NAMNA YA KUJIFUNZA
Tafuta Fasi ya Muzuri ya Kujifunzia
Unapenda funzo yako ikuletee faida zaidi? Pima kufanya hii mambo:
Tafuta fasi ya muzuri. Kama inawezekana, tafuta fasi yenye kuwa safi na yenye kuwa na mwangaza. Unaweza kuikala mbele ya meza, ao unaweza kuikala inje fasi ya muzuri.
Ukuwe peke yako. Yesu aliamua kusali “asubui sana” na “mahali kwenye hapakukuwa watu.” (Mk. 1:35) Kama haiwezekane kupata fasi kwenye unaweza kuwa weye peke juu ya kujifunza, unaweza kuambia batu ya familia yako ao batu benye unaishi nabo juu ya programe yako ya funzo, na ubaombe basikusumbue wakati uko najifunza.
Tia akili fasi moya. Epuka mambo yenye kukengeusha akili. Kama uko najifunzia mu telefone ao mu tablete, uitie mu hali yenye haitakusumbua. Na kama wakati uko najifunza unakumbuka jambo fulani yenye unapaswa kufanya, uiandike pembeni juu uifanye saa ingine. Kama unashindwa kutia akili yako fasi moya, usimame na utembee kidogo, ao ujinyoroshe kidogo.