Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g20 na. 1 uku. 4
  • Ni Mambo Gani Yenye Inaleta Mukazo?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ni Mambo Gani Yenye Inaleta Mukazo?
  • Amuka!—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Mukazo Ni Nini?
    Amuka!—2020
  • Uko na Mukazo?
    Amuka!—2020
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2020
  • Namna ya Kupambana na Mukazo
    Amuka!—2020
Amuka!—2020
g20 na. 1 uku. 4

KITULIZO KWA WALE WENYE KUWA NA MUKAZO

Ni Mambo Gani Yenye Inaleta Mukazo?

Kituo kimoja chenye kujulikana sana chenye kuitwa Mayo Clinic kinasema hivi: “Watu wazima wengi wanasema kama wako na mukazo wenye kuendelea kuongezeka. Maisha katika ulimwengu wa leo, ni yenye kujaa mabadiliko na wasiwasi kuhusu wakati wenye kuja.” Mambo yenye kufuata ni kati ya mambo yenye kufanya watu wakuwe na mukazo:

  • ndoa kuvunjika

  • kifo cha mupendwa

  • ugonjwa mukali

  • aksidenti kali

  • uvunjaji wa sheria

  • kuwa na mambo mingi sana ya kufanya mu maisha

  • misiba ya asili ao yenye kuletwa na watu

  • mikazo kwenye masomo ao kwenye kazi

  • wasiwasi kuhusu kupata na kuchunga kazi yenye itakusaidia kupata feza za kutosha ili kuhangaikia familia

“KUPOTEZA KAZI”

Shirika la Saikolojia la Amerika linasema kama “kupoteza kazi kunaweza kuleta matokeo ya mubaya sana, kama vile kufanya watu wenye wamepoteza kazi wakuwe mu hatari ya kupata magonjwa, matatizo katika ndoa, mahangaiko, kushuka moyo, na hata kujiua. Kupoteza kazi kunagusa kila sehemu ya maisha.”

KUWA NA MUKAZO WAKATI MUTU ANGALI MUTOTO

Ni kawaida kwa watoto kuwa na mukazo. Watoto fulani wanachokozwa kwenye masomo ao wanakosa kuhangaikiwa nyumbani. Wengine wanatendewa mubaya kimwili, kiakili, ao kingono. Watoto wengi wako na mahangaiko kwa sababu ya mashindano na alama zenye wanapata kwenye masomo. Na wengine wanaona namna wazazi wao wanavunja ndoa. Watoto wenye kuwa na mukazo wanaweza kuota ndoto zenye kuogopesha, kuwa na matatizo ya kujifunza, kushuka moyo, ao kuwa na muelekeo wa kujitenga na watu wengine. Watoto fulani wanaonekana kama hawawezi kuzuia hisia zao. Mutoto mwenye kuwa na mukazo anapaswa kusaidiwa bila kukawia.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine