Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 2-8/04
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 26
“Mambo Yenye Kufanana na Yenye Kutofautiana Kati ya Pasaka na Ukumbusho”
(Mathayo 26:17-20) Siku ya kwanza ya Mikate Yenye Haina Chachu, wanafunzi wakakuja mahali Yesu alikuwa, na kusema: “Ni mahali gani unataka tukutayarishie ukule Pasaka?” 18 Akasema: “Muende katika muji kwa Fulani-wa-fulani na mumuambie, ‘Mwalimu anasema: “Wakati wangu wenye uliwekwa umekaribia; nitafanya sikukuu ya Pasaka pamoja na wanafunzi wangu katika nyumba yako.”’” 19 Basi wanafunzi wakafanya kama vile Yesu aliwaagiza, na wakafanya matayarisho ya Pasaka. 20 Wakati ilikuwa mangaribi, Yesu alikuwa amekaa kwenye meza pamoja na wale wanafunzi kumi na mbili (12).
nwtsty picha na video
Chakula cha Pasaka
Vitu vya lazima sana kwenye Pasaka ilikuwa: nyama ya kondoo ya kuchoma (mifupa ya kondoo haikupaswa kuvunjwa) (1); mukate wenye haukutiwa chachu (levure) (2); na mboga za majani za uchungu (3). (Kut 12:5, 8; Hes 9:11) Kulingana na maandishi ya Mishnah, pengine mboga hizo za majani za uchungu zilikumbusha Waisraeli mateso makali yenye walipata wakati walikuwa katika utumwa huko Misri. Yesu alitumia mukate wenye haukutiwa chachu ili kufananisha mwili wake wenye haukukuwa na zambi. (Mt 26:26) Na mutume Paulo alimuita Yesu mwana-kondoo wetu wa Pasaka. (1Kor 5:7) Wakati wa mitume, divai (4) ilikuwa pia kati ya vitu vyenye vilitumiwa kwenye chakula cha Pasaka. Yesu alitumia divai ili kufananisha damu yake, yenye ingemwangwa kuwa zabihu.—Mt 26:27, 28.
(Mathayo 26:26) Wakati waliendelea kula, Yesu akakamata mukate, na kisha kutoa baraka, akauvunja, akaupatia wanafunzi na kusema: “Mukamate, mukule. Huu unamaanisha mwili wangu.”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 26:26
unamaanisha: Neno la Kigiriki e·stinʹ (lenye kutafsiriwa neno kwa neno “ni”) hapa liko na maana ya “onyesha; fananisha; maana yake; wakilisha.” Mitume walijua maana ya neno hilo, kwa sababu wakati huo mwili wa Yesu wenye haukukuwa na zambi ulikuwa mbele yao na pia mukate wenye haukutiwa chachu wenye walikuwa karibu kula. Kwa hiyo, mukate haungekuwa mwili wake wa nyama. Ni muzuri kuona kama neno hilohilo la Kigiriki linatumiwa katika Mathayo 12:7, na tafsiri nyingi za Biblia zinalitafsiri “unamaanisha.”
(Mathayo 26:27, 28) Na akakamata kikombe, akatoa shukrani, na kuwapatia, na kusema: “Mukunywe ninyi wote divai yenye kuwa ndani, kwa maana hii inamaanisha ‘damu yangu ya agano,’ yenye itamwangwa kwa ajili ya wengi kwa musamaha wa zambi.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 26:28
damu ya agano: Zabihu ya Yesu ndiyo ilifanya agano jipya kati ya Yehova na Wakristo watiwa-mafuta ianze kutumika. (Ebr 8:10) Hapa Yesu anatumia maneno ileile yenye Musa alitumia wakati alikuwa mupatanishi na wakati aliwapatia Waisraeli agano la Sheria kwenye Mulima Sinai. (Kut 24:8; Ebr 9:19-21) Kama vile tu damu ya ngombe na mbuzi ilifanya agano la Sheria kati ya Mungu na taifa la Israeli lianze kutumika, damu ya Yesu ilifanya agano jipya kati ya Yehova na Israeli wa kiroho lianze kutumika. Agano hilo lilianza kutumika kwenye Pentekoste ya mwaka wa 33.—Ebr 9:14, 15.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 26:17
Siku ya kwanza ya Mikate Yenye Haina Chachu: Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu ilianza tarehe 15 Nisani, siku yenye kufuata Pasaka (tarehe 14 Nisani), na ilifanya siku saba. (Ona Nyongeza B15.) Lakini, wakati wa Yesu, Pasaka ilifikia kufanana sana na Siku ya kwanza ya Mikate Yenye Haina Chachu hivi kwamba, kisha kila siku munane, hata kisha tarehe 14 Nisani, mara nyingi ilikuwa inaitwa “Sikukuu ya Mikate Yenye Haina Chachu.” (Lu 22:1) Hapa, maneno “siku ya kwanza ya” inaweza kutafsiriwa “Siku yenye ilitangulia.” (Linganisha na Yoh 1:15, 30, kwenye neno la Kigiriki [proʹtos] lenye kutafsiriwa “kwanza” liko na maana ya “mbele” katika hali yenye kufanana na hiyo, ni kusema, “aliishi mbele [proʹtos] yangu.”) Kwa hiyo, Kigiriki cha zamani, na pia desturi ya Wayahudi, viliruhusu wanafunzi kuuliza Yesu ulizo hilo tarehe 13 Nisani. Muchana wa tarehe 13 Nisani, wanafunzi walifanya matayarisho kwa ajili ya Pasaka, yenye ilifanywa “wakati ilikuwa mangaribi” mwanzoni mwa tarehe 14 Nisani.—Mk 14:16, 17.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 26:39
kikombe hiki kipite mbali na mimi: Katika Biblia, mara nyingi neno “kikombe” linatumiwa kwa njia ya mufano ili kumaanisha mapenzi ya Mungu, ao “mugao wenye kutolewa,” kwa mutu fulani. (Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 20:22.) Ni wazi kwamba Yesu alihangaikia sana matokeo yenye kifo chake kingeleta juu ya jina la Mungu, kwa sababu angekufa kisha kushitakiwa kuwa amemutukana Mungu na amevuruga watu. Jambo hilo lilimufanya asali na kusema “kikombe hiki” kipite mbali naye.
TAREHE 9-15/04
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATHAYO 27-28
“Muende, na Mufanye Wanafunzi—Sababu Gani, Wapi, na Namna Gani?”
w04 1/7 uku. 8 fu. 4
‘Muende, na Mufanye Wanafunzi’
Yesu iko na mamlaka juu ya kutaniko lake, na tangu mwaka wa 1914 amekuwa na mamlaka juu ya Ufalme wa Mungu wenye ulisimamishwa hivi karibuni. (Wakolosai 1:13; Ufunuo 11:15) Yeye ni malaika mukubwa na kwa hiyo iko na mamlaka juu ya jeshi la mbinguni la mamia ya mamilioni ya malaika. (1 Wathesalonike 4:16; 1 Petro 3:22; Ufunuo 19:14-16) Baba yake amemupatia mamlaka ili kuangamiza ‘serikali zote na mamlaka yote na nguvu zote’ zenye zinapinga kanuni za haki. (1 Wakorintho 15:24-26; Efeso 1:20-23) Mamlaka ya Yesu haiko tu juu ya wale wenye kuwa wazima. Pia ni mwamuzi wa wenye kuwa wazima na wafu, na iko na nguvu zenye Mungu alimupatia ili kufufua wale wenye wamelala usingizi katika kifo. (Matendo 10:42; Yohana 5:26-28) Bila shaka, amri yenye kutolewa na Mutu mwenye alipewa mamlaka makubwa kama hayo inapaswa kukamatwa kwa uzito sana. Kwa hiyo, tunatii kwa heshima na kwa kujipendea amri ya Kristo ya ‘kuenda na kufanya wanafunzi.’
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 28:19
mufanye wanafunzi: Kitenzi cha Kigiriki ma·the·teuʹo kinaweza kutafsiriwa “kufundisha” na kusudi la kufanya wanafunzi ao wafuasi. (Linganisha na namna linatumiwa katika Mathayo Mt 13:52, kwenye linatafsiriwa “mwenye kufundishwa.”) Maneno “muwabatize” na “muwafundishe” inaonyesha maana ya amri “mufanye wanafunzi.”
watu wa mataifa yote: Maneno haya inatafsiriwa neno kwa neno “mataifa yote;” lakini hapa, inamaanisha watu kutoka mataifa yote, kwa sababu neno la Kigiriki “wa” katika maneno muwabatize linamaanisha watu wanaume, hapana neno “mataifa,” lenye katika Kigiriki linaweza kumaanisha wanaume ao wanamuke. Amri hiyo ya kukutana na “watu wa mataifa yote” ilikuwa mupya. Mbele Yesu aanze kazi yake ya kuhubiri, Maandiko inaonyesha kama watu wa Mataifa walikaribishwa katika Israeli kama walikuja kumutumikia Yehova. (1Fal 8:41-43) Lakini, kulingana na amri hii, Yesu anaamuru wanafunzi wake waeneze kazi ya kuhubiri hata kwa watu wenye hawakukuwa Wayahudi, na hivyo kukazia kazi ya kufanya wanafunzi katika dunia yote.—Mt 10:1, 5-7; Ufu 7:9; ona kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 24:14.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 28:20
muwafundishe: Neno la Kigiriki lenye kutafsiriwa “kufundisha” linamaanisha pia elimu, mafasirio, kuonyesha mambo kwa kusadikisha, na kutoa ushuhuda. (Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 3:1; 4:23.) kuwafundisha kushika mambo yote yenye Yesu alikuwa ameamuru ingekuwa kazi yenye kuendelea, yenye ingemaanisha pia kufundisha mambo yenye alifundisha, kutumikisha mafundisho yake, na kufuata mufano wake.—Yoh 13:17; Efe 4:21; 1Pet 2:21.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 27:51
pazia: Nguo hii ya muzuri sana ya kupamba nayo iligawanya sehemu mbili za hekalu, ni kusema, Patakatifu na Patakatifu Zaidi. Desturi za Wayahudi zinaonyesha kama pazia hiyo kubwa ilikuwa na urefu wa metre 18 hivi, upana wa metre 9 hivi, na unene wa sentimetre 7 hivi. Kwa kugawanya pazia hiyo katika sehemu mbili, Yehova anaonyesha kasirani yake kubwa juu ya watu wenye waliua Mutoto yake, lakini kunamaanisha pia kama inawezekana sasa kuingia katika mbingu yenyewe.—Ebr 10:19, 20; ona Maana ya Maneno.
patakatifu: Hapa neno la Kigiriki na·osʹ linamaanisha chumba cha katikati cha hekalu pamoja na Patakatifu na Patakatifu Zaidi.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 28:7
muambie wanafunzi wake kwamba amefufuliwa: Wanamuke hao ni wanafunzi wa kwanza wenye walijulishwa juu ya kufufuka kwa Yesu; lakini pia ni wao walipewa daraka la kujulisha wanafunzi wengine. (Mt 28:2, 5, 7) Kulingana na desturi za Wayahudi zenye hazikupatana na Maandiko, mwanamuke hakuruhusiwa kushuhudia mbele ya tribinali. Lakini, malaika wa Yehova alionyesha wanamuke hao heshima kwa kuwapatia mugao huo wenye kuleta furaha.
TAREHE 16-22/04
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MARKO 1-2
“Zambi Zako Zimesamehewa”
“Zambi Zako Zimesamehewa”
Wakati Yesu iko anafundisha katika chumba chenye kujaa watu, wanaume ine wanakuja na mwanaume mwenye kupooza juu ya kitanda. Wanapenda Yesu aponyeshe rafiki yao. Lakini, kwa sababu ya watu wengi, wanashindwa “kumupeleka moja kwa moja kwenye Yesu alikuwa.” (Marko 2:4) Wazia namna walivunjika moyo sana. Wanapanda juu ya sehemu ya juu ya nyumba na kutoboa tundu. Kisha wanateremusha kitanda chenye kuwa na mwanaume huyo mwenye kupooza ndani ya nyumba.
Je, Yesu anakasirika kwa sababu wanamukatiza mazungumuzo? Hapana, kabisa! Anashangazwa sana na imani yao na anaambia mwanaume huyo mwenye kupooza hivi: “Zambi zako zimesamehewa.” (Mathayo 9:2) Lakini, Yesu anaweza kabisa kusamehe zambi? Waandishi na Wafarisayo wanapinga maneno yake, na wanaambiana hivi: “Sababu gani mutu huyu anasema namna hii? Anamutukana Mungu. Ni nani anaweza kusamehe zambi isipokuwa mumoja tu, Mungu?”—Marko 2:7.
Yesu anatambua mawazo yao, na kuwaambia hivi: “Sababu gani munawaza mambo haya katika mioyo yenu? Ni jambo gani lenye kuwa mwepesi zaidi, kumuambia mutu mwenye kupooza, ‘Zambi zako zimesamehewa,’ ao kusema, ‘Simama, kamata kitanda chako na utembee’?” (Marko 2:8, 9) Ndiyo, kwa musingi wa zabihu ya ukombozi yenye Yesu atafikia kutoa, anaweza kusamehe zambi za mwanaume huyo.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mk 2:9
Ni jambo gani lenye kuwa mwepesi zaidi: Ingekuwa mwepesi kwa mutu fulani kusema kama angesamehe zambi, kwa sababu hakungekuwa ushuhuda wenye kuonekana ili kuhakikisha maneno yake. Lakini kusema, Simama . . . na uende kuliomba muujiza wenye ungeonyesha watu wote kama Yesu alikuwa na mamlaka ya kusamehe zambi. Habari hiyo na Isaya 33:24 inaonyesha kama magonjwa inatokana na hali yetu ya kuwa watenda-zambi.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mk 1:11
sauti ikatokea mbinguni: Mara ya kwanza kati ya mara tatu katika Injili mahali Yehova anazungumuza moja kwa moja na wanadamu.—Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Mk 9:7; Yoh 12:28.
Wewe ni Mwana wangu: Kwa sababu ni kiumbe wa roho, Yesu alikuwa Mutoto wa Mungu. (Yoh 3:16) Kuanzia wakati alizaliwa kama mwanadamu, Yesu alikuwa “mwana wa Mungu” kama vile tu mukamilifu Adamu alikuwa. (Lu 1:35; 3:38) Lakini, inaeleweka hapa kama maneno ya Mungu inamaanisha mengi zaidi kuliko tu kumutambulisha Yesu. Kupitia maneno hayo na kushushwa kwa roho takatifu, Mungu alionyesha kama Yesu alizaliwa kama Mutoto Wake wa kiroho, ‘alizaliwa tena’ na tumaini la kuishi tena mbinguni na kutiwa mafuta kwa roho ili kuwa Mufalme na Kuhani Mukubwa mwenye kukubaliwa na Mungu.—Linganisha na Yohana 3:3-6; 6:51; Lu 1:31-33; Ebr 2:17; 5:1, 4-10; 7:1-3.
Nimekukubali: Ao “Ninapendezwa sana na wewe; Ninakufurahia sana.” Maneno hayo inatumiwa katika Mathayo 12:18, yenye ilichukuliwa katika Isaya 42:1 kuhusu Masiya mwenye aliahidiwa, ao Kristo. Kushushwa kwa roho takatifu na maneno yenye Mungu alisema juu ya Mutoto wake ilionyesha wazi kama Yesu ndiye Masiya mwenye aliahidiwa.—Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 3:17; 12:18.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mk 2:28
Bwana . . . wa Sabato: Yesu anatumia maneno hayo kwake mwenyewe (Mt 12:8; Lu 6:5) ili kuonyesha kama angetumia Sabato ili kufanya kazi yenye Baba yake wa mbinguni alimuomba afanye. (Linganisha na Yohana 5:19; 10:37, 38.) Siku ya Sabato, Yesu alifanya miujiza fulani kati ya miujiza yake mikubwa sana; katika muujiza moja, aliponyesha mugonjwa. (Lu 13:10-13; Yoh 5:5-9; 9:1-14) Hilo lilionyesha mbele ya wakati kitulizo chenye atatolea watu katika utawala wake, wenye utakuwa kama mapumuziko ya siku ya Sabato.—Ebr 10:1.
TAREHE 23-29/04
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MARKO 3-4
“Kuponyesha Mutu Siku ya Sabato”
Ni Nini Inaruhusiwa Kufanya Siku ya Sabato?
Kwenye siku ingine ya Sabato, Yesu anaenda kwenye sinagogi fulani, pengine katika Galilaya. Huko anakuta mwanaume mumoja mwenye kuwa na mukono wenye kukauka. (Luka 6:6) Waandishi na Wafarisayo wako wanaangalia Yesu kwa uangalifu. Sababu gani? Wanaonyesha waziwazi mawazo yao wakati wanauliza hivi: “Je, inaruhusiwa kuponyesha siku ya Sabato?”—Mathayo 12:10.
Viongozi wa dini ya Kiyahudi wanaamini kuwa kuponyesha mutu kunaruhusiwa siku ya Sabato ikiwa tu uzima uko katika hatari. Kwa mufano, hairuhusiwe siku ya Sabato kuunganisha mufupa ao kufunga sehemu yenye kuteguka, hali zenye hazitie uzima katika hatari. Kwa kweli, waandishi na Wafarisayo hawaulize Yesu maulizo kwa sababu wanahangaikia kabisa mateso ya mwanaume huyo. Wako wanajikaza kupata visababu ili kumuhukumu Yesu.
Ni Nini Inaruhusiwa Kufanya Siku ya Sabato?
Lakini, Yesu anajua mawazo yao ya mubaya. Anatambua kama wamekuwa na mawazo yenye kuvuka mipaka na yenye haitegemee Maandiko kuhusu kuvunja sheria yenye kukataza kufanya kazi siku ya Sabato. (Kutoka 20:8-10) Amekwisha kulaumiwa bila sababu juu ya matendo yake ya muzuri. Sasa Yesu anafanya jambo lenye litatokeza mabishano makubwa kwa kuambia ule mutu mwenye kuwa na mukono wenye kupooza hivi: “Simama na ukuje katikati.”—Marko 3:3.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mk 3:5
kwa kasirani, akiwa amehuzunika sana: Ni Marko tu ndiye anaeleza namna Yesu alijisikia wakati anaona mioyo migumu ya viongozi wa dini wakati huo. (Mt 12:13; Lu 6:10) Pengine ni Petro, mwanaume mwenye hisia nyingi ndiye alimutolea Marko habari zenye kuwa wazi zenye aliandika juu ya kazi za Yesu na namna alijisikia.—Ona “Utangulizi wa Kitabu cha Marko.”
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mk 3:29
anatukana roho takatifu: Kutukana kunamaanisha kuchambua, kuumiza, ao kutumia maneno yenye haifae juu ya Mungu ao juu ya mambo matakatifu. Kwa sababu roho takatifu inatoka kwa Mungu mwenyewe, kuipinga kwa makusudi ao kukataa matendo ya roho hiyo ni kumutukana Mungu. Kama vile inaonyeshwa kwenye Mathayo 12:24, 28 na Marko 3:22, viongozi wa dini ya Kiyahudi waliona roho ya Mungu inatenda ndani ya Yesu wakati alifanya miujiza; lakini, walisema kama nguvu hiyo ilitoka kwa Shetani Ibilisi.
hatia ya zambi ya milele: Pengine maneno haya inahusu zambi ya makusudi yenye kuleta matokeo ya mubaya milele; hakuna zabihu yenye inaweza kufunika zambi hiyo.—Ona kwa ajili ya funzo kuhusu anatukana roho takatifu katika andiko hilo na kwa ajili ya funzo kuhusu Mt 12:31, habari yenye kufanana na hii.
w14 12/15 uku. 12-13 fu. 6-8
Unaelewa “Maana”?
Mufano huo unaweza kutufundisha nini? Kwanza, tunapaswa kutambua kama hatuwezi kumulazimisha mwanafunzi wa Biblia afanye maendeleo ya kiroho. Unyenyekevu utatusaidia tusitafute kumukaza mwanafunzi wa Biblia abatizwe. Tunajikaza kumusaidia mwanafunzi, lakini tunapaswa kuwa wanyenyekevu na kukubali kama ni yeye mwenyewe ndiye anapaswa kuamua kujitoa kwa Yehova katika sala. Mutu anapaswa kuchochewa na upendo wakati anaamua kujitoa kwa Mungu katika sala, na anafanya hivyo kwa kujipendea. Ni jambo hilo tu ndilo Yehova anakubali.—Zab. 51:12; 54:6; 110:3.
Pili, mambo yenye tunajifunza katika mufano huo itatusaidia tusivunjike moyo ikiwa mwanzoni hatupate matokeo katika kazi yetu ya kuhubiri. Ni lazima tuonyeshe uvumilivu. (Yak 5:7, 8) Ikiwa sisi tulifanya yetu yote ili kusaidia mwanafunzi, lakini hafanye maendeleo, tujue kama hilo halimaanishe kama sisi hatujue kufundisha. Yehova anafanya mbegu ya kweli izae matunda katika moyo munyenyekevu wenye utakuwa tayari kufanya mabadiliko. (Mt. 13:23) Kwa hiyo hatupaswe kusema kama kazi yetu ya kuhubiri ni ya muzuri ao hapana kwa sababu tu ya matokeo. Yehova haone kama tumeshindwa kwa sababu wale wenye tunajifunza nao wamekataa kufanya maendeleo. Lakini, anaona bidii yetu kuwa ya lazima sana ikuwe tunapata matokeo ya muzuri ao hapana.—Soma Luka 10:17-20; 1 Wakorintho 3:8.
Tatu, mara nyingi hatutambue mabadiliko yenye kufanyika katika moyo wa mutu. Kwa mufano, mwanaume moja na bibi yake walikuja kumuona misionere moja mwenye alikuwa anajifunza nao na kumuambia kama wanapenda kuwa wahubiri wasiobatizwa. Misionere huyo aliwakumbusha kama ikiwa wanataka kuwa wahubiri, walipaswa kuacha kuvuta tumbako. Lakini alishangaa sana wakati mwanaume huyo na bibi yake walimuambia kama waliacha kuvuta tumbako kumepita miezi mingi. Sababu gani waliacha? Walitambua kama, ikiwa wangeendelea kuvuta, Yehova angewaona na kama anachukia unafiki. Mioyo yao iliwachochea kuchagua kati ya kuvuta mbele ya misionere huyo ao kuachana kabisa na tumbako. Upendo wao kwa Yehova uliwasaidia wachukue uamuzi muzuri. Walifanya maendeleo ya kiroho, hata kama misionere huyo hakuwa anaona mabadiliko yenye ilikuwa inafanyika katika mioyo yao.
TAREHE 30/04–6/05
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MARKO 5-6
“Yesu Iko na Uwezo wa Kufufua Wapendwa Wetu Wenye Wamekufa”
(Marko 5:38) Basi wakafika kwenye nyumba ya ule ofisa-musimamizi wa sinagogi, na akaona watu wenye kuleta fujo sana na wale wenye kulia na kufanya makelele makubwa ya kuomboleza.
(Marko 5:39-41) Kisha kuingia ndani, akawaambia: “Sababu gani munalia na kuleta fujo hivi? Mutoto hakukufa lakini amelala usingizi.” 40 Basi wakaanza kumucheka kwa zarau. Lakini kisha kuwaambia wote waende inje, akamuchukua baba na mama ya ule mutoto pamoja na wale wenye walikuwa pamoja naye, na akaingia mahali kwenye ule mutoto alikuwa. 41 Kisha akakamata mukono wa ule mutoto na kumuambia: “Talita kumi,” maneno yenye wakati yanatafsiriwa yanamaanisha: “Mutoto mwanamuke, ninakuambia, simama!”
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mk 5:39
hakukufa lakini amelala usingizi: Katika Biblia, mara nyingi kifo kinafananishwa na usingizi. (Zab 13:3; Yoh 11:11-14; Mdo 7:60; 1Kor 7:39; 15:51; 1Tes 4:13) Yesu alikuwa karibu kufufua mutoto huyo mwanamuke; kwa hiyo pengine alisema maneno hayo kwa sababu alipenda kuonyesha kwamba, kama vile tu watu wanaweza kuamushwa kutoka katika usingizi muzito, ni vile wanaweza kufufuliwa kutoka katika kifo. Uwezo wa Yesu wa kufufua mutoto huyo mwanamuke ulitoka kwa Baba yake, “mwenye anafanya wafu kuwa wazima na anaita mambo yenye hayako kama vile yako.”—Rom 4:17.
Mutoto Mwanamuke Anaishi Tena!
Katika miujiza mingine yenye Yesu alifanya mbele ya hapo, aliambia watu wenye aliponyesha wasitangaze mambo yenye amefanya; anaambia wazazi hawa hivyohivyo. Hata hivyo, wazazi hao wenye furaha sana na watu wengine wanatangaza habari hiyo “katika eneo hilo lote.” (Mathayo 9:26) Ni wazi kwamba, ikiwa unaona mutu mwenye unapenda anafufuliwa, utakuwa kabisa na furaha ya kuambia wengine juu ya jambo hilo, haiko vile? Huu ndio ufufuo wa pili wenye Yesu anafanya wenye umeandikwa katika vitabu vya Injili.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mk 5:19
uwaelezee: Kwa kawaida kisha kufanya muujiza, Yesu alikataza watu kuitangaza (Mk 1:44; 3:12; 7:36); lakini alimuruhusu mwanaume huyu ajulishe watu wa jamaa yake mambo yenye ilifanyika. Pengine ni kwa sababu walimuomba Yesu aondoke katika eneo hilo na hangeweza kuwatolea ushahidi yeye mwenyewe; ingesaidia pia ili watu wenye walijionea namna kundi la nguruwe lilitawanyika wasitoe ripoti za uongo.
nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Mk 6:11
mukungute mavumbi yenye kuwa kwenye miguu yenu: Kufanya hivyo kulimaanisha kama wanafunzi hawakukuwa na hatia juu ya matokeo yenye Mungu angeleta. Maneno kama hayo inapatikana katika Mathayo 10:14; Luka 9:5. Marko na Luka waliongeza maneno ili kuwa ushahidi juu [ao, “zidi”] yao. Paulo na Barnaba walitumikisha maagizo hayo katika Antiokia ya Pisidia (Mdo 13:51), na wakati Paulo alifanya alama yenye kufanana na hiyo katika Korintho kwa kukunguta mavazi yake, aliongeza maneno haya: “Damu yenu ikuwe juu ya vichwa vyenu. Mimi niko safi.” (Mdo 18:6) Pengine wanafunzi walikuwa wanajua alama hizo; Wayahudi wenye kumuogopa Mungu wenye walikuwa wanasafiri katika eneo la Watu wa Mataifa walikuwa wanakunguta kutoka kwenye viatu vyao kila kitu chenye waliona kuwa kichafu, mbele ya kuingia tena katika eneo la Wayahudi. Lakini, Yesu alikuwa anafikiria mambo mengine wakati alitolea wanafunzi wake maagizo hayo.