Vichapo Vyenye Kutajwa katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 7-13/01
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 21-22
“Mapenzi ya Yehova Yatendeke”
15 Wakati Paulo alikuwa anaikala na Filipo, mugeni mwengine mwenye kuheshimiwa alifika. Jina yake Agabo. Wale wenye walikuwa wamekusanyika mu nyumba ya Filipo walijua kama Agabo ni nabii; alikuwa ametabiri njaa kubwa wakati wa utawala wa Klaudio. (Mdo. 11:27, 28) Pengine walianza kujiuliza: ‘Juu ya nini Agabo amekuja? Iko na ujumbe gani?’ Wakati walikuwa wanamuangalia sana, alikamata mukaba ya Paulo—kipande kirefu cha nguo chenye mutu anaweza kutia ndani feza na vitu vingine, ile mukaba ilikuwa inafungwa ku kiuno. Agabo akaitumia ili kufunga miguu na mikono yake mwenyewe. Kisha akaanza kuzungumuza. Ujumbe wake ulikuwa muzito: “Roho takatifu inasema hivi, ‘Mwanaume mwenye mukaba huu, Wayahudi watamufunga hivi kule Yerusalemu na kumutia katika mikono ya watu wa mataifa.’”—Mdo. 21:11.
16 Kulingana na ile unabii, ni wazi kwamba Paulo angeenda Yerusalemu. Ile unabii ilionyesha tena kama Wayahudi wangemutia “katika mikono ya watu wa mataifa.” Ile unabii iliwahangaisha sana wale wenye walikuwa pale. Luka anaandika: “Sasa wakati tulisikia vile, sisi na wale wenye walikuwa pale tukaanza kumuomba asipande kuenda Yerusalemu. Kisha Paulo akasema: ‘Sababu gani munalia na kujaribu kuregeza azimio langu? Mukuwe hakika kwamba niko tayari hapana kufungwa tu lakini pia kufa kwa ajili ya jina la Bwana Yesu kule Yerusalemu.’”—Mdo. 21:12, 13.
“Mapenzi ya Yehova Yatendeke”
17 Wazia hali hii: Ndugu fulani, pamoja na Luka, wanamubembeleza Paulo asiende. Wengine wanalia. Wakati anaona vile wanamuhangaikia kwa upendo, Paulo anawaambia kwa upole kama wako ‘wanaregeza azimio lake,’ ao kama vile tafsiri fulani zinasema, wako ‘wanamuvunja moyo.’ Hata vile, hatabadilisha azimio lake, na kama vile ilikuwa wakati alikutana na ndugu wa Tiro, hataacha maombi yao ao machozi yao imufanye abadilishe azimio lake. Lakini, anawaambia juu ya nini anapaswa kuenda. Alionyesha kabisa kama alikuwa na uhodari na kama hangebadilisha azimio lake! Kama vile Yesu alifanya, Paulo ameazimia kabisa kuenda Yerusalemu. (Ebr. 12:2) Haiko kusema Paulo alipenda tu akufe juu ya imani, lakini hata kama angekufa, angeona kama ni pendeleo kufa kwa sababu ya kuwa mufuasi wa Kristo Yesu.
“Mapenzi ya Yehova Yatendeke”
18 Ndugu walifanya nini? Waliheshimia uamuzi wake. Tunasoma hivi: “Wakati tulishindwa kumushawishi, tukaacha kumupinga na tukasema: ‘Mapenzi ya Yehova yatendeke.’” (Mdo. 21:14) Wale wenye walipima kubembeleza Paulo asiende Yerusalemu hawakumukaza afanye vile wanapenda. Walisikiliza Paulo na kuacha afanye vile anaona. Walitambua kama ni mapenzi ya Yehova na wakaacha itendeke, hata kama haikukuwa mwepesi kwao. Paulo alikuwa amekamata uamuzi wenye ungemupeleka ku kifo. Mambo ilikuwa nguvu zaidi kwa Paulo juu ndugu zake wapendwa walikuwa wamejaribu kumubembeleza asiende.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
“Musikilize Sasa Namna Ninajitetea”
10 Lakini, Paulo alielewa wale wenye walipenda kuendelea kufuata desturi fulani za Wayahudi, kama vile kutokufanya kazi siku ya Sabato ao kutokula chakula fulani. (Ro. 14:1-6) Na hakuweka sheria kuhusu kutahiriwa. Paulo alikamata mipango juu Timoteo atahiriwe kusudi Wayahudi wasikuwe na mashaka juu ya Timoteo, mwenye baba yake alikuwa Mugiriki. (Mdo. 16:3) Kutahiriwa ilikuwa jambo ya mutu kujiamulia. Paulo aliambia Wagalatia hivi: “Kutahiriwa ao kutokutahiriwa hakuna faida yoyote, lakini imani yenye inatenda kupitia upendo ndiyo iko na faida.” (Gal. 5:6) Lakini, kutahiriwa juu ya kufuata Sheria ao kusema kama mutu anapaswa kutahiriwa juu akubaliwe na Yehova ni kukosa imani.
11 Hata kama habari zenye zilienea juu ya Paulo hazikukuwa za kweli, ziliendelea kusumbua waamini Wayahudi. Njo maana wanaume wazee waliambia Paulo hivi: “Tuko na wanaume ine wenye walijiwekea wenyewe naziri. Chukua watu hawa na ujitakase pamoja nao kulingana na desturi na uwalipie mambo yenye wako nayo lazima, ili wanyolewe vichwa vyao. Kisha wote watajua kwamba habari zenye waliambiwa juu yako haziko za kweli, lakini unatembea kwa utaratibu na pia unashika Sheria.”—Mdo. 21:23, 24.
12 Paulo angeweza kuwaonyesha kama tatizo haikukuwa zile habari zenye zilienea juu yake, lakini tatizo ilikuwa maoni yenye waamini Wayahudi walikuwa nayo juu ya Sheria ya Musa. Kuliko kufanya vile, alikuwa tayari kubadilika kulingana na hali wakati kufanya vile hakungevunja kanuni za Mungu. Wakati fulani, mbele ya pale, aliandika hivi: “Kwa wale wenye kuwa chini ya sheria nilikuwa kama mwenye kuwa chini ya sheria, hata kama mimi mwenyewe siko chini ya sheria, ili nipate wale wenye kuwa chini ya sheria.” (1 Ko. 9:20) Kwa hiyo, Paulo aliamua kufuata maagizo ya wazee wa Yerusalemu na kuwa “kama mwenye kuwa chini ya sheria.” Kwa kufanya vile, alituachia mufano muzuri: Tunapaswa kufuata maagizo ya wazee kuliko kutafuta tu kufanya mambo vile tunapenda.—Ebr. 13:17.
nwtsty, maelezo kuhusu Mdo 22:16
ujisafishe na kuondolea mbali zambi zako kwa kuitia jina lake: Ao “ujisafishe na kuondolea mbali zambi zako na uitie jina lake.” Haiko ubatizo wa maji tu njo ungefanya zambi za mutu ziondolewe, lakini iliomba pia kuitia jina la Yesu. Kuitia jina la Yesu maana yake kuamini Yesu na kuonyesha ile imani kupitia matendo ya Kikristo.—Mdo 10:43; Yak 2:14, 18.
TAREHE 14-20/01
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 23-24
“Alishitakiwa Kuwa Muleta-Muvurugo na Mwenye Kuchochea Uasi”
“Ukuwe Hodari!”
5 Paulo alitiwa moyo ku wakati wenye kufaa. Siku ya kufuata, wanaume Wayahudi zaidi ya 40, ‘walifanya shauri na wakajifunga kwa kiapo, wakisema kwamba hawatakula ao kunywa mupaka wakuwe wamemuua Paulo.’ ‘Ile shauri ya kujifunga wenyewe kwa kiapo,’ ilionyesha kama wale Wayahudi waliazimia kabisa kuua mutume Paulo. Waliamini kama, ikiwa mupango wao ungeshindikana, wangepata laana, ao mambo ya mubaya. (Mdo. 23:12-15) Mupango wao ulikubaliwa na wakubwa wa makuhani na wazee. Kwa hiyo, walirudisha Paulo mbele ya Sanhedrini juu ajibie maulizo ingine, ikuwe sawa vile kulikuwa mambo ingine yenye walipenda awafasirie muzuri. Lakini, kusudi yao ilikuwa kumutega Paulo juu wamuue.
6 Lakini, mutoto mwanaume wa dada yake na Paulo alisikia ile mambo na akajulisha Paulo. Kisha, Paulo akaambia ule kijana aambie Klaudio Lisia, kiongozi wa jeshi la Roma. (Mdo. 23:16-22) Bila shaka, Yehova anapenda vijana wenye wanatenda kwa uhodari, sawa ule mutoto wa dada yake na Paulo, na kutia faida ya watu wa Mungu pa nafasi ya kwanza na kufanya kwa uaminifu yao yote juu ya kuendelesha kazi ya Ufalme.
“Ukuwe Hodari!”
10 Kule Kaisaria, Paulo ‘aliwekwa chini ya ulinzi katika nyumba ya kifalme ya Herode’ akingojea wenye walimushitaki wafike kutoka Yerusalemu. (Mdo. 23:35) Kisha siku tano, walifika—Kuhani Mukubwa Anania, musemaji wa mbele ya watu wote mwenye kuitwa Tertulo, na kikundi cha wanaume wazee. Tertulo alianza kumutapa-tapa Feliksi juu ya mambo yenye alikuwa anafanyia Wayahudi, pengine juu Feliksi amukubali. Kisha, wakati alianza mashitaka yake, Tertulo alisema kama Paulo ni “muleta-muvurugo, mwenye kuchochea uasi katikati ya Wayahudi wote katika dunia yote yenye kuikaliwa na watu, na ni kiongozi mukubwa wa zehebu la Wanazareti.” Alisema tena kama ‘alijaribu kuchafua hekalu,’ kwa hiyo ‘walimukamata.’ Wayahudi wengine ‘walijiunga katika shambulio hilo, wakisema kwa mukazo kwamba mambo hayo ni ya kweli.’ (Mdo. 24:5, 6, 9) Kuchochea uasi, kuongoza zehebu hatari, na kuchafua hekalu, ilikuwa mashitaka ya nguvu sana yenye ingeweza kufanya mutu ahukumiwe kifo.
“Ukuwe Hodari!”
13 Paulo alituachia mufano ya muzuri ya kufuata kama wanatushitaki kwa sababu ya ibada yetu na kusema kama tuko waleta-muvurugo, waasi, ao watu wa “zehebu hatari.” Paulo hakujaribu kujipendekeza mbele ya gavana, kwa kumusifu-sifu kama vile Tertulo alifanya. Paulo alitulia na alimuheshimia. Kwa busara, alitoa ushahidi wenye kusadikisha na wa kweli. Paulo alionyesha kama “Wayahudi fulani kutoka jimbo la Asia” wenye walimushitaki kama alichafua hekalu hawakukuwa pale, na kulingana na sheria walipaswa kuwa pale juu watoe mashitaka yao.—Mdo. 24:18, 19.
14 Zaidi ya yote, Paulo hakujizuia kutoa ushahidi juu ya mambo yenye aliamini. Bila kuogopa, alisema tena na tena kama anaamini ufufuo, jambo yenye ilileta muvurugo wakati alikuwa mbele ya Sanhedrini. (Mdo. 23:6-10) Wakati alikuwa anajitetea, Paulo alikazia tumaini ya ufufuo. Juu ya nini? Juu, Paulo alikuwa anatoa ushahidi juu ya Yesu na ufufuo wake—jambo yenye wale wapinzani hawakukubali. (Mdo. 26:6-8, 22, 23) Ndiyo, ni habari ya ufufuo, zaidi sana imani katika Yesu na ufufuo wake njo ilitokeza muvurugo.
nwtsty, maelezo kuhusu Mdo 23:6
Mimi ni Mufarisayo: Watu fulani kati ya wasikilizaji walijua Paulo. (Mdo 22:5) Wangeweza kuelewa kama, kwa kujiita mwana wa Wafarisayo, Paulo alikubali kama yeye pia alikuwa Mufarisayo zamani. Walielewa kama Paulo hamaanishe kama angali Mufarisayo, kwa sababu Wafarisayo wa mu Sanhedrini walijua kama alishakuwa Mukristo mwenye bidii. Lakini hapa, wakati Paulo anasema kama iko Mufarisayo inaweza kuwa na maana ingine; Paulo alijiita kuwa Mufarisayo hapana Musadukayo, kwa sababu naye alikuwa anaamini ufufuo sawa vile Wafarisayo. Kwa kujiita vile, alionyesha jambo yenye yeye na Wafarisayo wenye walikuwa pale wanakubaliana. Pengine aliwaza kama kuzungumuzia ile jambo yenye ilikuwa inaleta ubishi ingefanya washiriki fulani wa Sanhedrini wamuunge mukono, na ile mayele ilikuwa na matokeo ya muzuri. (Mdo 23:7-9) Maneno ya Paulo mu Mdo 23:6 inapatana na mambo alisemaka juu yake wakati alikuwa anajitetea mbele ya Mufalme Agripa. (Mdo 26:5) Na wakati Paulo aliandikia Wakristo wa Filipi na iko Roma, alijiita tena kuwa Mufarisayo. (Flp 3:5) Ona pia namna Wakristo wengine wenye zamani walikuwa Wafarisayo wanazungumuziwa mu Mdo 15:5.—Ona maelezo kuhusu Mdo 15:5, hapa chini.
nwtsty, maelezo kuhusu Mdo 15:5 wale wa zehebu la Wafarisayo: Inaonekana, wale Wakristo walikuwa wangali wanaitwa Wafarisayo, dini yao ya zamani.—Linganisha na maelezo kuhusu Mdo 23:6, pale juu.
nwtsty, maelezo kuhusu Mdo 24:24
Drusila: Ni mutoto mwanamuke wa tatu na wa mwisho wa Herode mwenye kutajwa mu Mdo 12:1, ni kusema, Herode Agripa wa Kwanza. Drusila alizaliwa mu mwaka 38 hivi K.K.Y. na alikuwa dada yake na Agripa wa Pili na Bernike. (Ona maelezo kuhusu Mdo 25:13 yenye kuwa hapa chini, na Maana ya Maneno ya Biblia, “Herode.”) Gavana Feliksi alikuwa bwana yake wa pili. Kwanza aliolewa na Mufalme wa Asiria Azizu wa Emesa lakini alivunja ndoa kisha kuishi naye miaka 16 hivi. Inawezekana, Drusila alikuwa pale wakati Paulo alizungumuza mbele ya Feliksi “juu ya haki, kujizuia, na hukumu yenye itakuja.” (Mdo 24:25) Wakati gavana Feliksi alirudishia Festo utawala, aliacha Paulo mu gereza sababu “alitamani kukubaliwa na Wayahudi.” Watu fulani wanawaza kama alifanya vile juu ya kufurahisha bibi yake Muyahudi, mwenye alikuwa angali kijana.—Mdo 24:27.
nwtsty, maelezo kuhusu Mdo 25:13
Bernike: Dada yake na Herode Agripa wa Pili, lakini walikuwa wanaishi kama bibi na bwana. Mbele Tito akuwe mufalme wa Roma, Bernike alikuwa pia bibi yake.
TAREHE 21-27/01
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 25-26
“Paulo Anaomba Aende Kusamba Mbele ya Kaisari na Kisha Anatolea Mufalme Herode Agripa Ushahidi”
“Ninapeleka Kesi Yangu ya Hukumu kwa Kaisari!”
6 Tamaa ya Festo ya kufurahisha Wayahudi ingeweza kufanya waue Paulo. Kwa hiyo, Paulo alitumia haki yake ya kuwa mwanainchi wa Roma. Aliambia Festo: “Nimesimama mbele ya kiti cha hukumu cha Kaisari, kwenye ninapaswa kuhukumiwa. Sikutendea Wayahudi kosa, kama vile wewe pia unaelewa muzuri sasa . . . Ninapeleka kesi yangu ya hukumu kwa Kaisari!” Kisha hapo ilipaswa kusikilizwa. Festo alikazia ile jambo kwa kusema: “Umeomba kesi yako ya hukumu isikilizwe na Kaisari; utaenda kwa Kaisari.” (Mdo. 25:10-12) Kwa kuomba aende kusamba ku tribinali ya juu zaidi, Paulo aliachia Wakristo wa kweli leo mufano ya kufuata. Wakati wapinzani wanajaribu kutunga “matatizo kwa kutumia sheria,” Mashahidi wa Yehova wanatumia mipango yenye sheria inatoa juu watetee habari njema.—Zb. 94:20.
“Ninapeleka Kesi Yangu ya Hukumu kwa Kaisari!”
10 Paulo alishukuru kwa heshima Mufalme Agripa juu alimupatia nafasi ya kujitetea. Alionyesha kama mufalme anajua muzuri desturi zote na mabishano kati ya Wayahudi. Kisha, Paulo alizungumuzia maisha yake ya zamani: “Niliishi nikiwa Mufarisayo kulingana na musimamo mukali wa ibada katika zehebu letu.” (Mdo. 26:5) Wakati alikuwa Mufarisayo, Paulo alikuwa anangojea Masiya. Sasa wakati anakuwa Mukristo, alionyesha bila kuogopa kama Yesu njo ule mwenye walikuwa wanangojea tangu zamani. Paulo alishitakiwa kwa sababu ya jambo yenye yeye na wenye kumushitaki walikuwa wanaamini, ni kusema, tumaini ya kuona namna ahadi yenye Mungu alipatiaka mababu zao inatimia. Maelezo ya Paulo ilimuchochea Agripa aendelee kumusikiliza.
11 Akikumbuka vile alikuwa anatendea Wakristo kwa ukali zamani, Paulo alisema: “Mimi kwa upande wangu, niliamini kwamba nilipaswa kufanya matendo mengi ili kupinga jina la Yesu Munazareti . . . Kwa sababu nilikuwa nimewakasirikia sana [wafuasi wa Kristo], nilifikia kuwatesa hata katika miji ingine.” (Mdo. 26:9-11) Paulo hakukuwa anatia chumvi. Watu mingi walijua vile alikuwa amewatendea Wakristo kwa jeuri. (Gal. 1:13, 23) Pengine Agripa alitaka kujua nini njo ilibadilisha Paulo.
12 Hii maneno ya Paulo inatoa jibu: “Wakati nilikuwa katika safari ya kuenda Damasko na nilikuwa na mamlaka na maagizo kutoka kwa wakubwa wa makuhani, katikati ya muchana niliona katika barabara, Ee Mufalme, mwangaza kutoka mbinguni wenye kupita mwangaza wa jua ukanizunguka mimi na wale wenye walikuwa wanasafiri pamoja na mimi. Na wakati tulikuwa tumeanguka chini, nikasikia sauti inaniambia katika luga ya Kiebrania: ‘Sauli, Sauli, sababu gani unanitesa? Kuendelea kupiga-piga miguu yako kwenye michokoo kutafanya uumie.’ Lakini nikasema: ‘Wewe ni nani Bwana?’ Na Bwana akasema: ‘Mimi ni Yesu, mwenye unatesa.’”—Mdo. 26:12-15.
13 Mbele ile jambo yenye haiko ya kawaida kutokea, Paulo alikuwa ‘anapiga-piga miguu yake kwenye michokoo.’ Kama vile nyama ya kubeba mizigo ingejiumiza kwa kupiga-piga miguu kwenye sehemu ya makali ya muchokoo, Paulo alikuwa amejiumiza kiroho kwa kupinga mapenzi ya Mungu. Kwa kumutokea Paulo mu barabara ya kuenda Damasko, Yesu mwenye alikuwa amefufuliwa alichochea ule mutu wa moyo muzuri, mwenye alikuwa anatenda bila kujua, abadilishe maoni yake.—Yoh. 16:1, 2.
14 Bila shaka Paulo alifanya mabadiliko makubwa mu maisha yake. Aliambia Agripa: “Sikukosa kutii maono hayo kutoka mbinguni, lakini kwanza kwa wale wenye kuwa Damasko kisha kwa wale wenye kuwa Yerusalemu, na katika inchi yote ya Yudea, na pia kwa mataifa, nilipeleka ujumbe kwamba wanapaswa kutubu na kugeukia kwa Mungu kwa kufanya matendo yenye yanaonyesha kwamba wametubu.” (Mdo. 26:19, 20) Mu miaka mingi, Paulo alikuwa ametimiza mugao yenye Yesu Kristo alimupatia mu ile maono yenye alipataka katikati ya muchana. Matokeo ilikuwa nini? Watu wenye walikubali habari njema yenye Paulo alikuwa anahubiri walitubu mwenendo wao muchafu, wa bila haki, kisha wakageuka ili kufuata Mungu. Wale watu walifikia kuwa wanainchi wazuri, wenye kuheshimia sheria na mamlaka.
15 Lakini, ile haikukuwa na maana yoyote kwa Wayahudi wenye walipinga Paulo. Paulo alisema: “Ndiyo sababu Wayahudi walinikamata katika hekalu na wakataka kuniua. Lakini, kwa sababu nimepata musaada kutoka kwa Mungu, ninaendelea mupaka leo kutoa ushahidi kwa wadogo na kwa wakubwa pia.”—Mdo. 26:21, 22.
16 Sisi Wakristo wa kweli, tunapaswa ‘sikuzote kuwa tayari kutetea’ imani yetu. (1 Pe. 3:15) Wakati tunazungumuza na waamuzi na watawala juu ya imani yetu, inaweza kuwa muzuri kuiga namna Paulo alifanya wakati alikuwa anazungumuza na Agripa na Festo. Kwa kuwaelezea kwa heshima namna kweli za Biblia zimebadilisha maisha yetu na ya wengine wenye wanakubali ujumbe wetu, tunaweza kugusa moyo ya wale watu wenye mamlaka.
“Ninapeleka Kesi Yangu ya Hukumu kwa Kaisari!”
18 Lakini, Paulo alijibia ule gavana hivi: “Mimi sipoteze akili, Ee Mutukufu Festo, lakini ninasema maneno ya kweli na ya akili ya muzuri. Kwa maana, kwa kweli, mufalme mwenye ninazungumuza naye kwa uhuru anajua muzuri mambo haya . . . Mufalme Agripa, je, unaamini Manabii? Ninajua unawaamini.” Lakini Agripa aliambia Paulo: “Kwa wakati kidogo ungenishawishi nikuwe Mukristo.” (Mdo. 26:25-28) Ikuwe ile maneno ilitoka ku moyo ao hapana, inaonyesha kama ushahidi wenye Paulo alitoa uligusa sana moyo ya mufalme.
nwtsty, maelezo kuhusu Mdo 26:14
kupiga-piga miguu kwenye michokoo: Muchokoo ni fimbo yenye chongo yenye inatumiwa ili kuongoza nyama. (Amu 3:31) Maneno “kupiga-piga miguu kwenye michokoo” ni mezali ya mu vitabu vya Wagiriki. Ile maneno inatokana na tendo ya ngombe-dume yenye iko kichwa-nguvu yenye inakatala kuongozwa kwa kupiga-piga miguu ku muchokoo, na kwa hiyo inajiumiza yenyewe. Ni vile Saulo alijiendesha mbele akuwe Mukristo. Kwa kupigana na wafuasi wa Yesu, wenye walikuwa wanaongozwa na Yehova Mungu, Paulo alitafuta kujiumiza sana. (Linganisha na Mdo 5:38, 39; 1Ti 1:13, 14.) Mu Muh. 12:11, “michokoo” inazungumuziwa mu maana ya mufano ili kufananisha maneno ya mutu mwenye hekima yenye inachochea mwenye anaisikia atii shauri.
nwt, maana ya maneno ya Biblia
Muchokoo. Fimbo ya murefu yenye chongo kali ya chuma, yenye walimaji walitumia juu ya kuongoza nyama kwa kuitobola-tobola nayo. Maneno ya mutu mwenye hekima yenye inachochea musikilizaji kutii shauri yenye hekima inafananishwa na muchokoo. Maneno “kupiga-piga miguu kwenye michokoo” inatokana na tendo ya ngombe-dume yenye kuwa kichwa-nguvu yenye inakatala kufuata muongozo ya muchokoo kwa kupiga-piga miguu kwenye muchokoo, na inajiumiza yenyewe.—Mdo 26:14; Amu 3:31.
Usaidie Wengine Wakubali Ujumbe ya Ufalme
14 Paulo alijua kama Agripa alikuwa Muyahudi wa jina tu. Kwa kusema mambo yenye Agripa alikuwa anajua kuhusu Dini ya Kiyahudi, Paulo alionyesha kama mahubiri yake ilihusu zaidi sana ‘kutosema jambo lolote isipokuwa tu yale yenye Manabii na pia Musa walisema yatatokea’ juu ya kufa na kufufuka kwa Masiya. (Matendo 26:22, 23) Wakati alizungumuza na Agripa moja kwa moja, Paulo aliuliza: “Mufalme Agripa, je, unaamini Manabii?” Ile ulizo ilihangaisha Agripa. Kama alisema hakuamini manabii, watu wangetambua kama haamini mambo ya Wayahudi. Na kama aliitika mawazo ya Paulo, ingeonekana kama anakubaliana waziwazi na mawazo ya Paulo na watu wangeanza kusema kama yeye pia ni Mukristo. Paulo alijibu ulizo yake mwenyewe kwa hekima, kwa kusema: “Ninajua unawaamini.” Moyo ya Agripa ilimuchochea ajibu namna gani? Alijibu: “Kwa wakati kidogo ungenishawishi nikuwe Mukristo.” (Matendo 26:27, 28) Hata kama Agripa hakufikia kuwa Mukristo, ni wazi kwamba Paulo alimugusa moyo kwa kadiri fulani kupitia ujumbe yake.—Waebrania 4:12.
TAREHE 28/01–TAREHE 3/02
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MATENDO 27-28
“Paulo Anaenda Roma”
“Hakuna Hata Mumoja Wenu Mwenye Atapotea”
15 Inaonekana kama Paulo alihubiria watu mingi mu ile mashua juu ya ‘tumaini la ahadi yenye Mungu alitoa.’ (Mdo. 26:6; Kol 1:5) Sasa, vile mashua yao ilikaribia kuvunjika, Paulo alitoa sababu yenye kusadikisha ya kuwasaidia wakuwe hakika kama jambo fulani iko karibu kutokea. Aliwaambia: “Usiku huu malaika . . . , alisimama karibu yangu, na akasema, ‘Usiogope, Paulo. Unapaswa kusimama mbele ya Kaisari, na angalia! Mungu amekupatia wale wote wenye wanasafiri pamoja na wewe.’” Kisha Paulo akawatia moyo: “Musiogope; kwa maana ninamuamini Mungu kwamba itakuwa kabisa kama vile niliambiwa. Hata hivyo, lazima tutupwe kwenye inchi kavu kwenye kisiwa fulani.”—Mdo. 27:23-26.
“Hakuna Hata Mumoja Wenu Mwenye Atapotea”
18 Wale wenye waliokoka walijikuta ku kisiwa ya Malta, ngambo ya kusini ya Sisili. Watu wa ile kisiwa wenye wanasema luga ya kigeni ‘waliwatendea kwa fazili nyingi sana.’ (Mdo. 28:2). Watu walifika ku inchi kavu wenye kulobana na kutetemeka kwa sababu ya baridi, kwa hiyo waliwawakishia moto, hata kama hawakuwajua. Ile moto iliwasaidia kupata kifukutu kwa sababu kulikuwa baridi na mvua. Ile ilitokeza tena muujiza fulani.
“Hakuna Hata Mumoja Wenu Mwenye Atapotea”
21 Publio, tajiri mwenye kuwa na mashamba, alikuwa anaishi mu ile eneo. Pengine alikuwa ofisa Muroma mwenye kujulikana sana mu kisiwa ya Malta. Luka anamutaja kuwa “mukubwa wa kisiwa hicho.” Ile jina ya cheo inapatikana mu vitabu viwili vya luga ya Kimalta. Publio alikaribisha na kuonyesha ukarimu Paulo na wenzake kwa siku tatu. Lakini, baba yake alikuwa mugonjwa. Luka anafasiria waziwazi ugonjwa yenye alikuwa nayo. Anasema kama alikuwa mwenye kulala mu kitanda na alikuwa na “ugonjwa wa homa na wa kuhara damu.” Paulo alisali na kuweka mikono juu yake, naye akapona. Ile muujiza ilishangaza sana watu wa ile kisiwa, kwa hiyo walileta wagonjwa wengine juu awaponyeshe, na wakaleta zawadi ya vitu vyote vyenye Paulo na wenzake walikuwa navyo lazima.—Mdo. 28:7-10.
“Kutoa Ushahidi Kamili”
10 Wakati Paulo na wale wenye walisafiri naye walifika Roma, “Paulo aliruhusiwa kukaa peke yake akiwa na askari wa kumulinda.” (Mdo. 28:16) Mutu mwenye alifanya makosa ya kidogo-kidogo, walikuwa wanamufunga na munyororo, na kisha walifungia ile munyororo ku askari wa kumuchunga juu asikimbie. Vile Paulo alikuwa mutangazaji wa Ufalme, ile munyororo haikumunyamazisha. Kwa hiyo, kisha kupumuzika siku tatu, aliita wakubwa wa Wayahudi wenye walikuwa Roma juu awaambie kama yeye ni nani na juu awahubirie.
nwtsty, maelezo kuhusu Mdo 27:9
Kipindi cha Kufunga cha Siku ya Kufunika Zambi: Ao “mafungo ya kipindi cha mvua ya kwanza.” Neno kwa neno, “mafungo.” Neno ya Kigiriki “mafungo” inahusu tu ile amri ya kufunga yenye ilitolewa chini ya Sheria ya Musa, ni kusema, mafungo yenye ilikuwa inafanywa Siku ya kila mwaka ya Kufunika Zambi, siku yenye inaitwa tena Yom Kippur (Mu Kiebrania, yohm hak·kip·pu·rimʹ, “siku ya kufunika”). (Law 16:29-31; 23:26-32; Hes 29:7; ona Maana ya Maneno ya Biblia, “Siku ya Kufunika Zambi.”) Watu wanawaza kama neno “kujitesa,” yenye inatumiwa kuhusu Siku ya Kufunika Zambi, inamaanisha njia mbalimbali za kujiima mambo fulani, na pia kufunga. (Law 16:29, maelezo ya chini.) Wakati neno “kufunga” inatumiwa mu Mdo 27:9, ile inaonyesha kama jambo yenye watu walikuwa wanajiima zaidi sana mu Siku ya Kufunika Zambi ilikuwa chakula. Kufunga ya Siku ya Kufunika Zambi ilikuwa inaangukia ku mwisho-mwisho ya Mwezi ya 9 ao ku mwanzo-mwanzo ya Mwezi ya 10.
nwtsty, maelezo kuhusu Mdo 28:11
Wana wa Zeu: Kulingana na Hadisi za Wagiriki na Waroma, “Wana wa Zeu” (Mu Kigiriki, Di·oʹskou·roi) walikuwa Castor na Pollux, ndugu watoto wanaume mapasa ya mungu Zeu (Jupiter) na malkia Leda wa Spartan. Watu waliona wana wa Zeu kuwa walinzi wa wafanyakazi wa mashua, wenye kuwa na uwezo wa kuwaokoa wakati mashua inataka kuzama. Habari hii kuhusu sanamu yenye ilikuwa ku sehemu ya mbele ya mashua ni jambo ingine yenye inahakikisha kama ile habari iliandikwa na mutu mwenye alijionea mambo na macho yake.