Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g16 na. 2 uku. 3-7
  • Biblia Ni Kitabu Kizuri Tu?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Biblia Ni Kitabu Kizuri Tu?
  • Amuka!—2016
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Biblia Iko na Kanuni za Mwenendo na Ujuzi wa Mambo ya Kiroho
  • Biblia Inaeleza Sababu Gani Watu Wanateseka na Wanakosa Kuelewana
  • Biblia Inaleta Tumaini
  • Mambo ya Muzuri na ya Mubaya: Biblia Ni Muongozo Wenye Kutumainika
    Munara wa Mulinzi Unatangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti ya Watu Wote)—2024
  • Mungu Anakuwaka? Faida 4 za Kujua Hivyo
    Amuka!—2015
  • Habari Njema Yenye Iko mu Biblia Inatoka Kabisa kwa Mungu?
    Habari Njema Yenye Inatoka kwa Mungu!
Amuka!—2016
g16 na. 2 uku. 3-7
Mwanaume mwenye kusoma Biblia

HABARI KUBWA

Biblia Ni Kitabu Kizuri Tu?

Kuandikwa kwa Biblia kulimalizika kumepita miaka karibu 2000. Tangu wakati huo, vitabu vingi vimetokea na kupita, lakini Biblia iko tu. Fikiria mambo yenye kufuata.

  • Biblia imeokoka mashambulizi mengi makali ya watu wenye nguvu. Kwa mufano, katika inchi fulani za “Kikristo” kati ya mwaka wa 1201 na 1500, kitabu kimoja kinasema kama “kuwa na Biblia na kuisoma katika luga ya kizalikio [luga ya watu wa kawaida] kuliendelea kuonekana kuwa uasi-imani na upinzani.” (An Introduction to the Medieval Bible) Watu wenye elimu ambao walitafsiri Biblia katika luga ya watu wa kawaida ao wenye walitia wengine moyo kujifunza Biblia, waliweka uzima wao katika hatari. Wengine waliuawa.

  • Hata kama Biblia ilipata maadui wengi, ilikuwa na inaendelea kuwa kitabu chenye kugawanywa sana katika dunia yote. Inasemekana kuwa Biblia miliare tano, ikuwe yote nzima ao sehemu, zimechapishwa katika luga zaidi ya 2800. Hilo ni tofauti sana na vitabu vingine vya filozofia, sayansi, na vya mambo mengine, vyenye pengine havigawanywe sana na vyenye vinaweza kupoteza maana haraka.

  • Biblia imesaidia kulinda luga fulani ambamo imetafsiriwa na pia imesaidia kufanya luga hizo ziendelee zaidi. Tafsiri moja ya Kijerumani ya Martin Luther ilisaidia sana luga hiyo. Biblia ya kwanza ya King James Version imeonyeshwa kuwa, “pengine kitabu cha pekee chenye kilifanya kazi sana kuliko tafsiri zingine” katika luga ya Kiingereza.

  • Kitabu kimoja kinasema kama, Biblia imeleta “mabadiliko makubwa katika desturi na namna ya kuishi ya watu wa inchi za Ulaya na za Amerika ya kaskazini, haikubadilisha tu mambo yenye wanaamini na desturi zao, lakini ilibadilisha pia ufundi wao katika mambo mbalimbali, sheria, siasa, namna yao ya kuandika luga, na mambo mengine mengi sana yenye hatutaweza kutaja.” (The Oxford Encyclopedia of the Books of the Bible)

Hayo ni mambo fulani tu kati ya mambo yenye kufanya Biblia ikuwe tofauti. Lakini, sababu gani inajulikana sana? Sababu gani watu wametia maisha yao katika hatari juu ya Biblia? Kuko sababu nyingi, lakini sababu moja ni hii: Biblia iko na mafundisho yenye hekima juu ya mwenendo na namna ya kufanya urafiki wa sana pamoja na Mungu. Biblia inatusaidia kujua sababu gani watu wanateseka na wanakosa kuelewana. Jambo la muzuri zaidi ni kwamba, Biblia inaahidi kama magumu hayo yatamalizika, na inaonyesha hata namna jambo hilo litafanyika.

MAELEZO MAFUPI

Biblia yenye kufunguliwa

Biblia inafanyizwa na vitabu 66; vitabu hivyo vitakatifu viliandikwa katika kipindi cha miaka 1600 hivi.

Biblia iliandikwa na waandikaji ao waandishi 40 hivi, wamoja kati yao walikuwa walimaji, wavuaji wa samaki, waamuzi, wafalme, na wapiga muziki.

Habari kubwa ya Biblia ni Ufalme wa Mungu, ni kusema, serikali ya mbinguni yenye itatawala dunia. (Danieli 2:44; 7:13, 14) Ufalme huo utamaliza ubaya, mateso, na kifo kwa kufanya watu waishi katika umoja chini ya uongozi wa Muumbaji mwenye Mamlaka Makubwa Zaidi, ni kusema, Yehova Mungu.—1 Wakorintho 15:24-26.

Biblia Iko na Kanuni za Mwenendo na Ujuzi wa Mambo ya Kiroho

Masomo ya ulimwengu ni ya maana, lakini gazeti moja katika inchi ya Kanada linasema hivi: “Hata kama ulisoma sana, hilo halimaanishe kuwa unaweza kukamata maamuzi ya muzuri juu ya mwenendo.” (Ottawa Citizen) Watu wengi wenye kusoma sana, kama vile viongozi katika biashara na serikali, wanasema uongo, wanatumia njia za udanganyifu, na kuiba. Na kulingana na uchunguzi wenye ulichapishwa na Edelman, shirika la uhusiano kati ya watu, hilo linafanya watu “wasiwaaminie kabisa.”

Biblia inakazia sana mwenendo na ujuzi wa mambo ya kiroho. Inatusaidia kuelewa “uadilifu [haki] na hukumu na unyoofu, njia yote ya yaliyo mema.” (Methali 2:9) Kwa mufano, mwanaume mumoja wa miaka 23 mwenye tunaweza kuita Stephen, alikuwa katika gereza moja la inchi ya Polandi. Wakati alikuwa katika gereza, alianza kujifunza Biblia na alipendezwa na mashauri ya Biblia. Aliandika hivi: “Sasa ninaelewa maana ya kanuni ya ‘kuheshimu baba na mama.’ Nimejifunza pia kuzuia mawazo yangu ya moyoni, zaidi sana tabia yangu ya kukasirika sana.”—Waefeso 4:31; 6:2.

Kanuni moja yenye iligusa sana moyo wa Stephen ni ile yenye kupatikana katika andiko la Methali 19:11: ‘Ufahamu wa mutu hakika unapunguza hasira yake, na ni jambo lenye kupendeza anapopita kosa.’ Leo, wakati Stephen anapatwa na hali ngumu, anajaribu kuichunguza kwa upole na kutumikisha kanuni za Biblia zenye zinaweza kumusaidia katika hali hiyo. Alisema hivi: “Nilifikia kuona kama Biblia ni kitabu chenye kuwa na muongozo muzuri sana.”

Maria, ambaye ni Shahidi wa Yehova, alitukanwa mbele ya watu wengi na mwanamuke mumoja mwenye mawazo ya mubaya juu ya Mashahidi, na mwanamuke huyo alifanya fujo nyingi. Lakini, Maria alienda zake kwa upole kuliko kumutukana pia. Mwanamuke mwenye alimutukana alijisikia mubaya juu ya namna alitenda na alitafuta Mashahidi wa Yehova. Kisha mwezi moja hivi, wakati alionana tena na Maria, alimukumbatia na kumuomba musamaha. Zaidi ya hiyo, mwanamuke huyo alitambua kama upole wa Maria na namna alijizuia vilionyesha mambo yenye aliamini. Hilo lilikuwa na matokeo gani? Mwanamuke huyo mwenye alikuwa na mawazo ya mubaya juu ya Mashahidi wa Yehova na watu wengine tano wa familia yake waliamua kujifunza Biblia pamoja na Mashahidi wa Yehova.

Yesu alisema kama hekima inaonekana kupitia matendo. (Mathayo 11:19) Kuko mambo mengi yenye kuonyesha kama kanuni za Biblia zinaleta matokeo ya muzuri! Kanuni hizo zinatufanya tukuwe watu wazuri zaidi. Tena, ‘zinamufanya asiye na uzoefu akuwe na hekima,’ na ‘zinafanya moyo ushangilie,’ na ‘zinafanya macho yangae’ kwa sababu ya mafundisho ya kweli ya kiroho na ya mwenendo.—Zaburi 19:7, 8.

Biblia Inaeleza Sababu Gani Watu Wanateseka na Wanakosa Kuelewana

Wakati wachunguzi wanajifunza juu ya ugonjwa fulani wenye kuambukiza, wanajaribu kujua sababu yenye ilitokeza ugonjwa huo. Ni vile pia juu ya kujua sababu yenye kufanya watu wateseke na wakose kuelewana. Jambo lingine ni kwamba, Biblia inasaidia sana kwa sababu iko na historia yetu ya tangu zamani, wakati matatizo yetu yalianza.

Kitabu cha Mwanzo kinaonyesha namna mateso ya wanadamu yalianza wakati wanadamu wa kwanza walimuasi Mungu. Walijiwekea wao wenyewe kanuni juu ya mambo ya muzuri na ya mubaya; Mungu tu ndiye alikuwa na haki ya kufanya hivyo. (Mwanzo 3:1-7) Jambo la kuhuzunisha ni kwamba watu wengi wamejipatia haki hiyo ya kujiamulia. Hilo lilikuwa na matokeo gani? Kuliko kujaa mambo yenye kuleta uhuru na furaha, historia ya watu inajaa vita, kuoneana, na kukosa kupatana katika mambo ya Mungu na ya mwenendo. (Mhubiri 8:9) Ndiyo maana Biblia inasema hivi: “Mwanadamu . . . hana uwezo wa kuongoza hatua yake.” (Yeremia 10:23) Habari njema ni hii: uasi wa mwanadamu uko karibu kuisha.

Biblia Inaleta Tumaini

Biblia inatuhakikishia kama Mungu hataachilia ubaya na mateso viendelee, kwa sababu anapenda watu wenye kuheshimu mamlaka yake na kufuata kanuni zake. Watu wabaya “watakula matunda ya njia yao.” (Methali 1:30, 31) Lakini, “wapole wataimiliki dunia, nao watapata furaha yao tele katika wingi wa amani.”—Zaburi 37:11.

Biblia yenye kufunguliwa pembeni ya kopo kahawa

“Mapenzi yake [Mungu] ni kwamba watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.”—1 Timotheo 2:3, 4

Kupitia “Ufalme wa Mungu,” Mungu atatimiza ahadi yake ya kufanya dunia ikuwe na amani. (Luka 4:43) Ufalme huo ni serikali yenye itatawala dunia yote, na kupitia serikali hiyo Mungu ataonyesha haki yake ya kutawala wanadamu wote. Yesu alionyesha kama kuko uhusiano kati ya Ufalme na dunia. Alisema hivi katika sala yake ya mufano: “Ufalme wako na uje. Mapenzi yako na yatendeke duniani.”—Mathayo 6:10.

Kwa kweli, watu wenye watatawaliwa na Ufalme wa Mungu watafanya mapenzi yake kwa kukubali kama yeye ndiye Muumbaji mwenye haki ya kuwa Mutawala, haiko mwanadamu. Rushwa (kata-midomo, hongo), tamaa ya mubaya, matatizo ya feza, ubaguzi wa rangi ya ngozi na vita vitaisha. Kutakuwa dunia moja, serikali moja, na kanuni zilezile za kiroho na za mwenendo.—Ufunuo 11:15.

Siri ya kuingia katika dunia hiyo mupya ni kupata ujuzi. Andiko la 1 Timotheo 2:3, 4 linasema hivi: “Mapenzi yake [Mungu] ni kwamba watu wa namna zote waokolewe na kupata ujuzi sahihi wa kweli.” Kweli hiyo inamaanisha pia mafundisho ya Biblia juu ya kile tunaweza kuita katiba ya Ufalme, ni kusema, sheria na kanuni zenye kuongoza Ufalme huo. Mifano fulani ya sheria na kanuni hizo inaweza kupatikana katika Mahubiri ya Yesu Kristo ya Mulimani. (Mathayo, sura ya 5 mupaka sura ya 7) Wakati unasoma sura hizo tatu, jaribu kuona katika akili yako namna maisha yatakuwa wakati kila mutu atafuata hekima ya Yesu.

Ni jambo la kushangaza kuona kama Biblia ni kitabu chenye kugawanywa sana katika dunia yote? Hapana kabisa! Mafundisho ya Biblia yanahakikisha kama Biblia iliongozwa na roho ya Mungu. Na namna Biblia inagawanywa inaonyesha kama Mungu anapenda watu wa luga zote na mataifa yote wajifunze juu yake na wapate baraka zenye Ufalme wake utaleta.—Matendo 10:34, 35.

Mbingu zenye nyota

Biblia inasema kama mbingu zinaongozwa na sheria

KITABU CHENYE KUFUNUA KWELI KUHUSU MAMBO YA KUWAZIA YA UCHAWI

Kitabu kimoja kinasema kama, “watu wa zamani walikuwa wanaamini kuwa ulimwengu ulikuwa unaongozwa na miungu.” (Encyclopedia of Science and Religion) Lakini, Biblia inasema kama ulimwengu unaongozwa na sheria za asili. Kwa mufano, kumepita miaka 3500 hivi tangu Biblia ilizungumuzia “sheria za mbingu [na] dunia.” (Ayubu 38:33) Katika andiko la Yeremia 31:35, inazungumuzia “sheria za mwezi na nyota.” Watu wenye waliitika kweli juu ya jambo hilo waliepuka ibada ya uongo na mambo ya kuwazia ya uchawi.—Ayubu 31:26-28; Isaya 47:1, 13.

KITABU CHENYE KUSEMA KWELI

Jambo la kuvutia sana juu ya waandikaji wa Biblia ni kwamba waliandika mambo ya kweli, hata makosa yao. Kwa mufano, kisha Mufalme Daudi kufanya uasherati na mwanamuke mwenye kuitwa Bath-sheba, alisema waziwazi hivi: “Nami nimefanya lililo baya machoni pako [Mungu].” (Zaburi 51:4) Mutume Yohana alisema waziwazi kuwa alianguka chini mara mbili ili kuabudu malaika. Malaika alimuambia hivi: ‘Ukuwe muangalifu! Usifanye hivyo! . . . Umuabudu Mungu!’ (Ufunuo 19:10; 22:8, 9) Jambo la kuhuzunisha ni hili: waandikaji wa zamani hawakuonyesha makosa yao, lakini waandikaji wa Biblia walifanya vile.

KITABU CHENYE KUSAIDIA WATU KUWA NA AFYA YA MUZURI YA AKILI

Biblia inatutia moyo tukuwe na sifa zenye kusaidia kuwa na afya ya muzuri ya akili, sifa kama vile huruma na kusamehe. Andiko la Waefeso 4:32 linasema hivi: ‘Mukuwe wenye fazili ninyi kwa ninyi, wenye huruma nyororo, mukisameheana kwa hiari [kwa kupenda].’

Kichapo fulani cha hospitali ya Mayo katika inchi ya Amerika, kinasema hivi: “Kama hauzoee kusamehe wengine, utajiumiza wewe mwenyewe.” Kichapo hicho kinaeleza kama kusamehe kunaweza kusaidia mutu akuwe na “urafiki muzuri zaidi pamoja na wengine; hali ya muzuri zaidi ya kiroho na ya kiakili; kupunguza mahangaiko na chuki; kufanya damu isitembee haraka sana katika mwili; alama kidogo za kushuka moyo; na hatari kidogo sana za kutumia dawa za kulewesha na kunywa pombe sana.”

KITABU CHENYE KUJIBU MAULIZO YA MAANA JUU YA MAISHA

Kiini-tete cha mwanadamu

Kiini-tete cha mwanadamu

Sayansi iko na majibu ya maulizo ya namna zote. Lakini, hata kama sayansi inaweza kutufasiria mambo mengi, iko na mipaka. Kitabu kimoja kinasema hivi: “Wanasayansi wengi, wanganga, na wanafilozofia wanakubali kama sayansi haiwezi kujibu maulizo juu ya dini na juu ya mwenendo muzuri.” (Biotechnology—Changing Life Through Science)

  • SAYANSI INAWEZA kutupatia maagizo ya hesabu juu ya sheria zenye kuongoza ulimwengu, lakini haiwezi kutuambia sababu gani ulimwengu uko ao sababu gani unaongozwa na sheria zenye kupangwa muzuri.

  • SAYANSI INAWEZA kufasiria namna viungo vya uzazi vinafanya kazi, lakini haiwezi kuleta kanuni zenye zinaweza kukusaidia kukamata maamuzi ya muzuri juu ya ngono.

  • SAYANSI INAWEZA kufasiria namna kiini-tete cha mwanadamu kinakomaa, lakini haiwezi kukusaidia ukamate maamuzi ya muzuri kuhusu kutoa mimba.

Biblia inajibia maulizo hayo na maulizo mengine ya maana. Kwa hiyo, inatusaidia ‘kuelewa uadilifu [haki] na hukumu na unyoofu, njia yote ya yaliyo mema.’ —Methali 2:9.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine