Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w12 1/12 uku. 10
  • Sababu gani watu wengine hawafanye sikukuu ya Noeli?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Sababu gani watu wengine hawafanye sikukuu ya Noeli?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Juu ya Nini Mashahidi wa Yehova Hawasherehekeake Noeli?
    Maulizo Yenye Watu Wanaulizaka Sana Juu ya Mashahidi wa Yehova
  • Noeli ni ya Wakristo?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Shuguli za Watu Wakati wa Noeli
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2012
w12 1/12 uku. 10

Wasomaji Wetu Wanauliza . . .

Sababu gani watu wengine hawafanye sikukuu ya Noeli?

▪ Duniani pote, karibu watu miliare mbili wanafanya sikukuu ya Noeli kila tarehe 25 Mwezi wa 12, huku wengine karibu milioni 200 wanafanya sikukuu ya kuzaliwa kwa Yesu Kristo tarehe 7 Mwezi wa 1. Hata hivyo, kuna pia watu wengine wengi ambao wanaamua kutofanya sikukuu hiyo. Sababu gani?

Sababu moja ni kwamba inawezekana watu hao si wa dini zinazojiita kuwa za Kikristo. Wanaweza kuwa Wayahudi, Wahindu, ao Washinto, na kazalika. Watu wengine, kama vile wale wanaoamini hakuna Mungu, wale wanaokana mambo ya dini, ao wasomi wa elimu ya binadamu, wote hao wanaona Noeli kuwa hadisi ya uongo.

Hata hivyo, jambo la kushangaza ni kwamba watu wengi sana ambao wanamuamini Yesu hawakubali desturi zinazofanywa wakati wa Noeli. Sababu gani? Wanatoa karibu sababu ine.

Sababu ya kwanza: Hawaamini kuwa Yesu alizaliwa katika Mwezi wa 12 wala katika Mwezi wa 1. Biblia haionyeshe tarehe ya kuzaliwa kwa Yesu. Inasema tu hivi: ‘Katika inchi hiyo kulikuwako pia wachungaji wakiishi inje, wakichunga makundi yao usiku. Na kwa gafula malaika wa Yehova akasimama kando yao, na malaika akawaambia: Mwokozi ambaye ni Kristo Bwana, amezaliwa kwenu.’—Luka 2:8-11.

Mambo ya hakika yanaonyesha kuwa Yesu alizaliwa karibu mwanzoni mwa Mwezi wa 10 hivi, wakati ambapo wachungaji walikuwa wanapitisha usiku inje wakichunga makundi yao. Katika Mwezi wa 12 na Mwezi wa 1, kuna baridi kali kandokando ya muji wa Bethlehemu. Kwa hiyo, ili wanyama wao wasikufe na baridi, waliwaingiza katika nyumba.

Sababu ya pili: Tukio moja tu ambalo Yesu aliwaagiza wafuasi wake kukumbuka ni kifo chake, wala si kuzaliwa kwake, na tukio hilo la kukumbuka kifo chake lingepaswa kufanywa kwa kutumia tu mukate na divai. (Luka 22:19, 20) Pia, ona kwamba Injili ya Marko na Yohana haiseme juu ya kuzaliwa kwa Yesu.

Sababu ya tatu: Hakuna maandishi yoyote ya kihistoria yanayoonyesha kuwa Wakristo wa kwanza walikumbuka kuzaliwa kwa Kristo. Lakini walikumbuka kifo chake. (1 Wakorintho 11:23-26) Ilikuwa zaidi ya miaka 300 kisha kuzaliwa kwa Yesu ndipo dini zinazojiita kuwa za Kikristo zilianza kufanya sikukuu ya Noeli tarehe 25 Mwezi wa 12. Jambo la kupendeza ni kwamba katikati ya miaka ya 1600, baraza la kutunga sheria la Angleterre lilikataza sikukuu ya Noeli katika inchi hiyo. Katika États-Unis, Mahakama ya Juu ya Massachusetts ilikataza pia sikukuu ya Noeli. Sababu gani? Kitabu fulani (The Battle for Christmas) kinasema hivi: “Hakuna sababu yoyote inayotegemea Biblia ao historia inayoonyesha kuwa Yesu alizaliwa tarehe 25 Mwezi wa 12.” Juu ya maoni ya Wapuriti, kitabu hicho kinasema tena hivi: “Noeli ilikuwa sikukuu ya kipagani iliyofanywa kwa uongo kuwa sikukuu ya Kikristo.”

Sababu ya ine ni hii: Sikukuu hiyo haina mwanzo muzuri. Sikukuu ya Noeli ilianzishwa na taifa la kipagani la Roma, na ilitokana na muchanganyiko wa sikukuu za kumuheshimu mungu wao wa kilimo aliyeitwa Saturne na mungu wao jua aliyeitwa Sol Invictus, ao Mithra. Christian Rätsch na Claudia Müller-Ebeling, watu wenye elimu ya mambo ya wanadamu, ambao waliandika kitabu fulani (Pagan Christmas) wanasema hivi: “Kama vile desturi na imani nyingi za mbele ya Ukristo, karamu ya zamani ya kukumbuka kila mwaka kurudi kwa jua ilifanywa sasa ili kukumbuka kuzaliwa kwa Kristo.”

Kulingana na mambo yanayosemwa hapo juu, je, unaelewa sababu gani Wakristo wa kweli hawafanye sikukuu ya Noeli?

[Wazo la fungu kwenye ukurasa 10]

Tukio moja tu ambalo Yesu aliwaagiza wafuasi wake kukumbuka ni kifo chake, wala si kuzaliwa kwake

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine