa, Yesu anaita viongozi wa dini ya Kiyahudi “wanafiki.”​—Mt 6:5, 16.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 15:26

watoto . . . imbwa wadogo: Kwa sababu imbwa hawakuwa safi kulingana na Sheria ya Musa, mara nyingi Maandiko ilitumia maneno hayo ili kuonyesha zarau. (Law 11:27; Mt 7:6; Flp 3:2; Ufu 22:15) Lakini, wakati Marko (7:27) na Mathayo wanafasiria mazungumuzo ya Yesu, wanatumia maneno yenye kumaanisha “imbwa mudogo” ao “imbwa wa nyumbani,” ili kupunguza ukali wa ulinganifu huo. Hilo linaonyesha kama, pengine Yesu alitumia neno la muzuri lenye watu wa mataifa walikuwa wanatumia ili kutaja imbwa wao wa nyumbani. Kwa kulinganisha Waisraeli na “watoto,” na watu wa mataifa na ‘imbwa wadogo,’ ni wazi kama Yesu alipenda kuonyesha ni nani alipaswa kuhangaikiwa kwanza. Katika familia zenye zilikuwa na imbwa na watoto, ni watoto walipaswa kula kwanza.

TAREHE 19-25/02

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 16-17

“Uko na Mawazo ya Nani?”

w07 15/2 uku. 16 fu. 17

Wanaume, Mutambue Ukichwa wa Kristo

Wakati mwengine, Yesu alielezea mitume wake kama ni lazima aende Yerusalemu, kwenye angeteswa na ‘wanaume wazee na wakubwa wa makuhani na waandishi, na kuuawa, na siku ya tatu afufuliwe.’ Wakati Petro alisikia hivyo alimuchukua Yesu pembeni na kuanza kumukemea hivi: ‘Ujitendee kwa fazili, Bwana; wewe hautapatwa hata kidogo na jambo hili.’ Ni wazi kama mawazo ya Petro ilichochewa mubaya na namna alikuwa anajisikia. Alikuwa na lazima ya kurekebishwa. Kwa hiyo, Yesu akamuambia: ‘Enda nyuma yangu, Shetani! Wewe ni kikwazo kwangu, kwa sababu wewe unafikiri, si fikira za Mungu, bali za wanadamu.’​—Mathayo 16:21-23.

w15 15/5 uku. 13 fu. 16-17

Ukuwe Macho Shetani Anapenda Kukumeza!

Shetani anaweza kudanganya hata watumishi wa Yehova wenye kumutumikia kwa bidii. Kwa mufano, fikiria jambo lenye lilitokea wakati Yesu aliwaambia mitume wake kama watu wanakaribia kumuua. Mutume Petro alikuwa anamupenda Yesu; kwa hiyo, alimuchukua pembeni na kumuambia hivi: ‘Ujitendee kwa fazili [kwa wema], Bwana; wewe hautapatwa hata kidogo na jambo hili.’ Yesu alimujibu waziwazi hivi: ‘Enda nyuma yangu, Shetani!’ (Mt. 16:22, 23) Sababu gani Yesu alimuita Petro “Shetani”? Kwa sababu Yesu alijua jambo lenye lilikuwa karibu kutokea. Saa ilikuwa imekaribia ili kupitia kifo chake atoe zabihu ya ukombozi na kuonyesha kabisa kama Ibilisi ni musema-uongo. Kwa sababu wakati huo ulikuwa wa maana katika historia ya wanadamu, Yesu aliona kama haiko wakati wa ‘kujitendea’ kwa wema. Kama Yesu angeregeza musimamo wake wa kuendelea kuwa macho, Shetani angefurahi sana.

Kwa sababu mwisho wa ulimwengu huu muovu unakaribia, sisi pia tunaishi wakati wa hatari. Shetani anapenda tusiendelee kuwa macho, ni kusema, ‘tujitendee’ kwa wema kwa kutafuta kujulikana katika ulimwengu huu ili tusione kama ni jambo la lazima tutende kwa haraka. Usikubali Shetani akuzuie kuendelea kuwa macho! Kwa hiyo, ‘uendelee kukesha.’ (Mt. 24:42) Shetani anadanganya watu kwamba mwisho wa ulimwengu huu ungali mbali ao kwamba hautakuja hata siku moja. Usiamini uongo huo.

w06 1/4 uku. 23 fu. 9

‘Muende Mukafanye Wanafunzi, Mukiwabatiza’

Namna gani tunaweza kufuata mufano wa Yesu wa kufanya mapenzi ya Mungu? Yesu aliwaambia wanafunzi wake hivi: ‘Mutu yeyote akitaka kunifuata, na ajikane mwenyewe na kuuchukua muti wake wa mateso na kunifuata sikuzote.” (Mathayo 16:24) Hapa Yesu alitaja mambo tatu yenye tunapaswa kufanya. Kwanza, ‘tunajikana’ wenyewe, ni kusema, tunaachana na mielekeo yetu ya uchoyo ya kutokamilika, na tunafuata mashauri na muongozo wa Mungu. Pili, ‘tunachukua muti wetu wa mateso.’ Katika siku za Yesu, muti wa mateso ulimaanisha aibu (haya) na kuteseka. Kwa sababu tuko Wakristo, tunakubali kuteseka kwa ajili ya habari njema. (2 Timotheo 1:8) Hata kama watu wa ulimwengu wanaweza kutucheka ao kutusema mubaya, kama Kristo ‘tunazarau aibu’, na tunapata furaha kwa kujua kama tunamupendeza Mungu. (Waebrania 12:2) Mwishowe, tunamufuata Yesu “sikuzote.”​—Zaburi 73:26; 119:44; 145:2.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 16:18

Wewe ni Petro, na juu ya mwamba huu: Neno la Kigiriki peʹtros linamaanisha “mwamba; jiwe.” Hapa linatumiwa kama jina la mutu (Petro), maana ya Kigiriki ya jina lenye Yesu alimupatia Simoni. (Yoh 1:42) Neno lingine la Kigiriki peʹtra linamaanisha “mwamba,” na linaweza kumaanisha musingi, mwamba, ao kikundi cha miamba. Neno hilo la Kigiriki linapatikana pia katika Mt 7:24, 25; 27:60; Lu 6:48; 8:6; Rom 9:33; 1Kor 10:4; 1Pet 2:8. Inaonekana kama Petro hakujiona kuwa jiwe kwenye Yesu angejenga kutaniko lake, kwa sababu kwenye 1 Petro 2:4-8 aliandika kama Yesu alikuwa ‘jiwe la pembeni la musingi’ lenye lilitabiriwa tangu zamani, lenye Mungu mwenyewe alichagua. Vilevile, mutume Paulo alimutaja Yesu kuwa ‘musingi’ na “mwamba wa kiroho.” (1Kor 3:11; 10:4) Ni wazi kama Yesu alitumia maneno ya usemi, kwa kusema: ‘Weye, mwenye nimeita Petro, ni kusema “Mwamba,” umetambua kabisa kama Kristo ndiye “mwamba huu”, mwenye atakuwa musingi wa kutaniko la Kikristo’

kutaniko: Ni hapa neno la Kigiriki ek·kle·siʹa linaonekana kwa mara ya kwanza. Linatokana na maneno mbili ya kigiriki, ek, ni kusema, “inje ya,” na ka·leʹo, ni kusema, “kuita.” Linatumiwa kwa ajili ya kikundi cha watu wenye wanakutana pamoja kwa kusudi fulani ao ili kufanya kazi fulani. (Ona Maana ya Maneno.) Hapa, Yesu anatabiri kuanzishwa kwa kutaniko la Kikristo, lenye kufanyizwa na Wakristo watiwa-mafuta, wenye kuwa “majiwe yenye kuwa hai,” wenye ‘wanajengwa kuwa nyumba ya kiroho.’ (1Pet 2:4, 5) Neno hilo la Kigiriki linatumiwa mara nyingi katika tafsiri ya Septante ili kumaanisha neno la Kiebrania lenye kutafsiriwa “kutaniko,” lenye mara nyingi linamaanisha taifa muzima la watu wa Mungu. (Kum 23:3; 31:30) Kwenye Matendo 7:38, Waisraeli wenye walikombolewa kutoka Misri wanaitwa “kutaniko.” Vilevile, Wakristo wenye ‘wanaitwa kutoka katika giza’ na ‘kuchaguliwa kutoka ulimwenguni’ wanafanyiza “kutaniko la Mungu.”​—1Pet 2:9; Yoh 15:19; 1Kor 1:2.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 16:19

funguo za Ufalme wa mbinguni: Katika Biblia, wale wenye walikuwa wanapewa funguo, ikuwe za kweli ao za mufano, walikuwa wanapewa mamlaka fulani. (1Nya 9:26, 27; Isa 22:20-22) Kwa hiyo, neno “funguo” lilifikia kumaanisha mamlaka ao madaraka. Petro alitumia “funguo” hizo zenye alipewa ili kuwatolea Wayahudi (Mdo 2:22-41), Wasamaria (Mdo 8:14-17), na watu wa mataifa (Mdo 10:34-38) nafasi ya kupokea roho takatifu ya Mungu yenye ingewawezesha kuingia katika Ufalme wa mbinguni.

TAREHE 26/02–4/03

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 18-19

“Epuka Kukwazika na Kukwaza Wengine”

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 18:6, 7

jiwe la kusagia lenye linazungushwa na punda: Ao “jiwe kubwa la kusagia.” Neno kwa neno “jiwe la kusagia la punda.” Pengine jiwe hili la kusagia lenye lilikuwa na urefu wa metre 1.20 mupaka 1.50 muviringo, lilikuwa muzito sana; kwa hiyo, lilipaswa kuzungushwa na punda.

vikwazo: Inasemekana kama maana ya kwanza ya neno la Kigiriki skanʹda·lon, lenye kutafsiriwa “kikwazo,” ilikuwa mutego; watu wengine wanasema kama ilikuwa fimbo (muti) kwenye walifungia chambo katika mutego. Tena, neno hilo lilifikia kumaanisha kitu chochote chenye kingefanya mutu ajikwae ao aanguke. Katika njia ya mufano, linamaanisha tendo ao hali yenye inamupeleka mutu katika njia ya mubaya, ni kujikwaa ao kuanguka, ao ni kuangukia katika zambi. Katika Mathayo 18:8, 9, neno lenye kufanana na hilo skan·da·liʹzo, lilitafsiriwa “kukwaza,” linaweza pia kutafsiriwa “kuwa mutego; kufanya mutu atende zambi.”

nwtsty picha na video

Jiwe la kusagia

Majiwe ya kusagia ilitumiwa ili kuponda mbegu na kutoa mafuta ya mizeituni (olives). Majiwe fulani haikukuwa kubwa na ilitumiwa kwa mukono, lakini ingine ilikuwa kubwa sana na iliomba kutumia munyama ili kuizungusha. Inawezekana jiwe la kusagia lenye Wafilisti walimukaza Samsoni azungushe lilikuwa kubwa sana kama hili. (Amu 16:21) Tabia ya kusaga mbegu kwa kutumia wanyama ilijulikana sana katika Israeli na katika Utawala wote wa Waroma.

Jiwe la Juu la Kusagia na Jiwe la Chini la Kusagia

Jiwe kubwa la kusagia kama lile lenye kuonyeshwa hapa lingeweza kuzungushwa na munyama wa kufuga, kama vile punda, na lingetumiwa ili kuponda mbegu ao mizeituni. Jiwe la juu la kusagia lingeweza kufikia urefu wa metre 1.50 muviringo na lingeweza kuzungushwa juu ya jiwe kubwa sana la chini la kusagia.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 18:9

Gehena: Neno “Gehena” linatokana na neno la Kiebrania geh hin·nomʹ, “bonde la Hinomu” lenye lilikuwa kusini-mangaribi mwa Yerusalemu ya zamani. (Ona Nyongeza B12, karte “Yerusalemu na Eneo la Pembeni-pembeni.”) Wakati wa Yesu, bonde hilo lilikuwa mahali pa kulunguzia uchafu; kwa hiyo, neno “Gehena” lilikuwa mufano wenye kufaa wa uharibifu wa milele.

nwtstg Maana ya Maneno

Gehena

Jina la Kigiriki la Bonde la Hinomu, lenye lilikuwa upande wa kusini-mangaribi mwa Yerusalemu ya zamani. (Yer 7:31) Ilitabiriwa kama maiti mbalimbali ingetupwa mahali hapo. (Yer 7:32; 19:6) Hakuna ushuhuda hata moja wenye kuonyesha kama watu na wanyama wazima walikuwa wanatupwa katika Gehena ili kulunguzwa ao kuteswa. Kwa hiyo, Gehena haifananishe mahali fulani penye hapaonekane penye nafsi za wanadamu zinateswa milele katika moto wa kweli. Lakini, Yesu na wanafunzi wake walitumia neno Gehena ili kufananisha malipizi ya milele ya “kifo cha pili,” ni kusema, uharibifu wa milele, kuharibiwa kabisa-kabisa.​—Ufu 20:14; Mt 5:22; 10:28.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 18:10

wanaangalia uso wa Baba yangu: Ao “wanamukaribia Baba yangu.” Kwa sababu wanaweza kumukaribia Mungu mwenyewe, ni viumbe wa roho tu ndio wanaweza kuona uso wa Mungu.​—Kut 33:20.

w10 1/11 uku. 16

Viumbe wa Roho Wana Uvutano Gani Juu Yetu?

Yesu alionyesha kama malaika wamepewa daraka la kuwasaidia watumishi wa Mungu wakuwe na hali ya muzuri kiroho. Ndiyo sababu, wakati aliwashauria wanafunzi wake kuhusu kuwakwaza wengine, alisema hivi: ‘Angalieni musimuzarau mumoja wa hawa wadogo; kwa maana ninawaambia ninyi kwamba malaika zao mbinguni sikuzote wanauona uso wa Baba yangu aliye mbinguni.’ (Mathayo 18:10) Yesu hakumaanisha kama kila mutu iko na malaika mulinzi wake mwenye anamulinda. Lakini alionyesha kama malaika, wenye wanafanya kazi pamoja na Yehova wanapendezwa sana na Wakristo wa kweli.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 18:22

mara makumi saba na saba (77): Neno kwa neno “makumi saba saba.” Tunaweza kuelewa maneno haya ya Kigiriki kuwa “makumi saba (70) na saba (7),” ni kusema, (mara 77) ao “Makumi saba (70) mara saba (7),” ni kusema (mara 490). Maneno hayo yenye inapatikana pia katika tafsiri ya Septante kwenye Mwanzo 4:24 inatoa maana ya Kiebrania “mara makumi saba na saba (77).” Iwe tunaielewa namna gani, kurudilia namba 7 kulilingana na hesabu “yenye kuendelea” ao “yenye haina mipaka.” Kwa kusema mara 77 kuliko mara 7, Yesu hakukuwa anaambia wanafunzi wake waamue ni mupaka mara ngapi wangeweza kusamehe. Lakini, Talmud ya Wababiloni (Yoma 86b) inasema hivi: “Kama mutu anafanya kosa mara ya kwanza, ya pili, na ya tatu, atasamehewa; lakini mara ya ine hatasamehewa.”

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 19:7

cheti cha kumufukuza: Ao “cheti cha kuvunja ndoa.” Kwa kuomba mwanaume mwenye alikuwa anapanga kuvunja ndoa atayarishe cheti kulingana na sheria na pengine azungumuze na wazee, ilikuwa kumupatia wakati wa kufikiria tena uamuzi huo muzito sana. Ni wazi kama kusudi la Sheria ilikuwa kuepusha watu wavunje ndoa mbio-mbio na kutolea wanamuke ulinzi fulani wenye kujulikana na sheria. (Kum 24:1) Lakini wakati wa Yesu, viongozi wa dini walikuwa wamefanya ikuwe mwepesi sana kuvunja ndoa. Mwanahistoria wa wakati wa mitume mwenye kuitwa Yosefo, Mufarisayo mwenye alikuwa amevunja ndoa yake, alisema kama watu waliruhusiwa kuvunja ndoa “kwa sababu yoyote (na wanaume ndio walikuwa wanaleta sababu nyingi).”

nwtsty picha na video

Cheti cha Kuvunja Ndoa

Cheti hicho cha kuvunja ndoa, cha mwaka wa 71 ao 72, kiliandikwa katika luga ya Kiaramu. Kilipatikana upande wa kaskazini wa Wadi Murabbaat, mutoni wenye kukauka katika jangwa la Yuda. Cheti hicho kinasema kama katika mwaka wa sita wa kuasi kwa Wayahudi, Yosefu, mutoto wa Naqsan, alivunja ndoa yenye alifanya na Miriamu, mutoto mwanamuke wa Yonathani, mwenye alikuwa anaishi huko Masada.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine