Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 13-19/4
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 31
“Yakobo na Labani Wanafanya Agano la Amani”
it-1-F uku. 943
Galeedi
Kisha kushugulikia kwa amani mambo yenye ilifanya wasielewane, Yakobo na Labani walifanya agano. Kwa hiyo, Yakobo alisimamisha nguzo ya majiwe na akaambia “ndugu” zake wafanye rundo la majiwe, pengine lenye kufanana na meza, na ni pale walikulia chakula kisha kufanya agano. Kisha Labani akapatia ile fasi jina la lile rundo, aliipatia jina la Kiaramu (Kisiria) “Yegar-sahaduta,” lakini Yakobo akaita ile fasi “Galeedi,” jina ileile lakini katika Kiebrania. Labani akasema hivi: “Rundo hili [Kiebrania, gal] ni ushahidi [Kiebrania, ʽedh] kati yangu na wewe leo.” (Mwa 31:44-48) Lile rundo la majiwe (na ile nguzo ya majiwe) lilikuwa kama ushahidi kwa wapita-njia wote. Lilikuwa kama vile mustari wa 49 unasema, “Munara wa Mulinzi [Kiebrania, mits·pahʹ],” wenye kuonyesha kama Yakobo na Labani walikuwa wamekubaliana kama kutaendelea kuwa amani kati yao na kati ya familia zao. (Mwa 31:50-53) Kisha pale, wakati fulani majiwe iliendelea kutumiwa katika ile njia ili kutoa ushahidi bila neno.—Yos 4:4-7; 24:25-27.
it-2-F uku. 1089-1090
Munara wa Mulinzi
Yakobo alisimamisha rundo la majiwe na kuliita “Galeedi” (maana yake, “Rundo la Ushahidi”) na “Munara wa Mulinzi.” Kisha Labani akasema hivi: “Yehova aendelee kuchungulia kati yako na mimi wakati tutakuwa hatuonane.” (Mwa 31:45-49) Lile rundo la majiwe lingeonyesha kama Yehova alikuwa anachungulia ili kuona kama Yakobo na Labani walikuwa wanaheshimia agano lao la amani.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
it-2-F uku. 1062
Terafimu
Vitu vya zamani vyenye vilivumbuliwa ndani ya udongo kule Mesopotamia vinaonyesha kama ule mwenye alikuwa na sanamu za terafimu angepokea uriti wa familia. Kulingana na kibao kimoja chenye kilipatikana Nuzi, kama mwana-mukwe angekuwa na miungu ya familia, katika hali fulani angekuwa na haki ya kuenda kwenye tribinali na kuomba mali ya baba-mukwe wake mwenye amekufa. (Ancient Near Eastern Texts, yenye iliandikwa na J. Pritchard, 1974, uku. 219, 220, na maelezo ya chini 51) Inawezekana ile njo ilifanya Raheli, awaze kama alikuwa na haki ya kubeba ile terafimu sababu ya udanganyifu wenye baba yake alifanyia bwana yake Yakobo. (Linganisha na Mwa 31:14-16.) Kwa sababu terafimu ilikuwa ya maana sana na ilipatia mutu haki ya kupata uriti, ile inaweza kutusaidia kuelewa juu ya nini Labani alihangaika sana ili aipate, na akafikia hata kufanya safari ya siku saba yeye na ndugu zake ili kumufuata Yakobo. (Mwa 31:19-30) Kwa kweli, Yakobo hakujua hata kidogo jambo lenye Raheli alifanya (Mwa 31:32), na Biblia haisema kama kuko siku yenye alijaribu kutumikisha ile terafimu ili apate uriti kutoka kwa watoto wa Labani. Yakobo hakuwa na lazima ya kutumia zile sanamu. Kisha wakati fulani, inawezekana Yakobo alizika ile terafimu pamoja na miungu yote ya kigeni yenye watu wa jamaa yake walimupatia, aliizika chini ya muti mukubwa wenye ulikuwa karibu na shekemu.—Mwa 35:1-4.
Yehova Ni Makao Yetu
Yakobo alipofika Harani, mujomba wake Labani alimukaribisha kwa uchangamufu na kisha akamutolea Lea na Rachel, binti zake, ili wawe bibi zake. Ni kweli kwamba baadaye Labani alijaribu kumupunja Yakobo, kwa kubadili mushahara wake mara kumi! (Mwa. 31:41, 42) Hata hivyo, Yakobo alivumilia ukosefu huo wa haki akiwa hakika kwamba Yehova ataendelea kumushugulikia, na kweli Yehova alimushugulikia. Kwa kweli, wakati Mungu alimuambia Yakobo arudi Kanaani, muzee huyo alikuwa amekwisha pata “makundi makubwa na wajakazi na watumishi wanaume na ngamia na punda.” (Mwa. 30:43) Yakobo alishukuru sana na kusali hivi: ‘Mimi sistahili fazili zote zenye upendo na uaminifu wote ambao umemuonyesha mutumishi wako, kwa maana nilivuka huu muto Yordani nikiwa na fimbo yangu tu na sasa nimekuwa kambi mbili.”— Mwa. 32:10.
TAREHE 20-26/4
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 32-33
“Uko Unapigana ili Kupata Baraka?”
Yehova Ni Makao Yetu?
Maandiko yana mifano mingi ya wale waliojitahidi sana kumtafuta Yehova. Mmoja wao ni Yakobo, ambaye alipigana mweleka kwa bidii na malaika wa Mungu aliyekuwa amejivika mwili wa binadamu. Kwa sababu hiyo, Yakobo akapewa jina Israeli (Aliyeshindana na Mungu) kwa sababu ‘alishindana’ naye, au alikuwa mwenye udumifu, alijitahidi, alistahimili. Malaika huyo alimbariki kwa bidii yake.—Mwanzo 32:24-30.
it-1-F uku. 356
Kilema, Ulemavu
Ulemavu wa Yakobo. Wakati Yakobo alikuwa na miaka 97 hivi, alipigana usiku muzima na malaika wa Mungu mwenye alikuwa amevaa mwili wa wanadamu. Aliendelea kumuzuia malaika asiende mupaka ule malaika amubariki. Wakati walikuwa wanapigana, malaika aligusa tundu la maungio ya kiuno cha Yakobo, na kuiondoa mahali pake. Njo maana Yakobo alianza kutembea kwa kukokota muguu wake. (Mwa 32:24-32; Ho 12:2-4) Ile ilimusaidia Yakobo akumbuke kwamba, hata kama alikuwa ‘ameshindana na Mungu [malaika wa Mungu] na wanadamu na mwishowe alishinda,’ kama vile malaika alisema, kwa kweli hakushinda malaika mwenye nguvu wa Mungu. Ilikuwa tu kusudi la Mungu kuruhusu Yakobo ashindane na malaika ili kuona kama alipenda kabisa kupata baraka ya Mungu.
it-1-F uku. 1212
Israeli
1. Ni jina lenye Mungu alipatia Yakobo wakati alikuwa na miaka 97 hivi. Yakobo alianza kupigana na malaika usiku wenye alivuka bonde la Yaboki wakati alikuwa anaenda kukutana na ndugu yake. Kwa sababu Yakobo aliendelea kupigana, jina lake lilibadilishwa na kuwa Israeli, ili kuonyesha kama Mungu alimubariki. Ili kukumbuka ile mambo yote, Yakobo aliita ile fasi Penieli ao Penueli. (Mwa 32:22-31; ona YAKOBO Na. 1.) Kisha wakati fulani, kwenye Beteli Mungu alihakikisha kama alibadilisha jina la Yakobo, na tangu ile siku mupaka mwisho wa maisha yake, mara mingi watu walikuwa wanamuita Israeli. (Mwa 35:10, 15; 50:2; 1Ny 1:34) Jina Israeli linapatikana katika Biblia zaidi ya mara 2500, lakini mara mingi linatumiwa ili kuzungumuzia taifa la wazao wa Yakobo.—Ku 5:1, 2.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
Matendo ya Fadhili Yanadumisha Mahusiano Mazuri
10 Kusema maneno yenye neema na kuzungumza kwa njia nzuri kunaweza kusitawisha na kudumisha mahusiano yenye amani. Kwa kweli, kufanya yote tunayoweza ili kuboresha mahusiano yetu na wengine kunaweza kuboresha mazungumzo yetu pamoja nao. Kuchukua hatua ya kuwatendea wengine mambo ya fadhili kutoka moyoni, na kutafuta nafasi za kuwasaidia, kuwapa zawadi kwa nia nzuri, na kuwakaribisha, kunaweza kuchangia mazungumzo mazuri. Hata kunaweza ‘kukusanya makaa yenye moto’ juu ya mtu na kumfanya aonyeshe sifa nzuri, na hivyo inakuwa rahisi zaidi kuzungumza waziwazi na kusuluhisha matatizo.—Rom. 12:20, 21.
11 Mzee wa ukoo Yakobo alielewa jambo hilo. Esau, ndugu yake pacha, alimkasirikia sana hivi kwamba Yakobo akakimbia kwa sababu aliogopa kuwa Esau angemuua. Baada ya miaka mingi kupita, Yakobo alirudi. Esau alienda na wanaume 400 ili akutane naye. Yakobo alisali ili Yehova amsaidie. Kisha, kabla ya kukutana na Esau, akapeleka zawadi kubwa ya wanyama wa kufugwa. Zawadi hiyo ilitimiza kusudi lake. Walipokutana, moyo wa Esau ulikuwa umebadilika, akakimbia na kumkumbatia Yakobo.—Mwa. 27:41-44; 32:6, 11, 13-15; 33:4, 10.
it-1-F uku. 641
Mungu, Mungu wa Israeli
Yakobo alipewa jina Israeli kwa sababu ya mambo yenye ilifanyika Penieli kati yake na malaika wa Yehova. Kisha kukutana kwa amani na ndugu yake Esau, alianza kuishi katika Sukoti kisha katika Shekemu. Kule aliuza sehemu ya shamba ya wana wa Hamori na akasimamisha hema yake pale. (Mwa 32:24-30; 33:1-4, 17-19) Kisha “akasimamisha mazabahu mahali pale na kuipatia jina Mungu, Mungu wa Israeli,” ao “Mungu ni Mungu wa Israeli.” (Mwa 33:20) Kwa kupatanisha ile mazabahu na jina Israeli, jina lake la mupya lenye alikuwa amepewa, alionyesha kama analikubali na iko mwenye shukrani kwa jina hilo na kwa sababu Mungu alimuongoza ili arudie kwa usalama katika Inchi ya Ahadi. Ile jina inapatikana mara moja tu katika Maandiko.
TAREHE 27/4–3/5
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 34-35
“Matokeo ya Mubaya Sana ya Kufanya Urafiki na Watu Wabaya”
w97 1/2 uku. 30 fu. 4
Shekemu—Lile Jiji Katika Bonde
Wanaume vijana wa hilo jiji wangemwonaje bikira huyu kijana aliyezuru jiji lao kwa ukawaida—yaonekana akiwa bila mwandamani? Mwana wa mkuu “akamwona akamtwaa, akalala naye, akambikiri.” Kwa nini Dina alitafuta hatari kwa kushirikiana na Wakanaani wasio wenye adili? Je, ni kwa sababu alikuwa akihisi kwamba alihitaji ushirika wa wasichana wa umri wake mwenyewe? Je, alikuwa mwenye kichwa kigumu na mwenye kujitegemea sawa na baadhi ya ndugu zake? Soma simulizi la Mwanzo, na ujaribu kufahamu ule msononeko na aibu ambayo lazima Yakobo na Lea walihisi kwa sababu ya matokeo yenye kuhuzunisha ya ziara za binti yao huko Shekemu.—Mwanzo 34:1-31; 49:5-7; ona pia Munara wa Mulinzi, Juni 15, 1985, ukurasa 31 (katika Kifaransa).
“Kimbia Uasherati!”
14 Shekemu alifanya jambo lenye lilionekana kuwa la kawaida na lenye kukubalika kwake. Kwa kuwa alimutamani Dina, ‘alimukamata’ na “kumulala kinguvu.” (Soma Mwanzo 34:1-4.) Ile kosa ilikuwa njo mwanzo wa matukio yenye kufuatana yenye iliumiza Dina na familia yake yote.”—Mwanzo 34:7, 25-31; Wagalatia 6:7, 8.
w09 1/9 uku. 21 fu. 1-2
Wakati Mtu Anapokuudhi
Mara nyingi, watu wanaotaka kulipiza kisasi wanajaribu kujituliza baada ya kuumizwa hisia. Kwa mfano, Biblia inatuambia kwamba wana wa mzee wa ukoo Mwebrania Yakobo walipogundua kwamba Mkanaani anayeitwa Shekemu alikuwa amemnajisi dada yao Dina, “wakaumia hisia zao, wakakasirika sana.” (Mwanzo 34:1-7) Ili walipize kisasi kwa uovu ambao dada yao alikuwa ametendewa, wana wawili wa Yakobo walipanga njama dhidi ya Shekemu na familia yake. Wakitumia ujanja, Simeoni na Lawi waliingia kwenye jiji hilo la Wakanaani na kuwaua wanaume wote, kutia ndani Shekemu.—Mwanzo 34:13-27.
Je, damu hiyo yote iliyomwagwa ilisuluhisha tatizo hilo? Yakobo alipojua kuhusu matendo ya watoto wake, aliwakemea na kusema: “Mmefanya nitengwe kwa kunifanya kuwa kitu chenye kunuka kwa wakaaji wa nchi hii, . . . nao watakusanyika pamoja juu yangu wanishambulie, nami nitaangamizwa, mimi na nyumba yangu.” (Mwanzo 34:30) Ndiyo, badala ya kusuluhisha tatizo, matendo yao ya kulipiza kisasi yalikuwa na matokeo mabaya; sasa familia ya Yakobo ilipaswa kujihadhari isishambuliwe na majirani wenye hasira. Huenda ili kuzuia shambulizi kama hilo, Mungu alimwagiza Yakobo ahamishe familia yake kutoka eneo hilo hadi Betheli.—Mwanzo 35:1, 5.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
it-1-F uku. 603 fu. 9
Debora
1. Mulezi wa Rebeka. Debora alisindikiza Rebeka wakati alitoka ku nyumba ya baba yake Betueli na kuenda Palestina ili aolewe na Isaka. (Mwa 24:59) Kisha kutumika kwa miaka mingi katika nyumba ya Isaka, Debora akaanza kuishi katika nyumba ya Yakobo, pengine ilikuwa kisha kifo cha Rebeka. Kwa kweli, miaka 125 hivi kisha ndoa ya Rebeka na Isaka, Debora alikufa na akazikwa chini ya muti mukubwa katika Beteli. Jina lenye ile muti ilipewa (Alon-bakuti, maana yake “Muti wa Mwaloni wa Kilio”) lilionyesha ni kwa kiasi gani Yakobo na familia yake walimupenda.—Mwa 35:8.
Maulizo ya Wasomaji Wetu
Katika Israeli ya zamani, kizazi chenye kuongoza kwa Masiya kilipitishwa tu kupitia haki ya kuwa muzaliwa wa kwanza?
Wakati fulani tumesema kuwa mambo yalikuwa hivyo. Jambo hilo lilionekana kuwa linapatana na andiko la Waebrania 12:16. Andiko hilo linasema kuwa Esau ‘hakusamini mambo matakatifu’ na ‘alitoa [kwa Yakobo] haki zake za kuwa muzaliwa wa kwanza kwa kubadilishana na mulo mumoja.’ Ilionekana kuwa andiko hilo linaonyesha kuwa wakati Yakobo alipata ‘haki zake za kuwa muzaliwa,’ akakuwa pia katika ya kizazi chenye kilitokeza Masiya.—Mt. 1:2, 16; Lu. 3:23, 34.
Lakini, kisha kuchunguza tena habari zenye kuzungumuziwa katika Biblia, tumeona kuwa mwanaume hakupaswa tu akuwe muzaliwa wa kwanza ili kuwa katika kizazi chenye kingetokeza Masiya. Fikiria ushuhuda fulani:
Muzaliwa wa kwanza wa Yakobo (Israeli), alikuwa Rubeni mwenye bibi yake Lea alizaa. Kisha muzaliwa wake wa kwanza kwa Raheli, bibi yake mwenye alipenda sana, alikuwa Yosefu. Wakati Rubeni alijiendesha mubaya, Yosefu akapewa haki ya kuwa muzaliwa wa kwanza. (Mwa. 29:31-35; 30:22-25; 35:22-26; 49:22-26; 1 Ny. 5:1, 2) Lakini Masiya hakutokea katika kizazi cha Rubeni ao katika kizazi cha Yosefu. Alitokea katika kizazi cha Yuda, mutoto wa ine wa Lea.—Mwa. 49:10.