Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp16 na. 6 uku. 3
  • Maulizo Kuhusu Wale Wenye Kuishi Katika Makao ya Roho

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Maulizo Kuhusu Wale Wenye Kuishi Katika Makao ya Roho
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Habari za Kufanana na Zile
  • “Mbingu Zilifunguka”
    Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
  • Maono Kuhusu Wale Wenye Kuishi Mbinguni
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
  • Mungu Iko Fasi Yote?
    Maulizo Juu ya Habari za Biblia Yanajibiwa
  • “Nitakaa Kati ya Watu”—Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa
    Ibada Safi ya Yehova Inarudishwa Tena!
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2016
wp16 na. 6 uku. 3

HABARI KUBWA | MAONO YENYE KUTUSAIDIA KUELEWA MAKAO YA ROHO

Maulizo Kuhusu Wale Wenye Kuishi Katika Makao ya Roho

Umekwisha kujiuliza kuhusu makao ya roho na kuhusu wale wenye kuishi katika makao hayo? Ikiwa jibu lako ni ndiyo, ujue kwamba hauko peke yako. Kwa miaka mingi, watu wamekuwa na mawazo mbalimbali juu ya jambo hilo. Watu fulani wanaamini kwamba katika makao ya roho kuna wazazi wa zamani wenye wanapaswa kuheshimiwa. Wengine wanawazia makao hayo kuwa nafasi ya usalama na furaha kubwa yenye kuitwa mbinguni, kwenye malaika na watu wazuri wenye wamekufa wanaishi. Tena, wengine wanawaza kama katika makao hayo kunaishi mamilioni ya miungu.

Watu wengi wanasema kwamba hatuwezi kujua jambo lolote juu ya makao ya roho kwa sababu hakuna mutu mwenye ametoka huko ili kutuletea habari kuhusu makao hayo. Lakini, kuwaza vile ni kosa. Yesu Kristo aliishi mbinguni, ni kusema, katika makao ya roho, mbele akuje duniani. Aliambia waziwazi hivi viongozi wa dini wa wakati wake: “Nimeshuka kutoka mbinguni kufanya, si mapenzi yangu, bali mapenzi yake aliyenituma.” Kwa hiyo, Yesu alikuwa anazungumuzia jambo lenye alijionea mwenyewe wakati aliambia mitume wake hivi: ‘Katika nyumba ya Baba yangu muna makao mengi.’—Yohana 6:38; 14:2.

Kwa kweli, Baba ya Yesu ni Mungu. Jina la Mungu huyo ni Yehova, na anaishi mbinguni. (Zaburi 83:18) Kwa hiyo, hakuna mwenye anaweza kufasiria makao ya roho muzuri zaidi kuliko Yehova Mungu na Yesu Kristo. Wamefunua mambo mengi kuhusu makao hayo kupitia maono ya ajabu yenye walionyesha waaminifu fulani.

Habari yenye kufuata inazungumuzia sehemu fulani za Biblia zenye kuonyesha mambo yenye watu waliona kupitia maono mbalimbali. Wakati unachunguza maono hayo, ukumbuke kwamba makao ya roho haiko nafasi ya kimwili yenye kuwa na vitu vyenye tunaweza kugusa ao kuona. Kwa hiyo, kuliko kufasiria mambo kupitia maneno yenye viumbe wa roho tu wanaweza kuelewa, Mungu alitumia maono ili kutufasiria makao ya roho kupitia maneno yenye sisi wanadamu tunaweza kuelewa. Maono hayo yatakusaidia kujua wale wenye kuishi katika “makao [hayo] mengi” ya roho.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine