Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/3 uku. 7
  • “Nimejulisha Jina Lako”

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • “Nimejulisha Jina Lako”
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Jina la Mungu
    Amuka!—2017
  • Tuliheshimu Jina Kubwa la Mungu
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2013
  • Jina la Mungu Ni Nani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2019
  • Tujulishe Watu Jina la Mungu
    Huduma Yetu ya Ufalme—2003
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/3 uku. 7

“Nimejulisha Jina Lako”

“Nimejulisha jina lako kwa watu wenye ulinipatia kutoka katika ulimwengu. . . . Nimewajulisha jina lako na nitalijulisha.”​—YOHANA 17:6, 26.

Maana Yake Nini?: Yesu alijulisha jina ya Mungu kwa kuitumia wakati alikuwa nahubiri. Yesu alizoea kusoma Maandiko, na wakati alikuwa nafanya vile, bila shaka alikuwa nataya jina ya pekee ya Mungu. (Luka 4:16-21) Alifundisha wanafunzi wake kusali hivi: “Baba, jina lako litakaswe.”​—Luka 11:2.

Wakristo wa Kwanza-kwanza Walifanya Vile Namna Gani?: Mutume Petro aliambia wazee katika Yerusalemu kama Mungu alikuwa amechukua kutoka katika mataifa “watu kwa ajili ya jina lake.” (Matendo 15:14) Mitume na wengine walihubiri kama “kila mutu mwenye anaitia jina la Yehova ataokolewa..” (Matendo 2:21; Waroma 10:13) Tena, walitumia jina ya Mungu mu maandishi yao. Mukusanyo wa sheria za Wayahudi wenye kuitwa The Tosefta, wenye ulimalizwa mu mwaka wa 300 kisha kuzaliwa kwa Yesu, unasema hivi kuhusu maandishi ya Wakristo yenye wapinzani walikuwa wanalunguza: “Wanalunguza vitabu vya waeneza-injili na vitabu vya minim [watu wenye waliwaziwa kuwa Wakristo Wayahudi], wanaviacha vilungule fasi kwenye vinapatikana, . . . hata kama mu vile vitabu muko jina ya Mungu.”

Nani Njo Wako Nafanya Vile Leo?: Tafsiri ya Biblia yenye kuitwa Revised Standard Version inasema hivi mu maneno yake ya utangulizi: “Ni kosa kwa kanisa ya Kikristo kutumia jina yoyote juu ya kuzungumuzia Mungu wa kweli, sababu hakuna lazima ya kumutofautisha na miungu ingine. Wayahudi waliacha kutumia jina ya Mungu miaka mingi mbele Yesu azaliwe.” Kwa hiyo, ile tafsiri ilitumia jina ya cheo “BWANA” pa nafasi ya jina ya Mungu. Hivi karibuni, Vatikani ilipatia maaskofu wake hii maagizo: “Jina ya Mungu yenye kuandikwa kwa kutumia tetragramatoni, ni kusema HYWHa haipaswe kutumiwa ao kutamukwa mu nyimbo ao mu sala.”

Leo, nani njo wanatumiaka jina ya Mungu na kuijulisha watu? Wakati Sergey alikuwa kijana mu inchi ya Kyrgyzstan, aliangalia filme yenye ilionyesha kama jina ya Mungu ni Yehova. Miaka kumi ilipita, na hakuna kwenye alisikiaka tena ile jina. Kisha, wakati alihamia Amerika, Mashahidi wawili wa Yehova walimutembelea na wakamuonyesha jina ya Mungu mu Biblia. Sergey alifurahi kupata watu wenye walikuwa natumia jina Yehova. Jambo ya kufurahisha ni kwamba, kamusi Webster’s Third New International Dictionary inatoa hii mafasirio ku maneno “Yehova Mungu”: “Mungu mukubwa zaidi mwenye Mashahidi wa Yehova wanatambua, na yeye tu njo wanaabudu.”

[Maelezo ya chini]

a Mu kiswahili, mara mingi jina ya Mungu inatafsiriwa “Yehova.”

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine