MAISHA YA MUKRISTO
Epuka Hatari ya Kutumia Site za Enternete za Kupashana Habari
SABABU GANI NI LAZIMA: Site za enternete za kupashana habari zinaweza kutusaidia ao kutuumiza. Wakristo fulani wameamua kukataa kabisa kutumia site hizo. Wakristo wengine wanazitumia ili kupashana habari na watu wa familia zao na marafiki. Lakini, Ibilisi anapenda tutumie site za kupashana habari bila hekima. Hilo linaweza kutuharibishia sifa na kutuharibishia urafiki wetu pamoja na Yehova. Kama Yesu, tunaweza kutumia kanuni zenye kupatikana katika Neno la Mungu ili kutambua hatari na kuziepuka.—Lu 4:4, 8, 12.
MITEGO YA KUEPUKA:
Kutumia site za enternete za kupashana habari kupita kiasi. Kutumia site za enternete za kupashana habari na vyombo vya kutangaza habari kwa saa murefu kunaweza kuchukua wakati wenye tunapaswa kutumia kwa ajili ya mambo ya kiroho
Kanuni za Biblia: Efe 5:15, 16; Flp 1:10
Kuangalia mambo ya mubaya. Kuangalia mambo ya mubaya kunaweza kuchochea mutu akuwe mutumwa wa ponografia ao afanye uasherati. Kusoma vitabu vya waasi-imani ao habari zao kwenye Enternete kunaweza kuharibu imani ya mutu
Kutia picha ao maelezo ya mubaya kwenye site hizo. Kwa sababu moyo ni mudanganyifu, mutu anaweza kushawishiwa kutia maelezo ya mubaya ao picha za mubaya kwenye site za kupashana habari. Hilo linaweza kuharibishia mutu sifa ao kufanya wengine wakwazike
Kanuni za Biblia: Rom 14:13; Efe 4:29
MUANGALIE VIDEO TUMIA KWA HEKIMA SITE ZA ENTERNETE ZA KUPASHANA HABARI, KISHA MUZUNGUMUZIE NAMNA YA KUEPUKA HALI KAMA HIZI: