Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • w14 1/8 uku. 6
  • Mungu Anakufariji

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Mungu Anakufariji
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Namna Mungu Anatolea Watu Kitulizo
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • ‘Wafariji Wote Wanaoomboleza’
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2011
  • Zawadi ya Mungu Yenye Kuwa Kubwa Zaidi—Sababu Gani Ni ya Maana Sana?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2017
  • Yesu Alikufa Kabisa kwa Ajili Yangu?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Funzo)—2019
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2014
w14 1/8 uku. 6

KICHWA | MUNGU ANAKUONA

Mungu Anaweza Kukufariji

‘Mungu, ambaye anawafariji wale walioshushwa chini [ao waliovunjika moyo], alitufariji.’ —2 WAKORINTHO 7:6.

Kijana mwanamuke anayesoma Biblia yake

‘Mwana wa Mungu alinipenda mimi na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.’ —WAGALATIA 2:20

SABABU INAYOFANYA WATU FULANI WAWE NA MASHAKA: Hata wakati wana lazima sana ya kufarijiwa, watu fulani wanaona kuwa ni kutafuta faida zao wenyewe ikiwa wanamuomba Mungu aingilie magumu waliyo nayo na kuwasaidia wapambane nayo. Mwanamuke anayeitwa Raquel anasema hivi: “Ninapoona hesabu kubwa ya watu walio katika dunia na matatizo makubwa wanayopambana nayo, mahangaiko yangu yanaonekana kuwa madogo sana, na hilo linafanya nisite kumuomba Mungu musaada.”

MAMBO NENO LA MUNGU LINAFUNDISHA: Tayari Mungu amefanya jambo fulani la pekee ili kusaidia na kufariji wanadamu. Leo, kila mutu duniani ameriti zambi inayofanya tushindwe kutimiza kwa ukamili mambo Mungu anataka. Hata hivyo, Mungu ‘alitupenda akamutuma Mwana wake [Yesu Kristo] kuwa zabihu ya upatanisho kwa ajili ya zambi zetu.’ (1 Yohana 4:10) Kupitia kifo cha Yesu cha kujizabihu, Mungu alifanya iwezekane kwetu kupata musamaha wa zambi, zamiri safi, na tumaini la uzima wa milele katika dunia mupya yenye amani.a Lakini je, zabihu hiyo ni kwa ajili tu ya wanadamu wote kwa ujumla, ao inaonyesha kwamba Mungu anakuhangaikia wewe kipekee?

Fikiria mutume Paulo. Aliguswa moyo sana na zabihu ya Yesu na kwa hiyo akaandika hivi: ‘Ninaishi kwa imani ambayo ni kumuelekea Mwana wa Mungu, aliyenipenda mimi na kujitoa mwenyewe kwa ajili yangu.’ (Wagalatia 2:20) Kwa kweli, Yesu alikufa mbele Paulo awe Mukristo. Lakini, Paulo aliona zabihu hiyo kuwa ni zawadi ya Mungu kwake.

Kifo cha Yesu cha kujizabihu ni zawadi ya Mungu kwako pia. Zawadi hiyo inaonyesha kwamba Mungu anakuona kuwa wa maana sana. Inaweza kukupatia ‘faraja ya milele na tumaini njema’ na kwa hiyo ‘kukuimarisha katika kila tendo na neno njema.’—2 Wathesalonike 2:16, 17.

Lakini, Yesu alitoa uzima wake kuwa zabihu kumepita karibu miaka 2000. Kuna jambo linaloonyesha kwamba Mungu anapenda kukukaribia wewe leo?

a Ili kujifunza mengi juu ya zabihu ya Yesu, soma sura ya 5 ya kitabu Biblia Inafundisha Kabisa Nini? kilichochapishwa na Mashahidi wa Yehova.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine