Vichapo Vyenye Kutajwa Katika Buku la Mukutano Utumishi na Maisha
TAREHE 2-8/3
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 22-23
“Mungu Anamujaribu Abrahamu”
Kwa Nini Mungu Alimwambia Abrahamu Amdhabihu Mwana Wake?
Fikiria maneno ambayo Yehova alimwambia Abrahamu: “Tafadhali, mchukue mwana wako, mwana wako wa pekee unayempenda sana, Isaka, . . . umtoe kama toleo la kuteketezwa.” (Mwanzo 22:2) Ona kwamba Yehova anamwita Isaka mwana “unayempenda sana.” Yehova alijua jinsi Isaka alivyokuwa mwenye thamani kwa Abrahamu. Mungu alijua pia jinsi alivyohisi kumhusu Mwana wake, Yesu. Yehova alimpenda Yesu sana hivi kwamba alizungumza mara mbili kutoka mbinguni, akimwita Yesu moja kwa moja “Mwanangu, mpendwa.”—Marko 1:11; 9:7.
Ona kwamba alipokuwa akizungumza na Abrahamu, Yehova alitumia neno “tafadhali.” Msomi mmoja wa Biblia anasema kwamba kwa kutumia neno hilo, “BWANA anaona uzito wa jambo ambalo anamwambia Abrahamu afanye.” Kama tunavyowazia, ombi hilo lingemhuzunisha sana Abrahamu; vivyo hivyo, tunaweza kuwazia uchungu mwingi ambao Yehova alihisi alipokuwa akimtazama Mwana wake akiteseka na kufa. Kwa kweli, huo ndio uchungu mwingi zaidi ambao Yehova amepata au atapata kuhisi.
Hivyo basi, ingawa huenda tusipendezwe na jambo ambalo Yehova alimwambia Abrahamu afanye, ni jambo la hekima kukumbuka kwamba Yehova hakumruhusu mzee huyo wa ukoo aliyekuwa mwaminifu amdhabihu mwana wake. Alimzuia Abrahamu asipatwe na pigo kubwa zaidi linaloweza kumpata mzazi; alimlinda Isaka kutokana na kifo. Ingawa hivyo, Yehova hakumkinga “Mwana wake mwenyewe bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote.” (Waroma 8:32) Kwa nini Yehova alijiruhusu apatwe na hali hiyo yenye kuumiza sana? Alifanya hivyo “ili tupate uzima.” (1 Yohana 4:9) Hicho ni kikumbusho kilichoje kuhusu upendo wa Mungu kutuelekea! Bila shaka, sisi pia tunachochewa kumpenda.
Umutii Mungu ili Ufaidike na Viapo Vyake
6 Kwa faida ya wanadamu wenye dhambi, Yehova Mungu ameapa pia kwa kutumia maneno, “‘Kama ninavyoishi,’ asema Bwana Mwenye Enzi Kuu Yehova.” (Eze. 17:16) Biblia inataja pindi zaidi ya 40 ambazo Yehova Mungu alifanya viapo rasmi. Huenda mfano unaojulikana zaidi ni kiapo ambacho Mungu alifanya aliposhughulika na Abrahamu. Kwa miaka mingi, Yehova alimpa Abrahamu ahadi kadhaa za maagano ambazo kwa ujumla zinaonyesha kwamba Uzao ulioahidiwa ungetokana na Abrahamu kupitia kwa mwana wake Isaka. (Mwa. 12:1-3, 7; 13:14-17; 15:5, 18; 21:12) Kisha Yehova akampa Abrahamu jaribu gumu kwa kumwamuru amtoe mwana wake mpendwa. Bila kukawia, Abrahamu alitii na alipokuwa karibu kumtoa Isaka kama dhabihu alizuiwa na malaika wa Mungu. Kisha Mungu akaapa hivi: “Naapa kwa nafsi yangu mwenyewe . . . kwamba kwa sababu ya uhakika wa kwamba wewe umefanya jambo hili nawe hukuzuia mwana wako, mwana wako wa pekee, hakika nitakubariki nami nitauzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni na kama chembe za mchanga zilizo kando ya bahari; na uzao wako utamiliki lango la adui zake. Na kupitia kwa uzao wako mataifa yote ya dunia hakika yatajibariki kwa sababu wewe umeisikiliza sauti yangu.”—Mwa. 22:1-3, 9-12, 15-18.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
Yehova Alimuita “Rafiki Yangu”
13 Mbele ya kuwaacha watumishi wake, Abrahamu alisema hivi: ‘Ninyi mukae hapa pamoja na punda, lakini mimi na huyu muvulana [mutoto mwanaume] tunataka kuenda mbele huko tukaabudu, halafu tutarudia hapa mulipo.’ (Mwanzo 22:5) Abrahamu alimaanisha nini? Kwa sababu alijua kwamba atamutoa mutoto wake, je, alikuwa anadanganya wakati alisema kwamba atarudia pamoja naye? Hapana. Biblia inasema kwamba Abrahamu alijua kama Yehova alikuwa na uwezo wa kumufufua Isaka. (Soma Waebrania 11:19.) Abrahamu alijua kwamba Yehova alikuwa amemuwezesha kupata mutoto hata kama yeye na Sara walikuwa wamezeeka sana. (Waebrania 11:11, 12, 18) Kwa hiyo, alielewa kwamba Yehova alikuwa na uwezo juu ya mambo yote. Abrahamu hakujua jambo lenye lingetokea siku hiyo. Lakini aliamini kwamba ikiwa ni lazima, Yehova angemufufua Isaka ili ahadi zake zote zitimie. Ndiyo sababu Abrahamu anaitwa “baba ya wale wote walio na imani”!
it-2-F uku. 642 fu. 2-3
Kujua Mambo Mbele ya Wakati, Kuchaguliwa Mbele ya Wakati
Mungu anachagua ni wakati gani atatumia uwezo wake wa kujua mambo mbele ya wakati. Uwezo wa Mungu wa kuchagua kujua mambo fulani mbele ya wakati unapatana na kanuni zake za haki na unapatana na mambo yenye anatuonyesha juu yake katika Biblia; na ile ni tofauti kabisa na uwezo wa kupanga mambo yote mbele ya wakati. Tofauti na fundisho lenye kusema kama Mungu anapanga mambo yote mbele ya wakati, maandiko mingi inatuonyesha kama Mungu anachunguzaka hali fulani yenye inatokea na kisha anakamata uamuzi wenye kutegemea uchunguzi wenye amefanya.
Kwa hiyo, Mwanzo 11:5-8 inaonyesha kama Mungu anaelekeza uangalifu wake ku dunia, anachunguza hali yenye kuwa katika Babeli, na wakati huo, anaamua jambo lenye atafanya ili kuvunja mupango wa kufanya ile kazi yenye haikukuwa sawa. Kisha ubaya kuenea sana katika Sodoma na Gomora, Yehova aliambia Abrahamu uamuzi wake wa kufanya uchunguzi (kwa kutumia malaika) ili ‘aone kama wanatenda kulingana na malalamiko yenye yalimufikia. Na kama haiko vile, atajua jambo hilo.’ (Mwa 18:20-22; 19:1) Mungu alizungumuzia kuhusu ‘kujuana na Abrahamu,’ na kisha Abrahamu kujaribu kumutoa Isaka kama zabihu, Yehova alisema hivi, “Kwa maana sasa ninajua kwamba unamuogopa Mungu kwa kuwa haukunikatalia mwana wako, mwana wako wa pekee.”—Mwa 18:19; 22:11, 12; linganisha na Ne 9:7, 8; Gal 4:9.
Hotuba
it-1-F uku. 608 fu. 8
Alitangazwa Kuwa Mwenye Haki
Kwa hiyo, kupitia imani ya Abrahamu pamoja na matendo yake, “ikahesabiwa kwake kuwa haki.” (Ro 4:20-22) Lakini, kwa kweli, ile haimaanishe kama yeye na watu wengine waaminifu wenye waliishi mbele ya kuzaliwa kwa Kristo walikuwa wakamilifu ao kama hawangeweza kufanya zambi; lakini, kwa musingi wa imani yao katika ahadi za Mungu kuhusu “uzao” na kwa sababu walijikaza sana kufuata amri ya Mungu, hawakuhesabiwa kuwa wenye hawako wenye haki, wenye hawakukubaliwa na Mungu, kama watu wengine. (Mwa 3:15; Zb 119:2, 3) Tofauti na watu wa ulimwengu wenye kutengwa na Mungu, kwa upendo Yehova alihesabia wale watumishi wake kuwa watu wenye hawakukuwa na hatia. (Zb 32:1, 2; Efe 2:12) Kwa hiyo, kwa sababu ya imani yao, Yehova angeweza kufanya nao mambo fulani na kuwabariki hata kama hawakukuwa wakamilifu, na wakati uleule aliendelea kushikamana na kanuni zake kamilifu za haki. (Zb 36:10) Lakini, wote walijua kama walikuwa na lazima ya kukombolewa kutoka katika zambi na walikuwa wanangojea kwa hamu wakati wenye kufaa wa Mungu wa kufanya vile.—Zb 49:7-9; Ebr 9:26.
TAREHE 9-15/3
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 24
“Kumutafutia Isaka Bibi”
‘Niko Tayari Kuenda’
Abrahamu alimuomba Eliezeri aape kama hatachagulia Isaka bibi kati ya wanawake wa Kanaani. Sababu gani? Kwa sababu Wakanaani hawakumuheshimia Yehova Mungu na hawakumuabudu. Abrahamu alijua kama Yehova alikusudia kupatia watu hao malipizi kwa wakati wenye kufaa kwa sababu ya matendo yao ya mubaya. Abrahamu hakutaka Isaka, mwana wake mupendwa, ajiunge na watu hao na njia zao za mubaya. Tena, alijua kama mwana wake alikuwa na daraka la maana katika kutimizwa kwa ahadi za Yehova.—Mwanzo 15:16; 17:19; 24:2-4.
‘Niko Tayari Kuenda’
Eliezeri aliendelea kuambia familia ya Bethueli kama wakati alifika kwenye kisima karibu na Harani, alisali kwa Yehova Mungu. Kwa kweli, alimuomba Yehova achague mwanamuke mwenye Isaka ataoa. Namna gani? Eliezeri aliomba Mungu aongoze mwanamuke mwenye anataka Isaka aoe akuje kwenye kisima. Wakati angemuomba maji ya kunywa, mwanamuke huyo angepaswa kujitolea kumupatia Eliezeri maji ya kunywa na apatie pia ngamia wake. (Mwanzo 24:12-14) Na ni nani alikuja na kufanya mambo hayo? Ni Rebeka! Wazia namna Rebeka angeweza kujisikia kama alikuwa anasikiliza habari yenye Eliezeri alikuwa anaambia watu wa familia yake!
wp16.3 uku. 14 fu. 6-7
‘Niko Tayari Kuenda’
Majuma fulani mbele ya hapo, Eliezeri alimuuliza Abrahamu jambo hilo, kwa kusema hivi: ‘Itakuwaje ikiwa mwanamuke huyo hatakuja pamoja nami?’ Abrahamu alikuwa amemujibia hivi: “Utakuwa bila wajibu kwangu kwa kiapo.” (Mwanzo 24:39, 41) Katika nyumba ya Bethueli pia, mawazo ya kijana huyo mwanamuke juu ya jambo hilo yalikuwa ya maana. Eliezeri alichangamuka sana kwa sababu safari yake ilipata matokeo ya muzuri. Kwa hiyo, asubui yenye ilifuata aliomba ikiwa angeweza kurudia Kanaani mara moja pamoja na Rebeka. Lakini, watu wa familia walipenda Rebeka abakie pamoja nao kwa siku zingine kumi hivi. Mwishowe, walikata maneno hivi: ‘Na tumuite huyo mwanamuke kijana tusikie kutoka kinywani mwake.’—Mwanzo 24:57.
Sasa, Rebeka alipaswa kukamata uamuzi mukubwa katika maisha yake. Angesema nini? Angeshawishi baba yake na ndugu yake wamusikilie huruma na kuwaomba sana ili asifanye safari hiyo ya kuenda mahali kwenye hajue? Ao angeona hilo kuwa pendeleo la kuchangia katika matukio yenye yalionekana waziwazi kuwa yaliongozwa na Yehova? Wakati alijibia, alionyesha namna aliona badiliko hilo la kushitukia, na pengine la kuogopesha lenye lilitokea katika maisha yake. Alisema tu hivi: ‘Niko tayari kuenda.’—Mwanzo 24:58.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
‘Niko Tayari Kuenda’
Siku moja mangaribi, kisha kujaza mutungi wake maji, mwanaume mumoja mwenye kuzeeka alikuja mbio kukutana naye. Mwanaume huyo alimuambia hivi: ‘Tafazali, unipe maji kidogo katika mutungi wako.’ Hilo lilikuwa ombi ndogo na la adabu! Rebeka aliona kama mwanaume huyo alikuwa amefanya safari ndefu. Kwa hiyo, alishusha haraka mutungi kwenye mabega yake na kumuacha mwanaume huyo akunywe. Hakukunywa tu maji kidogo, lakini alikunywa kabisa maji hayo ya baridi yenye hayakukuwa na chumvi. Kisha akatambua kama mwanaume huyo alikuwa na ngamia kumi wenye walikuwa wanapiga magoti karibu nao, na chombo cha kutilia wanyama maji hakikukuwa na maji. Rebeka aliona kama mwanaume huyo alikuwa anamuangalia kwa uangalifu, na alitaka kufanya yake yote ili amuonyeshe utoaji. Kwa hiyo, alisema hivi: ‘Nitateka [nitashota] maji pia kwa ajili ya ngamia zako mupaka wamalize kunywa.’—Mwanzo 24:17-19.
Ona kama Rebeka hakujitolea tu kushota maji kwa ajili ya ngamia kumi lakini alijitolea pia kuwashotea maji mupaka kiu yao iishe. Kama iko na kiu sana, ngamia mumoja anaweza kunywa litre 95 za maji! Kama ngamia wote hao kumi walikuwa na kiu, Rebeka angefanya kazi ngumu kwa saa nyingi. Lakini kama vile mambo yalitokea, inawezekana ngamia hao hawakukuwa na kiu sana. Lakini, Rebeka alijua hilo wakati alijitolea kushota maji kwa ajili ya ngamia? Hapana. Alikuwa na nia, pia alikuwa tayari kufanya kazi kwa bidii kama vile iliomba ili kumuonyesha ukaribishaji mwanaume huyo mugeni mwenye kuzeeka. Mwanaume huyo aliitika jambo Rebeka alijitolea kufanya. Alimuangalia Rebeka kwa uangalifu wakati alikuwa anaenda na kurudia, kujaza tena na tena mutungi wake wa maji na kumwanga tena na tena maji hayo katika chombo cha kutilia wanyama maji.—Mwanzo 24:20, 21.
wp16.3 uku. 13, maelezo ya chini.
‘Niko Tayari Kuenda’
Tayari ilikuwa mangaribi. Katika habari hiyo, hakuna jambo lolote lenye kuonyesha kama Rebeka alibakia kwenye kisima kwa saa nyingi. Tena, haionyeshe kama watu wa familia yake walikuwa wamelala wakati alimaliza kushota maji ao kama mutu fulani alikuja kuangalia sababu gani alikawia.
‘Niko Tayari Kuenda’
Mwishowe siku yenye tulizungumuzia kwenye mwanzo wa habari hii ikafika. Wakati kikundi cha wasafiri kilipita katika eneo la Negebu na giza lilianza kuingia, Rebeka aliona mwanaume mumoja mwenye alikuwa anatembea katika mashamba. Mwanaume huyo alionekana kuwa mwenye kufikiri sana. Tunasoma hivi: “Akaruka chini kutoka kwenye ngamia.” Pengine hakungojea hata ngamia ipige magoti, na kisha akauliza kiongozi wake hivi: ‘Ule mwanaume anayetembea pale shambani kuja kutupokea, ni nani?’ Wakati aliambiwa kama mwanaume huyo alikuwa Isaka, alifunika kichwa chake na kitambaa. (Mwanzo 24:62-65) Sababu gani? Pengine kufanya vile ilikuwa alama ya kumuonyesha heshima mwenye atakuwa bwana yake. Watu wengi leo wanaweza kuona aina hiyo ya ujitiisho kuwa jambo la zamani. Lakini, kwa kweli, wanawake na pia wanaume wanaweza kujifunza jambo la maana kupitia unyenyekevu wa Rebeka, kwa sababu sisi wote tuko na lazima sana ya sifa hiyo ya muzuri.
TAREHE 16-22/3
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 25-26
“Esau Anauzisha Haki Yake ya Kuwa Muzaliwa wa Kwanza”
it-1-F uku. 1224
Yakobo
Yakobo na Esau walikuwa tofauti. Baba yao alimupenda sana Esau mwenye alikuwa mutu wa pori, mwenye kukosa uvumilivu, muwindaji mwenye kutembea-tembea; lakini Biblia inasema kama Yakobo alikuwa “mutu mwenye hana lawama [neno la Kiebrania, tam], mwenye kukaa katika mahema,” alikuwa muchungaji mwenye sifa ya muzuri, na mwenye kutumainika kwa kuhangaikia mambo ya familia; mama yake alimupenda sana. (Mwa 25:27, 28) Neno la Kiebrania tam linatumiwa fasi ingine ili kuzungumuzia wale wenye kukubaliwa na Mungu. Kwa mufano, “watu wenye kiu ya damu wanachukia kila mutu mwenye hana lawama,” lakini Yehova anahakikisha kama “wakati wenye kuja wa mutu huyo [mwenye hana lawama] utakuwa wenye amani.” (Mez 29:10; Zb 37:37) Yobu, mutu muaminifu-mushikamanifu, alijionyesha “kuwa mutu mwenye hana lawama [neno la Kiebrania, tam] na munyoofu.”—Yob 1:1, 8; 2:3.
Juu ya Nini Tunapaswa Kuonyesha Shukrani?
11 Jambo la kuhuzunisha ni kwamba, watu fulani wenye kuzungumuziwa mu Biblia hawakuonyesha shukrani. Kwa mufano, hata kama wazazi wenye kumupenda na kumuheshimia Yehova njo walikomalisha Esau, hakuheshimia, ao hakuonyesha shukrani juu ya mambo matakatifu. (Soma Waebrania 12:16.) Namna gani roho yake ya kukosa shukrani ilionekana wazi? Bila kufikiri, Esau alimuuzishia Yakobo, mudogo yake, haki yake ya kuzaliwa, kwa ajili tu ya bakuli la muchuzi. (Mwa. 25:30-34) Kisha wakati fulani, Esau alihuzunika sana juu ya uamuzi wenye alikuwa amekamata. Lakini kwa sababu hakukuwa ameonyesha shukrani juu ya jambo lenye alikuwa nalo, hakukuwa na sababu ya kunungunika wakati hakupewa baraka ya muzaliwa wa kwanza.
it-2-F uku. 637
Muzaliwa wa kwanza
Zamani, mutoto mwanaume mwenye alizaliwa wa kwanza njo alikuwa anapewa cheo cha heshima mu familia na ni yeye alikuwa anakamata nafasi ya baba yake ya kusimamia nyumba kisha baba yake kufa. Alikuwa anariti sehemu mbili ya mali ya baba yake. (Kum 21:17) Wakati wa chakula, Yosefu alipatia Rubeni nafasi ya kukaa yenye kupatana na haki yake ya muzaliwa wa kwanza. (Mwa 43:33) Lakini mu Biblia, haiko kila mara njo muzaliwa wa kwanza anaheshimiwaka wakati watoto wanaume wanatajwa kulingana na wakati wenye walizaliwa. Mara mingi fasi ya kwanza inapewa mutoto wa maana sana ao muaminifu kati ya watoto kuliko kuipatia muzaliwa wa kwanza.—Mwa 6:10; 1Ny 1:28; linganisha na Mwa 11:26, 32; 12:4; ona HAKI YA KUZALIWA; URITI.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
Maulizo ya Wasomaji Wetu
Sasa tuchunguze tena andiko la Waebrania 12:16 lenye linasema hivi: ‘Kusiwe na muasherati wala yeyote asiyesamini mambo matakatifu, kama Esau, ambaye alitoa haki zake za kuwa muzaliwa wa kwanza kwa kubadilishana na mulo mumoja.’ Mutume Paulo alipenda kuzungumuzia jambo gani?
Hapa, Paulo hakukuwa anazungumuzia juu ya watu wenye kuwa katika kizazi chenye kilitokeza Masiya. Alikuwa tu ametoka kushauria Wakristo ‘wafanyie miguu yao mapito yaliyonyooka.’ Kwa kufanya hivyo, hawangekosa kupata ‘fazili zisizostahiliwa za Mungu,’ jambo la kuhuzunisha ni kwamba wangezikosa ikiwa wangeanza kufanya mambo ya uasherati. (Ebr. 12:12-16) Ikiwa wangefanya hivyo, wangekuwa kama Esau. Alishindwa ‘kusamini mambo matakatifu,’ na kwa njia ya moja kwa moja alifuatia mambo ya kimwili.
Esau aliishi wakati wa zamani, na pengine mara kwa mara alikuwa na pendeleo la kutoa zabihu. (Mwa. 8:20, 21; 12:7, 8; Ayu. 1:4, 5) Lakini, kwa sababu Esau aliona mambo kwa njia ya kimwili, aliacha mapendeleo kama hayo kwa sababu ya chakula. Pengine alipenda kuepuka mateso yenye yalikuwa yametabiriwa kuwa yangepata wazao wa Abrahamu. (Mwa. 15:13) Esau alionyesha pia kuwa anapenda mambo ya kimwili, na akakosa kuheshimia mambo matakatifu, kwa kuoa wanawake wawili wapagani na hilo lililetea sana uchungu wazazi wake. (Mwa. 26:34, 35) Alikuwa tofauti kabisa na Yakobo mwenye alijikaza kuoa mwanamuke mwenye kuabudu Mungu wa kweli!—Mwa. 28:6, 7; 29:10-12, 18.
it-2-F uku. 255 fu. 6
Uongo
Hata kama Biblia inakataza kusema uongo kwa nia ya mubaya, ile haimaanishe kama mutu anapaswa kusema habari yote ya kweli kwa watu wenye hawastahili kuijua. Yesu Kristo alishauria hivi: “Musipatie imbwa kitu kitakatifu, wala musitupe lulu zenu mbele ya nguruwe, ili wasizikanyange-kanyange chini ya miguu yao, kisha wageuke na kuwapasua-pasua.” (Mt 7:6) Njo maana wakati fulani Yesu alijizuia kusema habari yote ao kujibia moja kwa moja maulizo fulani yenye ingeweza kumutia katika hatari. (Mt 15:1-6; 21:23-27; Yoh 7:3-10) Na inaonekana ni vile Abrahamu, Isaka, Rahabu, na Elisha walifanya kwa kuficha habari fulani ao kujizuia kusema habari ya kweli kwa wale wenye hawakukuwa wanamuabudu Yehova.—Mwa 12:10-19; sura ya 20; 26:1-10; Yos 2:1-6; Yak 2:25; 2Fa 6:11-23.
TAREHE 23-29/3
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 27-28
“Yakobo Anapewa Baraka Yenye Iko na Haki ya Kupata”
w04 15/4 uku. 11 fu. 4-5
Rebeka—Mwanamke Mwenye Bidii Aliyemwogopa Mungu
Biblia haisemi kama Isaka anajua kwamba Esau anapaswa kumtumikia Yakobo. Vyovyote vile, Rebeka na Yakobo wanajua kwamba Yakobo ndiye anayepaswa kubarikiwa. Rebeka anachukua hatua mara moja anaposikia kwamba Isaka anataka kumbariki Esau wakati Esau atakapomletea chakula cha nyama ya mawindo. Bado Rebeka ana bidii na uwezo wa kuamua mambo aliokuwa nao alipokuwa msichana. ‘Anamwamuru’ Yakobo amletee wana-mbuzi wawili. Atatayarisha chakula ambacho mume wake anapenda. Kisha Yakobo anapaswa kujifanya kuwa Esau ili abarikiwe. Yakobo anakataa, akisema kwamba lazima baba yake atatambua ujanja wake na kumlaani! Rebeka anasisitiza afanye hivyo akisema, “Laana uliyokusudiwa wewe na iwe juu yangu, mwanangu.” Ndipo anatayarisha chakula, anamfanya Yakobo afanane na Esau, kisha anamtuma kwa mume wake.—Mwanzo 27:1-17.
Biblia haitaji ni kwa nini Rebeka anatenda hivyo. Wengi humshutumu kwa tendo lake, lakini Biblia haifanyi hivyo. Isaka pia hamshutumu anapotambua kwamba alimbariki Yakobo. Badala yake, Isaka anambariki Yakobo zaidi. (Mwanzo 27:29; 28:3, 4) Rebeka anajua yale ambayo Yehova alitabiri kuhusu wanawe. Hivyo, anachukua hatua ya kuhakikisha kwamba Yakobo anapata baraka ambazo ni haki yake. Ni wazi kwamba jambo hilo linapatana na mapenzi ya Yehova.—Waroma 9:6-13.
w07 1/10 uku. 31 fu. 2-3
Maswali Kutoka kwa Wasomaji
Biblia haielezi kwa undani kwa nini Rebeka na Yakobo walitenda hivyo, lakini inaonyesha kwamba hali iliyowakabili ilitokea ghafula. Tunapaswa kukumbuka kwamba Neno la Mungu halitetei wala kulaumu yale ambayo Rebeka na Yakobo walifanya. Hivyo, simulizi hilo halituwekei kielelezo cha kusema uwongo au kutenda kwa udanganyifu. Hata hivyo, Biblia inafunua yale yaliyotokea.
Kwanza, simulizi hilo linaonyesha wazi kwamba Yakobo alikuwa na haki ya kubarikiwa na baba yake; Esau hakuwa na haki. Mapema, Yakobo alikuwa amenunua kihalali haki ya mzaliwa wa kwanza kutoka kwa ndugu yake pacha ambaye hakuithamini, na ambaye aliiuza kwa mlo mmoja ili kutuliza njaa yake. Esau “aliidharau haki ya kuzaliwa.” (Mwanzo 25:29-34) Hivyo, kwa kumwendea baba yake, Yakobo alikuwa akitafuta baraka ambayo ilikuwa haki yake.
it-1-F uku. 295 fu. 6
Baraka
Zamani katika jamaa, mara mingi baba alikuwa anabariki watoto wake wanaume wakati kidogo mbele akufe. Ile ilikuwa jambo kubwa na la maana kabisa. Kwa hiyo Isaka alimubariki Yakobo na iko anawaza kama ni Esau, mutoto wake wa kwanza. Isaka alisema kama Yakobo angekuwa na mapendeleo na hali ya muzuri zaidi kuliko ndugu yake Esau, na kwa kweli alikuwa anamuomba Yehova atimize ile baraka, juu Isaka yeye mwenyewe alikuwa kipofu na muzee. (Mwa 27:1-4, 23-29; 28:1, 6; Ebr 11:20; 12:16, 17) Isaka alimubariki Yakobo zaidi hata kisha kujua kama hakukuwa mutoto wake wa kwanza. (Mwa 28:1-4) Mbele akufe, Yakobo alibariki kwanza watoto wawili wa Yosefu, na kisha akabariki watoto wake mwenyewe. (Mwa 48:9, 20; 49:1-28; Ebr 11:21) Vilevile, mbele Musa akufe, alibariki taifa lote la Israeli. (Kum 33:1) Mambo yenye ilitokea mu zile hali zote ilionyesha kama walisema katika njia ya kiunabii. Katika hali fulani, wakati wa kutoa baraka za vile, mwenye kubariki alikuwa anatia mukono wake juu ya kichwa cha ule mwenye alikuwa anabarikiwa.—Mwa 48:13, 14.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
w06 15/4 uku. 6 fu. 3-4
Mambo Yanayoweza Kukusaidia Kuwasiliana na Mwenzi Wako
Je, Isaka na Rebeka walisitawisha ustadi wa kuwasiliana? Baada ya mwana wao Esau kuoa binti wawili wa Hethi, kulitokea tatizo kubwa la familia. Rebeka “akawa akimwambia” Isaka: “Nimekuja kuyachukia sana haya maisha yangu kwa sababu ya binti za Hethi. Yakobo [mwana wao mdogo] akichukua mke kutoka kwa binti za Hethi . . . , basi maisha yana faida gani kwangu?” (Mwanzo 26:34; 27:46) Ni wazi kwamba alieleza hangaiko lake waziwazi.
Isaka alimwambia Yakobo, ndugu pacha wa Esau, asichukue mke kutoka kwa binti za Kanaani. (Mwanzo 28:1, 2) Naam, Rebeka alikuwa amejieleza vizuri. Wenzi hao walifaulu kuzungumza jambo zito la familia, na hivyo kutuwekea mfano mzuri leo. Namna gani wenzi wa ndoa wasipokubaliana? Wanaweza kufanya nini?
w04 15/1 uku. 28 fu. 6
Mambo Makuu Kutoka Kitabu cha Mwanzo—II
28:12, 13—Ndoto ya Yakobo iliyohusisha “ngazi” ilimaanisha nini? “Ngazi” hiyo ambayo huenda ilifanana na mawe yaliyokuwa yamepangwa kama ngazi, ilionyesha kwamba kuna mawasiliano kati ya dunia na mbingu. Kupanda na kushuka kwa malaika wa Mungu kulionyesha kwamba malaika huhudumu kwa njia fulani ya pekee kati ya Yehova na wanadamu walio na kibali chake.—Yohana 1:51.
TAREHE 30/3–5/4
UTAJIRI WA NENO LA MUNGU | MWANZO 29-30
“Yakobo Anaoa”
Yakobo Alithamini Mambo ya Kiroho
Ahadi ya ndoa ilifanywa kwa kulipa mahari kwa familia ya bibi-arusi. Baadaye Sheria ya Musa iliweka malipo ya shekeli 50 za fedha kwa ajili ya mabikira walioshawishiwa. Msomi Gordon Wenham anasadiki kwamba hayo ndiyo yaliyokuwa “malipo ya juu zaidi ya mahari,” lakini malipo mengi ya mahari yalikuwa ya “chini zaidi.” (Kumbukumbu la Torati 22:28, 29) Kwa kuwa Yakobo hangeweza kupata malipo hayo, alikubali kumtumikia Labani kwa muda wa miaka saba. Wenham aendelea kusema, “Kwa kuwa nyakati za Wababuloni wa kale wafanyakazi wa muda walipokea kati ya nusu shekeli na shekeli moja kwa mwezi (kutoka shekeli 42 mpaka 84 kwa miaka saba kamili), Yakobo alikubali kumpa Labani kiasi kikubwa sana cha mahari ili kumwoa Raheli.” Labani alikubali kwa furaha.—Mwanzo 29:19.
w07 1/10 uku. 8-9
Dada Waliotaabika Ambao ‘Waliijenga Nyumba ya Israeli’
Je, ni Lea aliyepanga njama ya kumdanganya Yakobo? Au je, alilazimika tu kumtii baba yake? Naye Raheli alikuwa wapi? Je, alijua kile kilichokuwa kikiendelea? Ikiwa ndivyo, alihisi namna gani? Je, angepinga uamuzi na mamlaka ya baba yake? Biblia haijibu maswali hayo. Haidhuru Raheli na Lea walifikiri nini kuhusu jambo hilo, njama hiyo ilimkasirisha Yakobo. Na Yakobo alibishana na Labani, wala si na mabinti wake: “Je, sikukutumikia kwa ajili ya Raheli? Basi kwa nini umenifanyia ujanja?” Labani alijibu namna gani? “Si desturi . . . kumtoa mwanamke mdogo kabla ya mzaliwa wa kwanza. Sherehekea kikamili juma la mwanamke huyu. Baadaye utapewa pia mwanamke huyu mwingine kwa utumishi ambao wewe unaweza kunitumikia kwa miaka saba zaidi.” (Mwanzo 29:25-27) Hivyo, Yakobo alidanganywa na kuingizwa katika ndoa ya wake wengi ambayo ingesababisha wivu mkali.
it-2-F uku. 222 fu. 5
Ndoa
Sherehe. Hata kama katika Israeli watu hawakufanya sherehe ya ndoa, wakati wa ndoa ulikuwa wenye kufurahisha sana. Siku ya ndoa, bibi-arusi alikuwa anafanya mambo mingi ili kujitayarisha wakati angali kwao. Kwanza alikuwa anaoga na kujipakaa mafuta ya harufu ya muzuri ya marashi. (Linganisha na Rut 3:3; Eze 23:40.) Wakati fulani alikuwa anasaidiwa na watumishi wanamuke, alikuwa anavaa nguo za kifua na kanzu ya mweupe, kwa kawaida ile kanzu ilikuwa na michoro mingi ya uzi, kulingana na feza zenye alikuwa nazo. (Yer 2:32; Ufu 19:7, 8; Zb 45:13, 14) Alikuwa anajipamba kwa kutumia vitu mbalimbali vya kujipamba, kama alikuwa na uwezo wa kufanya vile (Isa 49:18; 61:10; Ufu 21:2), na kisha alikuwa anajifunika nguo ya mwepesi yenye kuwa kama kitambaa, yenye ilianzia ku kichwa mupaka ku miguu. (Isa 3:19, 23) Ile inasaidia kuelewa ni juu ya nini Labani aliweza kumudanganya Yakobo kwa vyepesi kwa kufanya ashindwe kujua kama Labani alikuwa anamupatia Lea pa nafasi ya Raheli. (Mwa 29:23, 25) Rebeka alijifunikaka kitambaa ku kichwa wakati alikuwa karibu kukutana na Isaka. (Mwa 24:65) Kufanya vile, ilikuwa alama ya kuonyesha kama bibi-arusi anajishusha chini ya mamlaka ya bwana-arusi.—1Ko 11:5, 10.
Chimba ili Kupata Mali ya Kiroho
it-1-F uku. 49 fu. 2
Kufanywa kuwa mutoto
Raheli na Lea waliona watoto wenye watumishi wao walimuzalia Yakobo, kuwa sawa vile watoto wao wenyewe, wenye ‘walizaliwa kwenye magoti yao.’ (Mwa 30:3-8, 12, 13, 24) Wale watoto walikuwa na haki ya kuriti mali ya Yakobo sawasawa na watoto wa Raheli na Lea. Walikuwa watoto wa baba moja na juu wale watumishi wanamuke walikuwa mali ya Raheli na Lea, basi Raheli na Lea walikuwa na haki ya kupewa mali kupitia wale watoto.
w04 15/1 uku. 28 fu. 7
Mambo Makuu Kutoka Kitabu cha Mwanzo—II
30:14, 15—Kwa nini Raheli aliachilia nafasi ya kulala na mume wake kwa kubadilishana na baadhi ya dudai? Nyakati za kale, dudai zilitumiwa kama dawa ya kulevya na ya kuzuia au kupunguza mkazo wa ghafula wa misuli. Pia tunda hilo lilidhaniwa kwamba lilikuwa na uwezo wa kuchochea tamaa ya ngono na kuongeza uwezo wa mwanadamu wa kuzaa au lilisaidia katika kupata mimba. (Wimbo wa Sulemani 7:13) Ingawa Biblia haifunui nia ya Raheli ya kufanya hivyo, huenda alifikiri kwamba dudai hizo zingemsaidia kupata mimba na hivyo kuondoa aibu yake ya kuwa tasa. Hata hivyo, Yehova “alifungua tumbo lake la uzazi” baada ya miaka kadhaa kupita.—Mwanzo 30:22-24.