WIMBO 16
Tumusifu Yehova na Mwana Wake Mutiwa-Mafuta
Maandishi
1. Yehova alichagua
Yesu atutawale.
Atatutawala kwa haki,
Tutaishi kwa furaha.
(REFREE)
Tusifu Yehova na Yesu, mutiwa-mafuta wake,
Tufuate njia zake zote na kumutii sana.
Tusifu Yehova na Yesu, mutawala wa Ufalme,
Mwenye ataitukuza jina takatifu ya Mungu.
2. Mungu anawachagua
Ndugu za Yesu Kristo.
Watawale pamoja naye;
Na kuleta Paradiso.
(REFREE)
Tusifu Yehova na Yesu, mutiwa-mafuta wake,
Tufuate njia zake zote na kumutii sana.
Tusifu Yehova na Yesu, mutawala wa Ufalme,
Mwenye ataitukuza jina takatifu ya Mungu.
(Ona pia Mez. 29:4; Isa. 66:7, 8; Yoh. 10:4; Ufu. 5:9, 10.)