Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr19 Mwezi wa 2 uku. 1-5
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2019)
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 4-10/02
  • TAREHE 11-17/02
  • TAREHE 18-24/02
  • TAREHE 25/02–3/03
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha (2019)
mwbr19 Mwezi wa 2 uku. 1-5

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 4-10/02

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAROMA 1-3

“Endelea Kuzoeza Zamiri Yako”

lv uku. 16 fu. 6

Unaweza Kufanya Nini ili Zamiri Yako Iendelee Kuwa Safi?

6 Ni watumishi wa Yehova tu ndio wana zamiri? Ili kujibu ulizo hilo, tuchunguze maneno mutume Paulo aliandika kwa uongozi wa roho takatifu: ‘Wakati watu wa mataifa wasio na sheria wanapofanya kwa asili mambo ya sheria, watu hawa, ijapokuwa hawana sheria, wao ni sheria kwao wenyewe. Wao ndio wanaoonyesha kuwa yaliyomo katika sheria yameandikwa ndani ya mioyo yao, huku zamiri yao ikiwatolea ushahidi na, katikati ya fikira zao wenyewe, wanashitakiwa ao hata kutetewa.’ (Waroma 2:14, 15) Wakati fulani, hata wale wasiojua hata kidogo sheria za Yehova wanaweza kusukumwa na shahidi wao wa ndani, ni kusema, zamiri yao, ili watende kupatana na kanuni za Mungu.

lv uku. 17-18 fu. 8-9

Unaweza Kufanya Nini ili Zamiri Yako Iendelee Kuwa Safi?

8 Namna gani unaweza kutumia zamiri yako ili kuchukua uamuzi? Inaonekana kama watu wengine wanafuata tu mawazo ya moyo wao ao jinsi wanavyojisikia, na kisha wanaamua kile watafanya. Kisha wanaweza kusema, “Kulingana na zamiri yangu sione ubaya wowote.” Tamaa za moyo wa mutu zinaweza kuwa na nguvu sana hata kufikia kuharibisha zamiri yake. Biblia inasema hivi: “Moyo ni wenye hila kuliko kitu kingine chochote nao ni hatari. Ni nani anayeweza kuujua?” (Yeremia 17:9) Kwa hiyo, hatupaswe kufuata haraka-haraka tamaa ya moyo wetu. Tunapaswa kwanza kujiuliza ikiwa yale moyo wetu unatamani yatamupendeza Yehova ao hapana.

9 Ikiwa tunachukua uamuzi kwa sababu tunaongozwa kabisa na zamiri iliyofundishwa, hilo litaonyesha kama sisi ni watu wenye kumuogopa Mungu na hatufuate tamaa zetu za kichoyo. Ili kuelewa jambo hilo, tuchukue mufano wa liwali (ao guvernere) mwaminifu Nehemia. Kwa sababu alikuwa guvernere, alikuwa na haki ya kuomba watu wa Yerusalemu watoe kodi na michango fulani. Lakini hakufanya hivyo. Sababu gani? Hakutaka kuwatesa watu wa Mungu na hivyo kumuchukiza Yehova. Alisema hivi: ‘Mimi sikufanya hivyo kwa sababu ya kumuogopa Mungu.’ (Nehemia 5:15) Ni jambo la lazima kumuogopa Mungu bila unafiki, ni kusema, kuogopa kwa moyo wote kufanya jambo lolote linaloweza kumuchukiza Baba yetu wa mbinguni. Heshima na woga kama huo vitatusukuma kutafuta uongozi wa Neno la Mungu kila wakati tunapotaka kuchukua maamuzi.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w08 15/6 uku. 30 fu. 5

Mambo Makubwa ya Kitabu cha Waroma

3:4. Wakati maneno ya wanadamu inapingana na ile yenye Mungu anasema mu Neno lake, tunaacha ‘Mungu aonekane kuwa wa kweli’ kwa kuamini mambo yenye Biblia inasema na kutenda kulingana na mapenzi ya Mungu. Wakati tunahubiri na kufanya wanafunzi kwa bidii, tunasaidia wengine wamuone Mungu kuwa wa kweli.

w08 15/6 uku. 29 fu. 6

Mambo Makubwa ya Kitabu cha Waroma

3:24, 25​—Namna gani “bei ya ukombozi yenye Kristo Yesu alilipa” ingeweza kufunika “zambi zenye zilifanywa wakati wenye ulipita”? Unabii kuhusu Masiya wenye uliandikwa mu Mwanzo 3:15, ulitimia mwaka wa 33, wakati Yesu aliuawa ku muti wa mateso. (Gal. 3:13, 16) Lakini, wakati Yehova alitoa ile unabii, ku maoni yake, ni sawa vile bei ya ukombozi ilikuwa tayari imelipwa, sababu hakuna kitu chenye kinaweza kuzuia Mungu asitimize makusudi yake. Kwa hiyo, kwa musingi wa zabihu yenye Yesu Kristo angetoa mu siku zenye kuja, Yehova alikuwa anasamehe zambi za wazao wa Adamu wenye walionyesha kama wanaamini ile ahadi. Tena, bei ya ukombozi itawezesha wale wenye walikufa mbele Ukristo uanze wafufuliwe.​—Mdo. 24:15.

TAREHE 11-17/02

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAROMA 4-6

“Mungu Anapendekeza Upendo Wake Mwenyewe Kwetu”

w11 15/6 uku. 12 fu. 5

Mungu Anapendekeza Upendo Wake Mwenyewe Kwetu

5 Juu ya kueleza ile jambo, Paulo alianza kwa kusema hivi: “Kupitia mutu mumoja zambi iliingia katika ulimwengu na kifo kupitia zambi, na ni vile kifo kilienea kwa watu wote kwa sababu wote walikuwa wamefanya zambi.” (Ro. 5:12) Tunaweza kuelewa ile jambo juu Mungu aliandikisha habari yenye inaonyesha namna maisha ya mwanadamu ilianza. Yehova aliumba wanadamu wawili, Adamu na Eva. Muumbaji ni mukamilifu, na wanadamu wa kwanza, ni kusema wazazi wetu wa kwanza, walikuwa pia wakamilifu. Mungu aliwapatia sheria moja tu yenye walipaswa kufuata na aliwaambia kama wangekufa ikiwa hawangetii ile sheria. (Mwa. 2:17) Lakini, walichagua kuasi, kwa kupuuza sheria ya Mungu yenye haikukuwa nguvu. Kwa kufanya vile walikataa Mungu asikuwe Mupaji-Sheria wao na Bwana wao Mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi.​—Kum. 32:4, 5.

w11 15/6 uku. 12 fu. 6

Mungu Anapendekeza Upendo Wake Mwenyewe Kwetu

6 Adamu alizala watoto kisha kufanya zambi, na ni vile aliwapitishia wote zambi na matokeo yake ya mubaya. Wale watoto hawakukuwa wamevunja sheria ya Mungu, kwa hiyo hawakushitakiwa kwamba walifanya zambi sawa ya Adamu; tena ile wakati hakukukuwa sheria yoyote yenye ilikuwa imeandikwa. (Mwa. 2:17) Lakini, wazao wa Adamu waliriti zambi. Ni vile zambi na kifo vilitawala mupaka wakati Mungu alipatia Waisraeli sheria yenye kuandikwa, yenye ilionyesha wazi kama walikuwa watenda-zambi. (Soma Waroma 5:13, 14.) Matokeo ya mubaya ya zambi yenye tuliriti inaweza kufananishwa na magonjwa na kasoro fulani yenye mutu anariti kama vile kupungukiwa na damu, ao hemofilia, ni kusema, ugonjwa wenye unafanya damu isigande. Pengine umesoma habari ya Alexis, mutoto wa mutawala wa Urusi Nicholas wa Pili na Alexandra bibi yake, mwenye aliriti ugonjwa wa hemofilia. Ni kweli kwamba mu familia za vile, watoto fulani hawasumbuliwe na ile magonjwa, lakini wako nayo mu mwili. Sasa, haiko vile kabisa kuhusu zambi. Mutu hawezi kuepuka matokeo ya mubaya ya zambi ya Adamu. Watu wote wanapatwa na matokeo ya ile zambi. Inawapelekaka tu ku kifo. Na watoto wote wanariti matokeo ya zambi. Je, kuko siku itaondolewaka?

w11 15/6 uku. 13 fu. 9-10

Mungu Anapendekeza Upendo Wake Mwenyewe Kwetu

9 Maneno ya Kigiriki yenye kutafsiriwa “kutangazwa kuwa wenye haki” inamaanisha nini? Mutafsiri moja wa Biblia aliandika hivi juu ya ile maneno: “Ni maneno ya mufano yenye inatumiwa mu mambo ya sheria. Inaonyesha badiliko fulani mu uhusiano wa mutu na Mungu, hapana badiliko yenye inafanyika ndani ya mutu . . . Ile maneno inaonyesha namna Mungu anatenda kama muamuzi mwenye anaamua kuhurumia mushitakiwa, mwenye aliletwa mbele ya tribinali yake, juu ya kujiendesha bila haki. Lakini Mungu anamuhurumia.”

10 Uamuzi wa ‘Muamuzi mwenye haki wa dunia yote’ wa kuhurumia mutu mwenye kujiendesha bila haki unategemea nini? (Mwa. 18:25) Ule uamuzi unategemea jambo lenye Mungu alifanya wakati kwa upendo alituma Mwana wake muzaliwa-pekee ku dunia. Yesu alifanya mapenzi ya Baba yake kwa ukamili, hata kama alijaribiwa, alitukanwa, na kuchekelewa sana. Aliendelea kuwa muaminifu-mushikamanifu mupaka kufikia kufa ku muti wa mateso. (Ebr. 2:10) Kwa kutoa uzima wake mukamilifu, Yesu alitoa zabihu ya ukombozi yenye ingekomboa wazao wa Adamu mu zambi na kifo.​—Mt. 20:28; Ro. 5:6-8.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w08 15/6 uku. 29 fu. 7

Mambo Makubwa ya Kitabu cha Waroma

6:3-5​—Kubatizwa “katika Kristo Yesu” na kubatizwa “katika kifo chake” maana yake nini? Wakati Yehova anatia mafuta wafuasi wa Kristo kupitia roho yake takatifu, wanaunganishwa na Yesu na wanakuwa washiriki wa kutaniko, lenye ni mwili wa Kristo, na yeye njo Kichwa. (1 Ko. 12:12, 13, 27; Kol. 1:18) Njo maana ya kubatizwa katika Kristo Yesu. Tena, Wakristo watiwa-mafuta ‘wanabatizwa katika kifo cha Kristo’ kwa kuishi maisha ya kujitoa na kuachana na tumaini yoyote ya kuishi milele ku dunia. Kwa hiyo, wanakufa kifo cha kujitoa, sawa vile Yesu. Lakini, kifo chao hakina uwezo wa kukomboa. Ubatizo wao katika kifo cha Kristo unaisha wakati wanakufa na kufufuliwa juu waende kuishi mbinguni.

w14 1/6 uku. 11 fu. 1

Kuko Tumaini Gani kwa Ajili ya Mababu Zangu?

Wakati watu wenye hawako wenye haki watafufuliwa, je, watahukumiwa juu ya zambi zao za zamani? Hapana. Andiko ya Waroma 6:7 inasema: “Ule mwenye amekufa ameondolewa zambi yake.” Wakati watu wenye hawako wenye haki wanakufa, wanalipia zambi zao. Kwa hiyo, watahukumiwa juu ya mambo watafanya kisha wao kufufuliwa, hapana juu ya mambo yenye walifanyaka mbele wakufe juu ya kutokujua. Watakuwa na nafasi ya kufanya nini?

TAREHE 18-24/02

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAROMA 7-8

“Uko ‘Unangojea na Kutazamia kwa Hamu’?”

w12 15/7 uku. 11 fu. 17

Acha Yehova Akuongoze Kwenye Uhuru wa Kweli

17 Paulo alizungumuzia uhuru wenye Yehova ametayarishia watumishi wake wenye wataishi ku dunia; aliandika hivi: “Uumbaji unangojea na kutazamia kwa hamu kufunuliwa kwa wana wa Mungu.” Kisha aliongeza hivi: “Uumbaji wenyewe pia utawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu na kuwa na uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” (Ro. 8:19-21) “Uumbaji” unamaanisha wanadamu wenye wako na tumaini ya kuishi milele hapa ku dunia wenye watafaidika na “kufunuliwa” kwa wana wa Mungu wenye kutiwa mafuta na roho yake. Kufunuliwa kwao kutaanza wakati Kristo atatumika kule mbinguni pamoja na wale “wana” wa Mungu juu ya kuondoa ubaya wote ku dunia na kuingiza ‘kundi kubwa’ mu ulimwengu mupya.​—Ufu. 7:9, 14

w12 15/3 uku. 23 fu. 11

Tushangilie Katika Tumaini Letu

11 Yehova alitolea wanadamu “musingi wa tumaini” wakati aliahidi kama kutatokea “uzao” wenye utaharibu “nyoka ya zamani,” Shetani Ibilisi, na hivyo kukomboa wanadamu. (Ufu. 12:9; Mwa. 3:15) Yesu Kristo njo sehemu ya kwanza ya ule “uzao.” (Gal. 3:16) Kupitia kifo na ufufuo wake, Yesu alifanya iwezekane wanadamu wakuwe na tumaini hakika ya kuwekwa huru, na watoke mu utumwa wa zambi na kifo. Kuko uhusiano kati ya kutimizwa kwa ile tumaini na “kufunuliwa kwa wana wa Mungu.” Watiwa-mafuta wenye kutukuzwa wao njo sehemu ya pili ya ule “uzao.” ‘Watafunuliwa’ wakati watatumika na Kristo juu ya kuharibu ulimwengu muovu wa Shetani. (Ufu. 2:26, 27) Ile italetea wokovu kondoo wengine wenye wataokoka taabu kubwa.​—Ufu. 7:9, 10, 14.

w12 15/3 uku. 23 fu. 12

Tushangilie Katika Tumaini Letu

12 Utawala wa Kristo wa Miaka Elfu moja utafariji wanadamu kabisa! Ile wakati, “wana wa Mungu” wenye kutukuzwa ‘watafunuliwa’ mu njia ingine. Wakiwa makuhani pamoja na Kristo, watatumika juu ya kusaidia wanadamu wapate faida ya zabihu ya ukombozi ya Yesu. “Uumbaji,” ni kusema, wanadamu wenye watakuwa raia wa Ufalme wa Mungu, wataanza kukombolewa kutoka katika matokeo ya zambi na kifo. Hatua kwa hatua wanadamu watiifu ‘watawekwa huru kutoka katika utumwa wa uharibifu.’ Ikiwa wanabakia waaminifu kwa Yehova wakati wa utawala wa Miaka Elfu moja na wakati wa jaribu la mwisho lenye litatokea ku mwisho wa Utawala wa Miaka Elfu, majina yao itabakia yenye kuandikwa milele mu “kitabu cha uzima.” Wataingia mu “uhuru wenye utukufu wa watoto wa Mungu.” (Ufu. 20:7, 8, 11, 12) Ile ni tumaini ya muzuri kabisa!

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w17.06 uku. 3

Unakumbuka?

Kuko tofauti gani kati ya “kukaza akili juu ya mwili” na “kukaza akili juu ya roho”? (Rom. 8:6)

Mutu mwenye kukaza akili juu ya mwili anakaza akili yake juu ya tamaa na mielekeo ya mwili wenye haukamilike, kila mara anazungumuzia mambo ya kimwili na kuyasifu. Mutu mwenye kukaza akili juu ya roho, anakaza akili yake juu ya mambo yenye kuhusu Mungu na mawazo yake katika maisha; Mukristo kama huyo anaongozwa na roho takatifu. Kukaza akili juu ya mwili kunaongoza kwenye kifo na kukaza akili juu ya roho kunaongoza kwenye uzima na amani.​—w16.12, uku. 15-17.

w09 15/11 uku. 7 fu. 20

Sala Zako Zinafunua Nini Kukuhusu?

20 Wakati fulani, tunaweza kukosa mambo ya kusema mu sala zetu za kipekee. Paulo aliandika: “Tatizo ni kwamba hatujue kile chenye tuko na lazima ya kusali juu yake, lakini roho yenyewe inatuombea pamoja na vilio vya maumivu vyenye havitamukwe. Lakini [Mungu] mwenye anachunguza mioyo anajua maana ya roho.” (Ro. 8:26, 27) Yehova aliandikisha sala mingi mu Maandiko. Anaona kama maneno yenye iko mu zile sala zenye ziliongozwa na roho yake inapatana na mambo yenye tungependa kumuambia na anazijibia. Mungu anatujua na anajua pia maana ya maneno yenye aliongoza roho yake iseme kupitia waandikaji wa Biblia. Yehova anajibia sala zetu za kumulilia wakati roho “inaomba,” ao kumulilia kwa ajili yetu. Lakini kadiri tunajua muzuri zaidi Neno la Mungu, ni vile tutakumbuka kwa urahisi zaidi mambo yenye tunapenda kuomba.

TAREHE 25/02–3/03

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | WAROMA 9-11

“Mufano wa Muzeituni”

w11 15/5 uku. 23 fu. 13

‘Oh! Hekima ya Mungu Ni Kubwa Sana!’

13 Mutume Paulo analinganisha wale wenye wanakuwa sehemu ya uzao wa Abrahamu na matawi ya muzeituni wa mufano. (Ro. 11:21) Ule muzeituni wenye ulipandwa unafananisha kutimizwa kwa mambo yenye Mungu alipenda kufanya kupitia agano lake na Abrahamu. Muzizi wa ule muti ni mutakatifu na unafananisha Yehova juu yeye njo anapatia Israeli wa kiroho uzima. (Isa. 10:20; Ro. 11:16) Shina linafananisha Yesu juu yeye njo sehemu ya kwanza ya uzao wa Abrahamu. Matawi yote kwa pamoja inafananisha “hesabu kamili” ya wale wenye wanafanyiza sehemu ya pili ya uzao wa Abrahamu.

w11 15/5 uku. 24 fu. 15

‘Oh! Hekima ya Mungu Ni Kubwa Sana!’

15 Basi, Yehova alifanya nini ili kutimiza kusudi lake? Paulo anaeleza kwamba matawi kutoka ku muzeituni wa pori ilipandikizwa ku muzeituni wenye ulipandwa ili kuchukua nafasi ya matawi yenye ilikatwa. (Soma Waroma 11:17, 18.) Kwa hiyo, Wakristo watiwa-mafuta wenye walitoka mu mataifa ingine, kama vile Wakristo fulani katika kutaniko la Roma, walipandikizwa kwa njia ya mufano ku ule muzeituni wa mufano. Ni vile walifikia kuwa sehemu ya uzao wa Abrahamu. Ku mwanzo, walikuwa sawa vile matawi ya muzeituni wa pori, kwa sababu hawakukuwa mu agano yenye Mungu alifanya na Abrahamu. Lakini Yehova aliwatolea nafasi ya kuwa Wayahudi wa kiroho.​—Ro. 2:28, 29.

w11 15/5 uku. 25 fu. 19

‘Oh! Hekima ya Mungu Ni Kubwa Sana!’

19 Ndiyo, kusudi la Yehova kuhusu “Israeli wa Mungu” linatimia kwa njia ya ajabu sana. (Gal. 6:16) Kama vile Paulo alisema, “Israeli wote wataokolewa.” (Ro. 11:26) Wakati wenye Yehova ameweka, “Israeli wote,” ni kusema, hesabu kamili ya Waisraeli wa kiroho, watakuwa wafalme na makuhani mbinguni. Hakuna kitu chenye kinaweza kuzuia kusudi la Yehova lisitimie!

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w13 15/6 uku. 25 fu. 5

Acha Nizamu ya Yehova Ikufinyange

5 Namna gani Yehova, Mufinyanzi Mukubwa, anatumia mamlaka yake wakati wanadamu wanakatala kwa kiburi kufinyangwa naye? Fikiria jambo yenye inaweza kutokea kama udongo haufae juu ya kutengeneza chombo fulani. Mufinyanzi anaweza kutumia ule udongo juu ya kutengeneza chombo kingine ao anaweza tu kuutupa. Kwa kawaida udongo unaweza kuwa haufae kama mufinyanzi hakuufinyanga muzuri. Lakini, Mufinyanzi wetu hawezi kukosea hata kidogo wakati anatufinyanga. (Kum. 32:4) Wakati mutu anakatala Yehova amufinyange, ule mutu njo mwenye kosa. Yehova anabadilishaka namna yake ya kufinyanga wanadamu kulingana na namna wanatenda wakati anawafinyanga. Wale wenye wanaitika awafinyange wanakuwa watu wa maana kwake. Kwa mufano, Wakristo watiwa-mafuta ni “vyombo vya rehema” vyenye vimefanywa kuwa ‘vyombo kwa ajili ya matumizi yenye kuheshimika.’ Lakini, wale wenye wanakatala kwa kiburi kufinyangwa na Mungu wanakuwa ‘vyombo vya kasirani kali vyenye viko tayari kwa ajili ya uharibifu.’​—Ro. 9:19-23.

it-1-F uku. 1234 fu. 6

Wivu, Mwenye Wivu

Bidii Yenye Inatumiwa Mubaya. Mutu anaweza kuwa na bidii ao wivu kwa ajili ya jambo fulani, lakini kumbe anajidanganya na kumuchukiza Mungu. Ilikuwa vile kuhusu Wayahudi mingi mu karne ya kwanza (1-100). Walitafuta kuwa wenye haki kwa kufuata Sheria ya Musa. Lakini, Paulo alionyesha kama walitumia mubaya bidii yao kwa sababu hawakukuwa na ujuzi wa kweli. Njo maana hawakufikia kuwa wenye haki, juu haki ya kweli inatoka kwa Mungu. Kusudi wakuwe wenye haki na kutoka mu laana ya Sheria, iliomba watambue kosa yao na wamurudilie Mungu kwa kumuamini Yesu. (Ro 10:1-10). Sauli wa Tarso alikuwa mumoja wao, alikuwa na bidii sana kwa ajili ya dini ya Kiyahudi, na ‘alitesa sana kutaniko la Mungu na kuliharibu’. Alikuwa anashika sana Sheria; alikuwa “mutu mwenye hakukuwa na kosa.” (Ga 1:13, 14; Flp 3:6.) Lakini, alitumia mubaya wivu wenye alikuwa nao kwa ajili ya dini ya Kiyahudi. Juu hakukuwa na nia ya mubaya, Yehova alimuonyesha fazili zenye hazistahiliwe kupitia Kristo kwa kumusaidia atambue namna ya muzuri ya kumuabudu Mungu.​— 1Ti 1:12, 13.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine