Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr18 Mwezi wa 11 uku. 1-5
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2018)
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 5-11/11
  • TAREHE 12-18/11
  • TAREHE 19-25/11
  • TAREHE 26/11–2/12
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2018)
mwbr18 Mwezi wa 11 uku. 1-5

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 5-11/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | YOHANA 20-21

“Unanipenda Kuliko Hawa?”

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 21:15, 17

Yesu akamuuliza Simoni Petro: Hii mazungumuzo kati ya Yesu na Petro ilifanyika wakati fulani kisha Petro kumukatala Yesu mara tatu. Yesu alimuuliza Petro maulizo tatu kwa kukazia ili kuona kadiri gani Petro anamupenda, mupaka “Petro akahuzunika.” (Yoh 21:17) Mu Yoh 21:15-17, Yohana anatumia tendo mbili tofauti za Kigiriki: a·ga·paʹo na phi·leʹo; hizo tendo zote mbili zinatafsiriwa upendo mu Kiswahili. Mara tatu Yesu alimuuliza Petro hivi: “Unanipenda?” Na mara tatu Petro alimuhakikishia Yesu kama anamupenda. Kila mara, wakati Petro alimuhakikishia Yesu kama anamupenda, Yesu alikazia kama ule upendo ndio ungemuchochea Petro alishe na “kuchunga” kiroho wanafunzi wa Yesu, wenye hapa wanaitwa wana-kondoo wa Yesu, ao “kondoo wadogo.” (Yoh 21:16, 17; 1Pe 5:1-3) Yesu alimupatia Petro nafasi ya kuonyesha mara tatu kama anamupenda, na kisha alimupatia daraka la kuhangaikia kondoo. Kwa kufanya vile, Yesu alionyesha wazi kama amemusamehe Petro, mwenye alimukatala mara tatu.

unanipenda kuliko hawa?: Kulingana na sarufi, maneno “kuliko hawa” inaweza kueleweka katika maana mbalimbali. Watu fulani wenye elimu ya Biblia wanapendelea kuitafsiri “unanipenda kuliko namna unawapenda hawa wanafunzi wengine?” ao “unanipenda kuliko namna hawa wanafunzi wananipenda?” Lakini, pengine maana ya kweli ni “unanipenda kuliko vitu hivi (mambo haya)?” ni kusema, samaki zenye walikamata ao mambo yenye kuhusu kuuzisha samaki. Kwa hiyo, pengine wazo kubwa la hii andiko ni: ‘Unanipenda kuliko vitu vya kimwili ao kuliko kufuatilia vitu vya kimwili? Kama ni vile, lisha wana-kondoo wangu.’ Kulingana na maisha ya Petro ya zamani, iliomba kabisa wamuulize vile. Hata kama Petro alikuwa kati ya wanafunzi wa kwanza-kwanza wa Yesu (Yoh 1:35-42), hakumufuata mara moja Yesu wakati wote. Lakini, alirudilia kazi yake ya kuvua samaki. Kisha miezi fulani, Yesu alimuita tena Petro na kumuambia aache kazi ya kuvua samaki ili aanze ‘kuvua watu.’ (Mt 4:18-20; Lu 5:1-11) Tena, wakati fulani tu kisha Yesu kufa, Petro alisema kama anapenda kuenda kuvua samaki, na mitume wengine walimufuata. (Yoh 21:2, 3) Kwa hiyo, pengine hapa Yesu anavuta uangalifu wa Petro ili kumuonyesha kama anapaswa kuchagua kitu kimoja: Kutia kazi ya kuvua samaki pa nafasi ya kwanza mu maisha yake, jambo lenye kufananishwa na furushi ya samaki yenye ilikuwa mbele yao, ao kutia pa nafasi ya kwanza kazi ya kulisha kiroho kondoo wa Yesu, ni kusema, wanafunzi.​—Yoh 21:4-8.

mara ya tatu: Petro alimukatala Bwana wake mara tatu; sasa Yesu anamutolea nafasi ya kuonyesha mara tatu kama anamupenda. Wakati Petro anasema kama anamupenda, Yesu anamuambia aonyeshe upendo huo kwa kutia utumishi mutakatifu pa nafasi ya kwanza. Petro, pamoja na ndugu wengine wenye mamlaka, wangelisha, wangetia nguvu, na kuchunga kundi la Kristo la wanafunzi waaminifu. Wale wanafunzi walikuwa watiwa-mafuta, lakini walikuwa na lazima ya kulishwa kiroho.​—Lu 22:32.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 20:17

Acha kunishika: Tendo la Kigiriki haʹpto·mai linaweza kuwa na maana ya “kugusa” ao “kushika; kushikilia.” Biblia fulani zinatafsiri maneno ya Yesu hivi: “Usiniguse.” Lakini, Yesu hakukuwa anakataza Maria Magdalene amuguse, kwa sababu hakuzuia wanamuke wengine wenye walimuona kisha kufufuliwa “kushika miguu yake.” (Mt 28:9) Inaonekana kama Maria Magdalene aliogopa kwa sababu aliwaza kama Yesu anataka kupanda mbinguni. Kwa sababu alipenda sana kubakia pamoja na Yesu, Bwana wake, akamushika nguvu sana, hakutaka aende. Ili kumuhakikishia kama hajaenda mbinguni, Yesu alimuambia Maria aache kumushika, lakini aende kuwaambia wanafunzi wake kama amefufuliwa.

nwtsty kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 20:28

Bwana wangu na Mungu wangu!: Neno kwa neno, “Bwana wa mimi na Mungu [ho the·osʹ] wa mimi!” Watu fulani wenye elimu ya Biblia wanasema kama Tomasi anaambia Yesu hii maneno ili kuonyesha kama anashangaa, lakini iko anailekezea Mungu, Baba yake. Wengine wanasema kama, kulingana na Kigiriki cha zamani, Tomasi anaelekezea Yesu hii maneno. Hata kama ni vile, maana ya maneno “Bwana wangu na Mungu wangu” inaeleweka muzuri kama tunailinganisha na Maandiko ingine yenye kuongozwa na roho. Kwa sababu habari yenye kuzungumuziwa hapa inasema kama Yesu alikuwa amewatumia wanafunzi ujumbe huu: “Ninapanda kuenda kwa Baba yangu na Baba yenu na kwa Mungu wangu na Mungu wenu,” hakuna sababu ya kusema kama Tomasi alikuwa anaamini kama Yesu ndiye Mungu mweza-yote. (Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 20:17.) Tomasi alisikia Yesu akimuomba “Baba” yake na kumuita “Mungu wa pekee wa kweli.” (Yoh 17:1-3) Kwa hiyo, pengine Tomasi alimuita Yesu “Mungu wangu” kwa sababu hizi: Alimuona Yesu kuwa “mungu,” hapana Mungu mweza-yote. (Ona kwa ajili ya funzo kuhusu Yoh 1:1.) Ao pengine alizungumuza na Yesu namna watumishi wa Mungu walizungumuza na malaika wa Yehova, kama vile inaonyeshwa mu Maandiko ya Kiebrania. Inawezekana Tomasi alijua habari za watu fulani, pengine hata mwandikaji fulani wa Biblia, wenye walijibiaka ao walizungumuzaka na malaika wa Mungu kama vile walikuwa wanazungumuza na Yehova Mungu mwenyewe. (Linganisha na Mwa 16:7-11, 13; 18:1-5, 22-33; 32:24-30; Amu 6:11-15; 13:20-22.) Kwa hiyo, pengine Tomasi alimuita Yesu “Mungu wangu” katika maana hiyo, ili kuonyesha kama anatambua Yesu kuwa mujumbe na musemaji wa Mungu wa kweli.

TAREHE 12-18/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 1-3

“Roho Takatifu Inashuka juu ya Kutaniko la Kikristo”

w86 1/12 uku. 29 fu. 4-5, 7

Michango Yenye Inafurahisha Moyo

Ile ile siku ya kuzaliwa kwa kutaniko la Kikristo mu mwaka wa 33, wale watu 3 000 wenye walibatizwa walianza ‘kufanya mambo yote pamoja, kula pamoja, na kusali pamoja.’ Sababu gani walifanya vile? Kufanya vile kuliwasaidia kutia nguvu imani yao mupya kwa ‘kujitoa kwa fundisho la mitume’​—Matendo 2:41, 42.

Wayahudi na wageuzwa-imani wenye walikuja Yerusalemu walipanga kubakia kule kwa ajili ya Sikukuu ya Pentekoste tu. Lakini wale wenye waligeuka na kuwa Wakristo walipenda kubakia kule wakati murefu zaidi ili kujifunza mambo mingi zaidi na kutia nguvu imani yao mupya. Hii jambo ilifanya kukuwe lazima ya haraka ya chakula na makao. Wageni fulani hawakukuwa na feza za kutosha, lakini wengine walikuwa na feza nyingi. Kwa hiyo, wote walitia vitu vyao pamoja kwa muda, na walivigawanyia wale wenye walikuwa na lazima ya musaada.​—Matendo 2:43-47.

Kuuzisha shamba na makao na kugawanya mali ilikuwa uamuzi wa mutu yeye mwenyewe; hakuna mutu mwenye walilazimisha kuuzisha ao kutoa kitu chake. Haikukuwa pia kuchochea watu ili wakuwe masikini. Wazo haikukuwa kwamba Wakristo matajiri wauzishe vitu vyao vyote ili wakuwe masikini. Kusikilia huruma waamini wenzao wenye walikuwa na lazima ya musaada wakati huo ndio kulichochea Wakristo wauzishe vitu vyao na kutoa feza zote ili kuendelesha faida za Ufalme.​—Linganisha na 2 Wakorinto 8:12-15.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 25 fu. 2

Yesu Kristo

“Kiongozi Mukubwa wa uzima.” Wakati Yesu Kristo alitoa uzima wake mukamilifu, ile ilionyesha fazili zenye hazistahiliwe za Baba yake. Kupitia ile zabihu, wanafunzi wenye Kristo alichagua wangetawala pamoja naye mbinguni, na mipango ingekamatwa kwa ajili ya wanadamu wenye Ufalme wake ungetawala. (Mt 6:10; Yoh 3:16; Efe 1:7; Ebr 2:5; ona RANÇON.) Ni kwa njia hiyo Yesu akakuwa “Kiongozi mukubwa [“prince (mukubwa),” Jé; PB; Sg] wa uzima” kwa ajili ya wanadamu wote. (Mdo 3:15) Maana ya kwanza ya neno la Kigiriki lenye kutumiwa hapa ni “kiongozi mukubwa,” neno lenye kufanana na lile lenye kutumiwa juu ya Musa (Mdo 7:27, 35), “mukubwa” wa Israeli.

cl uku. 265 fu. 14

Mungu Mwenye Iko “Tayari Kusamehe”

14 Andiko ya Matendo 3:19 inaeleza zaidi namna Yehova anasamehe: “Kwa hiyo, mutubu na mugeuke ili zambi zenu zipate kufutwa.” Neno “kufutwa” limetafsiriwa kutokana na tendo la Kigiriki lenye linaweza kuwa na maana ya “kupanguza, . . . kufuta ao kuharibu.” Watu fulani wenye elimu ya Biblia wanasema kama ile maana inaleta wazo la kufuta maandishi. Iliwezekana namna gani? Wino yenye ilitumiwa wakati wa zamani ilitengenezwa kwa kuchanga karbone, kole, na maji. Kisha tu kuandika kupitia ile wino, mutu aliweza kuchukua sifongo (chiffon) yenye kuwa na maji na kufuta kabisa ile maandishi. Hii inatufundisha somo ya muzuri sana juu ya rehema ya Yehova. Wakati anatusamehe zambi zetu, ni kama vile anakamata chiffon na kuzifuta kabisa.

TAREHE 19-25/11

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 4-5

“Waliendelea Kusema Neno la Mungu Bila Woga”

w08 1/9 uku. 15, kisanduku

Namna Wakristo wa Kwanza-Kwanza Waliandika Maandishi Matakatifu

Je, Mitume Hawakujua Kusoma na Kuandika?

Watawala na wanaume wazee wa Yerusalemu “wakati waliona namna Petro na Yohana walikuwa wanasema bila woga, na wakati walitambua kwamba walikuwa watu wenye hawana elimu na watu wa kawaida, wakashangaa.” (Matendo 4:13) Je, kweli mitume hawakujua kusoma na kuandika? Kuhusu hii jambo, kitabu The New Interpreter’s Bible, kinasema hivi: “Inaonekana kama ile maneno ni ya mufano tu, haimaanishe kama Petro [na Yohana] hawakukuwa na elimu na hawangeweza kusoma ao kuandika. Inamaanisha tu kama mitume walikuwa wa hali ya chini sana kuliko wale wenye waliwahukumu.”

w08 15/5 uku. 30 fu. 6

Mambo Makubwa Katika Kitabu cha Matendo

4:13​—Je, Petro na Yohana hawakujua kusoma na kuandika ao hawakukuwa na elimu? Hapana, walikuwa na elimu. Waliitwa “watu wasio na elimu na wa kawaida tu” kwa sababu hawakusoma masomo ya marabi ili kupata elimu ya mambo ya dini.

it-1-F uku. 141 fu. 1

Mutume

Kazi yao mu kutaniko la Kikristo. Mitume walitiwa moyo sana wakati roho takatifu ilishuka juu yao kwenye Pentekoste. Sura tano za kwanza za kitabu cha Matendo zinaonyesha namna walihubiri habari njema na ufufuo wa Yesu kwa ujasiri na uhodari mukubwa hata kama viongozi waliwafunga, waliwapiga, na kuwaogopesha kama watawaua. Siku zenye zilifuata Pentekoste, mitume walipata nguvu kupitia roho takatifu na waliongoza kutaniko la Kikristo bila woga na kukakuwa ongezeko kubwa. (Mdo 2:41; 4:4) Walihubiri kwanza Yerusalemu, kisha kazi yao ikaendelea kuenea mupaka Samaria na ikafika mu sehemu ya mbali zaidi ya dunia ya ile wakati.​—Mdo 5:42; 6:7; 8:5-17, 25; 1:8.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 591 fu. 2

Jiwe Kubwa la Pembe

Zaburi 118:22 inaonyesha kama jiwe lenye wajenzi walikatala lingekuwa “jiwe kubwa la pembe” (ao mu Kiebrania, roʼsh pin·nahʹ). Yesu alitaja unabii huu na alisema kama umetimia juu yake, kwa kujiita “jiwe kubwa la pembe” (ao mu Kigiriki, ke·pha·leʹ go·niʹas, jiwe kubwa la pembe). (Mt 21:42; Mk 12:10, 11; Lu 20:17) Jiwe la juu kabisa la jengo fulani linaonekana sana; ni vile pia kuhusu Yesu Kristo, jiwe la juu la kutaniko la Kikristo lenye kufanyizwa na Wakristo watiwa-mafuta, lenye kulinganishwa na hekalu la kiroho. Mutume Petro alisema pia kama Zaburi 118:22 ilitimia juu ya Kristo, kwa kuonyesha kama alikuwa “jiwe kubwa” lenye watu walikatala, lakini lenye Mungu amechagua ili kuwa “jiwe kubwa la pembe.”​—Mdo 4:8-12; ona pia 1Pe 2:4-7.

w13 1/3 uku. 15 fu. 4

Petro na Anania Walisema Uongo; Tunaweza Kujifunza Somo Gani?

Anania na bibi yake wanauzisha shamba lao ili wapate feza zenye watatumia ili kuwasaidia wanafunzi wapya wenye wametoka tu kubatizwa. Wakati Anania analeta zile feza kwa mitume, anasema kama analeta feza zote zenye alipata wakati waliuzisha shamba. Lakini ni uongo! Anaficha kiasi fulani cha feza! Lakini Mungu anasaidia Petro ajue kama Anania anasema uongo, kwa hiyo Petro anamuambia Anania hivi: “Haukudanganya wanadamu, lakini umemudanganya Mungu.” Pale pale, Anania anaanguka chini na anakufa! Kisha saa tatu hivi, Safira, bibi ya Anania anaingia. Kwa sababu hajue jambo yenye imemupata bwana yake, yeye pia anasema uongo na anaanguka chini na kukufa.

TAREHE 26/11–2/12

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 6-8

“Kutaniko Mupya la Kikristo Linajaribiwa”

bt uku. 41 fu. 17

“Tunapaswa Kumutii Mungu Kuwa Mutawala”

17 Jambo fulani yenye kutia amani ya kutaniko katika hatari ilikuwa imeanza kutokea. Ni jambo gani? Wanafunzi wengi wenye walibatizwa walikuwa wageni Yerusalemu nao walitaka kujifunza mengi mbele warudie kwao. Wanafunzi wenye walikuwa Yerusalemu walitoa michango ya kujipendea ili kuwakulisha wale wageni na kuwatimizia mahitaji ingine. (Matendo 2:44-46; 4:34-37) Kisha, hali ya nguvu ikatokea. Wajane wenye kusema Kigiriki “hawakukuwa wanapewa sehemu yao katika ugawaji wa chakula wa kila siku.” (Matendo 6:1) Lakini, mahitaji ya wajane Waebrania hayakukosa kutimizwa. Kwa hiyo, inaonekana kama tatizo ilikuwa ubaguzi. Ubaguzi iko kati ya matatizo yenye inaleta mugawanyiko mukubwa.

bt uku. 42 fu. 18

“Tunapaswa Kumutii Mungu Kuwa Mutawala”

18 Mitume, wenye walikuwa baraza lenye kuongoza la kutaniko la ile wakati lenye lilikuwa linaendelea kuongezeka, waliona kama haifae ‘kuacha neno la Mungu ili kugawa chakula.’ (Matendo 6:2) Ili kumaliza ile tatizo, waliomba wanafunzi watafute wanaume saba “wenye kujaa roho na hekima,” wenye mitume wangeweza kuweka ili wasimamie “kazi [hiyo] ya lazima.” (Matendo 6:3) Zaidi ya kugawa chakula, pengine walishugulikia pia feza, kununua chakula, na kuandika ripoti ya feza. Ndiyo sababu kulikuwa lazima ya wanaume wenye wanastahili. Wanaume wote wenye walichaguliwa walikuwa na majina ya Kigiriki, pengine ile ingefanya wajane wenye walibaguliwa waone kama watatendewa kwa haki. Kisha kusali na kufikiri sana juu ya mapendekezo yenye ilitolewa, mitume waliweka wanaume hao saba washugulikie “kazi [hiyo] ya lazima.”

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

bt uku. 45 fu. 2

Stefano; “Akiwa Amekubaliwa na Mungu na Akiwa Amejaa Nguvu”

2 Sura ya Stefano inaonekana tofauti kabisa. Wakati waamuzi wanamuangalia sana, wanaona kama uso wake uko “kama uso wa malaika.” (Matendo 6:15) Malaika ni wajumbe wa Yehova Mungu, nao hawana sababu yoyote ya kuogopa; ni watulivu na wenye amani. Ni vile Stefano iko; hata waamuzi hao wenye chuki sana wanaona vile waziwazi. Ni nini inafanya akuwe mutulivu vile?

bt uku. 58 fu. 16

Kutangaza “Habari Njema juu ya Yesu”

16 Leo, Wakristo wako na pendeleo ya kufanya kazi kama ile yenye Filipo alifanya. Mara mingi, wakati wako mu safari wanatumia ile nafasi ili kuwahubiria watu ujumbe wa Ufalme. Katika hali mingi, wakati wanapata mutu mwenye kupendezwa, hawashangae kwa sababu Biblia inaonyesha wazi kama malaika wanaongoza kazi ya kuhubiri ili ule ujumbe ufikie “kila taifa na kabila na luga na watu.” (Ufu. 14:6) Yesu alitabiri kama malaika wangeongoza kazi ya kuhubiri. Katika mufano wa ngano na magugu, Yesu alisema kama wakati wa mavuno, ao umalizio wa mufumo wa mambo, “wavunaji ni malaika.” Pia, alisema kama, wale viumbe wa kiroho “watakusanya kutoka katika Ufalme wake vitu vyote vyenye vinafanya watu wakwazike na pia watu wenye matendo ya kuvunja sheria.” (Mt. 13:37-41) Wakati ule ule, malaika watakusanya watu wenye watariti Ufalme wa mbinguni, kisha watakusanya “kundi kubwa la watu” wa “kondoo wengine,” wenye Yehova anavuta mu tengenezo lake.​—Ufu. 7:9; Yoh 6:44, 65; 10:16.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine