Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • mwbr23 Mwezi wa 3 uku. 1-13
  • Vichapo “Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Vichapo “Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha”
  • Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2023
  • Vichwa Vidogo
  • TAREHE 6-12/3
  • Hotuba: Juu ya Nini Wakristo Wanapangwa Muzuri?
  • w11-SW 1/6 uku. 14-15
  • Je, Mungu Ana Watu Wanaomtumikia kwa Utaratibu?
  • Wonyesho wa Upendo wa Mungu
  • TAREHE 13-19/3
  • TAREHE 20-26/3
  • TAREHE 27/3–2/4
  • Hotuba: Tutafanya Nini Ikiwa Hali Fulani ya Pekee Inatuzuia Kufika ku Ukumbusho?
  • w93-SW 1/2 uku. 31
  • Maswali Kutoka kwa Wasomaji
  • Mkristo akiwa mgonjwa au anasafiri na hivyo asiweze kuwa kwenye mwadhimisho wa Ukumbusho, je, anapaswa auadhimishe mwezi mmoja baadaye?
  • TAREHE 10-16/4
  • TAREHE 17-23/4
  • Hotuba: Uzoeze Wanafunzi Wako wa Biblia Wakati Wanaomba Mashauri
  • be-SW uku. 69 fu. 4-5
  • Jua Jinsi Unavyopaswa Kujibu
  • TAREHE 24-30/4
Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha—2023
mwbr23 Mwezi wa 3 uku. 1-13

Vichapo Vyenye Kutajwa mu Buku ya Mukutano Utumishi na Maisha

© 2022 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania

TAREHE 6-12/3

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 MAMBO YA NYAKATI 23-26

“Ibada Yenye Kufanywa mu Hekalu Inapangwa Muzuri Sana”

it-2-F uku. 133 fu. 2

Walawi

Kazi ya Walawi ilipangwa muzuri sana wakati Daudi alikuwa mufalme. Aliweka viongozi, maofisa, waamuzi, walinzi wa milango, wachunga hazina, na hesabu ingine kubwa ya Walawi wa kusaidia makuhani mu hekalu, mu kiwanja ya hekalu, na mu vyumba vya kukulia. Walisaidia mu kazi ya matoleo, kazi ya kutoa zabihu, kazi ya kutakasa, kazi ya kupima na kazi zingine za ulinzi. Waimbaji Walawi walipangwa mu vikundi 24, sawa vikundi vya makuhani na walikuwa wanatumika kwa kubadilishana. Walikuwa napiga kura juu ya kuamua ni nani njo atafanya kazi fulani. Walikuwa nafanya pia vile juu ya kujua ni walinzi gani watachunga mulango fulani.​—1Ny 23, 25, 26; 2Ny 35:3-5, 10.

it-2-F uku. 657 fu. 7

Makuhani

Mu hekalu, makuhani walipangwa chini ya uongozi wa maofisa mbalimbali. Walipiga kura juu ya kuamua ni nani njo angefanya kazi fulani. Mu vile vikundi 24, kila kikundi kilikuwa kinatumika juma moya moya, mara mbili ku mwaka. Bila shaka makuhani wote walikuwa wanatumika mu vipindi vya sikukuu juu watu walitoa maelfu ya zabihu, sawa vile ilikuwa siku ya kumutolea Yehova hekalu. (1Ny 24:1-18, 31; 2Ny 5:11; linganisha na 2Ny 29:31-35; 30:23-25; 35:10-19.) Kuhani angeweza kutumika wakati ingine, kama tu ile haitasumbua makuhani wenye walikuwa wanatumika mu ile wakati. Kulingana na maandishi ya marabi, wakati Yesu alikuwa ku dunia, makuhani walikuwa wengi, kwa hiyo kikundi ya makuhani ilikuwa nagawanya mu mafamilia mbalimbali yenye kufanyiza ile kikundi kazi yenye walipaswa kufanya mu juma yao. Kwa kutegemea wingi wa familia zenye zilikuwa mu kikundi, kila familia ingeweza kutumika siku moya ao Zaidi.

it-2-F uku. 358 fu. 7

Muziki

Kuhusiana na matayarisho ya hekalu ya Yehova, Daudi alichagua Walawi 4000 kwa ajili ya muziki. (1Ny 23:4, 5) Kati yao, 288 “walizoezwa ili kumuimbia Yehova, wote wenye ujuzi.” (1Ny 25:7) Waimbaji wote walikuwa chini ya uongozi wa waimbaji wenye uzoefu sana, ni kusema Asafu, Hemani, na Yedutuni (mwenye inawezekana anaitwa pia Etani). Wote watatu walikuwa wazao wa mumoja kati ya wana Walawi; Asafu muzao wa Gershomu, Hermani muzao wa Kohati, na Yedutuni muzao wa Merari. Kwa hiyo, familia tatu za Walawi ziliwakilishwa mu mupango wa muziki wa hekalu. (1Ny 6:16, 31-33, 39-44; 25:1-6) Wana wa wale wanaume tatu, walikuwa 24, wote walikuwa kati ya wanamuziki 288 wenye uzoefu wenye tulishazungumuzia. Kila mumoja wa wale wana alichaguliwa kupitia kura ili asimamie kikundi moya ya wanamuziki. Chini ya uongozi wake, kulikuwa wanaume wengine 11 wenye “ujuzi,” wenye walichaguliwa kati ya wana wake na Walawi wengine. Kwa hiyo, kama tu vile makuhani, wanamuziki wenye ujuzi 288 ([1+11]×24=288) waligawanywa mu vikundi 24. Kama wale wengine ‘wanafunzi’ wapiga muziki 3712 wenye kubakia waligawanywa, kwa kukadiria mu kila kikundi ya vile vikundi 24 mungekuwa wanaume wengine karibu 155, ni kusema kila mwanamuziki mwenye uzoefu alikuwa na Walawi karibu 13 wenye alikuwa anazoeza kwa ajili ya muziki. (1Ny 25:1-31) Juu wapiga-tarumpeta walikuwa makuhani, wangeongezwa ku hesabu ya wanamuziki Walawi.​—2Ny 5:12; linganisha na Hes 10:8.

it-2-F uku. 620 fu. 3

Mulinzi wa mulango

Ku Hekalu. Wakati kidogo mbele Mufalme Daudi akufe, alipanga muzuri kazi ya Walawi na watumishi wa hekalu, kutia ndani walinzi wa milango wenye walikuwa 4000. Mu vikundi vyao walikuwa natumika siku 7 za kufuatana. Kazi yao ilikuwa kulinda nyumba ya Yehova na kuhakikisha kama milango inafunguliwa na kufungwa kwa wakati wenye kufaa. (1Ny 9:23-27; 23:1-6) Zaidi ya kazi ya ulinzi, wamoja walikuwa wanashugulikia michango yenye watu walikuwa wanaleta ku hekalu. (2Fa 12:9; 22:4) Wakati Yehoyada kuhani mukubwa alimuweka Yehoashi kuwa mufalme, walinzi wa pekee waliwekwa ku milango ya hekalu ili kumulinda Mufalme Yehoashi asishambuliwe na Malkia Atalia. (2Fa 11:4-8) Wakati Mufalme Yosia aliharibu sanamu zenye watu walikuwa wanaabudu, walinzi wa mulango walisaidia kutosha mu hekalu vyombo vyenye vilitumiwa juu ya ibada ya Baali. Kisha vikaunguzwa inje ya muji.​—2Fa 23:4.

Mali ya Kiroho

w22.03 uku. 22 fu. 10

Ibada ya Kweli Itaongeza Furaha Yako

10 Tunamuabudu Yehova wakati tunaimba. (Zb. 28:7) Waisraeli waliona kuimba kuwa sehemu ya maana sana ya ibada yao. Mufalme Daudi alipatia Walawi 288 mugao wa kuwa waimbaji mu hekalu. (1 Ny. 25:1, 6-8) Leo, tunaweza kuonyesha kama tunamupenda Mungu wetu kwa kumuimbia nyimbo za sifa. Sauti yetu haiko njo ya maana sana. Fikiria hii jambo: Mu kuzungumuza “sisi sote tunajikwaa mara nyingi,” lakini ile haiko njo yenye inatuzuiaka kusema mu kutaniko na mu mahubiri. (Yak. 3:2) Vilevile, hata kama hatuna sauti ya muzuri, tusiache ile ituzuie kumuimbia Yehova nyimbo za sifa.

Hotuba: Juu ya Nini Wakristo Wanapangwa Muzuri?

w11-SW 1/6 uku. 14-15

Je, Mungu Ana Watu Wanaomtumikia kwa Utaratibu?

Mitume na wanafunzi wa Yesu walihubiri kwa bidii, hivyo makutaniko mengi ya Kikristo yakaanzishwa katika sehemu nyingi za Asia na Ulaya katika karne ya kwanza. Ingawa makutaniko hayo yalikuwa yametawanyika, hayakufanya mambo bila mwongozo, wala kwa njia yao wenyewe. Badala yake, yalikuwa na utaratibu mzuri na yalinufaika kutokana na usimamizi wenye upendo wa mitume. Kwa mfano, mtume Paulo alimpa Tito mgawo wa kwenda Krete “ili kupanga mambo yote huko.” (Tito 1:5, The Jerusalem Bible) Paulo pia aliliandikia kutaniko la Korintho kwamba ndugu fulani walikuwa na “uwezo wa kupanga mambo.” (1 Wakorintho 12:28, The New Testament in Modern Speech) Lakini ni nani aliyesaidia kutaniko hilo kuwa na utaratibu huo? Paulo alisema kwamba Mungu ‘ameliweka,’ kutaniko “katika mpango.”​—1 Wakorintho 12:24, Biblia Habari Njema.

Waangalizi katika kutaniko la Kikristo hawakuwa mabwana wakubwa juu ya waamini wenzao. Badala yake walikuwa “wafanyakazi wenzi” waliofuata mwongozo wa roho ya Mungu, na walitazamiwa kuwa “vielelezo kwa kundi.” (2 Wakorintho 1:24; 1 Petro 5:2, 3) Yesu Kristo aliyefufuliwa ndiye “kichwa cha kutaniko,” bali si mwanadamu wala kikundi fulani cha watu wasio wakamilifu.​—Waefeso 5:23.

Wakati kutaniko la Korintho lilipoanza kufanya mambo tofauti kabisa na makutaniko mengine, Paulo aliwaandikia hivi: “Kwani! Je, neno la Mungu lilitoka kwenu, au je, liliwafikia ninyi tu?” (1 Wakorintho 14:36) Paulo alitumia swali hilo lisilohitaji jibu ili kurekebisha maoni yao na kuwasaidia waelewe kwamba hawakupaswa kufanya mambo kwa kufuata njia zao wenyewe. Makutaniko yaliongezeka na kusitawi yalipofuata mwongozo wa mitume.​—Matendo 16:4, 5.

Wonyesho wa Upendo wa Mungu

Namna gani leo? Watu fulani wanaweza kusita kujiunga na shirika fulani la kidini. Hata hivyo, Biblia inathibitisha kwamba wakati wote Mungu ametumia watu wake wenye utaratibu na umoja ili kutimiza kusudi lake. Alihakikisha kwamba waabudu wake katika Israeli la kale, na vilevile Wakristo wa karne ya kwanza, wanamwabudu kwa utaratibu.

Kwa hiyo, ni jambo linalopatana na akili kusema kwamba Yehova Mungu bado anawaongoza watu wake kama alivyofanya zamani. Ndiyo, Yehova anaonyesha kuwa anawapenda na kuwajali waabudu wake kwa kuhakikisha kwamba wana utaratibu na umoja. Leo, Yehova anatumia watumishi wake wenye utaratibu na umoja kutimiza kusudi lake kwa wanadamu. Mtu anaweza kuwatambua jinsi gani? Fikiria mambo yanayofuata:

▪ Wakristo wa kweli wamepangwa kwa utaratibu ili kutimiza kazi fulani. (Mathayo 24:14; 1 Timotheo 2:3, 4) Yesu aliwaamuru wafuasi wake wahubiri habari njema za Ufalme kwa mataifa yote, kazi ambayo haingewezekana bila kuwa na watu kutoka katika mataifa yote ambao wanaifanya kwa utaratibu na kwa umoja. Kwa mfano, unaweza kumlisha mtu mmoja peke yako, lakini kama ingekupasa kulisha maelfu ya watu, hata mamilioni, ungehitaji kikundi cha watu chenye utaratibu mzuri na kinachofanya kazi kwa ushirikiano. Ili kutimiza kazi yao, Wakristo wa kweli wanatumikia “bega kwa bega,” au “kwa moyo mmoja.” (Sefania 3:9; BHN) Je, ingewezekana kufanya kazi inayohusisha mataifa, lugha, na jamii mbalimbali bila kuwa na watu wenye utaratibu na umoja? Jibu ni wazi.

▪ Wakristo wa kweli wana mpangilio mzuri wa kutegemezana na kutiana moyo. Mtu anayepanda mlima akiwa peke yake anaweza kuamua ni upande gani wa mlima anaotaka kupanda, na si lazima ajishughulishe na wapandaji wengine wasio na uzoefu. Hata hivyo, akipatwa na aksidenti au tatizo lingine, atakuwa katika hatari kubwa, kwa sababu hakutakuwa na yeyote wa kumsaidia. Kwa hiyo, si jambo la hekima hata kidogo kujitenga na wengine. (Methali 18:1) Ili Wakristo watimize amri ya Yesu, ni lazima wasaidiane na kutegemezana. (Mathayo 28:19, 20) Kutaniko la Kikristo linaandaa maagizo, mafundisho, na mashauri yenye kutia moyo kutoka katika Biblia​—mambo ambayo yanahitajiwa sana ili wote waendelee kumtumikia Mungu bila kuacha. Ni wapi ambapo mtu angepata mafundisho kuhusu njia za Yehova kama hakungekuwa na mikutano ya Kikristo yenye utaratibu na umoja kwa ajili ya mafundisho na ibada?​—Waebrania 10:24, 25.

▪ Wakristo wa kweli wamepangwa kwa utaratibu ili kumtumikia Mungu kwa umoja. Kondoo wa Yesu wanaposikiliza sauti yake, wanakuwa “kundi moja” chini ya uongozi wake. (Yohana 10:16) Hawajatawanyika katika makanisa na vikundi tofauti-tofauti; wala hakuna mgawanyiko kati yao kuhusu mafundisho. Badala yake, wote ‘husema kwa upatano.’ (1 Wakorintho 1:10) Ili kukaa pamoja kwa umoja, tunahitaji utaratibu, nao utaratibu unahitaji mpangilio. Mungu anawabariki tu wale wanaomwabudu kwa umoja.​—Zaburi 133:1, 3.

Kumpenda Mungu kikweli na kupenda kweli ya Biblia kumewavuta wengi kwenye kikundi cha watu ambao pia wanampenda Mungu na Neno lake Biblia. Wakiwa kikundi cha watu wenye utaratibu na umoja, Mashahidi wa Yehova duniani kote wanajitahidi kufanya mapenzi ya Mungu. Wana uhakika katika ahadi hii ya Mungu: “Mimi nitakaa katikati yao na kutembea katikati yao, nami nitakuwa Mungu wao, nao watakuwa watu wangu.” (2 Wakorintho 6:16) Unaweza kufurahia baraka hizo ukimwabudu Yehova Mungu ukiwa pamoja na watu wake wenye utaratibu na umoja.

TAREHE 13-19/3

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 1 MAMBO YA NYAKATI 27-29

“Shauri Yenye Upendo Yenye Baba Anapatia Mwana Wake”

w05-SW 15/2 uku. 19 fu. 9

Kulinda Utambulisho Wetu wa Kikristo

9 Jihakikishie kweli ya Biblia. Utambulisho wetu tukiwa watumishi wa Yehova unaweza kudhoofika usipotegemea kabisa ujuzi wa Biblia. (Wafilipi 1:9, 10) Kila Mkristo, kijana au mzee anahitaji kujihakikishia na kuridhika kwamba mambo anayoamini ndiyo kweli inayopatikana katika Biblia. Paulo aliwahimiza waamini wenzake hivi: “Hakikisheni mambo yote; shikeni sana yaliyo mazuri.” (1 Wathesalonike 5:21) Vijana Wakristo wanaotoka katika familia zinazomwogopa Mungu wanapaswa kutambua kwamba hawawezi kuwa Wakristo wa kweli kwa sababu tu ya imani ya wazazi wao. Daudi, baba ya Sulemani, alimhimiza ‘amjue Mungu wa baba yake, amtumikie kwa moyo kamili.’ (1 Mambo ya Nyakati 28:9) Haingetosha tu kijana Sulemani kutazama jinsi baba yake alivyositawisha imani katika Yehova. Alipaswa kumjua Yehova yeye mwenyewe, naye alifanya hivyo. Alimsihi Mungu hivi: “Sasa unipe hekima na ujuzi ili nitoke mbele ya watu hawa na ili niingie ndani.”​—2 Mambo ya Nyakati 1:10.

w12 15/4 uku. 16 fu. 13

Endelea Kuwa na Moyo Usiogawanyika Kumuelekea Yehova

13 Somo tunalopata kutokana na mufano huo liko wazi. Kukusanyika kwa ukawaida, na kuhubiri ni mambo yenye kusifiwa. Lakini ndugu ao dada anaweza kufanya mambo hayo bila kumutumikia Yehova kwa moyo wote. (2 Nya. 25:1, 2, 27) Ikiwa Mukristo anaendelea kupenda “mambo yaliyo nyuma” katika moyo wake, yaani, anaendelea kupenda mambo fulani ya maisha ya ulimwengu huu, Mukristo kama huyo anapatikana katika hatari ya kukataliwa na Mungu. (Luka 17:32) Tutakuwa watu wenye ‘kufaa kwa ajili ya Ufalme wa Mungu’ ikiwa tu ‘tunachukia mabaya, na kushikamana na mema.’ (Rom. 12:9; Luka 9:62) Kwa hiyo, sisi wote tunapaswa kuhakikisha kama tunatia faida za Ufalme pa nafasi ya kwanza na kama haturuhusu jambo lolote katika ulimwengu huu wa Shetani liturudishe nyuma na kutuzuia tusimutumikie Yehova kwa moyo wote, hata kama jambo hilo linaonekana kuwa la lazima ao lenye kuvutia.​—2 Kor. 11:14; soma Wafilipi 3:13, 14.

w17.09 uku. 32 fu. 20-21

“Ukuwe Hodari . . . na Utende’”

20 Mufalme Daudi alimukumbusha Sulemani kuwa Yehova angekuwa pamoja naye mupaka kazi ya kujenga hekalu imalizike. (1 Nya. 28:20) Sulemani aliweka maneno hayo ya baba yake katika moyo na akili yake, kwa hiyo, hata kama alikuwa kijana na hakukuwa na uzoefu, hakuacha mambo hayo yamuzuie kufanya kazi. Alionyesha uhodari mukubwa, akatenda, na kwa musaada wa Yehova alimaliza kazi ya kujenga hekalu la muzuri sana katika miaka saba na nusu.

21 Kama vile Yehova alimusaidia Sulemani, anaweza kutusaidia tuonyeshe uhodari na tutimize kazi yetu, katika familia yetu na katika kutaniko. (Isa. 41:10, 13) Wakati tunaonyesha uhodari katika ibada yetu kwa Yehova, tunaweza kuwa hakika kuwa atatubariki sasa na wakati wenye kuja. Kwa hiyo, ‘ukuwe hodari . . . na utende.’

Mali ya Kiroho

w17.03 uku. 29 fu. 6-7

Utaendelea Kuwa Rafiki Wakati Urafiki Uko Katika Hatari?

Daudi alikuwa na marafiki wengine wenye walishikamana naye wakati wa magumu. Mumoja kati ya marafiki hao alikuwa Hushai, mwenye Biblia inazungumuzia kuwa “rafiki ya Daudi.” (2 Samweli 16:16; 1 Mambo ya Nyakati 27:33) Pengine alikuwa mukubwa wa makao ya mufalme na mwenye alikuwa rafiki yake wa sana, mwenye wakati fulani alikuwa anatimiza maagizo ya siri ya mufalme.

Wakati Absalomu, mutoto wa Daudi alikuwa anapenda kunyanganya kiti cha ufalme, Waisraeli wengi walijiunga na Absalomu, lakini Hushai hakufanya hivyo. Wakati Daudi alikuwa anakimbia, Hushai alienda kumuona. Daudi alivunjika moyo sana kwa sababu mutoto wake mwanaume na watu fulani wenye alikuwa anatumainia walimusaliti. Hushai aliendelea kuwa mushikamanifu, na alikuwa tayari kutia uzima wake katika hatari na kutimiza mugawo wenye ungefanya njama yao ishindwe. Hushai hakufanya hivyo tu kwa sababu alikuwa mukubwa wa makao ya mufalme. Alijionyesha kuwa rafiki mushikamanifu.​—2 Samweli 15:13-17, 32-37; 16:15–17:16.

TAREHE 20-26/3

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 1-4

“Mufalme Sulemani Anakamata Uamuzi Mubaya”

it-1-F uku. 181 fu. 3

Jeshi

Wakati wa utawala wa Sulemani, kulikuwa mabadiliko makubwa mu historia ya jeshi ya Israeli. Wakati wa utawala wake, mu Israeli mulikuwa amani kwa kiasi kikubwa, hata vile alijiongezea farasi na magari ya vita. (ona Magari ya Vita.) Sehemu kubwa ya zile farasi zilinunuliwa na kuletwa kutoka Misri. Miji ilipaswa kujengwa fasi mbalimbali mu Israeli kwa ajili ya vile vikundi vya mupya vya kijeshi. (1Fa 4:26; 9:19; 10:26, 29; 2Ny 1:14-17) Lakini, Yehova hakubariki ile mipango ya Sulemani. Kisha yeye kufa na ufalme wa Israeli kugawanyika, jeshi ya Israeli ilifikia mwisho. Sawa vile Isaya aliandika kisha pale: “Ole wao wale wenye wanashuka kuenda Misri ili kutafuta musaada, wenye wanategemea farasi, wenye wanategemea magari ya vita kwa sababu ni mengi sana, na farasi wa vita kwa sababu wako na nguvu, lakini hawamuangalie Mutakatifu wa Israeli, na hawamutafute Yehova.”​—Isa 31:1.

it-1-F uku. 430 fu. 4, 5

Magari ya Vita

Mbele Sulemani aanze kutawala, mu Israeli hamukukuwa jeshi yenye kutumia magari mingi ya vita. Ile ilikuwa juu Mungu alikuwaka alishaonya kama mufalme hakupaswa kujiongezea farasi, kwa sababu usalama wa inchi haukutokana na zile farasi. Ile ilifanya magari ya vita isitumiwe sana, juu farasi njo zilikuwa zinatumiwa ili kukokota ile magari. (Kum 17:16) Wakati Samweli alionya Waisraeli juu ya muzigo wenye wafalme wanadamu wangewaletea, aliwaambia hivi: “Atachukua wana wenu na kuwatia katika magari yake.” (1Sa 8:11) Ili kujaribu kunyanganya ufame, Adoniya na pia Absalomu, walikuwa na gari ya kukokotwa, na wanaume 50 walikuwa wanakimbia mbele yao. (2Sa 15:1; 1Fa 1:5) Wakati Daudi alipata ushindi juu ya mufalme wa Zoba, alilinda farasi 100 za kukokota magari ya vita.​—2Sa 8:3, 4; 10:18.

Wakati Mufalme Sulemani alikuwa anatia nguvu jeshi ya Israeli, aliongeza hesabu ya magari ya vita, mupaka ikafikia 1400. (1Fa 10:26, 29; 2Ny 1:14, 17) Zaidi ya Yerusalemu, kulikuwa miji ingine yenye ilijulikana kuwa miji ya magari ya vita yenye ilikuwa na majengo ya kushugulikia vile vyombo ya vita.​—1Fa 9:19, 22; 2Ny 8:6, 9; 9:25.

Mali ya Kiroho

w05-SW 1/12 uku. 19 fu. 6

Mambo Makuu Katika Kitabu cha Pili cha Mambo ya Nyakati

1:11, 12. Ombi la Sulemani lilimthibitishia Yehova kwamba kupata hekima na ujuzi ndilo lililokuwa jambo muhimu kwa mfalme. Kwa kweli, sala zetu kwa Mungu hufunua yaliyo muhimu kwetu. Ni jambo la hekima kuchunguza yale tunayosema katika sala zetu.

TAREHE 27/3–2/4

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 5-7

‘Moyo Wangu Utakuwa Pale Sikuzote’

w02-SW 15/11 uku. 5 fu. 1

Msiache Kukusanyika Pamoja

Baadaye, Daudi alipokuwa mfalme huko Yerusalemu, alitamani sana kumjengea Yehova nyumba ya kudumu ambayo ingemletea Yehova utukufu. Hata hivyo, kwa kuwa Daudi alipigana vita vingi sana, Yehova alimwambia hivi: “Hutajenga nyumba kwa ajili ya jina langu.” Badala yake, alimchagua Solomoni, mwana wa Daudi, amjengee hekalu. (1 Mambo ya Nyakati 22:6-10) Solomoni alizindua hekalu hilo mwaka wa 1026 K.W.K., baada ya kulijenga kwa muda wa miaka saba u nusu. Yehova alilikubali jengo hilo na kusema: “Nimeitakasa nyumba hii uliyoijenga ili niweke jina langu humo milele; tena macho yangu na moyo wangu utakuwapo hapo sikuzote.” (1 Wafalme 9:3) Nyumba hiyo ingeendelea kuwa na kibali cha Yehova maadamu Waisraeli wangedumu wakiwa waaminifu. Lakini iwapo wangeacha kutenda mema, Yehova angeondoa kibali chake kutoka mahali hapo, na ‘nyumba hiyo ingebomoka na kuwa magofu.’​—1 Wafalme 9:4-9, NW; 2 Mambo ya Nyakati 7:16, 19, 20.

it-2-F uku. 1048 fu. 5

Hekalu

Historia. Mwisho wa hekalu ulifika mu mwaka wa 607 M.K.Y., wakati iliharibiwa na majeshi ya Wababiloni yenye iliongozwa na Mufalme Nebukadneza. (2Fa 25:9; 2Ny 36:19; Yer 52:13) Juu Waisraeli walianza kuabudu miungu ya uongo, Mungu aliruhusu mataifa mbalimbali ishambulie Yuda na Yerusalemu. Wakati fulani ile mataifa ilichukua vitu vya samani vya mu hekalu. Na wakati ingine watu hawakuhangaikia hekalu. Mufalme Shishaki wa Misri alikamata vitu vya samani vya mu hekalu (993 M.K.Y.) wakati wa utawala wa Rehoboamu mwana wa Sulemani; ilikuwa karibu miaka 33 tu kisha hekalu kutolewa kwa Yehova. (1Fa 14:25, 26; 2Ny 12:9) Mufalme Asa (977-937 M.K.Y.) aliheshimia nyumba ya Yehova, lakini juu ya kulinda Yerusalemu alitenda kwa upumbavu kwa kumupatia mufalme wa Waasiria, Ben-hadadi wa Kwanza, feza na zahabu kutoka mu hazina ya hekalu, ili Ben-hadadi avunje mapatano yenye alikuwa nayo na Mufalme Baasha wa Israeli.​—1Fa 15:18, 19; 2Ny 15:17, 18; 16:2, 3.

Mali ya Kiroho

w10-SW 1/12 uku. 11 fu. 7

Anajua “Moyo wa Wanadamu”

Tunaweza kufarijiwa na sala ya Sulemani. Huenda wanadamu wenzetu wasielewe hisia zetu za ndani​—‘pigo letu’ na ‘maumivu yetu’ wenyewe. (Methali 14:10) Lakini Yehova anaujua moyo wetu, na anatujali sana. Kumweleza hisia zetu za moyoni kupitia sala, kunaweza kufanya mizigo yetu iwe rahisi kubeba. Biblia inasema: ‘Tupeni mahangaiko yenu yote juu yake, kwa sababu yeye anawajali ninyi.’​—1Petro 5:7.

Hotuba: Tutafanya Nini Ikiwa Hali Fulani ya Pekee Inatuzuia Kufika ku Ukumbusho?

w93-SW 1/2 uku. 31

Maswali Kutoka kwa Wasomaji

Mkristo akiwa mgonjwa au anasafiri na hivyo asiweze kuwa kwenye mwadhimisho wa Ukumbusho, je, anapaswa auadhimishe mwezi mmoja baadaye?

Katika Israeli ya kale Sikukuu ya Kupitwa ilifanywa kila mwaka siku ya 14 ya mwezi wa kwanza, ulioitwa Nisani (au, Abibu). Lakini tunapata uandalizi wa pekee kwenye Hesabu 9:10, 11: “Nena na wana wa Israeli, na kuwaambia, Mtu wa kwenu, au wa vizazi vyenu, ye yote atakayekuwa na unajisi kwa ajili ya maiti, au akiwako mbali katika safari, na haya yote, ataishika Pasaka kwa BWANA [Yehova, NW]; mwezi wa pili [ulioitwa Iyyari, au Zivu], siku ya kumi na nne ya mwezi, wakati wa jioni, wataishika; watamla pamoja na mikate isiyotiwa chachu na mboga za uchungu.”

Ona kwamba hiyo haikuanzisha tarehe mbili tofauti za Sikukuu ya Kupitwa (Nisani 14 au Zivu 14), kwa Mwisraeli yeyote au watu wa nyumba yoyote kuchagua kwa hiari, kulingana na hali inayofaa zaidi. Uandalizi wa mlo wa Sikukuu ya Kupitwa katika mwezi wa pili ulikuwa na mpaka. Ilikuwa kwa hali ya pekee kwa Mwisraeli aliyekuwa mchafu kisherehe katika Nisani 14 au mbali sana na mahali ambapo mwadhimiso wa kawaida ulifanywa.

Kisa pekee kilichorekodiwa cha uandalizi huo kutumiwa sana kilikuwa wakati Mfalme Hezekia mwaminifu alipoanzisha tena mwadhimisho wa Sikukuu ya Keki Zisizochachishwa. Hakukuwa na wakati wa kutosha wa kujitayarisha kwa ajili ya mwezi wa kwanza (makuhani wakiwa si tayari wala watu wakiwa hawajakusanyika), kwa hiyo ilifanywa katika siku ya 14 ya mwezi wa pili.​—2 Mambo ya Nyakati 29:17; 30:1-5.

Isipokuwa kwa sababu ya hali hizo za pekee, Wayahudi waliadhimisha Sikukuu ya Kupitwa katika tarehe ambayo Mungu alikuwa ameweka. (Kutoka 12:17-20, 41, 42; Mambo ya Walawi 23:5) Yesu na wanafunzi wake waliadhimisha jinsi sheria ilivyotaka, bila kuona tarehe hiyo kivivi hivi. Luka aripoti hivi: “Ikafika siku ya mikate isiyotiwa chachu, ambayo ilipasa kuchinja pasaka. [Yesu] akawatuma Petro na Yohana, akisema, Nendeni, mkatuandalie pasaka tupate kuila.”​—Luka 22:7, 8.

Katika pindi hiyo Yesu alianzisha mwadhimisho wa kila mwaka ambao Wakristo huujua kuwa Chakula cha Jioni cha Bwana. Thamani ya Wakristo kuhudhuria haiwezi kukaziwa kupita kiasi. Hilo ndilo tukio la maana zaidi katika mwaka wa Mashahidi wa Yehova. Maneno ya Yesu huonyesha sababu ya hilo; alisema hivi: “Fanyeni [fulizeni kufanya, NW] hivi kwa ukumbusho wangu.” (Luka 22:19) Kwa hiyo, Mashahidi wa Yehova wote wapaswa wapange miezi mingi kimbele wasipangie mambo mengine kwenye tarehe hiyo ya mwadhimisho. Chakula cha Jioni cha Bwana kitaadhimishwa Ijumaa Aprili 6, 1993, baada ya jua kushuka kulingana na mahali.

Katika visa vya hali isiyotazamiwa, kama vile ugonjwa au kutatanika kwa safari, yaweza kumzuia Mkristo asihudhurie kama alivyokuwa amepanga. Jambo gani lifanywe katika hali hiyo?

Katika mwadhimisho huo mkate usiotiwa chachu na divai nyekundu hupitishwa, na wale ambao wamepakwa mafuta kwa roho takatifu ya Mungu na ambao wamechaguliwa kwa ajili ya uhai mbinguni hushiriki. (Mathayo 26:26-29; Luka 22:28-30) Ikiwa mwaka huu mmoja ambaye amekuwa akishiriki kila mwaka ni mgonjwa kitandani iwe nyumbani au hospitalini, wazee wa mahali hapo watapanga mmoja wao ampelekee mgonjwa huyo mkate na divai, azungumze maandiko yanayohusu habari hiyo, na kutoa mifano. Ikiwa Mkristo fulani aliye mpakwa-mafuta yu mbali na kundi lake la nyumbani, anapaswa apange kwenda kwenye kundi katika eneo ambamo atakuwamo tarehe hiyo.

Kulingana na hayo, ingekuwa chini ya hali za pekee sana kwamba Mkristo mpakwa-mafuta angelazimika aadhimishe Chakula cha Jioni cha Bwana siku 30 baadaye (mwezi mmoja wa luna), kwa kupatana na amri kwenye Hesabu 9:10, 11 na kile kielelezo kwenye 2 Mambo ya Nyakati 30:1-3, 15.

Wale ambao ni “kondoo wengine” wa Yesu, wenye tumaini la uhai wa milele kwenye dunia-paradiso, hawako chini ya ile amri ya kushiriki mkate na divai. (Yohana 10:16) Ni muhimu kuhudhuria mwadhimisho huo wa kila mwaka, lakini hawashiriki mifano. Kwa hiyo ikiwa mmoja wao ni mgonjwa au anasafiri na hivyo hayuko pamoja na kundi lolote jioni hiyo, yeye aweza kusoma kifaragha maandiko yanayohusu (kutia na ule usimulizi wa Yesu akianzisha mwadhimisho huo) na kusali kwa ajili ya baraka ya Yehova juu ya tukio hilo ulimwenguni pote. Lakini katika kisa hiki hakuna uhitaji wa kufanya mpango mwingine zaidi wa kuwa na mkutano au mazungumzo ya Kibiblia ya pekee mwezi ufuatao.

TAREHE 10-16/4

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 8-9

“Aliona Hekima Kuwa ya Maana”

w99-SW 1/11 uku. 20 fu. 4

Ukarimu Unapokuwa Mwingi

Bila shaka, malkia wa Sheba pia alitumia wakati wake mwingi na jitihada pia ili kumzuru Solomoni. Yaonekana Sheba ilikuwa katika eneo ambalo sasa ni Jamhuri ya Yemeni; hivyo malkia huyo, na msafara wake wa ngamia, alisafiri zaidi ya kilometa 1,600 kwenda Yerusalemu. Kama vile Yesu alivyosema, “alikuja kutoka miisho ya dunia.” Kwa nini malkia wa Sheba alifanya jitihada kubwa hivyo? Alikuja hasa “aisikie hekima ya Solomoni.”​—Luka 11:31.

w99-SW 1/7 uku. 30 fu. 4-5

Ziara Iliyothawabishwa Sana

Kwa vyovyote vile, malkia huyo aliwasili Yerusalemu “na wafuasi wengi sana, na ngamia wachukuao manukato, na dhahabu nyingi sana, na vito vya thamani.” (1 Wafalme 10:2a) Watu fulani husema kuwa hao “wafuasi wengi sana” walikuwa ni pamoja na kikosi chenye silaha. Hilo laeleweka, ukikumbuka kwamba malkia huyo alikuwa mheshimiwa mwenye nguvu, akisafiri na mali zenye thamani kubwa sana.

Hata hivyo, ona kwamba malkia alisikia umaarufu wa Solomoni “juu ya jina la BWANA.” Hivyo, safari hiyo haikuwa ya kibiashara tu. Yamkini, malkia alikuja hasa kusikiliza hekima ya Solomoni​—labda hata kujifunza jambo fulani kuhusu Mungu wa Solomoni, Yehova. Kwa vile yawezekana alikuwa wa uzao wa Shemu ama Hamu, waliokuwa waabudu wa Yehova, huenda alikuwa mdadisi kuhusu dini ya mababu wake.

w99-SW 1/7 uku. 30-31

Ziara Iliyothawabishwa Sana

Malkia wa Sheba alivutiwa sana na hekima ya Solomoni na ufanisi wa ufalme wake hivi kwamba “roho yake ilizimia.” (1 Wafalme 10:4, 5) Wengine husema kuwa fungu hilo lamaanisha malkia “alihemahema.” Msomi mmoja hata adokeza kwamba alizimia! Hata iweje, malkia alishangazwa na yale aliyoona na kusikia. Aliwatangaza watumishi wa Solomoni kuwa wenye furaha kwa kusikiliza hekima ya mfalme huyo, naye akamtukuza Yehova kwa kumweka Solomoni kwenye kiti cha ufalme. Kisha akampa mfalme zawadi zenye thamani kubwa, dhahabu pekee ilifikia, kwa bei ya sasa, dola 40000000 hivi. Naye Solomoni akamtunukia zawadi, akampa malkia “haja yake yote, kila alilotaka.”​— 1 Wafalme 10:6-13.

it-2-F uku. 873 fu. 6

Sulemani

Kisha malkia wa Sheba kuona utukufu wa hekalu na wa nyumba ya Sulemani, chakula ya meza yake na vinywaji vyake, nguo za watumishi wa meza yake, na zabihu zenye alitoa kwa ukawaida ku hekalu, “alibakia kinywa wazi.” Basi akamuambia mufalme: “Na angalia! sikukuwa nimeambiwa hata nusu yake. Hekima yako na mafanikio yako vimepita sana habari zenye nilisikia.” Kisha akaanza kutangaza watumishi wa mufalme kuwa wenye furaha. Ile yote ilimuchochea amusifu Yehova, mwenye alionyesha Waisraeli upendo kwa kuwapatia Sulemani kuwa mufalme ili kutenda haki na uadilifu.​—1Fa 10:4-9; 2Ny 9:3-8.

Mali ya Kiroho

it-2-F uku. 1110 fu. 1

Kiti cha Ufalme

Kati ya Wafalme Waisraeli, kiti ya ufalme yenye Sulemani alijitengenezea njo tu inazungumuziwa sana mu Biblia. (1Fa 10:18-20; 2Ny 9:17-19) Inaonekana ilikuwa mu “Jumba ya kiti cha ufalme,” moja kati ya majengo yenye ilikuwa ku Mulima Moria mu Yerusalemu. (1Fa 7:7) ilikuwa kiti yenye ilifanyizwa kwa pembe ya tembo yenye kufunikwa na zahabu safi na ilikuwa na mufuniko ya muviringo nyuma yake na ilikuwa na mikono. Hata kama inawezekana kuwa pembe ya tembo njo ilitumiwa sana juu ya kutengeneza ile kiti, ufundi wenye ulitumiwa kwa kawaida juu ya kutengeneza vitu ku hekalu unafanya ionekane sawa vile ilitengenezwa kwa mbao, kisha ikafunikwa kwa zahabu, na juu yake walitia mapambo ya mingi ya pembe ya tembo. Kwa mwenye angeangalia ile kiti, angeona kama imetengenezwa tu na pembe ya tembo na zahabu. Kisha kuzungumuzia vile vipandio sita vyenye kupeleka kwenye kiti ya ufalme, habari inaendelea hivi: “Simba wawili walikuwa wanasimama pembeni ya mikono ya kiti. Na kulikuwa simba kumi na mbili (12) wenye kusimama kwenye vile vipandio sita (6), wawili kwenye kila kipandio, mumoja upande huu na mwingine upande mwingine.” (2Ny 9:17-19) Ile ilifaa kabisa juu simba anafananisha mamlaka ya kutawala. (Mwa 49:9, 10; Ufu 5:5) Inaonekana kuwa wale simba 12 walifananisha makabila 12 ya Israeli, pengine juu ya kuonyesha kama wote walipaswa kujitiisha na kutegemeza ule mwenye kukaa juu ya kile kiti cha ufalme. Kulikuwa kiti ya zahabu ya miguu yenye ilishikamana kwa njia fulani na kiti cha Ufalme. Namna inazungumuziwa, ile kiti yenye kufanyizwa na pembe ya tembo na zahabu​—ya hali ya juu, yenye kufunikwa muzuri, yenye kuwa na simba za ajabu mbele yake​—inapita viti vingine vyote vya ufalme vya ile wakati. Mambo yenye watu wenye kuchimbua vitu vya zamani walivumbua, michoro yenye kuwa ku minara mbalimbali, na mafasirio yenye kuwa mu maandishi mbalimbali inaonyesha vile. Sawa vile mwenye aliandikaka kitabu ya Mambo ya Nyakati anaonyesha: “Hakuna ufalme mwingine wowote wenye ulifanya kitu kama hicho.”​—2Ny 9:19.

TAREHE 17-23/4

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 10-12

“Sikiliza Mashauri Yenye Hekima ili Upate Faida”

w18.06 uku. 13 fu. 3

Angekubaliwa na Mungu

Rehoboamu alipaswa kukamata uamuzi muzito. Ikiwa angefanya mambo yenye watu waliomba, yeye na familia yake na wale wenye waliishi katika nyumba ya mufalme wangelazimika kuishi bila vitu fulani vya hali ya juu vyenye walikuwa wamezoea. Lakini, ikiwa angekataa ombi la watu, wangeweza kumuasi. Alifanya nini? Alizungumuza kwanza na wanaume wazee wenye walitumika pamoja na baba yake. Walimuambia asikilize watu. Lakini, kisha Rehoboamu alizungumuza na vijana wa miaka yake na aliamua kutendea watu kwa ukali. Aliambia watu hivi: ‘Nitaifanya nira yenu ikuwe nzito zaidi, nami nitaizidisha. Baba yangu aliwatia ninyi adabu kwa fimbo, lakini mimi nitawatia adabu kwa mijeledi.’​—2 Nya. 10:6-14.

w01-SW 1/9 uku. 28-29

Jinsi Unavyoweza Kufanya Maamuzi ya Hekima

Yehova huandaa pia watu wakomavu katika kutaniko ambao tunaweza kuzungumza nao kuhusu maamuzi yetu. (Waefeso 4:11, 12) Hata hivyo, tunapotafuta shauri kutoka kwa wengine, tusiwe kama watu ambao humwendea mtu mmoja hadi mwingine mpaka mwishowe wapate mtu atakayewaunga mkono. Kisha wanafuata shauri lake. Pia twapaswa kukumbuka kielelezo chenye kuonya cha Rehoboamu. Alipokabili uamuzi mzito, alipokea shauri bora kabisa kutoka kwa wanaume wazee waliokuwa wametumikia pamoja na babake. Hata hivyo, badala ya kufuata shauri lao, aliendea vijana waliokua pamoja naye. Kwa kufuata shauri lao, alifanya uamuzi mbaya sana na kwa sababu hiyo akapoteza sehemu kubwa ya ufalme wake.​—1 Wafalme 12:1-17.

Unapotafuta shauri, litafute kutoka kwa watu wenye uzoefu katika maisha na wanaofahamu vizuri Maandiko na kustahi sana kanuni zinazofaa. (Mithali 1:5; 11:14; 13:20) Inapowezekana, chukua wakati kutafakari kanuni zinazohusika na habari zote ambazo umetafiti. Unapoanza kuona mambo kulingana na Neno la Yehova, yaelekea itakuwa dhahiri zaidi kufikia uamuzi unaofaa.​—Wafilipi 4:6, 7.

it-2-F uku. 754 fu. 5

Rehoboamu

Juu ya kiburi na kupenda kutawala watu kinguvu, Rehoboamu alifanya watu wengi wapotee. Kabila ya Yuda na ya Benyamini tu njo iliendelea kutegemeza nyumba ya Daudi. Makuhani Walawi wa falme zote mbili, na watu fulani kutoka mu ile makabila kumi, walitegemeza pia nyumba ya Daudi.​—1Fa 12:16, 17; 2Ny 10:16, 17; 11:13, 14, 16.

Mali ya Kiroho

it-1-F uku. 618 fu. 7-619 fu. 1

Pepo Muchafu Mwenye Kufanana na Mbuzi

Maneno ya Yoshua yenye kuwa mu Yoshua 24:14 inaonyesha kama Waisraeli walikuwa wameanza kuchochewa kwa kiasi fulani na ibada ya uongo ya Wamisri, na Ezekieli anaonyesha kama waliendelea kuwa na zile desturi za kipagani muda murefu kisha kutoka Misri. (Eze 23:8, 21) Njo maana watu fulani wenye elimu wanasema kama amri yenye Mungu alipatia Waisraeli mu jangwa ya kuwakataza kutoa “zabihu kwa pepo wachafu wenye kufanana mbuzi,” (Law 17:1-7) matendo ya Yeroboamu ya kuweka makuhani “kwa ajili ya mahali pa juu na kwa ajili ya pepo wachafu wenye kufanana na mbuzi na vitoto-dume vya ngombe vyenye alikuwa ametengeneza,” (2Ny 11:15) vinaonyesha kama mu Israeli mulikuwa aina fulani ya ibada ya mbuzi sawa yenye ilifanyika Misri, zaidi sana mu Misri ya Chini. Herodot (II, 46) alisema kama ni kutokana na ile ibada ya Wamisri njo Wagiriki walianzisha ibada ya mungu Pana na ya kiumbe nusu mutu nusu mbuzi​—miungu ya mapori​—yenye inaonyeshwa kuwa na mapembe, mukiya ya mbuzi, na miguu ya mbuzi. Watu fulani wanasema kama ile umbo ya nusu munyama ya ile miungu ya uongo njo ilitokeza zoea ya kuonyesha picha ao michoro ya Shetani akiwa na mukia, mapembe na miguu yenye kwato yenye kupasuka katikati. Ile zoea ilienea sana kati ya Wakristo wenye waliishi mu Kipindi ya Giza.

Lakini haionyeshwe wazi “yenye kuwa na manyoya mingi” (seʽi·rimʹ) ilikuwa nini. Watu fulani wanawaza kama ilikuwa mbuzi ao sanamu ya umbo wa mbuzi. Lakini ile haionyeshwe; na hakuna andiko ya Biblia yenye inaunga mukono Ile mawazo. Maneno yenye kutumiwa ingeweza tu kuonyesha mu akili za watu wenye kuziabudu kama ile miungu ilitengenezwa kwa umbo wa mbuzi ao ilikuwa Inaonekana kuwa na manyoya mingi. Ao, kutumiwa kwa neno “mbuzi” mu hii maandiko ni njia tu ya kuonyesha kama sanamu zote ni zenye kuchukiza, sawa vile mu maandiko mingi neno sanamu inatokana na neno yenye kumaanisha “mavi,” lakini ile haimaanishe kama zile sanamu zilitengenezwa kabisa na mavi.​—Law 26:30; Kum 29:17.

Hotuba: Uzoeze Wanafunzi Wako wa Biblia Wakati Wanaomba Mashauri

be-SW uku. 69 fu. 4-5

Jua Jinsi Unavyopaswa Kujibu

Mwanafunzi wa Biblia au mwamini mwenzako anapouliza afanyeje katika hali fulani hususa, utamjibuje? Huenda unajua jambo ambalo wewe binafsi ungefanya. Lakini ni lazima kila mtu abebe daraka la maamuzi yake mwenyewe maishani. (Gal. 6:5) Mtume Paulo alieleza kwamba aliwatia moyo watu aliowahubiria ‘watii kwa njia ya imani.’ (Rom. 16:26) Huo ni mfano mzuri tunaopaswa kuiga. Mtu ambaye anafanya maamuzi ili hasa kumpendeza mwalimu wake wa Biblia au kumpendeza mtu mwingine anatumikia wanadamu na haishi kwa imani. (Gal. 1:10) Basi, huenda haifai kumjibu kwa njia rahisi na ya moja kwa moja yule anayeuliza swali.

Basi, unawezaje kujibu kwa njia inayopatana na miongozo ya Biblia? Unaweza kuonyesha kanuni na mifano inayofaa iliyoko katika Biblia. Katika hali nyinginezo, unaweza kumwonyesha jinsi ya kufanya utafiti ili yeye mwenyewe apate kanuni hizo na mifano hiyo. Hata unaweza kuzungumzia kanuni hizo na faida ya mifano hiyo bila kuihusisha na suala mnalozungumzia. Mwulize kama anaona jambo lolote katika kanuni hizo na mifano hiyo linaloweza kumsaidia kufanya uamuzi wenye hekima. Akizingatia kanuni hizo na mifano hiyo, umtie moyo afikirie uamuzi ambao ungemfurahisha Yehova. Kwa njia hiyo unamsaidia ‘kuzoeza nguvu zake za ufahamu kutofautisha lililo sahihi na lililo kosa pia.’​—Ebr. 5:14.

TAREHE 24-30/4

UTAJIRI WA NENO YA MUNGU | 2 MAMBO YA NYAKATI 13-16

“Ni Wakati Gani Njo Unapaswa Kumutegeea Yehova?”

w21.03 uku. 5 fu. 12

Vijana​—Munaweza Kufanya Nini juu Wengine Wawatumainie?

12 Wakati alikuwa kijana, Mufalme Asa alikuwa na sifa ya unyenyekevu na uhodari. Kwa mufano, kisha baba yake Abiya kufa, Asa alianza kutawala. Na akaanza kuondoa mu inchi ibada ya sanamu. Pia, “aliambia Yuda wamutafute Yehova Mungu wa mababu zao na washike Sheria na amri.” (2 Ny. 14:1-7) Na wakati Zera Mwetiopia alishambulia Yuda pamoja na maaskari wake 1000000, kwa hekima, Asa alimuomba Yehova musaada. Alisema hivi: “Ee Yehova, haiko shida kwako ikuwe wale wenye unasaidia ni wengi ao hawana nguvu. Utusaidie, Ee Yehova Mungu wetu, kwa maana tunakutegemea wewe.” Hii maneno ya muzuri yenye Asa alisema, inaonyesha kuwa Asa alikuwa na imani yenye nguvu kama Yehova iko na uwezo wa kumuokoa na kuokoa watu wake. Asa alimutumainia Yehova, Baba yake wa mbinguni, na “Yehova akashinda Waetiopia.”​—2 Ny. 14:8-12.

w21.03 uku. 5 fu. 13

Vijana​—Munaweza Kufanya Nini juu Wengine Wawatumainie?

13 Bila shaka, kupigana na kikundi cha maaskari 1000000 ilikuwa jambo la kuogopesha sana, lakini Asa alipata ushindi juu alimutumainia Yehova. Lakini, jambo la kuhuzunisha, wakati Asa alipata tatizo lingine lenye haliko la kuogopesha sana, Asa hakumutumainia Yehova. Wakati Baasha, mufalme muovu wa Israeli alimuogopesha, Asa alienda kuomba mufalme wa Siria musaada. Ule uamuzi ulileta matokeo ya mubaya! Kupitia nabii Hanani, Yehova alimuambia Asa hivi: “Kwa sababu ulimutegemea mufalme wa Siria na haukumutegemea Yehova Mungu wako, jeshi la mufalme wa Siria limeponyoka kutoka katika mukono wako.” Kwa kweli, kuanzia pale, Asa alikuwa anapigana vita kila mara. (2 Ny. 16:7, 9; 1 Fa. 15:32) Ile habari inatufundisha nini?

w21.03 uku. 6 fu. 14

Vijana​—Munaweza Kufanya Nini juu Wengine Wawatumainie?

14 Uendelee kuwa munyenyekevu na uendelee kumutumainia Yehova. Wakati ulibatizwa, ulionyesha kama uko na imani yenye nguvu na ulimutumainia sana Yehova. Na Yehova alifurahi sana na akakupatia pendeleo la kuwa mu familia yake. Jambo lenye unapaswa kufanya sasa ni kuendelea kumutumainia Yehova. Inaweza kuonekana mwepesi kumutumainia Yehova wakati unapaswa kukamata maamuzi ya maana sana. Lakini utafanya nini wakati wa kukamata maamuzi ingine? Ni jambo la maana sana umutumainie Yehova wakati unakamata maamuzi, hata kama inahusu mambo ya kujifurahisha, kazi ya kimwili na miradi yenye unajiwekea. Usitegemee hekima yako mwenyewe. Kuliko kufanya vile, tafuta kanuni za Biblia zenye zinahusu hali yako na kisha utumikishe muongozo wenye umepata. (Mez. 3:5, 6) Kama unafanya vile, utamufurahisha Yehova na ndugu na dada mu kutaniko watakuheshimia.​—Soma 1 Timoteo 4:12.

Mali ya Kiroho

w17.03 uku. 19 fu. 7

Umutumikie Yehova kwa Moyo Mukamilifu!

7 Namna gani tunaweza kujua ikiwa tumejitoa kwa Yehova kwa moyo wetu wote? Tunaweza kujiuliza hivi: ‘Nitamutii Yehova hata wakati ni vigumu kufanya hivyo? Nimeazimia kabisa kufanya kutaniko lake liendelee kuwa safi?’ Asa alipaswa kuwa na ujasiri mwingi sana ili kutosha tate yake mwanamuke katika cheo chake cha malkia! Wakati fulani, unaweza kuwa na lazima ya kuwa na ujasiri kama Asa. Kwa mufano, utafanya nini ikiwa mutu fulani wa familia yako ao rafiki yako wa sana anafanya zambi, lakini hatubu, na anapaswa kutengwa na kutaniko? Utaazimia kukata urafiki na mutu huyo? Moyo wako utakuchochea kufanya nini?

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine