WIMBO 125
“Wenye Furaha Ni Wale Wenye Rehema!”
Maandishi
1. Mungu ni mwenye rehema,
Tena ni mwenye furaha.
Anatutimiziaka
Mahitaji yetu yote.
Tena tukitubu zambi,
Kweli atatusamehe.
Anakumbuka ya kama
Siye hatukamilike.
2. Kama tunafanya zambi,
Kweli tutubu kabisa.
Yesu alituambia
Tusali kwa baba yake;
Naye atatusamehe
Tukisamehe wengine.
Kama tunafanya vile
Tutakuwa na amani.
3. Tukisaidia watu
Wenye hawana uwezo,
Ikuwe kwa moyo wote,
Hapana kwa kujisifu.
Mungu iko anaona.
Yeye njo atatulipa.
Anafurahi kabisa
Tukionyesha rehema.
(Ona pia Mt. 6:2-4, 12-14.)