SOMO YA 36
Ukuwe Munyoofu mu Mambo Yote
Kila mutu anapendaka akuwe na marafiki wanyoofu, ni kusema waaminifu. Yehova naye, anapendaka marafiki wake wakuwe wanyoofu. Lakini ile haiko mwepesi juu watu wengi leo ni wadanganyifu. Kuwa munyoofu mu mambo yote kuko na faida gani?
1. Juu ya nini tunapaswa kujikaza sana kuwa wanyoofu?
Wakati tunajikaza kuwa wanyoofu, tunaonyesha kama tunamupenda Yehova na tunamuheshimia. Tusisahau kama Yehova anajua mambo yote yenye tunawazaka na kufanya. (Waebrania 4:13) Anaona wakati tunaepuka udanganyifu, na ile inamufurahishaka. Neno yake Biblia inasema hivi: “Yehova anachukia mutu mudanganyifu, lakini anafanya urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu.”—Mezali 3:32.
2. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wanyoofu?
Yehova anapenda ‘tukuwe tunasema kweli mumoja na mwingine.’ (Zekaria 8:16, 17) Maana yake nini? Wakati tuko nazungumuza na watu wa familia yetu, wafanyakazi wenzetu, ndugu na dada zetu, ao wakubwa wa serikali hatupaswe kusema uongo ao kuwapatia habari zenye haziko za kweli. Kama tuko wanyoofu, hatutaiba ao kutenda kwa udanganyifu. (Soma Mezali 24:28 na Waefeso 4:28.) Tutalipa kodi (taxes) zote zenye tunaombwa. (Waroma 13:5-7) Kwa kufanya vile, ‘tunajiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.’—Waebrania 13:18.
3. Tutapata faida gani kama tuko wanyoofu?
Wengine watatutumainia kama wanajua kuwa tuko watu wanyoofu. Tena, tutasaidia kila mutu mu kutaniko ajisikie salama sawa vile mu familia yenye watu wanapendana. Tutakuwa na zamiri safi. Zaidi ya ile, kama tuko wanyoofu, ‘tutapamba mafundisho ya Mwokozi wetu, Mungu,’ na tutafanya wengine wapende kumutumikia Yehova.—Tito 2:10.
TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
Tuone namna kuwa munyoofu kunaweza kumufurahisha Yehova na kukuletea faida, na namna unaweza kuwa munyoofu mu mambo mbalimbali.
4. Yehova anafurahi wakati tuko wanyoofu
Musome Zaburi 44:21 na Malaki 3:16, na kisha muzungumuzie hii maulizo:
Juu ya nini ni kukosa hekima kuwaza kama tunaweza kuficha kweli?
Unawaza Yehova anajisikiaka namna gani wakati tunasema kweli, hata wakati ni nguvu kufanya vile?
Wakati watoto wanasema kweli, wazazi wanafurahiaka. Na siye wakati tunasema kweli, Yehova anafurahiaka
5. Utende kwa unyoofu kila wakati
Watu wengi wanaamini kama haiwezekane kuwa munyoofu kila wakati. Lakini, ona juu ya nini tunapaswa kuwa wanyoofu kila wakati. Muangalie VIDEO.
Musome Waebrania 13:18, na kisha muzungumuzie namna tunaweza kuwa wanyoofu . . .
mu familia.
ku kazi ao ku masomo.
mu hali zingine.
6. Tutapata faida kama tuko wanyoofu
Wakati fulani, kuwa wanyoofu kunaweza kutuletea magumu. Hata vile, inakuwaka tu muzuri kuwa wanyoofu. Musome Zaburi 34:12-16, na kisha muzungumuzie hii ulizo:
Namna gani kuwa munyoofu kumefanya maisha yako ikuwe muzuri zaidi?
Bibi na bwana wanyoofu wanafanya ndoa yao ikuwe nguvu
Wakubwa wa kazi wanatumainiaka wafanyakazi wanyoofu
Wakubwa wa serikali wanakuwaka wanasifu watu wanyoofu
WATU FULANI WANASEMAKA: “Kusema uongo kidogo haiko mubaya.”
Juu ya nini unaamini kama Yehova anachukiaka kila uongo?
KWA KIFUPI
Yehova anapenda marafiki wake wakuwe wanyoofu mu mambo yote yenye wanasema na kufanya.
Maulizo ya kujikumbusha
Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wanyoofu?
Juu ya nini ni kukosa hekima kuwaza kama tunaweza kuficha kweli?
Juu ya nini unapenda kuwa munyoofu kila wakati?
HABARI ZINGINE
Namna gani wazazi wanaweza kufundisha watoto wao wakuwe wanasema kweli?
Juu ya nini ni muzuri tukuwe tunatimiza ahadi zenye tunatoa?
Ona ikiwa tunapaswa kulipa kodi hata wakati makuta yenye tunalipa inatumiwa mubaya.
“Ni Lazima Tu Tulipe Kodi?” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 9, 2011)
Nini njo ilisaidia mwanaume fulani mwenye hakukuwa munyoofu abadilishe maisha yake na akuwe munyoofu mu mambo yote?
“Nilielewa Kama Yehova Ni Mwenye Huruma na Mwenye Kusamehe” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 5, 2015)