Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g17 na. 6 uku. 3
  • Dunia hii Itaokoka ao Hapana?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Dunia hii Itaokoka ao Hapana?
  • Amuka!—2017
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Wanasayansi Wanasogeza Mukuki wa Saa ya Mwisho wa Dunia​—Biblia Inasema Nini?
    Habari Zingine
  • Mwisho wa Hii Dunia Uko Karibu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
    Huduma Yetu ya Ufalme—2012
  • Biblia Inasema Nini?
    Amuka!—2017
Amuka!—2017
g17 na. 6 uku. 3
Saa ya Mwisho wa Dunia

HABARI KUBWA | DUNIA HII ITAOKOKA AO HAPANA?

Dunia Hii Itaokoka Ao Hapana?

MWAKA wa 2017 ulianza na tangazo la mubaya la wanasayansi. Katika Mwezi wa 1, kikundi kimoja cha wanasayansi kilitangaza kwamba dunia inakaribia sana musiba mubaya zaidi wenye haujatokeaka. Kwa kutumia Saa ya Mwisho wa Dunia ili kuonyesha namna dunia inakaribia mwisho, wanasayansi walipeleka mbele, kwa segonde 30, mukuki wa kuonyesha dakika. Kwa sasa, Saa ya Mwisho wa Dunia iko kwenye saa 6 ya usiku kosa dakika mbili na nusu (23:57:30), ni kusema, karibu zaidi na musiba wa ulimwengu muzima kuliko wakati wowote katika kipindi cha miaka 60!

Katika mwaka wa 2018, wanasayansi wanapanga kupima tena kadiri gani tuko karibu na mwisho wa dunia. Saa ya Mwisho wa Dunia itaendelea kuonyesha kwamba musiba mukubwa kuliko yote unakaribia sana? Unawaza namna gani? Dunia hii itaokoka? Pengine unaona kwamba iko nguvu kupata majibu ya maulizo haya. Hata wanasayansi wako na mawazo tofauti kuhusu jambo hilo. Haiko kila mutu ndiye anaamini hatari hiyo yenye haiwezi kuepukwa.

Kwa kweli, mamilioni ya watu wanatumainia wakati muzuri wenye kuja. Wanaamini kwamba wako na mambo yenye kuhakikisha kwamba wanadamu na dunia wataokoka milele na maisha yetu yatakuwa muzuri. Unaweza kuamini mambo hayo? Dunia hii itaokoka ao hapana?

“Saa ya Mwisho wa Dunia ni saa ya mufano yenye kukubaliwa katika dunia yote yenye inaonyesha namna ulimwengu wetu unakaribia kuharibiwa kupitia teknolojia hatari zenye sisi wenyewe tunafanya. Hatari ya kwanza na kubwa kati ya teknolojia hizo ni silaha za kinyuklia, lakini hatari hizo zinatia ndani teknolojia zenye kutokeza kubadilika kwa hali ya hewa, kuongezeka kwa bioteknolojia, na teknolojia ya Internete yenye inaweza kutokeza hatari kubwa sana katika namna yetu ya kuishi na kwa dunia, ikuwe kimakusudi, kwa kukosea, ao kwa aksidenti.”​—Bulletin of the Atomic Scientists.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine