Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr20 Mwezi wa 5 uku. 1-8
  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2020
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 4-10/5
  • TAREHE 11-17/5
  • TAREHE 18-24/5
  • TAREHE 25-31/5
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2020
mwbr20 Mwezi wa 5 uku. 1-8

Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha

TAREHE 4-10/5

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 36-37

“Ndugu za Yosefu Wanamusikilia Wivu”

w14 1/8 uku. 12-13

‘Tafazali, Musikilize Ndoto Hii’

Biblia inajibu hivi: ‘Ndugu zake walipoona kwamba baba yao alimupenda kuliko ndugu zake wote, wakaanza kumuchukia, nao hawakusema naye kwa amani.’ (Mwanzo 37:4) Wivu wao unaweza kueleweka, lakini hawakuonyesha hekima walipojiacha waongozwe na chuki hiyo yenye kuua. (Methali 14:30; 27:4) Wakati fulani umejikuta ukiwa mwenye kujaa wivu mutu fulani anapopewa uangalifu ao pendeleo ambalo ulitaka? Kumbuka ndugu za Yosefu. Wivu wao uliwaongoza kufanya jambo ambalo lingewaletea huzuni kubwa baadaye. Mufano wao unawakumbusha Wakristo kwamba ni jambo la hekima ‘kushangilia pamoja na watu wanaoshangilia.’​—Waroma 12:15.

Bila shaka, Yosefu aliona kwamba ndugu zake hawakuwa wanamupenda. Je, alificha nguo yake hiyo ya hali ya juu sana wakati ndugu zake walikuwa karibu ili wasiione? Inawezekana alishawishiwa kufanya hivyo. Hata hivyo, kumbuka kwamba Yakobo alitaka kanzu hiyo iwe ishara ya kwamba anamukubali Yosefu na anamupenda. Yosefu alipenda baba yake aendelee kumuamini, kwa hiyo aliendelea kuvaa nguo hiyo. Mufano wake unaweza kutusaidia. Hata ikiwa baba yetu wa mbinguni hana ubaguzi hata siku moja, wakati fulani anachagua wale wanaomutumikia kwa uaminifu na kuwapa pendeleo fulani. Zaidi ya hayo, anawaomba wawe tofauti kabisa na ulimwengu huu muovu na usiokuwa na mwenendo muzuri. Kama vile kanzu ya pekee ya Yosefu, tabia ya Wakristo wa kweli inawafanya wawe tofauti na watu wanaowazunguka. Wakati fulani, tabia kama hiyo inachochea wivu na uadui. (1 Petro 4:4) Mukristo anaweza kuficha mambo yanayoweza kumutambulisha kwelikweli kuwa mutumishi wa Mungu? Hapana​—Yosefu pia hakuficha kanzu yake.​—Luka 11:33.

w14 1/8 uku. 13 fu. 2-4

‘Tafazali, Musikilize Ndoto Hii’

Ndoto hizo zilitoka kwa Yehova Mungu. Zilikuwa za kiunabii, na Mungu alimuambia Yosefu aeleze habari ya ndoto hizo. Katika njia fulani, Yosefu alipaswa kufanya kama vile manabii wa wakati uliopita walivyofanya wakati walieleza ujumbe wa Mungu na hukumu juu ya watu wake wasiotii.

Kwa heshima, Yosefu aliwaambia ndugu zake hivi: ‘Tafazali, musikilize ndoto hii ambayo nimeota.’ Ndugu zake walisikia ndoto hiyo na hawakuipenda hata kidogo. Walijibu hivi: ‘Je, kwa kweli utakuwa mufalme juu yetu? Ao utatutawala?’ Habari hiyo inaendelea hivi: ‘Basi wakapata sababu mupya ya kumuchukia kwa sababu ya ndoto zake na maneno yake.’ Wakati Yosefu alielezea baba yake na ndugu zake ndoto ya pili, nayo pia haikuwapendeza. Habari hiyo inasema hivi: ‘Baba yake akamukemea na kumuambia: Ndoto hii ambayo umeota inamaanisha nini? Je, mimi na pia mama yako na ndugu zako kwa kweli tutakuja na kukuinamia?’ Lakini, Yakobo aliendelea kufikiria maneno hayo. Inawezekana Yehova alikuwa anazungumuza na kijana huyo?​—Mwanzo 37:6, 8, 10, 11.

Yosefu hakuwa mutumishi wa Yehova wa kwanza wala wa mwisho aliyeombwa aeleze ujumbe wa kiunabii ambao haukuwa unapendwa na watu wengi na ambao hata ungemuletea mateso. Yesu alikuwa mujumbe mukubwa zaidi kati ya watu waliokuwa na ujumbe kama huo, na aliwaelezea wafuasi wake hivi: “Ikiwa wamenitesa mimi, watawatesa ninyi pia.” (Yohana 15:20) Wakristo wa miaka yote wanaweza kujifunza mambo mengi kutokana na imani na uhodari wa kijana Yosefu.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-F-1 uku. 693

Edomu

(Nyekundu), Waedomu.

Edomu ilikuwa jina lingine lenye Esau, ndugu pacha wa Yakobo, alipewa. (Mwa 36:1) Alipewa jina hilo kwa sababu aliuzisha haki yake ya kuwa muzaliwa wa kwanza kwa ajili ya muchuzi mwekundu. (Mwa 25:30-34) Na jambo la kushangaza ni kwamba, wakati Esau alizaliwa alikuwa na rangi ya mwekundu kabisa (Mwa 25:25), na udongo na majiwe yenye ilikuwa katika sehemu yenye yeye na wazao wake waliishi ilikuwa pia na rangi ya mwekundu.

it-F-1 uku. 964

Kulinda

Wakati muchungaji alisema kama angechunga kikundi cha wanyama, alikuwa anakubali kama atawalinda kulingana na vile sheria iliomba. Alikuwa anahakikishia mwenye wale wanyama kama atawapatia chakula na atawalinda ili wasiibwe, na kama angeshindwa kufanya vile, angemulipa. Lakini, daraka lake halikukuwa kamili, kwa sababu ile sheria iliondolea muchungaji kosa ikiwa kungetokea hali fulani yenye kupita uwezo wa mwanadamu, kama vile kushambuliwa na munyama wa pori. Lakini ili asionekane kuwa mwenye kosa, alipaswa kutoa ushuhuda kwa mwenye wale wanyama, kwa mufano angeonyesha munyama mwenye kufa mwenye alishambuliwa. Kisha mwenye wale wanyama kuchunguza ushuhuda, alipaswa kutangaza kama ule muchungaji hakuwa na kosa.

Ni kanuni ileile njo ilitumiwa kwa ujumla wakati mutu alipewa daraka la kulinda vitu fulani, hata katika uhusiano wa familia; kwa mufano kulingana na sheria, mutoto mwanaume wa kwanza alionwa kuwa mulinzi wa ndugu na dada zake wadogo. Kwa hiyo, tunaweza kuelewa juu ya nini Rubeni, ndugu mukubwa wa Yosefu, alihangaikia uzima wa Yosefu kama vile inaonyeshwa katika Mwanzo 37:18-30, wakati ndugu zake wengine walisema kama watamuua. “Akasema: ‘Tusiondoe uzima wake.’ . . . ‘Musimwange damu. . . . musimuumize.’ Alitaka kumuokoa kutoka katika mikono yao ili amurudishe kwa baba yake.” Na wakati Rubeni alitambua kama Yosefu hakukuwa tena, alihangaika sana mupaka “akapasua nguo zake” na kusema: “Mutoto haiko! Na mimi​—nitafanya nini?” Alijua kama yeye njo angeonekana kuwa mwenye kosa kwa sababu ya kupotea kwa Yosefu. Ili asionekane kuwa mwenye kosa, ndugu zake walifanya kwa uangalifu ushuhuda wa uongo wenye kuonyesha kama munyama wa pori alimuua Yosefu. Walifanya vile kwa kupasua-pasua nguo ya Yosefu na kuiingiza katika damu ya mbuzi. Kisha wakaonyesha baba yao Yakobo, muamuzi wa familia, ule ushuhuda, na Yakobo aliondolea Rubeni kosa, kwa sababu, kisha kuona nguo ya Yosefu yenye kujaa damu, Yakobo aliwaza kama Yosefu alikuwa ameuawa.​—Mwa 37:31-33.

Hotuba

w02 15/10 uku. 30-31

Je, Wakristo Wanapaswa Kuwa na Wivu?

Hata hivyo, wivu wa kimungu unafaa katika ibada ya kweli. Tunapoanza kuhangaikia mno sifa au haki zetu, wivu wa kimungu hutufanya tumfikirie Yehova. Hutuchochea tutafute njia za kutangaza ukweli kumhusu, tutetee njia zake na watu wake.

Akiko, mhudumu wa wakati wote wa Mashahidi wa Yehova, alizomewa vikali na mwenye-nyumba ambaye hakujua ukweli juu ya sheria ya Mungu kuhusu damu. Kwa busara, Akiko alilitetea Neno la Mungu, hata alitaja matatizo ya kitiba yanayosababishwa na kutiwa damu mishipani. Akiwa na hamu kubwa ya kusema kuhusu Yehova, Akiko aliyabadili mazungumzo hayo akitilia maanani sababu iliyomfanya mwanamke huyo ampinge​—kutoamini kwamba kuna Muumba. Akiko alimwonyesha mwenye-nyumba huyo jinsi uumbaji unavyothibitisha kwamba kuna Muumba. Ushahidi wake wa ujasiri uling’oa chuki isiyo na msingi ya mwanamke huyo naye akakubali kujifunza Biblia pamoja na Akiko. Sasa mwanamke huyo aliyekuwa na hasira hapo awali anamwabudu Yehova.

Wivu unaofaa, au bidii kwa ajili ya ibada ya kweli hutuchochea kuwa macho na kutumia fursa yoyote kuhubiri juu ya imani yetu na kuitetea kazini, shuleni, madukani, na tunaposafiri. Kwa mfano, Midori ameazimia kuwahubiria wafanyakazi wenzake kuhusu imani yake. Mfanyakazi mmoja mwenye umri wa miaka 40 hivi alisema kwamba hapendezwi kamwe na Mashahidi wa Yehova. Baadaye, walipokuwa wakizungumza pindi moja, mwanamke huyo alilalamika kwamba binti yake alikuwa ameanza kuharibika. Midori alimwonyesha kitabu Maswali Ambayo Vijana Huuliza​—Majibu Yafanyayo Kazi, na alijitolea kujifunza na bintiye kitabu hicho. Funzo lilianzishwa, lakini mama yake hakuhudhuria funzo hilo. Midori aliamua kumwonyesha mwanamke huyo video Jehovah’s Witnesses​—The Organization Behind the Name.* Hilo liliondoa maoni yake mengi yasiyofaa. Video hiyo ilimchochea kusema hivi: “Nataka kuwa kama Mashahidi wa Yehova.” Alijiunga na bintiye kujifunza Biblia.

Wivu unaofaa una manufaa kwa kutaniko la Kikristo. Huchangia roho ya upendo na shauku na hutuchochea kukataa katakata mambo ambayo yanaweza kuwaumiza ndugu zetu wa kiroho, kama vile porojo zenye kudhuru na uasi-imani. Wivu wa kimungu hutufanya tuunge mkono maamuzi ya wazee, ambao nyakati nyingine hulazimika kuwakaripia watenda-dhambi. (1 Wakorintho 5:11-13; 1 Timotheo 5:20) Paulo alieleza hivi kuhusu wivu aliokuwa nao kuelekea waamini wenzake wa kutaniko la Korintho: “Nina wivu juu yenu nikiwa na wivu wa kimungu, kwa maana mimi binafsi niliwaposea nyinyi mume mmoja ili nipate kuwatoa nyinyi mkiwa bikira safi kiadili kwa Kristo.” (2 Wakorintho 11:2) Vivyo hivyo, wivu wetu hutuchochea kufanya yote tuwezayo kulinda usafi wa kiroho, wa kiadili na wa mafundisho kutanikoni.

Naam, wivu unaofaa, yaani, wivu wa kimungu huwajenga wengine. Huleta kibali cha Yehova na ni moja ya sifa ambazo Wakristo wanadhihirisha leo.​—Yohana 2:17.

TAREHE 11-17/5

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 38-39

“Yehova Hakumuacha Yosefu”

w14 1/11 uku. 12 fu. 4-5

Namna Gani ‘Ninaweza Kufanya Ubaya Huu Mukubwa?’

‘Basi Yosefu akapelekwa Misri, na Potifa, ofisa wa makao ya Farao, mukubwa wa walinzi, Mumisri, akamununua kutoka kwa Waishmaeli waliokuwa wamemuleta huko.’ (Mwanzo 39:1) Katika maneno hayo machache, habari ya Biblia inatusaidia kuwazia namna kijana huyo mwanaume alizarauliwa alipouzishwa tena. Alikuwa tu kama kitu! Tunaweza kumufikiria Yosefu akifuata mukubwa wake wa kazi, ofisa wa makao ya mufalme wa Misri, wote wawili wanapita katika barabara za muji zenye watu wengi na zenye kujaa maduka, wanaelekea kwenye makao ao nyumba mupya ya Yosefu.

Nyumba hiyo ilikuwa tofauti kabisa na kila nyumba Yosefu alikuwa amekwisha kuona. Alikomalia katika familia yenye kuhama-hama iliyoishi katika mahema. Walikuwa wanahama-hama na kulisha makundi yao ya kondoo. Huko Misri, Wamisri wote waliokuwa matajiri kama Potifa waliishi katika nyumba nzuri sana zilizopakwa rangi zenye kuangara. Watu wanaochimba vitu vya zamani wanasema kuwa Wamisri walipenda bustani zenye kuwa muzuri sana. Bustani hizo zilizungukwa na kuta na miti yenye kivuli na visima vyenye utulivu kwenye walipanda mafunjo, yungiyungi na mimea mingine yenye kukomaa ndani ya maji. Nyumba fulani zilijengwa nafasi yenye kufichwa katikati ya bustani. Nyumba hizo zilikuwa na baraza (véranda) za kuvutia hewa, madirisha za juu ili kuingiza hewa ndani ya nyumba, na vyumba vingi, kutia ndani chumba kikubwa cha kulia chakula na vyumba vya watumishi.

w14 1/11 uku. 14-15

Namna Gani ‘Ninaweza Kufanya Ubaya Huu Mukubwa?’

Hatujue mambo mengi juu ya magereza ya Wamisri wakati huo. Watu wanaochimbua vitu vya zamani wamepata mabomoko ya nafasi kama hizo, majengo makubwa yaliyo kama ngome yenye kuwa na magereza na vyumba vya chini ya udongo. Baadaye Yosefu alieleza nafasi hiyo kwa kutumia neno linalomaanisha moja kwa moja “tundu.” Hilo linaonyesha kwamba hiyo ilikuwa nafasi yenye giza na bila tumaini. (Mwanzo 40:15) Kitabu cha Zaburi kinaonyesha kuwa Yosefu alipatwa na mateso mengine: ‘Walimufunga miguu kwa minyororo, na shingoni kwa nira ya chuma.’ (Zaburi 105:17, 18; Biblia Habari Njema) Nyakati fulani, Wamisri walitia wafungwa katika vizuizi vilivyofunga mikono yao nyuma kwenye viwiko vya mikono; wafungwa wengine walikuwa na mikufu ya chuma iliyofungwa kwenye shingo zao. Yosefu anapaswa kuwa aliteseka sana kwa kutendewa vibaya hivyo, wakati hakufanya jambo fulani mbaya lililostahili malipizi hayo!

Na zaidi ya hilo, mateso hayo hayakukuwa ya muda mufupi tu. Habari hiyo inasema kwamba Yosefu ‘aliendelea kuwa humo katika nyumba ya gereza.’ Alifanya miaka mingi katika nafasi hiyo mbaya! Na hakujua ikiwa siku moja atafunguliwa. Siku hizo za kwanza zenye kuhuzunisha zilipofikia kuwa majuma, na kisha miezi, ni nini kilimusaidia Yosefu asifikie kuvunjika moyo na kukosa tumaini?

Habari hiyo inatupatia jibu hili lenye kutia moyo: ‘Yehova akaendelea kuwa pamoja na Yosefu, akazidi kumufanyia fazili zenye upendo.’ (Mwanzo 39:21) Kuta za gereza, minyororo, vyumba vya chini ya udongo visivyokuwa na mwangaza, vyote hivyo haviwezi kuzuia upendo mushikamanifu wa Yehova kuwafikia watumishi wake. (Waroma 8:38, 39) Tunaweza kumufikiria Yosefu akimuelezea baba yake wa mbinguni mateso yake katika sala na kupata amani na utulivu ambao ni “Mungu wa faraja yote” tu anaweza kutoa. (2 Wakorintho 1:3, 4; Wafilipi 4:6, 7) Yehova alimufanyia tena Yosefu nini? Tunasoma kuwa Yosefu aliendelea ‘kupata kibali machoni pa ofisa mukubwa wa nyumba ya gereza.’

w14 1/11 uku. 15 fu. 2

Namna Gani ‘Ninaweza Kufanya Ubaya Huu Mukubwa?’

Habari hiyo inatupatia jibu hili lenye kutia moyo: ‘Yehova akaendelea kuwa pamoja na Yosefu, akazidi kumufanyia fazili zenye upendo.’ (Mwanzo 39:21) Kuta za gereza, minyororo, vyumba vya chini ya udongo visivyokuwa na mwangaza, vyote hivyo haviwezi kuzuia upendo mushikamanifu wa Yehova kuwafikia watumishi wake. (Waroma 8:38, 39) Tunaweza kumufikiria Yosefu akimuelezea baba yake wa mbinguni mateso yake katika sala na kupata amani na utulivu ambao ni “Mungu wa faraja yote” tu anaweza kutoa. (2 Wakorintho 1:3, 4; Wafilipi 4:6, 7) Yehova alimufanyia tena Yosefu nini? Tunasoma kuwa Yosefu aliendelea ‘kupata kibali machoni pa ofisa mukubwa wa nyumba ya gereza.’

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-F-2 uku. 445

Onani

(Onani) [jina lenye linatokana na muzizi wenye kumaanisha “mwanzo wa nguvu za uzazi; nguvu mingi”].

Mwana wa pili wa Yuda, mwenye alizaa na binti ya Shua, mwanamuke Mukanaani. (Mwa 38:2-4; 1Ny 2:3) Yehova alimuua Eri, ndugu ya Onani kwa sababu alikuwa anafanya mambo ya mubaya. Kwa sababu Eri alikufa bila kuzaa mutoto, Yuda alimuomba Onani aoe Tamari, bibi ya ndugu yake Eri. Kama angezaa naye mutoto mwanaume, ule mutoto hangeendelesha uzao wa familia ya Onani, na uriti wa muzaliwa wa kwanza ungekuwa wake kwa sababu angekuwa muriti wa Eri; Lakini, kama hakuna muriti mwenye angezaliwa, Onani njo angepata uriti. Wakati Onani alilala na Tamari, “alimwanga mbegu zake za uzazi chini” kuliko kuzipatia Tamari. Onani hakukuwa anafanya tendo la kugusa-gusa viungo vya uzazi ili kutimiza tamaa ya ngono, kwa sababu ile habari inasema kama “wakati alilala na bibi ya ndugu yake” alimwanga mbegu zake za uzazi chini. Inaonekana kama Onani alikuwa anafanya kimakusudi ili kuzuia mbegu zake za uzazi kuingia katika kiungo cha uzazi cha Tamari. Onani pia aliuawa na Yehova, bila kuwa na mutoto, haiko kwa sababu alifanya tendo la kugusa-gusa viungo vya uzazi ili kutimiza tamaa ya ngono, lakini kwa sababu hakumutii baba yake, alikuwa na pupa, na alifanya zambi kwa kukosa kuheshimia mupango wa Mungu kuhusu ndoa.​—Mwa 38:6-10; 46:12; Hes 26:19.

w04 15/1 uku. 30 fu. 4-5

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Yuda alikosea kwa sababu hakumtoa Shela kwa Tamari awe mume wake kama alivyoahidi. Pia alifanya ngono na mwanamke ambaye alifikiri kwamba ni kahaba wa hekalu. Jambo hilo lilipingana na kusudi la Mungu kwamba, mwanamume afanye ngono katika ndoa tu. (Mwanzo 2:24) Kwa kweli, Yuda hakufanya ngono na kahaba. Badala yake, alitimiza bila kujua daraka la mwana wake Shela kwa kufanya ndoa ya ndugu-mkwe na hivyo akawa baba ya mrithi halali.

Lakini Tamari hakuwa na mwenendo mbaya kiadili. Wana wake wawili mapacha hawakuonwa kuwa wana wa uasherati. Wakati Boazi wa Bethlehemu alipomuoa Ruthu Mmoabu katika ndoa ya ndugu-mkwe, wazee wa Bethlehemu walimsifu Perezi mwana wa Tamari na kumwambia Boazi hivi: “Nyumba yako na iwe kama nyumba ya Perezi, ambaye Tamari alimzalia Yuda, kutokana na uzao ambao Yehova atakupa kutoka kwa huyu mwanamke kijana.” (Ruthu 4:12) Pia Perezi anatajwa katika orodha ya mababu wa Yesu Kristo.​—Mathayo 1:1-3; Luka 3:23-33.

TAREHE 18-24/5

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 40-41

“yehova anamukomboa Yesefu”

w15 1/2 uku. 14 fu. 4-5

“Je, Tafsiri Si za Mungu?”

Labda mukubwa wa watumishi wa kumupatia mufalme kinywaji alimusahau Yosefu, lakini Yehova hakumusahau hata kidogo. Siku moja usiku, Yehova alimutumia Farao ndoto mbili zenye haziwezi kusahauliwa. Katika ndoto ya kwanza, mufalme aliona ngombe saba wanene na wenye sura ya muzuri waliotoka katika Muto Nile. Ngombe hao wanene walifuatwa na ngombe saba wenye sura mbaya na wenye kukonda. Ngombe wenye kukonda walimeza ngombe wanene. Kisha hapo, katika ndoto Farao aliona tawi moja la nafaka likitokeza masuke saba ya muzuri. Lakini baadaye masuke mengine saba, yaliyokaushwa na upepo na membamba, yakatokea na kumeza masuke hayo ya muzuri. Asubuhi, Farao aliamuka akiwa mwenye kuhangaishwa sana kwa sababu ya ndoto hizo. Kwa hiyo, aliita watu wake wote wenye hekima na makuhani wenye kufanya uchawi ili wamuelezee maana ya ndoto yake. Wote hawakuweza. (Mwanzo 41:1-8) Hatujue ikiwa ndoto hizo ziliwashangaza sana ao ikiwa walitoa mawazo yenye kupingana. Kwa vyovyote, Farao alivunjika moyo sana, lakini alitamani zaidi kuelewa maana ya ndoto zake zisizoeleweka.

Mwishowe, mukubwa wa watumishi wa kumupatia mufalme kinywaji alimukumbuka Yosefu! Zamiri yake ilimusumbua, kwa hiyo akamuambia Farao juu ya kijana mwanaume wa pekee katika gereza ambaye, miaka mbili iliyopita, alimuelezea bila kukosea maana ya ndoto yake na ya mukubwa wa watumishi wa kumupatia mufalme mukate. Mara moja, Farao aliagiza Yosefu aitwe kutoka katika gereza.​—Mwanzo 41:9-13.

w15 1/2 uku. 14-15

“Je, Tafsiri Si za Mungu?”

Yehova anapenda watu wanyenyekevu na waaminifu, kwa hiyo, haishangaze kuona kuwa alimupatia Yosefu jibu ambalo lilishinda watu wenye hekima na makuhani. Yosefu alieleza kuwa ndoto mbili za Farao zilikuwa na maana moja. Kwa kurudilia ujumbe huo mara mbili, Yehova alikuwa anaonyesha kuwa jambo hilo lilikuwa “limewekwa imara,” ni kusema, lingetimia kabisa. Ngombe wanene na masuke ya muzuri ya nafaka yalifananisha miaka saba ya chakula kingi katika Misri, lakini ngombe wenye kukonda na masuke membamba ya nafaka yalifananisha miaka saba ya njaa yenye ingefuata miaka ya chakula kingi. Njaa hiyo ingemaliza chakula katika inchi.​—Mwanzo 41:25-32.

w15 1/2 uku. 15 fu. 3

“Je, Tafsiri Si za Mungu?”

Farao alitimiza maneno yake. Yosefu alivalishwa nguo za kitani ya muzuri bila kukawia. Farao alimupatia mukufu wa zahabu, pete ya muhuri, gari la kifalme, na mamlaka ya kusafiri kotekote katika inchi na kutimiza mipango yake. (Mwanzo 41:42-44) Kwa hiyo, katika siku moja, Yosefu alitoka katika gereza na kuingia katika nyumba ya mufalme. Aliamuka asubuhi akiwa mufungwa wa hali ya chini, na alilala usiku akiwa kwenye cheo cha pili kisha Farao. Inaonekana wazi kuwa imani yake katika Yehova Mungu ilitetewa! Yehova aliona ukosefu wote wa haki mutumishi wake alitendewa kwa miaka mingi. Alishugulikia mambo hayo kwa wakati wenye kufaa na kwa njia yenye kufaa. Yehova alitaka kushugulikia mambo mabaya yenye Yosefu alitendewa lakini alitaka pia kulinda taifa la Israeli la wakati uliokuwa unakuja. Katika habari inayokuja ya sehemu hii, tutaona namna Yehova alifanya hivyo.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

w15 1/11 uku. 9 fu. 1-3

Ulijua?

Sababu gani Yosefu alikata ndevu mbele ya kuenda kuonana na Farao?

Kulingana na kitabu cha Mwanzo, Farao aliamuru kama Yosefu, mufungwa Muebrania, aletwe haraka mbele yake ili aeleze maana ya ndoto zake zenye zilimusumbua. Wakati huo, Yosefu alikuwa amefungwa kwa miaka mingi. Hata kama Farao alimuita haraka, Yosefu alichukua wakati wa kukata ndevu. (Mwanzo 39:20-23; 41:1, 14) Kwa sababu muandikaji alitaja jambo hilo lenye kuonekana kuwa halina maana, hilo linaonyesha kama alijua muzuri desturi za Wamisri.

Kuacha ndevu zikomae lilikuwa jambo la kawaida kwa mataifa mengi ya zamani, na hata kwa Waebrania. Tofauti na hilo, kitabu kimoja cha McClintock na Strong kinasema kama, “Wamisri wa zamani ndio tu taifa la Mashariki lenye lilipinga kukomalisha ndevu.” (Cyclopedia of Biblical, Theological, na Ecclesiastical Literature)

Iliomba mutu akate ndevu tu? Gazeti moja linasema kama, desturi za sherehe za Wamisri ziliomba mwanaume ajitayarishe ili kuingia mbele ya Farao kama vile alipaswa kujitayarisha mbele ya kuingia katika hekalu. (Biblical Archaeology Review) Katika hali hiyo, Yosefu alipaswa kukata nywele zote kwenye kichwa chake na kwenye mwili wake.

w09 15/11 uku. 28 fu. 14

Kuonyesha Adabu Tukiwa Wahudumu wa Mungu

14 Wazazi waliomwogopa Mungu katika nyakati za Biblia walihakikisha kwamba watoto wao walijifunza mambo ya msingi kuhusu kuonyesha adabu nyumbani. Fikiria jinsi Abrahamu na mwana wake Isaka walivyozungumza kwa heshima kwenye andiko la Mwanzo 22:7. Pia, kisa cha Yosefu kinaonyesha kwamba alizoezwa vizuri na wazazi wake. Alipofungwa gerezani, aliwatendea kwa adabu hata wafungwa wenzake. (Mwa. 40:8, 14) Maneno aliyomwambia Farao yanaonyesha kwamba alikuwa amejifunza njia inayofaa ya kuzungumza na mtu mwenye cheo kikubwa.​—Mwa. 41:16, 33, 34.

TAREHE 25-31/5

UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 42-43

“Yosefu Anaonyesha Kabisa Sifa ya Kujizuia”

w15 1/5 uku. 13 fu. 5

“Mimi Niko Mahali pa Mungu?”

Yosefu alitambua ndugu zake? Ndiyo, aliwatambua mara moja! Zaidi ya hilo, wakati aliona wanamuinamia, alikumbuka mara moja wakati alikuwa kijana. Biblia inatuambia kuwa, “Yosefu akakumbuka ndoto alizoota,” ndoto zenye Yehova alimuonyesha wakati alikuwa kijana. Ndoto hizo zilionyesha kuwa wakati fulani ndugu zake watamuinamia; na ni vile walikuwa wanafanya sasa! (Mwanzo 37:2, 5-9; 42:7, 9) Yosefu atafanya nini sasa? Atakumbatia ndugu zake? Ao atalipiza kisasi?

w15 1/5 uku. 14 fu. 1

“Mimi Niko Mahali pa Mungu?”

Pengine hautajikuta katika hali kama hiyo. Lakini katika ulimwengu wa leo kukosa kuelewana na kutengana katika familia ni mambo yenye kuenea sana. Kwa sababu ya hali yetu ya zambi, tunaweza kutaka tu kufuata mawazo yetu na kutenda bila kufikiri wakati tunapambana na magumu. Ni jambo la hekima sana kufuata mufano wa Yosefu na kujikaza kutambua namna Yehova anapenda tushugulikie mambo. (Methali 14:12) Kumbuka kuwa ni jambo la maana kufanya amani pamoja na watu wa familia, lakini ni jambo la maana hata zaidi kufanya amani pamoja na Yehova na Mwana wake.​—Mathayo 10:37

w15 1/5 uku. 14 fu. 2

“Mimi Niko Mahali pa Mungu?”

Ili kujua namna mioyo ya ndugu zake ilikuwa, Yosefu alitumia njia mbalimbali ili kuwajaribu. Kwanza alitumia mutafsiri ili kuzungumuza nao kwa ukali; aliwashitaki kuwa wapelelezi. Ili kujitetea, walimuelezea juu ya familia yao; hata walimuambia habari ya maana sana. Walimuambia kama walikuwa na mudogo yao wa mwisho aliyebaki nyumbani. Yosefu alijikaza ili wengine wasione namna alijisikia moyoni. Kweli mudogo yake alikuwa angali muzima? Sasa Yosefu alijua jambo la kufanya. Alisema hivi: ‘Hivyo ndivyo mutajaribiwa,’ kisha akawaambia kama ni lazima aone mudogo yao wa mwisho. Kisha wakati fulani, alikubali kuwaacha warudi kwao ili wamuletee mudogo yao wa mwisho ikiwa tu mumoja kati yao atakubali kubaki Misri kama mufungwa.​—Mwanzo 42:9-20.

it-2-F uku. 50 fu. 4

Yosefu

Mambo yenye ilitokea ilifanya ndugu za Yosefu waanze kuwaza kama Mungu alikuwa anawapatia malipizi kwa sababu walikuwa wameuzisha Yosefu ili akuwe mutumwa miaka mingi mbele ya pale. Walizungumuzia kosa lao mbele ya Yosefu, kwa sababu hawakukuwa wamemutambua. Wakati Yosefu alisikia maneno yao yenye kuonyesha kama walikuwa wametubu, aliguswa moyo sana mupaka akaondoka mbele yao ili kulia. Wakati alirudia alifunga Simeoni mupaka wakati wenye watarudia na kuleta ndugu yao mudogo.​—Mwa 42:21-24.

Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 835

Rubeni

Sifa fulani za Rubeni zilionekana wazi wakati alisadikisha ndugu zake kenda wasiue Yosefu lakini wamutupe ndani ya kisima chenye kukauka. Rubeni alipanga kurudia kwa siri ili kumutosha Yosefu ndani ya kile kisima. (Mwa 37:18-30) Kisha miaka zaidi ya 20 wakati walienda kule Misri, walishitakiwa kuwa wapelelezi. Wakati walikuwa wanasema kama walishitakiwa vile kwa sababu walimutendea Yosefu mubaya, Rubeni aliwakumbusha kama hakufanya pamoja nao mupango wa kuua Yosefu. (Mwa 42:9-14, 21, 22) Tena, wakati Yakobo alikataa kumuacha Benyamini aende nao katika safari yao ya pili ya kuenda Misri, Rubeni njo alitoa wana wake wawili ili kuhakikisha maneno yake, alisema hivi: ‘Unaweza kuwaua kama simulete [Benyamini] kwako.’​—Mwa 42:37.

w04 15/1 uku. 29 fu. 1

Mambo Makuu Kutoka Kitabu cha Mwanzo​—II

43:32​—Kwa nini lilikuwa chukizo kwa Wamisri kula chakula pamoja na Waebrania? Huenda sababu kuu ilikuwa hasa ubaguzi wa kidini au kiburi cha kijamii. Wamisri pia walichukia wachungaji. (Mwanzo 46:34) Kwa nini? Huenda wachungaji walikuwa karibu na tabaka la chini katika mfumo wa matabaka wa Wamisri. Au labda kwa kuwa hakukuwa na ardhi ya kutosha ya kulima, Wamisri waliwachukia watu waliotafuta malisho kwa ajili ya wanyama wao.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine