Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr20 Mwezi wa 6 uku. 1-8
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2020
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 1-7/6
  • TAREHE 8-14/6
  • TAREHE 15-21/6
  • TAREHE 22-28/6
  • TAREHE 29/6–5/7
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2020
mwbr20 Mwezi wa 6 uku. 1-8

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 1-7/6

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 44-45

“Yosefu Anasamehe Ndugu Zake”

w15 1/5 uku. 14-15

“Mimi Niko Mahali pa Mungu?”

Yosefu akatumia mutego huo ili kuwajaribu. Aliambia watumishi wake wawafuate, wawakamate, na kuwashitaki kuwa wameiba kikombe hicho. Wakati kilipatikana katika mufuko wa Benyamini wote walirudishwa tena kwa Yosefu. Wakati huo Yosefu alikuwa na nafasi ya kujua ndugu zake ni watu wa namna gani. Yuda ndiye alisema kwa ajili yao wote. Alimuomba sana Yosefu awahurumie na hata alisema kuwa wote 11 wako tayari kuwa watumwa huko Misri. Yosefu alijibia kama ni Benyamini tu ndiye atakuwa mutumwa lakini wengine walipaswa kurudi nyumbani.​—Mwanzo 44:2-17.

Yuda alisema maneno yenye kuonyesha mambo yenye kuwa katika moyo wake. Alisema hivi: ‘Yeye tu ndiye aliyesalia [aliyebaki] wa mama yake, na baba yake anamupenda.’ Bila shaka maneno hayo yalimugusa Yosefu kwa sababu alikuwa mutoto wa kwanza wa Raheli, bibi mupendwa wa Yakobo, aliyekufa wakati alikuwa anazaa Benyamini. Kwa kweli, Yosefu na Yakobo waliendelea kumukumbuka Raheli. Pengine ni jambo hilo lilifanya Yosefu amupende sana Benyamini.​—Mwanzo 35:18-20; 44:20.

Yuda aliendelea kumuomba Yosefu asimufanye Benyamini kuwa mutumwa. Hata alisema kuwa yeye iko tayari kuwa mutumwa pa nafasi ya Benyamini. Kisha alimalizia kwa kusema maneno haya yenye kutoka moyoni: ‘Kwa maana ninawezaje kwenda kwa baba yangu bila yeye nisije nikautazama musiba utakaomupata baba yangu!’ (Mwanzo 44:18-34) Ilikuwa wazi kabisa kuwa Yuda alikuwa amebadilika. Alionyesha moyo wa toba, lakini pia alionyesha moyo muzuri wa huruma, kuhangaikia wengine na kujitia pa nafasi ya wengine.

Yosefu hakuweza tena kujizuia. Alipaswa kufunua namna alikuwa anajisikia katika moyo. Kisha kuambia watumishi wake wote waondoke, alilia kwa sauti kubwa. Sauti yake ilifika hata kwenye nyumba ya Farao. Mwishowe alijitambulisha kwa ndugu zake: “Mimi ni Yosefu ndugu yenu.” Walishangaa sana, na Yosefu aliwakumbatia na kuwaambia kuwa amewasamehe kutoka moyoni mambo yote yenye walimufanyia. (Mwanzo 45:1-15) Kwa kufanya hivyo, alifuata mufano wa Yehova ambaye iko tayari kusamehe. (Zaburi 86:5) Sisi pia tuko tayari kusamehe wengine?

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-1-F uku. 606

Kupasua Nguo

Ilikuwa alama ya huzuni yenye Wayahudi na pia watu wa inchi za mashariki walikuwa wanazoea kufanya, zaidi sana kisha kusikia habari ya kifo cha mutu wa jamaa ya karibu. Mara mingi mutu alikuwa anapasua sehemu ya mbele ya nguo mupaka kifua kibakie wazi, haiko kupasua nguo sana mupaka ikuwe yenye haifae tena kuvaa.

Katika Biblia, Rubeni, mutoto wa kwanza wa Yakobo, njo mutu wa kwanza mwenye anazungumuziwa kuwa alifanya vile; wakati alirudia kwenye lile shimo na kuona kwamba Yosefu hakukuwa ndani, alipasua nguo yake na kusema hivi: “Mutoto haiko! Na mimi​—nitafanya nini?” Kwa sababu alikuwa mutoto wa kwanza, Rubeni alikuwa na daraka la kuchunga ndugu yake mudogo. Wakati waliambia Yakobo habari ya uongo kama mutoto wake amekufa, yeye pia alipasua nguo yake na akavaa nguo za gunia ili kuomboleza (Mwa 37:29, 30, 34), na kule Misri ndugu za Yosefu walionyesha huzuni yao kwa kupasua nguo zao wakati Benyamini alifanywa aonekane kuwa mwizi.​—Mwa 44:13.

w04 15/8 uku. 15 fu. 15

Wanachukiwa Bila Sababu

15 Ni nini kinachoweza kutusaidia tusiwe na kinyongo kuelekea wale wanaotuchukia bila sababu? Kumbuka kwamba Shetani na roho waovu ndio maadui wetu wakuu. (Waefeso 6:12) Ingawa watu fulani hututesa kimakusudi, wengi wanaowapinga watu wa Mungu hufanya hivyo kwa kutojua au kwa kutumiwa vibaya na wengine. (Danieli 6:4-16; 1 Timotheo 1:12, 13) Yehova anataka “watu wa namna zote” wapate nafasi ya ‘kuokolewa na kupata ujuzi sahihi wa kweli.’ (1 Timotheo 2:4) Kwa kweli, watu fulani waliokuwa wapinzani sasa wamekuwa ndugu zetu Wakristo kwa sababu ya kutazama mwenendo wetu usiolaumika. (1 Petro 2:12) Zaidi ya hayo, tunaweza kujifunza jambo fulani kutokana na kielelezo cha Yosefu mwana wa Yakobo. Ingawa Yosefu aliteseka sana kwa sababu ya ndugu zake wa kambo, hakuwawekea kinyongo. Kwa nini? Kwa sababu alitambua kwamba Yehova alihusika katika jambo hilo na kuelekeza mambo ili kutimiza kusudi Lake. (Mwanzo 45:4-8) Vivyo hivyo, Yehova anaweza kutumia mateso yoyote ambayo huenda tukapata isivyo haki ili kulitukuza jina lake.​—1 Petro 4:16.

Hotuba

w06 1/2 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Je, Yosefu, mtumishi mwaminifu wa Yehova, alitumia kikombe cha pekee cha fedha kusoma ishara za bahati, kama ambavyo huenda ikadokezwa na andiko la Mwanzo 44:5?

Kwa kweli, hakuna sababu ya kuamini kwamba Yosefu alitumia aina yoyote ya uaguzi.

Biblia inaonyesha maoni ya Yosefu kuhusu kufanya uchawi ili kujua mambo ya wakati ujao. Mapema, alipoombwa atafsiri ndoto za Farao, Yosefu alisisitiza tena na tena kwamba Mungu tu ndiye anayeweza ‘kutangaza’ matukio ya wakati ujao. Kwa sababu hiyo, Farao mwenyewe aliamini kwamba Mungu ambaye Yosefu anaabudu​—Mungu wa kweli, na si nguvu za uchawi​—alimwezesha Yosefu kujua mambo ya wakati ujao. (Mwanzo 41:16, 25, 28, 32, 39) Katika Sheria ambayo Musa alipewa baadaye, Yehova alikataza uchawi au uaguzi, hivyo akahakikisha kwamba ni Yeye tu anayetabiri matukio ya wakati ujao.​—Kumbukumbu la Torati 18:10-12.

Kwa nini basi Yosefu alionyesha kupitia mtumishi wake kwamba alitumia kikombe cha fedha “kusoma ishara za bahati kwa ustadi”? (Mwanzo 44:5) Tunahitaji kufikiria ni katika hali gani maneno hayo yalisemwa.

Kwa sababu ya njaa kali, ndugu za Yosefu walisafiri kwenda Misri ili kutafuta chakula. Miaka kadhaa mapema, ndugu haohao walimwuza Yosefu utumwani. Sasa, kwa kuwa hawakumtambua, waliomba msaada kwa ndugu yao ambaye alikuwa sasa msimamizi wa chakula nchini Misri. Yosefu hakujitambulisha kwao. Badala yake, aliamua kuwajaribu. Yosefu alitaka kujua ikiwa walikuwa wametubu kwelikweli. Pia, alitaka kujua ni kwa kadiri gani walimpenda ndugu yao Benyamini na baba yao, Yakobo, ambaye alimpenda sana Benyamini. Hivyo, Yosefu alitumia ujanja.​—Mwanzo 41:55–44:3.

Yosefu alimwamuru mmoja wa watumishi wake kujaza mifuko ya ndugu zake kwa chakula, na kumrudishia kila mmoja pesa zake katika kinywa cha mfuko wake, kisha atie kikombe cha fedha cha Yosefu katika kinywa cha mfuko wa Benyamini. Wakati wote huo, Yosefu alijitambulisha kuwa msimamizi wa nchi ya kipagani. Alijifanya, kwa matendo yake, na kwa lugha yake kuwa msimamizi huyo mpagani ili ndugu zake wasimtambue.

Yosefu alipowakabili ndugu zake, aliendelea kutumia mbinu yake kwa kuwauliza hivi: “Je, hamkujua kwamba mimi naweza kusoma ishara za bahati kwa ustadi?” (Mwanzo 44:15) Hivyo, inaonekana kikombe hicho kilitumiwa kama mbinu tu. Yosefu hakutumia kikombe hicho kusoma ishara za bahati, na pia Benyamini hakukiiba.

TAREHE 8-14/6

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 46-47

“Yosefu Anaokoa Familia Yake Wakati wa Njaa”

w87 1/5 uku. 15 fu. 2

Kuhifadhi Uhai Katika Wakati wa Njaa

2 Miaka ile saba ya utele ikaisha na njaa ikaanza sawa na vile Yehova alivyokuwa ametabiri​—njaa, si katika Misri tu, bali “juu ya uso wa dunia.” Wakati watu wenye kukumbwa na njaa katika Misri walipoanza kumulilia Farao awape mkate, aliwaambia: “Nendeni kwa Yusufu. Lolote awaambialo yeye, ndilo mtakalopasa kufanywa.” Yusufu aliuzia Wamisri nafaka mpaka pesa zao zikamalizika kabisa. Ndipo alipokubali mifugo yao iwe malipo. Mwisho, watu wakamjia Yusufu, wakisema: “Tununue sisi na nchi yetu kwa ajili ya mkate, nasi pamoja na nchi yetu tutakuwa watumwa kwa Farao.” Kwa hiyo, Yusufu akamnunulia Farao nchi yote ya Wamisri.​—Mwanzo 41:53-57; 47:13-20, NW.

kr uku. 235 fu. 11-12

Ufalme Unatimiza Mapenzi ya Mungu Duniani

11 Kuwa na vitu tele. Watu wa ulimwengu wana njaa sana ya kiroho. Biblia inasema hivi: ‘Tazama! Siku zinakuja, asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova, Nami nitaleta njaa katika inchi, wala si njaa ya mukate, nami nitaleta kiu, wala si kiu ya maji, bali ya kuyasikia maneno ya Yehova.’ (Amo. 8:11) Ujiulize, raia wa Ufalme wa Mungu nao wana njaa ya kiroho? Yehova alitabiri kwamba hali ya watu wake itakuwa tofauti na hali ya maadui wao. Alitabiri hivi: ‘Watumishi wangu watakula, lakini ninyi mutakuwa na njaa. Tazama! Watumishi wangu watakunywa, lakini ninyi mutakuwa na kiu. Tazama! Watumishi wangu watashangilia, lakini ninyi mutaona aibu [haya].’ (Isa. 65:13) Umejionea utimizo wa maneno hayo?

12 Tunapewa chakula cha kiroho kwa uwingi. Jambo hilo linafananishwa na muto mukubwa sana na wenye kujaa sana. Tuna vichapo ambavyo vinategemea Biblia, tuna habari mbalimbali ambazo zimerekodiwa na pia tuna video; mikutano na mikusanyiko; habari mbalimbali zenye kupatikana kwenye Internete. Mambo yote hayo yanafanyiza muto mukubwa ambao unaendelea kutiririka, ni kusema, tunapata miongozo mingi ya kiroho katika ulimwengu huu wenye kuwa na njaa kali ya kiroho. (Eze. 47:1-12; Yoe. 3:18) Wewe haufurahi kuona utimizo wa ahadi ya Yehova ya kutolea watu wake chakula cha kiroho kwa uwingi katika siku zetu? Unahakikisha kwamba unakula kwa kawaida kwenye meza ya Yehova?

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-1-F uku. 227 fu. 16

Tabia na Ishara Mbalimbali

Kuweka mukono juu ya macho ya mutu mwenye kufa. Maneno yenye Yehova aliambia Yakobo kama, “Yosefu ataweka mukono wake juu ya macho yako” (Mwa 46:4), ilipenda kuonyesha kama Yosefu njo angefunga macho ya Yakobo kisha kifo cha Yakobo, daraka lenye kwa kawaida lilikuwa la mutoto mwanaume wa kwanza. Kwa hiyo, hapa inaonekana kama Yehova alionyesha Yakobo kama Yosefu njo angepewa haki ya muzaliwa wa kwanza.​—1Ny 5:2.

nwtsty maelezo ya Mdo 7:14

Watu 75 kwa ujumla: Pengine Stefano hakukuwa anataja maneno ya andiko fulani la Maandiko ya Kiebrania wakati anatoa hesabu yote ya watu wa familia ya Yakobo katika Misri kuwa 75. Hii hesabu haipatikane katika maandishi ya Wamasora ya Maandiko ya Kiebrania. Mwa 46:26 inasema: “Wale wote wenye walikuwa wazao wa Yakobo na wenye waliingia Misri pamoja naye walikuwa makumi sita na sita (66), bila kuhesabu bibi za wana wa Yakobo.” Mustari wa 27 unaendelea hivi: “Watu wote wa nyumba ya Yakobo wenye waliingia Misri walikuwa makumi saba (70).” Hapa watu wanahesabiwa katika njia mbili tofauti, inaoekakana kuwa hesabu ya kwanza inatia ndani tu wazao wake mwenyewe, na ya pili ni jumla ya watu wenye walikuja Misri. Hesabu ya wazao wa Yakobo inatajwa pia mu Kut 1:5 na Kum 10:22, kwenye namba “70” inaonyeshwa. Inaonekana kama Stefano anaonyesha hesabu ya tatu yenye inatia ndani watu wengine wa jamaa ya mbali. Watu fulani wanawaza kama ile hesabu inatia ndani watoto na wajukuu wa watoto wa Yosefu, Manase na Efraimu, wenye wanatajwa katika tafsiri ya Septante katika Mwa 46:20. Wengine wanasema kama ile hesabu inatia ndani bibi za watoto wa Yakobo, wenye hawatajwe mu hesebu yenye kuwa katika Mwa 46:26. Kwa hiyo namba “75” ni jumla ya watu wote. Lakini pengine ile hesabu ilitoka katika kopi za Maandiko ya Kiebrania yenye watu walikuwa wanatumia mu karne ya kwanza, kisha kuzaliwa kwa Yesu. Kwa miaka mingi, watu wenye elimu wamejua kama namba “75” njo hesabu yenye ilipatikana kwenye Mwa 46:27 na Kut 1:5 katika Septante ya Kigiriki. Zaidi ya ile, katika miaka ya 1900 kulipatikana vipande mbili vya vitabu vya kukunjwa vya Bahari ya Chumvi vyenye kuwa na andiko la Kut 1:5 katika Kiebrania, na vinatumia pia namba “75.” Inawezekana hesabu yenye Stefano alitoa inategemea moja kati ya ile maandishi ya zamani. Hata ikuwe ni mawazo gani njo ya kweli, hesabu ya Stefano inaonyesha tu njia tofauti ya kuhesabia jumla ya wazao wa Yakobo.

TAREHE 15-21/6

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 48-50

“Wakristo Wenye Kukomaa, Mukuwe na Mambo Mingi ya Kuelezea Wengine”

it-1-F uku. 1228 fu. 8

Yakobo

Muda mufupi mbele ya kifo chake, Yakobo alibariki wajukuu wake, ni kusema watoto wa Yosefu, na Mungu alimuongoza ili atie Efraimu, mwenye alikuwa mudogo, mbele ya Manase mwenye alikuwa mukubwa. Kisha Yakobo akaambia hivi Yosefu mwenye angepewa sehemu mbili ya uriti yenye muzaliwa wa kwanza alikuwaka anapewa: “Ninakupatia sehemu moja zaidi ya inchi kuliko ndugu zako, yenye nilikamata katika mukono wa Waamori kwa upanga wangu na upinde wangu.” (Mwa 48:1-22; 1Ny 5:1) Kwa sababu Yakobo alikuwa ameuza kwa njia ya amani shamba lenye lilikuwa karibu na Shekemu kutoka kwa wana wa Hamori, (Mwa 33:19, 20) inaonekana kama ile ahadi yenye alimutolea Yosefu ilionyesha imani yenye Yakobo alikuwa nayo; mu ile ahadi alisema kwa njia ya unabii kama wakati wenye kuja wazao wake wangepata ushindi juu ya Kanaani, ilikuwa kama vile ile jambo ilikuwa imekwisha kutimia kupitia upanga wake na upinde wake. (Ona WAAMORI.) Sehemu mbili ya Yosefu ya inchi yenye wangeshinda ilikuwa sehemu mbili yenye kabila la Efraimu na kabila la Manase ilipewa.

it-1-F uku. 623 fu. 1

Siku za Mwisho

Unabii Wenye Yakobo Alitoa Mbele Akufe. Wakati Yakobo aliambia hivi watoto wake: “Mujikusanye pamoja ili niwaambie mambo yenye yatawapata katika kipindi cha mwisho cha zile siku” ao “siku zenye kuja” (AT), alimaanisha wakati wenye kuja, ni kusema, wakati maneno yake ingeanza kutimia. (Mwa 49:1) Zaidi ya miaka 200 mbele ya pale Yehova aliambia Abramu (Abrahamu), tate ya Yakobo, kama wazao wake wangeteseka kwa miaka 400. (Mwa 15:13) Kwa hiyo, katika hii hali, wakati wenye kuja wenye Yakobo aliita “kipindi cha mwisho cha zile siku” ungeanza kisha ile miaka 400 ya mateso. (ili kupata habari zaidi juu ya Mwanzo 49, ona habari zenye kuzungumuzia kila mutoto wa Yakobo.) Ingetazamiwa kama ule unabii ungefikia kutimia pia juu ya “Israeli wa Mungu.”​—Ga 6:16; Ro 9:6.

w07 1/6 uku. 28 fu. 10

Waliozeeka Ni Baraka Kwa Vijana

10 Pia, waliozeeka wanaweza kuwa na uvutano mzuri juu ya waamini wenzao. Yosefu, mwana wa Yakobo, alifanya tendo moja rahisi la imani katika uzee wake ambalo lilikuwa na matokeo makubwa juu ya mamilioni ya waabudu wa kweli walioishi baada yake. Yosefu alikuwa na umri wa miaka 110 ‘alipotoa amri kuhusu mifupa yake,’ kwamba wakati Waisraeli wangetoka Misri, wangepaswa kubeba mifupa yake. (Waebrania 11:22; Mwanzo 50:25) Amri hiyo ilitoa tumaini na uhakikisho wa kwamba baada ya kifo cha Yosefu, Waisraeli wangekombolewa kutoka katika maisha magumu ya utumwa wa miaka mingi.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w04 1/6 uku. 15 fu. 4-5

Wanaomtukuza Mungu Hubarikiwa

4 Kabla ya kuingia katika Nchi ya Ahadi, kabila la Israeli la Gadi liliomba liruhusiwe kuishi katika eneo la malisho, mashariki ya Yordani. (Hesabu 32:1-5) Kuishi katika eneo hilo kungemaanisha kwamba wangekabili hali ngumu sana. Makabila yaliyokuwa magharibi yangekingwa na Bonde la Yordani ambalo lilikuwa kizuizi cha asili kwa shambulizi la kijeshi. (Yoshua 3:13-17) Hata hivyo, kichapo The Historical Geography of the Holy Land, cha George Adam Smith, kinasema hivi kuhusu maeneo yaliyo mashariki ya Yordani: ‘Maeneo hayo yote ni tambarare, nayo yamesambaa juu ya uwanda mkubwa wa juu wa Uarabuni. Hivyo, yamekuwa yakishambuliwa kila mara na wahama-hamaji wenye njaa, ambao baadhi yao hufurika katika maeneo hayo kila mwaka wakitafuta malisho.’

5 Kabila la Gadi lingekabilianaje na tatizo hilo lenye kuendelea? Alipokaribia kufa, babu yao Yakobo alitabiri hivi: “Naye Gadi, atavamiwa na kikundi cha waporaji, lakini yeye atavamia upande wa nyuma kabisa.” (Mwanzo 49:19) Yakichukuliwa kijuujuu huenda maneno hayo yakaonekana kuwa yenye kuhuzunisha. Hata hivyo, ukweli ni kwamba wazao wa Gadi waliamuriwa walipize kisasi. Yakobo aliwahakikishia kwamba kama wangefanya hivyo, wavamizi hao wangerudi nyuma kwa aibu, nao wazao wa Gadi wangewafuatia upande wa nyuma kabisa.

it-1-F uku. 299 fu. 7

Benyamini

Uwezo wa kupigana wa wazao wa Benyamini ulionyeshwa katika unabii wenye Yakobo alisema wakati alikuwa karibu kufa; mu ule unabii alisema hivi juu ya mutoto wake mupendwa: “Benyamini ataendelea kupasua kama imbwa wa pori. Asubui atakula mawindo, na mangaribi atagawanya vitu vyenye vinachukuliwa katika vita.” (Mwa 49:27) Wapiganaji Wabenyamini walijulikana kwa sababu ya uwezo wao wa kutumia kombeo, walikuwa na uwezo wa kurusha jiwe kwa kombeo kwa kutumia mukono wa kuume ao wa kushoto na walikuwa wanalenga “unywele” bila kukosea. (Amu 20:16; 1Ny 12:2) Muamuzi Ehudi alikuwa Mubenyamini; alikuwa anatumikisha mukono wake wa kushoto, na ni yeye aliua Mufalme Egloni mwenye alikuwa anawatesa. (Amu 3:15-21) Tunaweza tena kusema kama ilikuwa “asubui” ya Ufalme wa Israeli njo kabila la Benyamini, hata kama lilikuwa “kabila la kidogo sana,” lilitoa mufalme wa kwanza wa Israeli, ni kusema, Sauli mwana wa Kishi, mwenye alionekana kuwa mupiganaji mwenye nguvu mwenye alipiganisha Wafilisti. (1Sa 9:15-17, 21) Vilevile “mangaribi,” kuhusu taifa la Israeli, kabila la Benyamini lilitoa Malkia Esta na Waziri Mukubwa Mordekai, wenye walisaidia ili kuokoa Waisraeli ili wasiangamizwe chini ya Utawala wa Uajemi.​—Est 2:5-7.

TAREHE 22-28/6

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUTOKA 1-3

“Nitakuwa Kile Ninachagua Kuwa”

w13 15/3 uku. 25 fu. 4

Tuliheshimu Jina Kubwa la Mungu

4 Soma Kutoka 3:10-15. Musa alipokuwa na miaka 80, Mungu alimupa daraka nzito, alimuamuru hivi: “Uwatoe watu wangu wana wa Israeli kutoka Misri.” Kwa heshima, Musa alikubali, lakini alimuuliza Mungu ulizo fulani lenye maana sana. Alimuuliza hivi: ‘Jina lako nani?’ Kwa kuwa jina la Mungu lilijulikana tangu zamani, Musa alitaka kujua nini kabisa? Ni wazi kwamba, Musa alitaka kujua mengi kuhusu mutu anayeitwa kwa jina hilo, jambo ambalo lingesadikisha watu wake kwamba kwa kweli Mungu angewakomboa. Musa alikuwa na haki ya kuuliza hivyo kwa sababu Waisraeli walikuwa wamepitisha miaka mingi katika utumwa. Bila shaka wangeweza kujiuliza ikiwa kweli Mungu wa mababu zao angewakomboa. Lakini pia, Waisraeli fulani walikuwa hata wameanza kuabudu miungu ya Wamisri.​—Eze. 20:7, 8.

kr 43, Sanduku

MAANA YA JINA LA MUNGU

JINA Yehova linatoka katika neno la Kiebrania, ambalo linamaanisha “kuwa.” Watu fulani wenye elimu ya Biblia wanawaza kwamba neno linalotumiwa hapa linatoa wazo la kufanya jambo fulani litendeke. Kwa hiyo, watu wengi wanaelewa kwamba jina la Mungu linamaanisha “Yeye Anayefanya Kuwa.” Maelezo hayo yanapatana kabisa na cheo cha Yehova cha kuwa Muumbaji. Ni yeye alifanya viumbe vyenye akili na ulimwengu kuwa, na anaendelea kufanya mapenzi yake na kusudi lake kuwa jambo la kweli.

Kwa hiyo, namna gani tunaweza kuelewa jibu ambalo Yehova alimupatia Musa linalopatikana katika andiko la Kutoka 3:13, 14? Musa aliuliza hivi: “Tuseme nimefika kwa wana wa Israeli nami niwaambie, ‘Mungu wa mababu zenu amenituma kwenu,’ nao waniambie, ‘Jina lake ni nani?’ Ninapaswa kuwaambia nini?” Yehova alimujibia hivi: ‘Nitakuwa Kile Nitachagua Kuwa.’

Tujue kwamba hapa Musa hakuwa anamuomba Yehova amuambie jina lake. Kwa sababu tangu zamani Musa na Waisraeli walikuwa wanajua vizuri jina la Mungu. Musa alipenda Yehova amufunulie jambo fulani lenye kutia imani nguvu na lenye kuonyesha kama yeye ni Mungu wa namna gani. Jambo fulani ambalo lingeweza pia kuonyeshwa na maana ya jina lake. Kwa hiyo, wakati Yehova anamujibia kwamba, ‘Nitakuwa Kile Nitachagua Kuwa,’ alikuwa anafunua namna iko, ni kusema, hali yake fulani yenye kufurahisha. Katika kila hali Yehova anakuwa chochote kinachohitajika ili kutimiza kusudi lake. Kwa mufano, Yehova alichagua kuwa Mwokozi, Mupana-sheria, na Mutoaji (ao Mwenye Kutimiza Mahitaji) kwa Musa na kwa Waisraeli, na mambo mengine. Yehova yeye mwenyewe anachagua kuwa chochote kinachohitajika ili kutimiza ahadi zake kwa watu wake. Hata kama jina Yehova linaweza kumaanisha anachagua kuwa, jina hilo lina maana zaidi ya hiyo. Linamaanisha pia kwamba yeye anaweza kufanya uumbaji wake uwe chochote anachotaka ili kutimiza kusudi lake.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

g04 8/4 uku. 6 fu. 4

Musa Mtu Halisi au wa Hadithi?

Hata hivyo, je, haishangazi kwamba binti ya Mfalme wa Misri angemlea mtoto kama huyo? Sivyo, kwa kuwa dini ya Wamisri ilifundisha kwamba matendo ya fadhili yalikuwa takwa la kwenda mbinguni. Kuhusiana na hatua ya kumlea mtoto huyo, mwanaakiolojia Joyce Tyldesley anasema: “Wanawake Wamisri walikuwa na usawa na wanaume Wamisri. Walipaswa kuwa na haki sawa kisheria na kiuchumi, na . . . wanawake wangewalea watoto wa wengine.” Hati moja ya kale ya mafunjo inayohusu kuwalea watoto wa wengine inasema kuhusu mwanamke Mmisri aliyewalea watumwa wake. Kuhusu jinsi mama ya Musa alivyopewa kazi ya kumnyonyesha, kitabu The Anchor Bible Dictionary kinasema: “Mpango wa kumlipa mama ya Musa amtunze Musa . . . unafanana na mipango ya kuwalea watoto huko Mesopotamia.”

w04 15/3 uku. 24 fu. 4

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Kutoka

3:1​—Yethro alikuwa kuhani wa aina gani? Nyakati za wazee wa ukoo kichwa cha familia alikuwa pia kuhani wa familia yake. Yaonekana Yethro alikuwa kichwa cha kabila fulani la Wamidiani. Kwa kuwa Wamidiani walikuwa wazao wa Abrahamu kupitia Ketura, yaelekea walifahamu ibada ya Yehova.​—Mwanzo 25:1, 2.

Hotuba

w02 15/6 uku. 11 fu. 1-4

Kitu Chenye Thamani Zaidi Kuliko Hazina za Misri

Akiwa na umri wa miaka 40, wakati ambapo Musa angetazamiwa kuwa Mmisri halisi, ‘alitoka kuwaendea ndugu zake, akatazame mizigo yao.’ Mambo aliyotenda baada ya hapo yanaonyesha kwamba hakuenda kuchunguza tu hali yao; alitamani sana kuwasaidia. Alipoona Mmisri akimpiga Mwebrania, aliingilia kati, na kumwua mwonezi huyo. Tendo hilo lilionyesha kwamba moyo wa Musa ulikuwa pamoja na ndugu zake. Yaelekea mtu aliyeuawa alikuwa ofisa ambaye alikuwa akifanya kazi yake. Wamisri walitazamia Musa awe mwaminifu kwa Farao. Hata hivyo, Musa alichochewa na kupenda haki, sifa aliyoidhihirisha siku iliyofuata ambapo aligombana na Mwebrania aliyekuwa akimpiga mwenzake isivyo haki. Musa alitaka kuwakomboa Waebrania kutoka kwenye utumwa mkatili, lakini Farao alipopata habari kwamba Musa si mwaminifu kwake, alitaka kumwua. Musa alilazimika kutorokea Midiani.​—Kutoka 2:11-15; Matendo 7:23-29.

Wakati wa Musa wa kuwakomboa watu wa Mungu ulitofautiana na ule wa Yehova. Hata hivyo, matendo yake yalidhihirisha kwamba alikuwa na imani. Andiko la Waebrania 11:24-26 linasema: “Kwa imani Musa, alipokuwa amekua akawa mtu mzima, alikataa kuitwa mwana wa binti ya Farao, akichagua kutendwa vibaya pamoja na watu wa Mungu badala ya kuwa na mfurahio wa muda wa dhambi.” Kwa nini? “Kwa sababu alikadiria shutumu la Kristo kuwa utajiri mkubwa zaidi kuliko hazina za Misri; kwa maana alikaza macho kuelekea malipo ya thawabu.” Neno hili “Kristo” ambalo limetumiwa kwa njia ya pekee linamaanisha “mtiwa-mafuta,” na linamfaa Musa kwa sababu baadaye Yehova alimpa kazi ya pekee kwa njia ya moja kwa moja.

Ebu wazia! Musa alilelewa kama mwana wa mfalme wa Misri. Angeweza kuwa na kazi nzuri maishani na kufurahia anasa za kila namna, hata hivyo alikataa mambo hayo yote. Aliona kwamba hangeweza kuishi katika nyumba ya Farao mwonevu na wakati uleule aonyeshe kwamba anampenda Yehova na kupenda haki. Ujuzi pamoja na kutafakari ahadi za Yehova kwa baba zake Abrahamu, Isaka, na Yakobo ulimchochea Musa atamani kibali cha Mungu. Kwa sababu hiyo, Yehova alimtumia Musa kwa njia ya pekee ili kutimiza makusudi Yake.

Sote tunapaswa kuamua ni mambo gani yaliyo muhimu zaidi. Labda unakabili uamuzi mzito kama Musa. Je, unapaswa kuacha mazoea fulani au mambo fulani yanayoonekana kuwa yenye faida, bila kujali hasara utakayopata? Ikiwa unakabili uamuzi kama huo, kumbuka kwamba Musa alithamini zaidi urafiki pamoja na Yehova kuliko hazina zote za Misri, naye hakujuta.

TAREHE 29/6–5/7

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | KUTOKA 4-5

“Nitakuwa Pamoja na Wewe Wakati Uko Unasema”

w10 15/10 uku. 13-14

Yehova Ana Maoni Gani Kuhusu Visingizio?

“Sina uwezo.” Huenda ukahisi kwamba hustahili kuwa mhudumu wa habari njema. Watumishi fulani waaminifu wa Yehova katika nyakati za Biblia walihisi kwamba hawakuwa na uwezo wa kutimiza migawo ambayo Yehova aliwapa. Fikiria mfano wa Musa. Alipopewa kazi ya pekee na Yehova, Musa alisema hivi: “Nakuomba radhi, Yehova, lakini mimi si msemaji mzuri, tangu jana wala tangu kabla ya hapo wala tangu uliposema na mtumishi wako, kwa maana kinywa changu ni kizito na ulimi wangu ni mzito.” Ingawa Yehova alimpa uhakikisho, Musa alijibu: “Nakuomba radhi, Yehova, lakini tuma, tafadhali, kupitia mkono wa yule utakayemtuma.” (Kut. 4:10-13) Yehova alitenda jinsi gani?

w14 15/4 uku. 9 fu. 5-6

Unamuona “Yeye Asiyeonekana”?

5 Mbele Musa arudi Misri, Mungu alimufundisha kanuni moja ya maana sana. Kisha Musa aliandika kanuni hiyo katika kitabu cha Ayubu inayosema hivi: ‘Kumuogopa Yehova​—hiyo ndiyo hekima.’ (Ayu. 28:28) Ili kumusaidia Musa awe na woga huo na kutenda kwa hekima, Yehova alimuonyesha tofauti iliyo kati ya wanadamu na Mungu Mweza-Yote. Yehova alimuuliza hivi: ‘Ni nani aliyekifanya kinywa kwa ajili ya mwanadamu ao ni nani ambaye humufanya mutu kuwa bubu ao kiziwi ao mwenye kuona vizuri ao kipofu? Je, si mimi, Yehova?​—Kut. 4:11.

6 Yehova alipenda kumufundisha somo gani? Musa hakupaswa kuogopa. Ni Yehova aliyemutuma, na ni yeye aliyemupatia kila kitu alichohitaji ili kumutolea Farao ujumbe. Tena, Farao hakuwa kitu mbele ya Yehova. Zaidi ya hilo, hiyo haikuwa mara ya kwanza watumishi wa Yehova wakuwe katika hatari katika utawala wa Misri. Pengine Musa alifikiri namna Yehova alivyolinda Abrahamu, Yosefu, na Musa mwenyewe wakati wa utawala wa Farao wengine. (Mwa. 12:17-19; 41:14, 39-41; Kut. 1:22–2:10) Kwa kuwa alikuwa na imani katika Yehova, “Yeye asiyeonekana,” Musa alifika mbele ya Farao kwa ujasiri na kutangaza kila neno ambalo Yehova alimuagiza aseme.

w10 15/10 uku. 14

Yehova Ana Maoni Gani Kuhusu Visingizio?

Yehova hakukubali visingizio vya Musa vya kukataa kutimiza mgawo huo. Hata hivyo, Yehova alimweka rasmi Haruni ili amsaidie Musa kutimiza mgawo huo. (Kut. 4:14-17) Zaidi ya hayo, katika miaka iliyofuata, Yehova alimtegemeza Musa na kumpa chochote alichohitaji ili kufanikiwa katika kutimiza migawo aliyopewa na Mungu. Leo, unaweza kuwa na hakika kwamba Yehova atawachochea waamini wenzako wenye uzoefu wakusaidie pia ili utimize huduma yako. Zaidi ya yote, Neno la Mungu linatuhakikishia kwamba Yehova atatuwezesha tuwe na sifa zinazostahili ili tutimize kazi ambayo ametuamuru kufanya.​—2 Kor. 3:5; ona sanduku “Miaka Yenye Furaha Zaidi Katika Maisha Yangu.”

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w04 15/3 uku. 28 fu. 4

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Maneno haya ya Sipora “wewe ni bwana-arusi wa damu kwangu” si ya kawaida. Yanaonyesha nini kumhusu Sipora? Kwa kukubaliana na matakwa ya agano la tohara, Sipora alikubali kuingia katika uhusiano wa agano pamoja na Yehova. Baadaye, agano la Sheria lililofanywa pamoja na Waisraeli lilionyesha kwamba katika uhusiano wa agano, Yehova anaweza kuonwa kuwa mume huku yule anayefanya agano naye akionwa kuwa mke. (Yeremia 31:32) Kwa hiyo, alipomtaja Yehova (kupitia malaika wake aliyemwakilisha) kuwa “bwana-arusi wa damu,” yaonekana Sipora alikuwa akikubali kutii matakwa ya agano hilo. Ilikuwa kana kwamba alikuwa amekubali kuwa mke katika agano la tohara, huku Yehova Mungu akiwa mume. Vyovyote vile, kwa sababu ya tendo lake muhimu la kutii takwa la Mungu, maisha ya mwana wake hayakuwa hatarini tena.

it-1-F uku. 1257 fu. 3

Yehova

Kwa hiyo, “kujua,” hakumaanishe tu kufahamu ao kutambua kitu fulani ao mutu fulani. Nabali, mwanaume mupumbavu, alijua jina la Daudi, lakini aliuliza, “Daudi ni nani?” ni kama vile alikuwa anauliza “Daudi ni nini? (1Sa 25:9-11; linganisha na 2Sa 8:13.) Kwa hiyo, Farao naye aliambia hivi Musa: “Yehova ni nani, ili nitii sauti yake kwa kuruhusu Israeli waende? Simujue Yehova hata kidogo, na tena, sitaruhusu Israeli waende.” (Kut 5:1, 2) Kwa kusema vile, kwa kweli Farao alimaanisha kama hakumujua Yehova kuwa Mungu wa kweli ao kuwa iko na mamlaka juu ya Mufalme wa Misri na mambo yenye alikuwa anafanya, na hakuona kama Yehova iko na nguvu ya kutimiza Mapenzi yake kama vile Musa na Haruni walikuwa wametangaza. Lakini sasa Farao na Misri yote, na pia Waisraeli, wangejua maana ya kweli ya jina hilo, ni kusema, mutu mwenye jina hilo linawakilisha. Kama vile Yehova aliambia Musa, ile ingefanya Mungu atimize kusudi lake kwa ajili ya Waisraeli, kwa kuwakomboa, na kuwapatia Inchi ya Ahadi, na kwa kufanya vile alitimiza agano lenye alifanyaka na mababu zao. Ni katika ile njia, kama vile Mungu alisema, ‘hakika wangejua kwamba yeye ni Yehova Mungu wao.’​—Kut 6:4-8; ona MWEZA-YOTE.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine