Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 9
“Watu wengi wanaamini kwamba siku moja Mungu atawahukumu kulingana na matendo yao. Wewe unawaza tunapaswa kuogopa siku hiyo ya hukumu ao kuingojea kwa furaha? [Acha mutu ajibu.] Ona wazo lililo katika gazeti hili.” Umupokeze musikilizaji Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 9, na muzungumuzie pamoja habari iliyo chini ya kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16 na kusoma hata andiko moja. Umuachie gazeti hilo, na upange kumurudilia ili kuzungumuzia ulizo linalofuata.
Munara wa Mulinzi 1/09/12
“Katika sehemu nyingi za dunia, wanawake wanabaguliwa na kutendewa vibaya. Inasikitisha kwamba mafundisho fulani ya dini yamewachochea watu kutenda hivyo. Wewe unawaza Mungu anawahangaikia kabisa wanawake? [Acha mutu ajibu.] Ona namna Biblia inavyomushauri bwana amutendee bibi yake. [Soma Waefeso 5:28, 29.] Gazeti hili linaonyesha maoni ya Biblia kuhusu jinsi Mungu anavyowaona wanawake.”
Amkeni! Mwezi wa 9
“Watu wengi wanasema kama siku fulani maisha yatakwisha duniani, labda kupitia vita ya mabombe ya nyukilia ao musiba wa asili, kama vile dunia kugongana na nyota inayoitwa asteroide ao mabadiliko makubwa ya hali ya hewa. Wewe unawaza kama mawazo hayo ni ya kweli ao ni ndoto tu? [Acha mutu ajibu.] Biblia inatutolea ahadi hii yenye kufariji. [Soma Zaburi 37:29.] Gazeti hili linazungumuzia mambo ambayo watu wengi wanawazia kuhusu mwisho wa dunia yetu, lakini inatoa pia maoni ya Biblia yenye kufaa kuhusu wakati ujao.”