Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • th somo ya 2 uku. 5
  • Namna ya Kuzungumuza

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kuzungumuza
  • Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Uchangamufu
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Kuzungumuza kwa Usadikisho
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Kuzungumuza kwa Upole na kwa Upendo
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
  • Kujikaza Kugusa Moyo
    Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
Ona Habari Zaidi
Fanya Bidii Katika Kusoma na Kufundisha
th somo ya 2 uku. 5

SOMO YA 2

Namna ya Kuzungumuza

Andiko

2 Wakorinto 2:17

JAMBO LA KUFANYA: Sema kwa njia ya kawaida, na useme mambo yenye inatoka mu moyo mu njia yenye inaonyesha namna unajisikia kuhusu habari na kuhusu wasikilizaji wako.

NAMNA YA KUFANYA VILE:

  • Sali na ujitayarishe muzuri. Umuombe Yehova akusaidie usikaze akili juu yako mwenyewe, lakini juu ya habari yenye utazungumuzia. Uweke mu akili yako mambo makubwa yenye unapenda kuzungumuzia. Sema mawazo yako mu maneno yako mwenyewe; usirudilie-rudilie tu maneno vile inaandikwa mu kichapo.

    Shauri

    Kama utasoma andiko mu Biblia ao habari fulani mu kichapo, ujikaze kujua muzuri maneno ya ile andiko ao ile habari kusudi usikwame-kwame ao kusita-sita wakati utaisoma. Kama unasoma maneno yenye watu fulani walisemaka ao yenye waliandikaka, usome maneno yao kwa hisia, lakini isikuwe sawa vile uko unafanya teatre.

  • Sema mambo yenye inatoka mu moyo. Fikiria juu ya nini ile habari ni ya lazima kwa wasikilizaji wako. Uwafikirie sana. Ukifanya vile, namna yako ya kusimama ao kukaa, ishara zako za mwili na za uso, yote itaonyesha kama uko mwenye uchangamufu na mwenye urafiki.

    Shauri

    Kusema kwa njia ya kawaida haimaanishe kukosa adabu. Ufanye habari yako iheshimiwe kwa kutumia maneno yenye iko wazi na kuheshimia sarufi, maana yake kanuni za luga.

  • Angalia wasikilizaji wako. Angalia wasikilizaji wako kama haiko mubaya kufanya vile kwenye unaishi. Wakati unatoa hotuba, angalia musikilizaji mumoja, kisha angalia mwengine, kuliko kuangalia watu wote mara moja.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine