Watchtower—MAKTABA KU ENTERNETE
Watchtower
MAKTABA KU ENTERNETE
Kiswahili (Congo)
  • BIBLIA
  • VICHAPO
  • MIKUTANO
  • wp21 na. 1 uku. 14-15
  • Kusali Kunaweza Kukuletea Faida Gani?

Hakuna video juu ya habari yenye umechagua.

Pole, kulikuwa kosa fulani wakati video ilikuwa inajaribu kusoma.

  • Kusali Kunaweza Kukuletea Faida Gani?
  • Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
  • Habari za Kufanana na Zile
  • Sala— Inaweza Kukuletea Faida Gani?
    Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova—2015
  • Namna ya Kumukaribia Mungu Katika Sala
    Biblia Inafundisha Kabisa Nini?
  • Sala Ni Zawadi Kutoka kwa Mungu
    Biblia Inatufundisha Nini?
  • Go Rapela Modimo go Nyoko go Šutetsa Thina Naye
    Furahia Maisha Milele!—Ujifunze Biblia kwa Njia ya Mazungumuzo
Ona Habari Zaidi
Munara wa Mulinzi Unaotangaza Ufalme wa Yehova (Gazeti la Watu Wote)—2021
wp21 na. 1 uku. 14-15

Kusali Kunaweza Kukuletea Faida Gani?

Wakati Pamela alikuwa na ugonjwa wa kansere, alienda kuona munganga ili amusaidie. Lakini, alisali pia kwa Mungu ili kumuomba nguvu ya kuvumilia ugonjwa wake. Kusali kulimusaidia?

Pamela anafasiria hivi: “Wakati walikuwa wananitunza ugonjwa wangu wa kansere, mara mingi nilikuwa naogopa sana. Lakini wakati nilisali kwa Yehova Mungu, nilijisikia kuwa mwenye kutulia na niliweza kuvumilia ile ugonjwa bila kuogopa. Ninaendelea kusikia maumivu, lakini sala inanisaidia niendelee kuwa na mawazo yenye kufaa. Wakati watu wananiuliza namna ninajisikia ninasema, ‘sijisikie muzuri, lakini niko na furaha!’”

Hata hivyo, hatupaswe kuchunga wakati tunakuwa na ugonjwa hatari ao tatizo la nguvu njo tusali. Sisi wote tunakuwaka na magumu, ya nguvu ao hapana, na mara mingi tunakuwaka na lazima ya musaada ili tuweze kupambana nayo. Kusali kunaweza kutusaidia?

Biblia inasema hivi: “Umutupie Yehova muzigo wako, naye atakutegemeza. Hataruhusu hata kidogo mwenye haki aanguke.” (Zaburi 55:22) Ile ni maneno yenye kutia moyo sana! Sasa, sala inaweza kukuletea faida gani? Wakati unasali kwa Mungu mu njia yenye kufaa, atakupatia mambo yenye uko nayo lazima ili uweze kuvumilia magumu yako.​—Ona kisanduku “Faida Mbalimbali za Kusali.”

Faida Mbalimbali za Kusali

Amani ya moyo

Ule mufanyabiashara mwenye alipoteza kazi yake, iko mwenye furaha na iko na tumaini.

“Maombi yenu yajulishwe Mungu; na amani ya Mungu yenye kupita uelewaji wote italinda mioyo yenu na nguvu zenu za akili kupitia Kristo Yesu.” (Wafilipi 4:6, 7) Wakati unamuambia Mungu mahangaiko yako atakusaidia uendelee kuwa mwenye kutulia na utende kwa hekima wakati wa ile mahangaiko.

Hekima yenye kutoka kwa Mungu

Ule mwanamuke mwenye alikuwa anasoma sala mu kitabu, iko anasoma Biblia yake ku nyumba.

“Kama mutu yeyote kati yenu anakosa hekima, aendelee kumuomba Mungu, kwa maana yeye anapatia wote kwa ukarimu na bila kulaumu, na atapewa hiyo.” (Yakobo 1:5) Wakati tuko na mukazo wa akili, siku zote hatukamatake maamuzi ya muzuri. Kama unaomba Mungu hekima, anaweza kukukumbusha kanuni mingi za kukusaidia zenye zinapatikana mu Neno lake, Biblia.

Nguvu na faraja

Bibi na bwana wenye walikuwa ku hopitali, wako wanatembea pamoja mu bustani. Bwana yake iko anamukamata ku mukono wakati iko anajikaza kutembea na fimbo.

“Kwa mambo yote niko na nguvu kupitia ule mwenye ananipatia nguvu.” (Wafilipi 4:13) Juu Yehova ni Mungu mweza-yote anaweza kukupatia nguvu yenye uko nayo lazima, ili kupambana na magumu ao kukusaidia wakati wa ile magumu. (Isaya 40:29) Biblia inamuita pia Yehova “Mungu wa faraja yote.” Anaweza “kutufariji katika majaribu yetu yote.”​—2 Wakorinto 1:3, 4.

UNAPENDA SALA IKUSAIDIE?

Kwa kweli, Yehova hakukaze usali kwake. Lakini anakuomba ufanye vile juu anakupenda. (Yeremia 29:11, 12) Tuseme nini ikiwa zamani ulijisikia kama Mungu hakujibia sala zako? Usivunjike moyo. Wakati fulani, wazazi wenye upendo hawapatiake watoto wao jambo lenye waliomba na mu wakati yenye walitazamia. Pengine wazazi wanajua jambo la muzuri zaidi. Lakini kusema kweli, wazazi wenye upendo wanasaidiaka watoto wao.

Yehova Mungu ni baba mwenye upendo zaidi na anapenda pia kukusaidia. Kama unachunguza kwa uangalifu mashauri yenye tumetoka kuzungumuzia na kujikaza kuitumikisha, Mungu anaweza kujibia sala zako mu njia ya muzuri zaidi!​—Zaburi 34:15; Matayo 7:7-11.

    Vichapo vya Swahili (Congo) (1996-2025)
    Toka
    Ingia
    • Kiswahili (Congo)
    • Tumia Wengine
    • Préférences
    • Copyright © 2025 Watch Tower Bible and Tract Society of Pennsylvania
    • Kanuni za Matumizi
    • Kanuni za Kutunza Siri
    • Paramètres Kuhusu Kutunza Siri
    • JW.ORG
    • Ingia
    Tumia Wengine