Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w20 Mwezi wa 9 uku. 31
  • Maulizo ya Wasomaji Wetu

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo ya Wasomaji Wetu
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • “Wenye Furaha Ni Wale Wenye Wanashika Uaminifu-Mushikamanifu” Kwa Yehova
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2022
  • Sababu Gani Tunapaswa Kuheshimu Mamlaka?
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2020
w20 Mwezi wa 9 uku. 31
Picha yenye kuonyesha utukufu wa Yehova kwenye kiti cha ufalme cha zumaridi. Mwangaza wenye kungaa unazunguka kile kiti cha ufalme.

Maulizo ya Wasomaji Wetu

Muhubiri 5:8 inazungumuzia watawala wanadamu tu, ao inamuhusu pia Yehova?

Ile andiko inasema hivi: “Kama unaona maskini wanakandamizwa kwa njia yoyote na haki inavunjwa na uadilifu havifuatwe katika wilaya yako, jambo hilo lisikushangaze. Kwa maana ofisa mukubwa iko anaangaliwa na ule mwenye kuwa juu zaidi kuliko yeye, na kuko wengine wenye wako tena juu yao.”​—Muh. 5:8.

Kwa maoni ya wanadamu, ile andiko inaweza kuonekana kama inahusu tu wanadamu wenye kuwa na mamlaka. Lakini, kama tunaifikiria zaidi, tutaona kama inazungumuzia jambo fulani juu ya Yehova. Na ile jambo inaweza kutufariji na kutupatia tumaini.

Muhubiri 5:8 inazungumuzia mutawala mwenye iko anatesa maskini na kuwatendea bila haki. Anapaswa kukumbuka kama kuko mutawala mwingine mwenye iko na mamlaka zaidi kuliko yeye, mwenye iko anaona mambo yote yenye iko anafanya. Na kunaweza kuwa watawala wengine wenye wako na mamlaka zaidi kuliko wale watawala wawili. Inahuzunisha kuona kama mu serikali za wanadamu, wale watawala wote, wanaweza kutendea wengine bila haki. Na ile inaweza kufanya wale wenye wako chini ya mamlaka yao wateseke.

Lakini tunajua kama Yehova iko anaona mambo yenye ‘maofisa wakubwa’ wa serikali za wanadamu wako wanafanya. Kwa hiyo, hata wakati wanatutendea bila haki na tunawaza kama hakuna tena tumaini, hatuache ile ituvunje moyo. Kuliko kufanya vile, tunasali kwa Yehova na kumuomba atusaidie. (Zb. 55:22; Flp. 4:6, 7) Tunajua kama “macho ya Yehova yanaenda huku na huku katika dunia yote ili kuonyesha nguvu zake kwa ajili ya wale wenye moyo wao ni kamili kumuelekea yeye.”​—2 Ny. 16:9.

Kwa kifupi, Muhubiri 5:8 inatukumbusha kama mu serikali za wanadamu, kunakuwaka mutu mwenye iko na mamlaka zaidi ya wengine. Na jambo la maana zaidi, ile andiko inatukumbusha kama Yehova njo iko na mamlaka ya juu zaidi. Na sasa iko anatawala mbinguni kupitia Mwana wake Yesu Kristo, Mufalme wa Ufalme wake. Yehova, Mungu Mweza-Yote, iko anaona mambo yote yenye iko inafanyika, na haiko sawa vile watawala wanadamu, yeye ni mwenye haki kabisa na Yesu Kristo Mwana wake ni mwenye haki pia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine