Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g 1/14 uku. 10-11
  • Namna ya Kushinda Vishawishi vya Vijana Wenzako

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Namna ya Kushinda Vishawishi vya Vijana Wenzako
  • Amuka!—2014
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TATIZO
  • Mkazo wa wenzako na pendeleo lako la kuhubiri
    Huduma Yetu ya Ufalme—2000
  • Nifanye Nini Kama Wenzangu Wananikaza Kufanya Jambo Fulani?
    Majibu ya Maulizo 10 Yenye Vijana Wanajiulizaka
Amuka!—2014
g 1/14 uku. 10-11
Kijana mwanaume anayepewa sigareti

MUSAADA KWA FAMILIA | VIJANA

Namna ya Kushinda Vishawishi vya Vijana Wenzako

TATIZO

Mwanafunzi wa sekondari anayeshindwa na vishawishi vya vijana wenzake

“Kwenye masomo ya musingi, sikukubaliwa na watoto wengine, na hilo liliniumiza moyoni. Kwa hiyo, nilipoanza masomo ya sekondari, nilibadilisha namna nilivyoonekana na namna nilivyoona mambo, na sikubadilika kwa njia nzuri. Nilihitaji sana marafiki na hilo likafanya nishindwe na vishawishi vya vijana wenzangu, ili tu wanipende.”​—Jennifer, aliye na miaka 16.a

Unapambana na vishawishi vya vijana wenzako? Ikiwa ndiyo, habari hii itakusaidia kuvishinda.

Unapojiacha ushindwe na vishawishi vya vijana wenzako, unakuwa kama roboti isiyo na akili kwa sababu unaacha watu wengine wakuongoze kama kipofu. Sababu gani uwaache wawe na uwezo huo juu yako?​—Waroma 6:16.

MAMBO UNAYOPASWA KUJUA

Vishawishi vya vijana wengine vinaweza kufanya watu wazuri wafanye mambo mabaya.

‘Mashirika mabaya yanaharibu tabia nzuri.’​—1 Wakorintho 15:33.

“Ni kama vile unajua kwamba jambo fulani ni mbaya, lakini unapopambana na vishawishi vya vijana wenzako, unafanya jambo hilo kwa sababu tu unataka kuwapendeza!”​—Dana.

Vishawishi havitokane tu na vijana wenzako.

‘Ninapotaka kufanya yaliyo sawa, yaliyo mabaya yapo pamoja na mimi.’​—Waroma 7:21.

“Vishawishi vingi vinatokana mara nyingi na mimi mwenyewe; kwa kweli, ni mimi ninatamani mambo ambayo vijana wenzangu wanazungumuzia na mambo hayo yanaonekana kuwa yenye kuvutia.”​—Diana.

Kushinda vishawishi vya vijana wenzako ni jambo unaloweza kujivunia.

‘Iweni na zamiri njema.’​—1 Petro 3:16.

“Wakati fulani, ilikuwa vigumu kwangu kushinda vishawishi vya vijana wenzangu, lakini sasa siogope tena kuwa tofauti na nina musimamo katika maamuzi yangu. Hakuna kitu kinachoshinda kulala usiku ukiwa na zamiri safi.”​—Carla.

MAMBO UNAYOWEZA KUFANYA

Unaposhawishiwa na vijana wenzako kufanya mambo mabaya, jaribu kufanya hivi:

Fikiria matokeo. Ujiulize, ‘Itakuwa namna gani ikiwa ninashindwa na vishawishi vya wenzangu na kisha nifanye jambo mbaya? Wazazi wangu watawaza nini juu yangu? Nitajiona kuwa mutu wa namna gani?’​—Kanuni ya Biblia: Wagalatia 6:7.

“Wazazi wangu wananiuliza maulizo kama vile, ‘Ikiwa unajiacha ushindwe na vishawishi vya vijana wenzako, ni jambo gani linaweza kukupata?’ Wananisaidia kuona namna kujiacha nishindwe na vishawishi hivyo kunaweza kuniletea matokeo mabaya wakati unaokuja.”​—Olivia.

Uwe hakika na mambo unayoamini. Ujiulize, ‘Sababu gani ninaamini kwamba kufanya hivi kuna matokeo mabaya, kwangu na kwa wengine?’​—Kanuni ya Biblia: Waebrania 5:14.

“Nilipokuwa mudogo, nilikuwa ninasema tu hapana ao kutoa jibu fupi, lakini sasa ninaweza kueleza vizuri sababu gani nitafanya ao sitafanya jambo fulani. Nina musimamo katika mambo ninayoamini kuhusu mema na mabaya. Ni mimi mwenyewe ninayetoa jibu​—si mutu mwengine anayejibia pa nafasi yangu.”​—Anita.

Fikiria sifa yako. Ujiulize, ‘Ninapenda kuwa mutu wa namna gani?’ Kisha fikiria vishawishi unavyopambana navyo na ujiulize, ‘Mutu wa namna hiyo anaweza kufanya nini katika hali hii?’​—Kanuni ya Biblia: 2 Wakorintho 13:5.

“Ninapendezwa na namna nilivyo, kwa hiyo sihangaikie mambo ambayo wengine wanawaza juu yangu. Na tena, watu wengi wanapenda kuwa na mutu kama mimi asiyejifanya namna haiko.”​—Alicia.

Fikiria wakati unaokuja. Ikiwa wewe ni mwanafunzi, ujue kuwa katika miaka michache ao hata miezi, hautakuwa na watu ambao unajaribu kufurahisha.

“Niliangalia picha niliyokamata na wanafunzi wengine kwenye masomo, na sikukumbuka hata majina ya wanafunzi fulani. Lakini nilipokuwa kwenye masomo pamoja nao, maoni yao yalikuwa ya maana sana kwangu kuliko kushikamana na mambo ninayoamini. Huo ulikuwa upumbavu kabisa!”​—Dawn, aliye sasa na miaka 22.

Ujitayarishe. Biblia inasema hivi: ‘Mujue jinsi munavyopaswa kumujibu kila mutu.’​—Wakolosai 4:6.

“Wazazi wangu wananisaidia mimi na dada yangu mudogo kufikiria hali zinazoweza kutokea, na kisha tunafanya mazoezi ili hali inayofanana na hizo ikitokea, tujue yale tunayoweza kufanya.”​—Christine.

a Majina fulani yamebadilishwa katika habari hii.

MAANDIKO YA MAANA

  • ‘Lolote lile analopanda mutu, atavuna hilo pia.’​—Wagalatia 6:7.

  • “Watu wakomavu, . . . nguvu zao za ufahamu zimezoezwa kutofautisha yaliyo sawa na yaliyo makosa pia.”​—Waebrania 5:14.

  • ‘Endeleeni kusibitisha ninyi wenyewe jinsi mulivyo.’​—2 Wakorintho 13:5.

Jessica

JESSICA

“Namna unavyofikiri juu yako mwenyewe inaweza kukusaidia sana kushinda vishawishi vya vijana wenzako. Ikiwa unajiamini, hauhangaikie mambo ambayo wengine wanafikiri juu yako, na hilo linakufanya ushinde kwa vyepesi vishawishi vya vijana wenzako.”

Kayley

KAYLEY

“Ikiwa unajizarau, unaweza kujikaza ukubaliwe na wengine ili tu ujisikie vizuri. Lakini ikiwa unajiamini, ni vyepesi sana kutambua vishawishi vya vijana wenzako na kuviepuka.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine