SOMO YA 5
Kusoma Bila Makosa
1 Timoteo 4:13
JAMBO LA KUFANYA: Soma mambo kwa sauti vile inaandikwa mu kichapo.
NAMNA YA KUFANYA VILE:
Jitayarishe muzuri. Wazia sababu yenye ilifanya ile habari iandikwe. Ufanye mazoezi ya kusoma makundi ya maneno, hapana tu neno moja-moja. Ukuwe muangalifu juu usiongeze maneno, ao kuruka maneno, ao kutia neno fulani lenye haliko. Heshimia alama za vituo, sawa vile nukta (.), mukato (,), alama ya kuuliza (?).
Sema kila neno muzuri. Kama haujue namna ya kusema neno fulani, iangalie mu diksionere, sikiliza usomaji wenye ulirekodiwa wa kichapo, ao omba musomaji muzuri akusaidie.
Sema maneno ya kusikilika. Sema maneno muzuri, simamisha kichwa na ufungue kinywa muzuri. Jikaze kusema kila silabe.