Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • km 2/12 uku. 3
  • Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi
  • Huduma Yetu ya Ufalme—2012
Huduma Yetu ya Ufalme—2012
km 2/12 uku. 3

Kujikumbusha Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi

Maulizo yanayofuata yatatumiwa kwenye Masomo ya Huduma ya Kiteokrasi katika juma tokea tarehe 27 mwezi wa 2, 2012. Tarehe ambayo kila wazo lilizungumuziwa inaonyeshwa pia ili kusaidia watu kutafuta majibu katika vitabu wanapotayarisha masomo ya huduma kila juma.

1. Je, ni sawa kusema kwamba rehema ya Yehova inasawazishwa na haki yake? (Isa. 30:18) [Juma tokea tarehe 9 mwezi wa 1, w02 1/3-F uku. 30]

2. Tunaweza kujifunza nini kutokana na jinsi Shebna aliachishwa kazi ya kuwa musimamizi-nyumba wa Hezekia? (Isa. 36:2, 3, 22) [Juma tokea tarehe 16 mwezi wa 1, w07 15/1 uku. 8 fu. 6]

3. Kuhusiana na jinsi ya kupambana na taabu, tunaweza kujifunza nini kutokana na habari iliyo katika Isaya 37:1, 14-20? [Juma tokea tarehe 16 mwezi wa 1, w07 15/1 uku. 9 fu. 1-2]

4. Namna gani mufano unaopatikana kwenye Isaya 40:31 unawatia watumishi wa Yehova moyo? [Juma tokea tarehe 23 mwezi wa 1, w96 15/6 uku. 10-11]

5. Maeno ya Yehova yaliyo kwenye Isaya 41:14 ni yenye kutia moyo hasa leo kwa sababu ya shambulio gani linalokaribia? [Juma tokea tarehe 23 mwezi wa 1, ip-2 uku. 24 fu. 16]

6. Namna gani tunamuonyesha Yehova kwamba ‘tunafuata uadilifu’? (Isa. 51:1) [Juma tokea tarehe 6 mwezi wa 2, ip-2 uku. 165 fu. 2]

7. “Wengi” wanaotajwa kwenye Isaya 53:12 ni nani, na tunajifunza nini kutokana na jinsi Yehova anavyowatendea? [Juma tokea tarehe 13 mwezi wa 2, ip-2 uku. 213 fu. 34]

8. Watu wa Yehova wamepata nini katika siku za mwisho kama inavyoelezwa kwa njia ya mufano kwenye Isaya 60:17? [Juma tokea tarehe 20 mwezi wa 2, ip-2 uku. 316 fu. 22]

9. “Maka wa nia njema” ambao Yesu na wafuasi wake waliamuriwa kutangaza unamaanisha nini? (Isa. 61:2) [Juma tokea tarehe 20 mwezi wa 2, ip-2 uku. 324-325 fu. 7-8]

10. Maneno yaliyo katika Isaya 63:9 yanakazia sifa nzuri gani ya Yehova? [Juma tokea tarehe 27 mwezi wa 2, w03 1/7 uku. 19 fu. 22-23]

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine