Utoaji Mbalimbali
Jinsi ya Kuanzisha Mafunzo ya Biblia Siku ya Posho ya Kwanza Katika Mwezi wa 8
“Watu wanapatikana katika dini mbalimbali na wanaabudu Mungu kwa njia tofauti-tofauti. Unafikiri Mungu anaona jambo hilo namna gani? [Acha mutu ajibu.] Ona yale ambayo Yesu alifundisha kuhusu habari hii.” Tolea msikilizaji Mnara wa Mlinzi wa tarehe 1 mwezi wa 8 na muchunguze pamoja habari iliyo kwenye kichwa kidogo cha kwanza kwenye ukurasa wa 16 na musome andiko moja hivi kati ya maandiko yanayotajwa. Tolea mutu magazeti, na ufanye mipango ya kurudia ili kuendelea na ulizo linalofuata.
Mnara wa Mlinzi 01/08/11
“Je, unafikiri kwamba watoto wanapaswa wafundishwe mambo yanayomhusu Mungu wakati wangali bado wachanga, ao ni vizuri kungojea watakapokomaa ili wajichagulie dini wanayopenda? [Acha mutu ajibu.] Ona jambo ambalo Biblia inaagiza baba wafanye. [Soma Waefeso 6:4.] Gazeti hili linatoa mapendekezo fulani kuhusu jinsi wazazi wanavyoweza kufundisha watoto wao kumhusu Mungu.”
Amkeni! Mwezi wa 8
“Ninapenda kujua maoni yako kuhusu andiko hili. [Soma 1 Samweli 16:23.] Kulingana na andiko hili, muziki una nguvu. Je, unafikiri kwamba nyimbo zingine zinaweza kuchochea watu wafanye mabaya? [Acha mutu ajibu.] Gazeti hili linazungumzia jinsi tunaweza kuchagua kwa hekima muziki na jinsi tunaweza kusaidia watoto kufanya hivyo pia.”