Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • g20 na. 1 uku. 14-15
  • Inawezekana Kuwa na Maisha Yenye Haina Mukazo

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Inawezekana Kuwa na Maisha Yenye Haina Mukazo
  • Amuka!—2020
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Habari Zenye Kuwa Ndani
    Amuka!—2020
  • Chini ya Ufalme wa Mungu “Amani Itakuwa Nyingi”
    Amuka!—2019
  • Namna ya Kupambana na Mukazo
    Amuka!—2020
  • Ufalme wa Mungu—Sababu Gani Yesu Anauona Kuwa wa Maana?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
Ona Habari Zaidi
Amuka!—2020
g20 na. 1 uku. 14-15
Mutoto mumoja mwanume na baba yake wanacheza katika zoruba ya bahari na mama na watoto wanamuke wako wanawaangalia na wako pembeni ya bahari.

KITULIZO KWA WALE WENYE KUWA NA MUKAZO

Inawezekana Kuwa na Maisha Yenye Haina Mukazo

Hekima yenye kuwa katika Biblia inaweza kutusaidia kuepuka mukazo wenye hauna maana. Sisi wenyewe hatuwezi kumaliza mambo yote yenye kutuletea mukazo. Lakini Muumbaji wetu anaweza. Amechagua hata mutu fulani ili atusaidie. Ule mutu ni Yesu Kristo. Hivi karibuni, atafanya mambo ya muzuri katika dunia yote, kupita mambo yenye alifanya wakati alikuwa ku dunia. Kwa mufano:

YESU ATAPONYESHA WAGONJWA KAMA VILE ALIFANYA WAKATI ALIKUWA KU DUNIA.

“Wakamuletea watu wote wenye walikuwa wanateswa na magonjwa . . . mbalimbali . . . , na akawaponyesha.”​—MATAYO 4:24.

YESU ATAFANYA WATU WOTE WAPATE CHAKULA NA NYUMBA.

“Watajenga [watu wenye watatawaliwa na Kristo] nyumba na kuishi ndani, na watapanda mashamba ya mizabibu na kula matunda yake. Hawatajenga ili mutu mwingine akae ndani, wala hawatapanda ili wengine wakule.”​—ISAYA 65:21, 22.

UTAWALA WA YESU UTALETA AMANI NA USALAMA KATIKA DUNIA YOTE.

“Katika siku zake mwenye haki atasitawi, na amani itakuwa nyingi mupaka wakati mwezi utakuwa hauko tena. Atakuwa na raia kutoka bahari mupaka bahari na kutoka ule Muto mupaka kwenye miisho ya dunia. . . . Maadui wake watalambula mavumbi.”​—ZABURI 72:7-9.

YESU ATAMALIZA UKOSEFU WA HAKI.

“Atamusikilia huruma mutu wa hali ya chini na maskini, na ataokoa uzima wa maskini. Atawaokoa katika ukandamizaji na katika jeuri.”​—ZABURI 72:13, 14.

YESU ATAMALIZA HATA MATESO NA KIFO.

“Kifo hakitakuwa tena, wala maombolezo wala kilio wala maumivu havitakuwa tena.”​—UFUNUO 21:4.

“NYAKATI ZA HATARI”

Muandikaji musimamizi wa shirika la Gallup, Mohamed S. Younis anasema hivi: “Leo watu wengi wako na mukazo sana, wasiwasi, huzuni na maumivu kuliko zamani.”

Juu ya nini mukazo umekuwa jambo la kawaida? Biblia inatoa jibu lenye kufaa kabisa. Inasema hivi kwenye 2 Timoteo 3:1: ‘Katika siku za mwisho kutakuwa nyakati za hatari za mukazo mukubwa na muvurugo.’ (The Amplified Bible) Kisha Biblia inatoa sababu yenye inafanya mukazo uenee sana kwa kueleza tabia za mubaya za watu. Tabia hizo zinatia ndani pupa, kujivuna, unafiki wa kidini, jeuri, kukosa upendo wa asili, na kukosa kujizuia. (2 Timoteo 3:2-5) Siku za mwisho zitamalizika wakati Yesu Kristo ataongoza dunia yote akiwa Mufalme wa Ufalme wa Mungu, wenye ni serikali ya mbinguni.​—Danieli 2:44.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine