Namna Mbalimbali za Kuanzisha Mazungumuzo
Namna ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza ya Mwezi wa 9
“Watu wengi wanaamini kwamba kuna Malaika. Wewe pia unaamini hivyo? [Acha mutu ajibu.] Malaika wana nguvu sana kwa sababu wao ni viumbe wa roho, lakini, unawaza wanaweza kutusaidia? Biblia inatuelezea namna Malaika wanasaidia wanadamu leo.” Umuonyeshe ukurasa wa mwisho wa Munara wa Mulinzi wa tarehe 1 Mwezi wa 9, muzungumuzie habari ya chini ya ulizo la kwanza na musome hata andiko moja. Umutolee magazeti, na upange kumurudilia ili muzungumuzie ulizo linalofuata.
MUNARA WA MULINZI 01/09
“Unafikiri wanadamu wanaharibu sana dunia hivi kwamba haiwezi tena kutengenezwa? [Acha mutu ajibu.] Mwanadamu hana uwezo wa kutengeneza mambo ambayo ameharibisha, lakini, Biblia inatuambia kwamba Mungu iko na uwezo huo na anatamani kufanya hivyo. Andiko la Zaburi 65:9 linatuhakikishia jambo hilo. [Soma.] Gazeti hili la Munara wa Mulinzi linafasiria namna Yehova atatengeneza dunia na namna tunaweza kufurahia baraka hizo za wakati ujao. Unapenda nikuachie gazeti hili ulisome?”
Amuka! Mwezi wa 9
“Watu wengi wanaona kwamba wanalazimika kutumika sana na wanawaza kwamba hakuna namna ya kuepuka jambo hilo. Waganga wanasema kwamba kutumika kupita kiasi kunaweza kuchokesha sana mwili na akili, na jambo hilo linaweza kuwa na matokeo mabaya juu ya afya ya mutu. Unafikiri ni jambo gani linaweza kusaidia mutu akuwe na kiasi katika maisha? [Acha mutu ajibu.] Ona andiko ambalo linaweza kutusaidia. [Soma Mhubiri 4:6.] Gazeti hili linaeleza njia ine ambazo zinaweza kutusaidia kufuatilia mambo ya lazima na kupambana na muchoko mwingi wa kazi.”