Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • lff somo 36
  • Ukuwe Munyoofu mu Mambo Yote

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Ukuwe Munyoofu mu Mambo Yote
  • Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
  • Vichwa Vidogo
  • Habari za Kufanana na Zile
  • TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI
  • KWA KIFUPI
  • HABARI ZINGINE
  • Ukuwe Munyoofu Katika Mambo Yote
    Namna ya Kubakia Katika Upendo wa Mungu
  • Uwe Mutu Mwenye Kuaminika Katika Mambo Yote
    Mubaki “Katika Upendo wa Mungu”
  • Kuwa Muaminifu Kuko na Faida?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Sifa Yenye Kumupendeza Mungu ya Maana Sana Kupita Alimasi
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2016
Ona Habari Zaidi
Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
lff somo 36
Somo ya 36. Mwanaume iko natia sinyatire ku karatasi.

SOMO YA 36

Ukuwe Munyoofu mu Mambo Yote

Maandishi
Maandishi
Maandishi

Kila mutu anapendaka akuwe na marafiki wanyoofu, ni kusema waaminifu. Yehova naye, anapendaka marafiki wake wakuwe wanyoofu. Lakini ile haiko mwepesi juu watu wengi leo ni wadanganyifu. Kuwa munyoofu mu mambo yote kuko na faida gani?

1. Juu ya nini tunapaswa kujikaza sana kuwa wanyoofu?

Wakati tunajikaza kuwa wanyoofu, tunaonyesha kama tunamupenda Yehova na tunamuheshimia. Tusisahau kama Yehova anajua mambo yote yenye tunawazaka na kufanya. (Waebrania 4:13) Anaona wakati tunaepuka udanganyifu, na ile inamufurahishaka. Neno yake Biblia inasema hivi: “Yehova anachukia mutu mudanganyifu, lakini anafanya urafiki wa karibu pamoja na watu wanyoofu.”​—Mezali 3:32.

2. Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wanyoofu?

Yehova anapenda ‘tukuwe tunasema kweli mumoja na mwingine.’ (Zekaria 8:16, 17) Maana yake nini? Wakati tuko nazungumuza na watu wa familia yetu, wafanyakazi wenzetu, ndugu na dada zetu, ao wakubwa wa serikali hatupaswe kusema uongo ao kuwapatia habari zenye haziko za kweli. Kama tuko wanyoofu, hatutaiba ao kutenda kwa udanganyifu. (Soma Mezali 24:28 na Waefeso 4:28.) Tutalipa kodi (taxes) zote zenye tunaombwa. (Waroma 13:5-7) Kwa kufanya vile, ‘tunajiendesha kwa unyoofu katika mambo yote.’​—Waebrania 13:18.

3. Tutapata faida gani kama tuko wanyoofu?

Wengine watatutumainia kama wanajua kuwa tuko watu wanyoofu. Tena, tutasaidia kila mutu mu kutaniko ajisikie salama sawa vile mu familia yenye watu wanapendana. Tutakuwa na zamiri safi. Zaidi ya ile, kama tuko wanyoofu, ‘tutapamba mafundisho ya Mwokozi wetu, Mungu,’ na tutafanya wengine wapende kumutumikia Yehova.​—Tito 2:10.

TUJIFUNZE MAMBO MINGI ZAIDI

Tuone namna kuwa munyoofu kunaweza kumufurahisha Yehova na kukuletea faida, na namna unaweza kuwa munyoofu mu mambo mbalimbali.

4. Yehova anafurahi wakati tuko wanyoofu

Musome Zaburi 44:21 na Malaki 3:16, na kisha muzungumuzie hii maulizo:

  • Juu ya nini ni kukosa hekima kuwaza kama tunaweza kuficha kweli?

  • Unawaza Yehova anajisikiaka namna gani wakati tunasema kweli, hata wakati ni nguvu kufanya vile?

Mutoto iko nazungumuza na baba yake mwenye ameshuka juu akuwe na urefu moja naye. Jus yenye ilikuwa mu kirauli imemwangikia ku meza na chini.

Wakati watoto wanasema kweli, wazazi wanafurahiaka. Na siye wakati tunasema kweli, Yehova anafurahiaka

5. Utende kwa unyoofu kila wakati

Watu wengi wanaamini kama haiwezekane kuwa munyoofu kila wakati. Lakini, ona juu ya nini tunapaswa kuwa wanyoofu kila wakati. Muangalie VIDEO.

VIDEO: Ni Nini Inaweza Kutuletea Furaha​—Zamiri Safi (2:32)

Picha ya mu video ‘Ni Nini Inaweza Kutuletea Furaha?​—Zamiri Safi.’ Kisha Ben kuambia mukubwa wake wa kazi kama aliharibisha kitu ya maana sana, wanapatiana mikono.

Musome Waebrania 13:18, na kisha muzungumuzie namna tunaweza kuwa wanyoofu . . .

  • mu familia.

  • ku kazi ao ku masomo.

  • mu hali zingine.

6. Tutapata faida kama tuko wanyoofu

Wakati fulani, kuwa wanyoofu kunaweza kutuletea magumu. Hata vile, inakuwaka tu muzuri kuwa wanyoofu. Musome Zaburi 34:12-16, na kisha muzungumuzie hii ulizo:

  • Namna gani kuwa munyoofu kumefanya maisha yako ikuwe muzuri zaidi?

A. Bibi na bwana wako nazungumuza na wako nakunywa kahawa. B. Fundi wa kurekebisha gari iko napongezwa na mukubwa wake wa kazi fasi ya kutumikia. C. Mwanaume mwenye iko mu gari naonyesha polisi kitambulisho yake.
  1. Bibi na bwana wanyoofu wanafanya ndoa yao ikuwe nguvu

  2. Wakubwa wa kazi wanatumainiaka wafanyakazi wanyoofu

  3. Wakubwa wa serikali wanakuwaka wanasifu watu wanyoofu

WATU FULANI WANASEMAKA: “Kusema uongo kidogo haiko mubaya.”

  • Juu ya nini unaamini kama Yehova anachukiaka kila uongo?

KWA KIFUPI

Yehova anapenda marafiki wake wakuwe wanyoofu mu mambo yote yenye wanasema na kufanya.

Maulizo ya kujikumbusha

  • Namna gani tunaweza kuonyesha kama tuko wanyoofu?

  • Juu ya nini ni kukosa hekima kuwaza kama tunaweza kuficha kweli?

  • Juu ya nini unapenda kuwa munyoofu kila wakati?

Pima kufanya hivi

HABARI ZINGINE

Namna gani wazazi wanaweza kufundisha watoto wao wakuwe wanasema kweli?

Useme Kweli (1:44)

Juu ya nini ni muzuri tukuwe tunatimiza ahadi zenye tunatoa?

Utimize Ahadi Zako Juu Upate Baraka (9:09)

Ona ikiwa tunapaswa kulipa kodi hata wakati makuta yenye tunalipa inatumiwa mubaya.

“Ni Lazima Tu Tulipe Kodi?” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 9, 2011)

Nini njo ilisaidia mwanaume fulani mwenye hakukuwa munyoofu abadilishe maisha yake na akuwe munyoofu mu mambo yote?

“Nilielewa Kama Yehova Ni Mwenye Huruma na Mwenye Kusamehe” (Munara wa Mulinzi, 1 Mwezi wa 5, 2015)

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine