Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • th somo ya 7 uku. 10
  • Kusema Mambo ya Kweli na Kusadikisha Wasikilizaji

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kusema Mambo ya Kweli na Kusadikisha Wasikilizaji
  • Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Kutanguliza Maandiko Muzuri
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Kuonyesha Wasikilizaji Namna ya Kutumikisha Habari
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Kutumia Maulizo
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Kujikaza Kugusa Moyo
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
Ona Habari Zaidi
Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
th somo ya 7 uku. 10

SOMO YA 7

Kusema Mambo ya Kweli na Kusadikisha Wasikilizaji

Andiko

Luka 1:3

JAMBO LA KUFANYA: Tumia chanzo cha habari chenye kutegemeka juu ya kusaidia wasikilizaji wako wafikie kuamua mambo mu njia ya muzuri.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Tafuta na utumie habari zenye zinatokana na chanzo cha habari chenye kutegemeka. Toa maelezo yenye inategemea Neno la Mungu, soma moja kwa moja mu Biblia wakati inawezekana. Kama unazungumuzia habari ya sayansi, jambo lenye lilizungumuziwa ku radio, ku televizyo ao mu gazeti fulani, jambo lenye lilionwa, ao jambo lingine la kutegemeza habari yako, chunguza mbele ya wakati juu ya kuhakikisha kwamba chanzo cha habari yako ni chenye kutumainika na ni cha sasa.

  • Tumia muzuri habari zenye umepata. Fasiria andiko kulingana na maandiko yenye inatangulia na yenye inafuata ile andiko, kulingana na ujumbe wa Biblia, na kulingana na vichapo vya “mutumwa muaminifu na mwenye busara.” (Mt. 24:45) Tumia maandishi yenye haizungumuzie mambo ya Biblia bila kubadilisha kitu na kulingana na wazo lenye muandikaji alitaka kusema.

    Shauri

    Usinenepeshe ao kutilia chumvi habari ao uwingi wa watu ao vitu. Ukuwe muangalifu juu “watu fulani” isigeuke kuwa “watu mingi,” “wakati fulani” isigeuke kuwa “kila wakati,” na “pengine” isigeuke kuwa “inawezekana.”

  • Fikiri na wasikilizaji wako. Kisha kusoma andiko ao kutaja habari fulani, uliza maulizo fulani kwa busara ao toa mufano juu ya kusaidia wasikilizaji wako wafikie kuamua mambo wao wenyewe.

MU MAHUBIRI:

Wakati unajitayarisha juu ya mahubiri, wazia mbele ya wakati maulizo yenye watu wanaweza kukuuliza, na utafute habari mu vichapo juu ya kujua namna utajibia. Kama mutu anakuuliza ulizo lenye haujue namna ya kujibia, umuambie kama utaenda kutafuta na utamuletea jibu.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine